Lowassa kuweka kambi Arumeru Mashariki kupangua mikakati yote ya CHADEMA

lowassa-top-safi.jpg
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa​

ADAIWA KUPIGWA 'STOP' ASISHIRIKI,ASEMA NI UZUSHI WA KIPUUZI, CHADEMA WALIA
Waandishi Wetu, Arumeru na Dar
USHIRIKI wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge Arumeru Mashariki unadaiwa kuigawa timu ya kampeni ya CCM inayomnadi mgombea wa chama hicho, Sioi Sumari.Lowassa ambaye yuko mkoani Arusha tangu Machi 20, mwaka huu, amekuwa akitajwa kwamba atamnadi Sioi lakini tofauti na makada wengine, hadi sasa hakuna ratiba yoyote ndani ya CCM inayoonyesha ni lini mbunge huyo wa Monduli atapanda jukwaani.

Habari zilizopatikana jana kutoka Arumeru na Dar es Salaam zinasema baadhi ya viongozi wa CCM na timu inayoongoza kampeni za uchaguzi huo wamegawanyika kuhusu Lowassa kupanda jukwaani, huku wengine wakipinga.

Kumekuwepo na kundi ambalo linaona kwamba Lowassa akiingia kwenye kampeni hizo anaweza kuzua mazingira ambayo yataipa ugumu CCM kushinda kutokana na kumbukumbu kuwa alijiuzulu kutokana na kashfa ya utoaji wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni tata ya Richmond Development LCC.

Chadema tayari kimetangaza kuwa endapo Lowassa atajitokeza kwenye kampeni hizo kumnadi mgombea wa CCM, watamuumbua kwa kile wanachodai wataweka hadharani tuhuma kinazodai zinamhusu.

Jana, mmoja wa viongozi wa chama hicho alisema: "Hatapanda jukwaani (Lowassa), wala hatothubutu kufanya hivyo kwani tayari ameambiwa aache na huyo aliyemwambia nadhani anamsikiliza, hawezi kukiuka."

Kauli ya kiongozi huyo inafanana na ile iliyotolewa na mmoja wa makada wakongwe wa CCM anayeshiriki kampeni za Arumeru Mashariki ambaye Machi 20 mwaka huu akiwa Usa River alsikika akisema: "Lowassa hana umuhimu wowote" kwenye kampeni hizo.

Kiongozi huyo alikuwa akichangia mjadala usio rasmi uliokuwa ukiwahusisha makada kadhaa wakongwe wa CCM, walipokuwa wakisubiri kuanza kwa msafara wa kwenda kwenye moja ya mikutano ya kampeni.
 
lowassa-top-safi.jpg
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa​

ADAIWA KUPIGWA 'STOP' ASISHIRIKI,ASEMA NI UZUSHI WA KIPUUZI, CHADEMA WALIA
Waandishi Wetu, Arumeru na Dar
USHIRIKI wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge Arumeru Mashariki unadaiwa kuigawa timu ya kampeni ya CCM inayomnadi mgombea wa chama hicho, Sioi Sumari.Lowassa ambaye yuko mkoani Arusha tangu Machi 20, mwaka huu, amekuwa akitajwa kwamba atamnadi Sioi lakini tofauti na makada wengine, hadi sasa hakuna ratiba yoyote ndani ya CCM inayoonyesha ni lini mbunge huyo wa Monduli atapanda jukwaani.

Habari zilizopatikana jana kutoka Arumeru na Dar es Salaam zinasema baadhi ya viongozi wa CCM na timu inayoongoza kampeni za uchaguzi huo wamegawanyika kuhusu Lowassa kupanda jukwaani, huku wengine wakipinga.

Kumekuwepo na kundi ambalo linaona kwamba Lowassa akiingia kwenye kampeni hizo anaweza kuzua mazingira ambayo yataipa ugumu CCM kushinda kutokana na kumbukumbu kuwa alijiuzulu kutokana na kashfa ya utoaji wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni tata ya Richmond Development LCC.

Chadema tayari kimetangaza kuwa endapo Lowassa atajitokeza kwenye kampeni hizo kumnadi mgombea wa CCM, watamuumbua kwa kile wanachodai wataweka hadharani tuhuma kinazodai zinamhusu.

Jana, mmoja wa viongozi wa chama hicho alisema: "Hatapanda jukwaani (Lowassa), wala hatothubutu kufanya hivyo kwani tayari ameambiwa aache na huyo aliyemwambia nadhani anamsikiliza, hawezi kukiuka."

Kauli ya kiongozi huyo inafanana na ile iliyotolewa na mmoja wa makada wakongwe wa CCM anayeshiriki kampeni za Arumeru Mashariki ambaye Machi 20 mwaka huu akiwa Usa River alsikika akisema: "Lowassa hana umuhimu wowote" kwenye kampeni hizo.

