Lusekelo anakata tawi alilokalia?

Mwanakijiji,

Sasa mbona wewe mkuu unawaogopa hawa watawala kwamba watakukolimba? Lusekelo yuko pale pale tena anaandika kwenye gazeti la serikali.

Tanzania hatuna freedom of press kama baadhi ya nchi za West lakini pia hali sio mbaya sana kama baadhi ya watu wanavyotaka tuamini. Huenda woga wetu na rushwa vinatuponza zaidi kuliko hata
watawala kutuandama.

Tuwaunge mkono waandishi wazuri ili waendeleze mapambano ya fikra. Mwanakijiji, usiache mapambano na PM, tunataka makala kama ile ya Kasungura ka Lowassa.

Hongera Lowassa kwa kubaki na msimamo wako miaka na miaka bila kuyumba.


Mtanzania, wanasema huku bongo kuwa ukimwandika PM sana anakutafuta na kumkabidhi kijana wake amalizane na wewe. Wengi waandishi wanaandika kwa nia ya kutaka baadaye wanunuliwe!

Kuwa macho.
 
So what are you trying to say....? Kwamba Mwanakijiji naye keshanunuliwa na ndio maana makala za kumpinga Lowassa zimepungua kama sio kuisha....
 
I have known lusekelo some years past when i used most of my time at the Guardian. We use to joke nd he is the guy. I mean kwa kitambo angeweza kuwa politician but he still remain faithful to serve society through his writting hand.

But let us remember Katabalo (|RIP) if am not mistaken the name, he went to ades after posting his famous makala's about early ufisadi in government. for such short recap let our prayes covers Lusekelo....

I heard alipata some wakati mgumu kitambo kidogo, how is he now?? does he quited the stuff??

I give five to him..
 
Mwanakijiji,

Sasa mbona wewe mkuu unawaogopa hawa watawala kwamba watakukolimba? Lusekelo yuko pale pale tena anaandika kwenye gazeti la serikali.

Mtanzania, siogopi kukolimbwa; ningekuwa nyumbani ningeandika ninayoyaandika kwa jina langu kamili... Ukiwa mbali kuna disadvantages nyingi tu... Hofu yangu kubwa ni kunyamazishwa au kutopewa nafasi ya kusema; Lusekelo ni Lusekelo na sijui mazingira yake yote ya kile anachokifanya. Mimi kama wewe nafurahia maandishi yake kwa kiasi kikubwa tu! Sithubutu kujilinganisha naye.

Tanzania hatuna freedom of press kama baadhi ya nchi za West lakini pia hali sio mbaya sana kama baadhi ya watu wanavyotaka tuamini. Huenda woga wetu na rushwa vinatuponza zaidi kuliko hata
watawala kutuandama.

Mzee kuna tofauti ya kuandika issues na kuna tofauti ya kuandika issues kwa namna ninayoandika mimi kwa mfano. Mimi nataja majina na kuyachambua bila kuzungushana;

Tuwaunge mkono waandishi wazuri ili waendeleze mapambano ya fikra. Mwanakijiji, usiache mapambano na PM, tunataka makala kama ile ya Kasungura ka Lowassa.

Mwenzio ameamini kuwa miye natumiwa na wabaya wake... Ilipotoka makala ya "Kasungura" waliamini kuwa "kwanini anamuandama waziri mkuu" Sasa wakati mwingine haya yote yanaweka pressure kubwa kwa baadhi ya waandishi kuzungumza kwa ujumla wake.
Hongera Lusekelo kwa kubaki na msimamo wako miaka na miaka bila kuyumba.


Absolutely!!!
 
Mtanzania, wanasema huku bongo kuwa ukimwandika PM sana anakutafuta na kumkabidhi kijana wake amalizane na wewe. Wengi waandishi wanaandika kwa nia ya kutaka baadaye wanunuliwe!

