Lusekelo anakata tawi alilokalia?

Mzee Mwanakijiji wewe una mapenzi binafsi na Mwalimu, hapo sikulaumu kabisa baba yetu wa Taifa ameifanyia Tanzania mambo mengi mazuri tu, wengi tulisoma bure, na wazazi wetu wamesoma bure, amani tunayo lugha moja n.k.

Kauli yako hapo juu ina-imply kuwa iliwezekana kumpinga Mwalimu, na kuwa uhuru wa vyombo vya habri ulikuwepo. Kwa mawazo yangu binafsi kumpinga nyerere haikuwepo kwenye agenda kabisa enzi zake hata kama hatuwezi kuthibitisha hayo kwa maandishi, uhuru wa kusema unachotaka haikuwepo kwenye agenda, achilia mbali magazeti hata kwenye vijiwe na washkaji watu walikuwa wanaogopa kusema vitu vya kupinga maana maofisa wa usalama wa taifa walikuwa wamepenyezwa kwenye kona zote za jamii na ole wako ujifanye unapenda uhuru ungekoma.

Mzee mwanakijiji hapo unamtetea mwalimu kwa mapenzi tu, hoja hapo hamna, aliyempinga mwalimu alikiona cha moto!

Achilia mbali uhuru wa kusema, enzi za Nyerere hata uhuru wa kumiliki chako haukuwepo, akiamua chako si chako basi hakitakuwa chako, anakuja kukuny'ang'anya mara moja, Azimio la Arusha pale aliwanyang'anya watu mali zao bila kujali haki zao za kumiliki kilicho chao, katika miaka ya 80 waziri wake mkuu aliwapelekesha watu kishenzi yeye akiwa raisi akiangalia tu, sijui majamaa ambao walikuwa wananunua mahindi na maharage na ku-supply shule za sekondari wengine wali-supply nyama n.k faida waliyopata katika mauzo hayo walinyang'anywa zote! polisi walikuwa wanakuja na kuwanyanyasa kishenzi kwa amri kutoka juu wakati watu wale walikuwa ni wafanyabiashara tu wanaojituma, ndio maana mpaka leo watanzania wakiona mtu mfanyabiashara anatengeneza pesa wanasema mbaya, wakiona mfanyabiashara anagombea cheo wanaona haifai, sharti uwe mkulima wa kahawa inayouzwa senti moja kwa gunia uwe fukara basi wewe safi.

Nyerere had his weaknesses vile vile hakuwa muumba, hilo lazima tutambue na kulikubali.

Kumbe na wewe umemstukia eehh? Mzee wetu huyu bwana ana mapenzi binafsi tu na Mwalimu na hayo mapenzi yamemgubika kabisaa kiasi kwamba haoni hata yale yaliyodhahiri...
 
Kumbe na wewe umemstukia eehh? Mzee wetu huyu bwana ana mapenzi binafsi tu na Mwalimu na hayo mapenzi yamemgubika kabisaa kiasi kwamba haoni hata yale yaliyodhahiri...

Ni kweli kabisa, Mwanakijiji haambiwi hapo, Mzee M huyo hata akiongea tu utafikiri nyerere;);)
 
Mzee Mwanakijiji wewe una mapenzi binafsi na Mwalimu, hapo sikulaumu kabisa baba yetu wa Taifa ameifanyia Tanzania mambo mengi mazuri tu, wengi tulisoma bure, na wazazi wetu wamesoma bure, amani tunayo lugha moja n.k.