Kiongozi huyo alikuwa akichangia mjadala usio rasmi uliokuwa ukiwahusisha makada kadhaa wakongwe wa CCM, walipokuwa wakisubiri kuanza kwa msafara wa kwenda kwenye moja ya mikutano ya kampeni.
mikakati gani jamani!!! the disgraced leader has been struggling day and night trying to buy his reputation back.
 
Ritz, Mimi si mwanasiasa, na sipendi kuzungumza kitu ambacho sina uhakika nacho. Ila kutokana na koments/post zako, zimenifanya nichukue hatua za ziada kwenda kwenye baadhi ya maeneo unayo taja ua kuhusisha na post zako.

Jana ilinibidi nikatembele vijiji vitatu (3) navitaja kwa majina japo nafahamu wazi kuwa huvifahamu ua hujawahi kufika: 1: Kijiji cha Malula 2: Kijiji cha Mareu, na 3: Kijiji cha Sakila. Katika vijijji hivi nilionana na baadhi ya viongozi/Makada wa CCM, walichosema ni kwamba CCM ipo kwenye wakati mgumu sana. Wametaja baadhi ya maeneo ambako wamesha kata tamaa ni Ngabobo - Kule ambako sendeka alisema WAMAASAI MSIKUBALI KUCHAGULIWA MTU WA KUWAONGOZA. Katika eneo hili vijana wa kimasai walimvisha NASARI Rubega na kumkabidhi fimbo/Rungu ili awe kiongozi wao. Eneo lingine ni mbuguni Ambako ndiko Lowasa aliko zaliwa, kule nako kimeumana/hapafai.

CDM wanatamani sana EL ajitokeze jukwaani ili wamalize kwani wamemwaka kiporo, ila EL amekuwa mjaja, na
anafanya kampeni za ndani, ila CDM itamfuata huko huko.

Leo naenda tena Malula kwenye kampeni za CDM, na nitazidi kukujuza yanayo jiri huko.

USHAURI WANGU KWAKO: FANYA UTAFITI KABLA HUJAUPOST CHOCHOTE:

Ulimbo,
Arumeru ni pakawaida unaposema kuwa unajua sijawahi kufika nakushangaa sana utadhani Arumeru unakwenda na Viza.

Hata mie nimefanya utafiti wangu kwenye vijiji vinne.
1. Kijiji cha Maroroni.
2. Kijiji cha Majichai.
3. Kijiji cha Singiss
4. Kijiji cha Haker.
Nadhani hivi unavijua hivi vijiji.
 
lowassa-top-safi.jpg
Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa​

ADAIWA KUPIGWA 'STOP' ASISHIRIKI,ASEMA NI UZUSHI WA KIPUUZI, CHADEMA WALIA
Waandishi Wetu, Arumeru na Dar
USHIRIKI wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa kwenye kampeni za uchaguzi mdogo wa Ubunge Arumeru Mashariki unadaiwa kuigawa timu ya kampeni ya CCM inayomnadi mgombea wa chama hicho, Sioi Sumari.Lowassa ambaye yuko mkoani Arusha tangu Machi 20, mwaka huu, amekuwa akitajwa kwamba atamnadi Sioi lakini tofauti na makada wengine, hadi sasa hakuna ratiba yoyote ndani ya CCM inayoonyesha ni lini mbunge huyo wa Monduli atapanda jukwaani.

Habari zilizopatikana jana kutoka Arumeru na Dar es Salaam zinasema baadhi ya viongozi wa CCM na timu inayoongoza kampeni za uchaguzi huo wamegawanyika kuhusu Lowassa kupanda jukwaani, huku wengine wakipinga.

Kumekuwepo na kundi ambalo linaona kwamba Lowassa akiingia kwenye kampeni hizo anaweza kuzua mazingira ambayo yataipa ugumu CCM kushinda kutokana na kumbukumbu kuwa alijiuzulu kutokana na kashfa ya utoaji wa zabuni ya kuzalisha umeme wa dharura iliyotolewa kwa kampuni tata ya Richmond Development LCC.

Chadema tayari kimetangaza kuwa endapo Lowassa atajitokeza kwenye kampeni hizo kumnadi mgombea wa CCM, watamuumbua kwa kile wanachodai wataweka hadharani tuhuma kinazodai zinamhusu.

Jana, mmoja wa viongozi wa chama hicho alisema: Hatapanda jukwaani (Lowassa), wala hatothubutu kufanya hivyo kwani tayari ameambiwa aache na huyo aliyemwambia nadhani anamsikiliza, hawezi kukiuka.

Kauli ya kiongozi huyo inafanana na ile iliyotolewa na mmoja wa makada wakongwe wa CCM anayeshiriki kampeni za Arumeru Mashariki ambaye Machi 20 mwaka huu akiwa Usa River alsikika akisema: "Lowassa hana umuhimu wowote kwenye kampeni hizo.

Kiongozi huyo alikuwa akichangia mjadala usio rasmi uliokuwa ukiwahusisha makada kadhaa wakongwe wa CCM, walipokuwa wakisubiri kuanza kwa msafara wa kwenda kwenye moja ya mikutano ya kampeni.