Kuwa macho.


yawezekana hilo ni kweli; lakini katika taifa letu kuna watu zaidi ya Lowassa na kuna issues zaidi ya Lowassa. Ninaandika kwa uhuru wangu; sasa hivi amekuwa kimya na sina sababu ya kumuandama ilimradi nimuandame. Nitakuwa siitendei haki dhamira yangu.
 
well written lakini ni yeye mtu mmoja tuu,Daily news at the end of the day ni la hao hao mafisadi na sitegemei mabadiliko yeyote,na hii ya Lusekelo kumsifia nyerere in relation to media is a big joke...nakubaliana na Nyerere vitu vingi lakini kwenye media alikuwa mkandamizaji tuu na kulikuwa hakuna uhuru wowote wakati wake kwa hiyo tuache unafiki hapo.
 
well written lakini ni yeye mtu mmoja tuu,Daily news at the end of the day ni la hao hao mafisadi na sitegemei mabadiliko yeyote,na hii ya Lusekelo kumsifia nyerere in relation to media is a big joke...nakubaliana na Nyerere vitu vingi lakini kwenye media alikuwa mkandamizaji tuu na kulikuwa hakuna uhuru wowote wakati wake kwa hiyo tuache unafiki hapo.


kobe wenzio walikuja na kusema hayo hayo na tukawakatalia! Kuwa na vyombo vingi vya habari siyo sawa na kuwa na uhuru wa habari. Kuwa na TV nyingi n.k siyo the same na kuwa huru kutoa mawazo. Kulikuwa na uhuru mkubwa wa habari na mawazo wakati wake kwa sababu alikuwa na uwezo wa kusimama na hoja; unajua mara ngapi alikuwa akienda Chuo Kikuu kufanya mazoezi ya kiakili na wasomi wenzake? Ni lini Mkapa, Mwinyi, au hata Kikwete ambao walikuwa comfortable kushiriki intellectual exchanges pale Mlimani? Kama hujawahi kuhudhuria mikutano ile ya Mwalimu pale Mlimani you have no idea how free those things were.. waulize kina Shivji, Mkapa mwenyewe na Othman na hata Mazrui...
 
well written lakini ni yeye mtu mmoja tuu,Daily news at the end of the day ni la hao hao mafisadi na sitegemei mabadiliko yeyote,na hii ya Lusekelo kumsifia nyerere in relation to media is a big joke...nakubaliana na Nyerere vitu vingi lakini kwenye media alikuwa mkandamizaji tuu na kulikuwa hakuna uhuru wowote wakati wake kwa hiyo tuache unafiki hapo.

Mbona hapo Lusekelo hajamsifia Nyerere kwa ujumla kuhus free press. Yeye amesisitiza kuwa lengo la Nyerere hasa kwenye Daily News (then, the standards) liwe huru kuandika. Hilo la free press enzi ya JKN is a whole another debate.
 
well written lakini ni yeye mtu mmoja tuu,Daily news at the end of the day ni la hao hao mafisadi na sitegemei mabadiliko yeyote,na hii ya Lusekelo kumsifia nyerere in relation to media is a big joke...nakubaliana na Nyerere vitu vingi lakini kwenye media alikuwa mkandamizaji tuu na kulikuwa hakuna uhuru wowote wakati wake kwa hiyo tuache unafiki hapo.

Koba,

Wapi Lusekelo anamsifia Nyerere kuhusu free press? Soma ile makala tena vizuri na utaelewa Lusekelo anasema nini. Maneno ya Nyerere kuhusu free press ndio anayasema, hilo halina maana yeye Nyerere alitekeleza au la na wala hasifii hicho.
 
...Yeboyebo Lusekelo najua ni makini sana na ninaikubali kazi yake & i dont mean to debate his crdibility,lakini kusema kama alivyosema Mwanakijiji wakati wa Nyerere press ilikuwa huru kuliko sasa huo ni uwongo mkubwa sana,kwanza mwanakijiji ujue uwezo wa kuanzisha media tuu ni one of the component ya hiyo free press,ilikuwepo? obvious haikuwepo...mpaka sasa wenzako jasho linawatoka ili kuondoa hizo sheria za Nyerere wewe unasema free press ilikuwepo sijui unaongelea wapi labda hiyo ya debate za huko mlimani ndio free press
 