Kauli yako hapo juu ina-imply kuwa iliwezekana kumpinga Mwalimu,

Iliwezekana kumpinga Mwalimu, but you had to be good enough kumpinga kwa hoja na umshinde! Kina Msuya walimpinga Mwalimu, Malecela mwenye alithubutu kumpinga Mwalimu, lakini aliwashinda kwa hoja au walishindwa kupangua hoja zake! Intellectually ni wachache waliweza kumpinga wakashinda!

na kuwa uhuru wa vyombo vya habri ulikuwepo. Kwa mawazo yangu binafsi kumpinga nyerere haikuwepo kwenye agenda kabisa enzi zake hata kama hatuwezi kuthibitisha hayo kwa maandishi, uhuru wa kusema unachotaka haikuwepo kwenye agenda, achilia mbali magazeti hata kwenye vijiwe na washkaji watu walikuwa wanaogopa kusema vitu vya kupinga maana maofisa wa usalama wa taifa walikuwa wamepenyezwa kwenye kona zote za jamii na ole wako ujifanye unapenda uhuru ungekoma.

this is the biggest myth ever! unajua ni mambo mangapi yalikuwa yanasemwa kuhusu Mwalimu? Ni lini ulisikia Waziri ametokea hadharani na kusema msimuite Rais Mchonga, Haambiliki n.k? Leo hii Rais kaitwa "msanii" tukatishiwa "Amiri Jeshi Mkuu" msimchokoze! Ni nani alipigwa au kunyang'anywa kamera kwa sababu ya uandishi wake? Nitafutie mwandishi aliyepigwa au kukatazwa kufanya kazi yake wakati wa Mwalimu, and I'll show you waliofanyiwa hivyo chini ya Mwinyi, Mkapa, na Kikwete!

Mzee mwanakijiji hapo unamtetea mwalimu kwa mapenzi tu, hoja hapo hamna, aliyempinga mwalimu alikiona cha moto!

Nipe hata mfano mmoja (hata kwa juu juu) wa tukio moja la mwandishi au mwana habari aliyekiona cha moto kwa kumpinga Mwalimu..

Achilia mbali uhuru wa kusema, enzi za Nyerere hata uhuru wa kumiliki chako haukuwepo, akiamua chako si chako basi hakitakuwa chako, anakuja kukuny'ang'anya mara moja,

Sasa hii ni hoja ya msingi lakini guess what, mataifa mengi yalipoanza yalifanya mambo mengi si sawa sawa! na watawala walifanya makosa, lakini kuna mambo yaliyofanyika wakati wa kuanzisha Taifa letu ambayo lazima yangefanyika. Leo hii sisi hatuna matatizo makubwa ya ardhi kwa sababu ya Azimio la Arusha; leo hii hatuna matatizo ya sisi wenyewe kumiliki vitu sababu ya Azimio la Arusha; Azimio la Arusha was a necessity ama sivyo yanayotokea Zimbabwe, yaliyotokea Uganda, na yanayofurukuta Kenya yangetokea kwetu. Ni lazima uende zaidi ya kuangalia kwa ubinafsi wa mtu tu! Ilifanywa kwa haki la? ilikuwa ni lazima absolutely! Ni lazima sasa hivi la hasha; japo kuna mambo ambayo yalikuwemo kwenye Azimio la Arusha ambayo hatuna budi kuyarudia!

Azimio la Arusha pale aliwanyang'anya watu mali zao bila kujali haki zao za kumiliki kilicho chao, katika miaka ya 80 waziri wake mkuu aliwapelekesha watu kishenzi yeye akiwa raisi akiangalia tu, sijui majamaa ambao walikuwa wananunua mahindi na maharage na ku-supply shule za sekondari wengine wali-supply nyama n.k faida waliyopata katika mauzo hayo walinyang'anywa zote!

Hakunyang'anya tu watu mali zao, nenda ujifunze Azimio la Arusha lilikuwa lina misingi gani na kwanini lilikuwa ni lazima! Kila kitu kina historia tatizo ni kujaribu kuliangalia hili kwa mtazamo wa "kuonewa" badala ya kuangalia kwanini lilihitajika. Tusingeweza kuwa na Taifa ambalo wakazi wengi hawana njia za kumiliki uchumi na sehemu kubwa iko mikononi mwa kikundi cha watu wachache! Kama Zimbabwe wakati wanapata uhuru wangefanya tulichofanya sisi, baadhi ya matatizo wasingekuwa nayo leo!

polisi walikuwa wanakuja na kuwanyanyasa kishenzi kwa amri kutoka juu wakati watu wale walikuwa ni wafanyabiashara tu wanaojituma, ndio maana mpaka leo watanzania wakiona mtu mfanyabiashara anatengeneza pesa wanasema mbaya, wakiona mfanyabiashara anagombea cheo wanaona haifai, sharti uwe mkulima wa kahawa inayouzwa senti moja kwa gunia uwe fukara basi wewe safi.