...Yeboyebo Lusekelo najua ni makini sana na ninaikubali kazi yake & i dont mean to debate his crdibility,lakini kusema kama alivyosema Mwanakijiji wakati wa Nyerere press ilikuwa huru kuliko sasa huo ni uwongo mkubwa sana,kwanza mwanakijiji ujue uwezo wa kuanzisha media tuu ni one of the component ya hiyo free press,ilikuwepo? obvious haikuwepo...mpaka sasa wenzako jasho linawatoka ili kuondoa hizo sheria za Nyerere wewe unasema free press ilikuwepo sijui unaongelea wapi labda hiyo ya debate za huko mlimani ndio free press


Koba, next time read what I actually wrote. Kwa vile naona hukusoma nilichoandika nitajinukuu mimi mwenyewe hapa:

Kulikuwa na uhuru mkubwa wa habari na mawazo wakati wake kwa sababu alikuwa na uwezo wa kusimama na hoja;

Sikusema hata kidogo hilo neno la "kuliko sasa". Huwa nachagua maneno ninayotumia sibahatishi. Now, kuwa na ugumu wa kuanzisha vyombo vya habari siyo tatizo la uhuru wa habari. Je vilikuwepo vyombo binafsi vya habari wakati wa Mwalimu, the answer is Yes!, je vilikuwa huru kuripoti habari walivyoziona na kuzitolea maoni absolutely! Je zilifanya hivyo katika mazingira bora zaidi ya kisheria absolutely NOT.. Sheria za wakati wa mwalimu ndiyo zile zile tulizonazo leo hii; Sheria ya Magazeti ya 1976 na ya Usalama wa Taifa ya 1970 bado zipo na zina nguvu...

Uwepo wa wingi sasa wa vyombo vya habari na urahisi wa kupatikana habari is not the same as freedom of the press. Ukisoma maneno ya Lusekelo utaona kuwa ana mashaka kuwa sasa hivi vyombo vya habari haviko huru kiasi cha kusifiwa hivyo. Vinaingiliwa sana na watawala. Waulizeni kina jenerali na waandishi wa enzi za Mwalimu akiwemo Mkapa mwenyewe ni mara ngapi Rais aliingilia kazi zao na kama kuna wakati aliwakemea viongozi kuingilia vyombo vya habari.
 
Mwanakijiji,
wakati wa Nyerere kulikuwa hakuna mwandishi mwenye ujasiri wa kumuandika/kumchambua kama ulivyomchambua Lowassa. Huo siyo UHURU wa habari.

Pia kulikuwa hakuna demokrasia. Mwalimu aliwahi kulivunja Bunge. Hebu jiulize kwanini? Au kwanini kuwe na sheria kama hiyo?

Waraka wa Aboud Jumbe kuhoji muundo wa Muungano uliibiwa kwenye desk lake kabla hata hajausaini!! Mpaka leo hii Watanzania hawaelewi kinaga ubaga Aboud Jumbe aliandika nini.

Mazingira yaliyopelekea Aboud Jumbe, na Brig.Ramadhani Haji Faki, kufukuzwa kazi yaliripotiwa na vyombo vya habari kama "kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar."

...Uhuru wa kuandika na kupashana habari umeanza miaka ya karibuni baada ya Nyerere kuondoka madarakani.
 
Mwanakijiji,
wakati wa Nyerere kulikuwa hakuna mwandishi mwenye ujasiri wa kumuandika/kumchambua kama ulivyomchambua Lowassa. Huo siyo UHURU wa habari.

too bad kama hawakuwepo, au Mwalimu hakuwa anatoa kauli za Kilowassa alikuwa anapima maneno yake!

Pia kulikuwa hakuna demokrasia. Mwalimu aliwahi kulivunja Bunge. Hebu jiulize kwanini? Au kwanini kuwe na sheria kama hiyo?

Mwalimu alivunja Bunge lini, inabidi unrefresh my memory. Najua aliwahi kutishia kuvunja Bunge hadi wabunge walipokaa kujadili mswada wa sheria aliyoitaka.

Rais kuvunja Bunge ipo kwenye nchi nyingi za jumuiya ya madola, na sheria hiyo ipo hata leo hii Tanzania. Kama ingekuwa mbaya hivyo wabunge wetu wasingemuondolea Rais uwezo huo? Baadhi ya nchi nyingi tu zinao utaratibu wa Bunge kuvunjwa au kujivunja lenyewe. Hakukuwa na Demokrasia kulinganisha na sasa? I'll tell you what.... uchaguzi wa wabunge wakati wa chama kimoja ulikuwa more demokratic kuliko ilivyosasa! Just think. Je ilikuwa bora zaidi la hasha, lakini kulinganisha na jinsi wabunge wetu wanavyopatikana sasa.. acha utani.

Waraka wa Aboud Jumbe kuhoji muundo wa Muungano uliibiwa kwenye desk lake kabla hata hajausaini!! Mpaka leo hii Watanzania hawaelewi kinaga ubaga Aboud Jumbe aliandika nini.

Jumbe bado yuko hai, na yeyote anayetaka kufahamu ukweli anaweza kuwatafuta waliouhusika. Na hakuna nchi yeyote ambayo mtu anayetuhumiwa uhaini au makosa dhidi ya Jamhuri akaachiliwa. Hakuna. Hata leo hii kwenye Katiba yetu kosa kubwa linaloweza kutendwa dhidi ya Jamhuri ni Uhaini, na adhabu yake ni kifo. Sijui Jumbe alifanya nini (wapo wanaojua vizuri tu) na sijui Sharrif alifanya nini (wapo wanaojua). Chochote walichofanya hakikuwastahilisha kuendelea na uongozi!

Mazingira yaliyopelekea Aboud Jumbe, na Brig.Ramadhani Haji Faki, kufukuzwa kazi yaliripotiwa na vyombo vya habari kama "kuchafuka kwa hali ya hewa ya kisiasa Zanzibar."

kama hali ya kisiasa ilikuwa imechafuka, ulitaka waseme vipi. Ndiyo maana tunataka sheria ya haki ya kupata habari toka serikali ipitishwe ili tuweze kupita historia yetu. Ni kujidanganya kudhania kuwa kwa vile nchi ni ya kidemokrasia basi mambo fulani hayatokei au hayapaswi kutokea. Believe me hakuna nchi kama hiyo! Na Tanzania is no exception, na usishangae uchafu kama ule ukitokea tena iwe Zanzibar au Bara mtaambiwa hali imechafuka!

...Uhuru wa kuandika na kupashana habari umeanza miaka ya karibuni baada ya Nyerere kuondoka madarakani.

Hili si kweli, uhuru wa kuandika na kupashana habari umekuwepo muda wote, tatizo ni level of participation kutokana na vyombo vya habari vyenyewe kuwa vichache, utaalamu, n.k Hivi tulipopata uhuru tulikuwa na vyuo vya habari vingapi, tulikuwa na wataalamu waliosema menejimenti wangapi, tulikuwa na vyombo vingapi vya kusimami fani mbalimbali n.k ! Inakuwa ni kichekesho mtu atokee leo na kusema mbona wakati wa mwalimu hatukuwa na Cable TV, Cell phones na internet! Kuna mambo yaliyowezekana na kuna mambo ambayo hayakuwezekana. Lakini hakuna mahali hata pamoja ambapo unaweza kunionesha kuwa ilikuwa ni sera ya mwalimu au CCM kudumaza vyombo vya habari, nakuthubutisha unionesha aidha iwe kauli, au vitendo vyovyote vya Mwalimu kuwa hakutaka watu wampinge au alipigia simu waandishi (yeye mwenyewe au wasaidizi wake) na kuwakataza waandishi wasiandike jambo fulani.
 
Koba, next time read what I actually wrote. Kwa vile naona hukusoma nilichoandika nitajinukuu mimi mwenyewe hapa:



Sikusema hata kidogo hilo neno la "kuliko sasa". Huwa nachagua maneno ninayotumia sibahatishi. Now, kuwa na ugumu wa kuanzisha vyombo vya habari siyo tatizo la uhuru wa habari. Je vilikuwepo vyombo binafsi vya habari wakati wa Mwalimu, the answer is Yes!, je vilikuwa huru kuripoti habari walivyoziona na kuzitolea maoni absolutely! Je zilifanya hivyo katika mazingira bora zaidi ya kisheria absolutely NOT.. Sheria za wakati wa mwalimu ndiyo zile zile tulizonazo leo hii; Sheria ya Magazeti ya 1976 na ya Usalama wa Taifa ya 1970 bado zipo na zina nguvu...