Wafanyabiashara "wanaojituma".. hivi unajua nani alikuwa anatoa ajira na nani walikuwa wamiliki wakubwa wa makampuni n.k Leo hii hata Marekani na nchi nyingi zina utaratibu wa kuzuia magendo! Hapa Marekani mfanyabiashara akijiamulia kupandisha bei ya bidhaa ili ajipatie faida zaidi wakati wa matatizo atafungwa kwa price gauging! Wakati ule wa njaa ya 1984 wakati tunakaribia kufa njaa, wafanyabiashara wakaanza kuficha bidhaa ili waziuze kwa magendo (interfered with supplies of essential commodities) na lazima serikali iingilie kati and I promise you.. that will happen again in case wafanyabiashara wetu wanataka kutengeneza faida zaidi kwenye migongo ya wakulima na wafanyakazi wa nchi yetu!


Nyerere had his weaknesses vile vile hakuwa muumba, hilo lazima tutambue na kulikubali.

Hilo halina mjadala na nina akili timamu kutambua Nyerere hakuwa muumba, kwani alikufa kama wanadamu wengine! I don't need a lecture on his humanity for I have never argued that he was a divine being! or a Son of a God!
 
Nipe hata mfano mmoja (hata kwa juu juu) wa tukio moja la mwandishi au mwana habari aliyekiona cha moto kwa kumpinga Mwalimu..

Hakuna!kwa sababu hakuna aliyethubutu kumpinga mwalimu, si ndo kama nilivyokuambia? hiyo haikuwa kwenye agenda kabisa, kumpinga mwalimu hakuna!haikuwepo.

Otherwise hizo hoja nyingine nakubali yaishe:)
 
Kumbe kuna wengine walimchukia Nyerere sana kama mzee N na P haa ha haaaaa......... kazi kweli kweli. Haya tuambieni hao askari kanzu walivyokuwa wanafanya.

Wakati wa mwalimu angalau tulikuwa na viwanda na mishahara ilikuwa inatosha hadi baada ya vita ya nduli, sasa tangu aachie hirizi tumefika wapi? Wako wapi hao viongozi mahiri na mashujaa wa kumzidi mwalimu?
 
Hivi ni RAIS gani pale Tanzania aliyeweka watu wengi vizuizini bila ya kuwafungulia mashtaka mahakamani kama si Nyerere.?? Nyerere ana mazuri yake mengi tu lakini pia alikuwa na mabaya yake hasa kuhusiana na kukosekana kwa freedom of speech na demokrasia ya kweli. Alitumia dola na usalama wa Taifa kuwadhibiti wengi waliompinga.
 
..wewe mwanakijiji ingekuwa enzi za Nyerere na hizo news zako za kisungura cha Lowassa usingethubutu kukanyaga DIA ungefia huko huko ulipo au ungerudi na kufia ukonga!
 
Hivi kuna mtu ana idadi kamili ya waliofungwa bila mashitaka? Vile vile aliowanyonga bila hatia na kwa makosa gani?

Idadi ya marafiki zake walioua na kuachiwa huru? na kadhalika.
 
Dua, majaribio yanayofanywa yalifanywa na baadhi ya waandishi waliopinga sera zake za kijamaa. There have been this attempt of dictatorization of Mwalimu!

a. Katika utawala wa Mwalimu kuna watu waliwekwa kizuizini kama watu wanavyowekwa kizuizini sehemu mbalimbali duniani na hawafunguliwi mashtaka. Na niyeye aliyeleta mabadiliko baadaye ya sheria ya kuwaweka watu kizuizini (prevention and detention act). Nchi yetu ilirithi kwa kiasi kikubwa sheria ya kikoloni na kwa muda tulienda nayo hivyo hivyo hasa baada ya kugoma kwa jeshi in 1964 ambapo Mwalimu alitambua kuwa siyo wote weusi ni wazalendo na siyo wote wanaosimama kuapa wana maslahi ya TAifa.

b. Rais Nyerere alitumia uwezo wake wa kisheria, uwezo ambao hata Kikwete leo anao na anaweza kuutumia akitaka. Hakuna mtu yeyote ambaye anaweza kuonesha kuwa Mwalimu alifanya jambo ambalo halikuwa ndani ya uwezo wake kisheria. Kama kuna wakati ambapo Mwalimu angetaka kuonesha ukiukaji wake wa sheria ni wakati wa kesi ya Uhaini. Leo hii wale wajemaa wangepigwa risasi na kuambiwa ni majambazi.

c. Siwezi kushangaa kuna watu ambao hadi leo hatujapewa maelezo nini kiliwapata. Mwalimu hayupo hai sasa na kama kuna watu wanatakiwa maelezo yao tunao viongozi ambao wanaweza kuruhusu historia yetu iangaliwe kwa karibu na iandikwe sawasawa. Kama Vaticani inaruhusu watu wapitie rekodi ya Papa Pius, nina uhakika kama kuna rekodi ya Mwalimu isiyo sahihi yenye utata inaweza kuchunguzwa.

d. Mzee Geeque, ni watu wangapi waliwekwa vizuizini wakati wa Mwalimu na kwa makosa gani. Tanzania ipo sheria ya Prevention and Detention Act ambayo bado inafanya kazi. Asikudanganye mtu hata Marekani sheria kama hiyo ipo, Uingereza wanayo na serikali nyingi zinazo uwezo huo duniani wa kuweza kumtia mtu kizuizini kwa muda fulani na kumuachia bila kumfikisha mahakamani. Zinatumika sana wakati wa maandamano au vurugu. Miye naomba nitajiwe mtanzania mmoja ambaye alikamatwa akatiwa kizuizini na hakufikishwa mahakamani. Inawezekana wapo lakini haiwezi kuwa kama ulivyosema. Hivi mzee mwenzangu umejuaje watu wengi waliwekwa kizuini bila kufikishwa mahakamani zaidi wakati wa Nyerere kuliko wakati wa marais wengine? Na mzee Geeque, Mwalimu alitumia dola vipi kuwadhibiti waliompinga. Mtei yupo. Babu karudi na kafia TAnzania, Kambona karudi na kafia Tanzania, Fundikira kaishi na kafia TAnzania na orodha goes on and on. Lakini msifanye makosa endapo kuna Mtanzania yeyote anafikiria uhaini ajue kabisa kuwa hakuna demokrasia au utawala bora utakaomuokoa. Hilo ni kosa kubwa katika jamhuri yetu. Wamerekani walishanyonga watu in the fifties kwa makosa ya Uhaini! Hata leo hii ukikutwa na hatia ya Uhaini umekwisha; ndio maana wale ndugu zetu wa Zanzibar waliodaiwa kufanya uhaini Zanzibar waliachiwa na Mahakama!

e. Katika utawala wake wa miaka 25 Mwalimu alitia sahihi hati mbili tu za kuruhusu waliohukumiwa kunyongwa wanyongwe. Yule aliyemuua Dr. Kleruu na mtu mwingine (sikumbuki moja kwa moja). Wakati wa utawala wa Mwinyi watu walikuwa wanapukutika kama njugu (nilipata nafasi ya kushuhudia akinyongwa mtu pale Butimba) in early 90s. Dikteta au kiongozi mwenye nguvu kama Mwalimu angewapukutisha waliompinga. Naomba mnishawishi wazee wenzangu kuwa Mwalimu alikuwa borderline dictator au ametumia madaraka asiyokuwa nayo.