Uwepo wa wingi sasa wa vyombo vya habari na urahisi wa kupatikana habari is not the same as freedom of the press. Ukisoma maneno ya Lusekelo utaona kuwa ana mashaka kuwa sasa hivi vyombo vya habari haviko huru kiasi cha kusifiwa hivyo. Vinaingiliwa sana na watawala. Waulizeni kina jenerali na waandishi wa enzi za Mwalimu akiwemo Mkapa mwenyewe ni mara ngapi Rais aliingilia kazi zao na kama kuna wakati aliwakemea viongozi kuingilia vyombo vya habari.

Haya tumeshawahi kuyazungumzia huko nyuma na sina uhakika kama wewe mwenyewe una uhakika na unachokisema!! Bado unadai tulikuwa na vyombo binafsi vya habari...hebu nitajie majina ya hivyo vyombo na wapi vilikuwa vikifanyia kazi na idadi ya watu vilivyokuwa vinawafikia. Na una uhakika gani, kama vilikuwepo, kuwa vilikuwa huru kuripoti na kutolea maoni kwa mtazamo wao habari walizokuwa wakiripoti.
 
Mwanakijiji,
Pia kulikuwa hakuna demokrasia. Mwalimu aliwahi kulivunja Bunge. Hebu jiulize kwanini? Au kwanini kuwe na sheria kama hiyo?

.


Sidhani kama hii ni sahihi, Nyerere alivunja bunge? No, labda alitishia kuvunja bunge. Lakini hata kama angelivunja bunge basi hilo lilikuwa chini ya uwezo wake kikatiba kwahiyo ilikuwa ni demokrasia na sio vinginevyo.

Si unajua nchi kama UK mara nyingi tu, waziri mkuu anavunja bunge kabla ya muda wake? Je hiyo tuiite ni ukosefu wa demokrasia?
 
Kuvunja bunge sio kosa kama sera zako wabunge hawazikubali ni lazima kulivunja ili uchaguzi ufanyike upya na wananchi wachague kile ambacho wanakihitaji. Tabia ya kung'ang'ania madaraka hata pale ambapo huna support ya wabunge na wananchi ni ya ki-dictactor.

Hivi waandishi wa habari wa mashirika kama Deusche welle, Reuters, BBC na mengineyo yalikuja Tanzania lini? Hawa hawakuwa huru?
 
Haya tumeshawahi kuyazungumzia huko nyuma na sina uhakika kama wewe mwenyewe una uhakika na unachokisema!! Bado unadai tulikuwa na vyombo binafsi vya habari...hebu nitajie majina ya hivyo vyombo na wapi vilikuwa vikifanyia kazi na idadi ya watu vilivyokuwa vinawafikia. Na una uhakika gani, kama vilikuwepo, kuwa vilikuwa huru kuripoti na kutolea maoni kwa mtazamo wao habari walizokuwa wakiripoti.


Nyani, hilo mbona tulishalisettle... vyombo vya habari vilikuwepo na vilikuwa huru. Ukija kwenye suala la kufikia watu na urahisi wa utengenezaji wake hilo ni suala jingine kabisa! Kwani hata vilivyopo sasa ni vingapi vinaifikia angalau asilimia 30 ya Watanzania? ukiondoa radio na TV vyombo vya maandishi bado havijafika kwa watu wengi miaka ishirini na mbili baada ya Mwalimu kung'atuka! Sasa kweli tutaendelea kumlaumu Mwalimu kuwa magazeti na vitabu haviwafikii watu wengi zaidi.
 
Lakini hakuna mahali hata pamoja ambapo unaweza kunionesha kuwa ilikuwa ni sera ya mwalimu au CCM kudumaza vyombo vya habari, nakuthubutisha unionesha aidha iwe kauli, au vitendo vyovyote vya Mwalimu kuwa hakutaka watu wampinge au alipigia simu waandishi (yeye mwenyewe au wasaidizi wake) na kuwakataza waandishi wasiandike jambo fulani.