Najua kuna watu ambao hawajamuelewa Mwalimu na hawataki kumuelewa Mwalimu. Madai mengi yanayotolewa dhidi ya Mwalimu hayana msingi katika ukweli ni fiction. Ndiyo maana alipokufa kuna waandishi wa habari wa Kimataifa waliripoti "The TAnzanian Dictator Died".. halafu wakashangaa mbona watu hawaruki ruki na kushangilia?.. Friends Mwalimu was a human being na alifanya makosa na yeye mwenyewe alikiri makosa (sikiliza hotuba yake ya Mei Mosi 1995) but he was not the terrible man and benevolent dictator some people are trying to potray him. No sir, he was not.
 
Nyi hapa mtakesha mkibishana na Mwanakijiji kuhusu Nyerere. Kwanza yeye mwenyewe anajidhania ndio Nyerere wa sasa....msikilizeni tu hata kwenye redio yake...anamuiga Nyerere...kuanzia sauti, lafudhi, hata vicheko vyake vinafanana na vya Nyerere...sasa kweli hapo mtamwambia nini?

Anyway, Mwanakijiji homework niliyokupa vipi...mbona unaonekana kama unaikwepa?
 
Acha porojo we nyani tutakurudisha msituni uende kukaa na ngedere wenzio. {JOKE}
 
Nyani Ngabu

Unafahamu nilikuwa najiuliza hivi mchonga kama kweli angekuwa na roho ya korosho kama viongozi wetu wa leo ni wangapi wangeweza kusoma enzi zile? Kumbuka vijana kama 27 walirudishwa kutoka Ukraine, Uchina kuna kiama kingine n.k. bila kusahau wanafunzi walikuwa wanasomeshwa pamoja na warrants za usafiri, chakula, malazi na elimu yenyewe n.k.
 
Mwanakiji kiboko,amembadilisha Dua dakika moja tuu mpaka dua katoa thanks bila kujua..keep it up bro lakini hapa bado!
 
Nyani Ngabu

Unafahamu nilikuwa najiuliza hivi mchonga kama kweli angekuwa na roho ya korosho kama viongozi wetu wa leo ni wangapi wangeweza kusoma enzi zile? Kumbuka vijana kama 27 walirudishwa kutoka Ukraine, Uchina kuna kiama kingine n.k.

Hakuna mtu aliyesema Mwalimu alikuwa na roho mbaya...angalau si mimi niliyesema hayo! Kinachozungumzwa hapa ni uhuru wa kujieleza/ kutoa maoni na uhuru wa vyombo vya habari wakati wa utawala wake. Tunaambiwa kulikuwa na vyombo vya habari binafsi ambavyo vilikuwa huru kuripoti, kukosoa, kupinga na kutoa hoja zenye mitazamo tofauti. Nimemwomba Mwanakijiji anitajie hivyo vyombo ili tuvijadili ipasavyo. Huwezi ukasema vilikuwepo na vilikuwa huru bila kuviangalia nje ndani jinsi vilivyotenda na kufanya kazi. Kusema tu vilikuwepo haitoshi. Vitajwe, tuvichambue kwa mapana na marefu na kwa mifano. Au wewe unasemaje Dua? Sasa kwa vile Mwanakijiji ameamua kunipiga chenga ya mwili, nakuomba wewe umpe tafu basi au siyo..?
 
Mwanakiji kiboko,amembadilisha Dua dakika moja tuu mpaka dua katoa thanks bila kujua..keep it up bro lakini hapa bado!

Ha ha ha haaaaa............ati Mwanakijiji nini? Hajanibadilisha kitu, mimi naangalia ukweli tu sina ushabiki ya Yanga na Simba.
 
Huoni Mugabe amewafukuza BBC kule kwake au? Kwani hivyo vyombo vya kimataifa hawaongelei yanayotokea ndani ya nchi. Hata VOA walikuwepo sasa ulitaka vyombo gani tena au unaongelea gazeti la Kiongozi kama sikosei hili lilikuwa la dini ya kikatoliki huenda jina nimechanganya.

Anyway weka definition yako vizuri.
 
Back
Top Bottom