Mzee Mwanakijiji wewe una mapenzi binafsi na Mwalimu, hapo sikulaumu kabisa baba yetu wa Taifa ameifanyia Tanzania mambo mengi mazuri tu, wengi tulisoma bure, na wazazi wetu wamesoma bure, amani tunayo lugha moja n.k.

Kauli yako hapo juu ina-imply kuwa iliwezekana kumpinga Mwalimu, na kuwa uhuru wa vyombo vya habri ulikuwepo. Kwa mawazo yangu binafsi kumpinga nyerere haikuwepo kwenye agenda kabisa enzi zake hata kama hatuwezi kuthibitisha hayo kwa maandishi, uhuru wa kusema unachotaka haikuwepo kwenye agenda, achilia mbali magazeti hata kwenye vijiwe na washkaji watu walikuwa wanaogopa kusema vitu vya kupinga maana maofisa wa usalama wa taifa walikuwa wamepenyezwa kwenye kona zote za jamii na ole wako ujifanye unapenda uhuru ungekoma.

Mzee mwanakijiji hapo unamtetea mwalimu kwa mapenzi tu, hoja hapo hamna, aliyempinga mwalimu alikiona cha moto!

Achilia mbali uhuru wa kusema, enzi za Nyerere hata uhuru wa kumiliki chako haukuwepo, akiamua chako si chako basi hakitakuwa chako, anakuja kukuny'ang'anya mara moja, Azimio la Arusha pale aliwanyang'anya watu mali zao bila kujali haki zao za kumiliki kilicho chao, katika miaka ya 80 waziri wake mkuu aliwapelekesha watu kishenzi yeye akiwa raisi akiangalia tu, sijui majamaa ambao walikuwa wananunua mahindi na maharage na ku-supply shule za sekondari wengine wali-supply nyama n.k faida waliyopata katika mauzo hayo walinyang'anywa zote! polisi walikuwa wanakuja na kuwanyanyasa kishenzi kwa amri kutoka juu wakati watu wale walikuwa ni wafanyabiashara tu wanaojituma, ndio maana mpaka leo watanzania wakiona mtu mfanyabiashara anatengeneza pesa wanasema mbaya, wakiona mfanyabiashara anagombea cheo wanaona haifai, sharti uwe mkulima wa kahawa inayouzwa senti moja kwa gunia uwe fukara basi wewe safi.

Nyerere had his weaknesses vile vile hakuwa muumba, hilo lazima tutambue na kulikubali.
 
Nyani, hilo mbona tulishalisettle... vyombo vya habari vilikuwepo na vilikuwa huru. Ukija kwenye suala la kufikia watu na urahisi wa utengenezaji wake hilo ni suala jingine kabisa! Kwani hata vilivyopo sasa ni vingapi vinaifikia angalau asilimia 30 ya Watanzania? ukiondoa radio na TV vyombo vya maandishi bado havijafika kwa watu wengi miaka ishirini na mbili baada ya Mwalimu kung'atuka! Sasa kweli tutaendelea kumlaumu Mwalimu kuwa magazeti na vitabu haviwafikii watu wengi zaidi.

Ok, offhand maybe you can't name them but my point is if they were there, how free and balanced were they? Kwa mfano, kama enzi za utawala wa Reagan kungekuwepo na Fox News, Drudge Report, Michael Savage, Laura Ingraham, Ann Coulter, mshikaji wako Sean Hannity na wengine wengi wanaofanana kifikra, kuna mtu ambaye angesema kulikuwa na uhuru wa habari na maoni kweli? Kama hivyo vyombo vilivyokuwepo Tanzania na vyenyewe vilikuwa vinaimba nyimbo za zidumu fikra "sahihi" or else, then kwangu mimi ni sawa na hatukuwanayo hiyo freedom of press na expression...Nakupa muda hadi kesho uyatafute hayo majina ya hivyo vyombo vilivyokuwepo (sijui ni magazeti, redio, au nini)halafu utuwekee hapa...au wewe unasemaje?
 
Back
Top Bottom