Mungi,
Mbona sijawaona hao waliompiga stop Lowassa. Kufika Arumeru kwenye hii habari yako?
 
Memo,
Hivi kweli uwa unaamini Nape, anaweza kumzuia kitu Lowassa ndani ya CCM? Uwa nawashangaa sana kumpa nafasi Nape.

Nape pale alipo kawekwa na Jk, na JK na Lowassa hawakukutana barabarani Nape kama angekuwa na nguvu ndani ya CCM asingekosa nafasi ya kugombea ubunge jimbo la Ubungo.

sasa wewe ritz uko upande gani? Yaani unamkataa hata kiongozi wako wa juu wa chama (Nape) wewe kumbe ni chadema ila hutaki kujionyesha kwasababu kupiga kura ni siri ya mtu
 
hivi wakuwazuia BOYS TO MEN wasifanye jambo wakwapi?...hawa ndo wenye nchi bwana,hakuna wakuongea kitu..hata kama una chukia jambo,ila useme ukweli,hapo utakua rafiki wa mungu.tusubiri vijana wadogo wenye uchungu na nchi waje baadae kushika nchi...ila kwa sasa hawa RO-KI-LO ndo wanatengeneza siasa....
 
Ritz, Mimi si mwanasiasa, na sipendi kuzungumza kitu ambacho sina uhakika nacho. Ila kutokana na koments/post zako, zimenifanya nichukue hatua za ziada kwenda kwenye baadhi ya maeneo unayo taja ua kuhusisha na post zako.

Jana ilinibidi nikatembele vijiji vitatu (3) navitaja kwa majina japo nafahamu wazi kuwa huvifahamu ua hujawahi kufika: 1: Kijiji cha Malula 2: Kijiji cha Mareu, na 3: Kijiji cha Sakila. Katika vijijji hivi nilionana na baadhi ya viongozi/Makada wa CCM, walichosema ni kwamba CCM ipo kwenye wakati mgumu sana. Wametaja baadhi ya maeneo ambako wamesha kata tamaa ni Ngabobo - Kule ambako sendeka alisema WAMAASAI MSIKUBALI KUCHAGULIWA MTU WA KUWAONGOZA. Katika eneo hili vijana wa kimasai walimvisha NASARI Rubega na kumkabidhi fimbo/Rungu ili awe kiongozi wao. Eneo lingine ni mbuguni Ambako ndiko Lowasa aliko zaliwa, kule nako kimeumana/hapafai.

CDM wanatamani sana EL ajitokeze jukwaani ili wamalize kwani wamemwaka kiporo, ila EL amekuwa mjaja, na
anafanya kampeni za ndani, ila CDM itamfuata huko huko.

Leo naenda tena Malula kwenye kampeni za CDM, na nitazidi kukujuza yanayo jiri huko.

USHAURI WANGU KWAKO: FANYA UTAFITI KABLA HUJAUPOST CHOCHOTE:
kaka anachosema huyu ritz ni upotoshaji mtupu! Hakuna lolote, anakurupuka ili awakatishe watu tamaa.. Ushauri kwamba afanye utafiti ni mzuri, nami namshauri asiache kuufanyia kazi ushauri wako.
 
Mungi,
Mbona sijawaona hao waliompiga stop Lowassa. Kufika Arumeru kwenye hii habari yako?

Wakafanye nini Arumeru Mkuu wakati wamewatuma Makamanda wao wakiongozwa na Mzinzi na Sokwe?
hakuna sababu ya kwenda wanajua hawajazidiwa kivile!
 
Watu wote wanaoenda kwenye kampeni za magamba ni kwaajili ya kwenda kuliona sokwe linalozungumza kwani maajabu ya dunia kwa mnyama kusema
 
moja ya sera za ccm nilizo bahatika kusikia katika moja ya mikunano yao
Nanukuu maneno ya Mwigulu
Tochi haiwezi kutumia Bettry zaidi aina moja,Arumeru Mash Mna madiwani wote CCM,Rais ni CCM,mkichagua CDM mtakuwa mnachanganya maberry tochi haita waka...
 
hivi wakuwazuia BOYS TO MEN wasifanye jambo wakwapi?...hawa ndo wenye nchi bwana,hakuna wakuongea kitu..hata kama una chukia jambo,ila useme ukweli,hapo utakua rafiki wa mungu.tusubiri vijana wadogo wenye uchungu na nchi waje baadae kushika nchi...ila kwa sasa hawa RO-KI-LO ndo wanatengeneza siasa....

Mie na Rais Jakaya Kikwete atajukutana barabarani na mie takuwa mtu wa mwisho kumsaliti..."Lowassa"
 
E.Lowasa kama ana nia ya kugombea uraisi 2015 asiende arumeru kwa sasa coz atajiharibia!! anachotakiwa kufanya sasa kwa watanzania ni kujisafisha kwanza na kueleza ukweli kuhusu kashfa zinazomhusu kabla ya kuanza kupanda majukwaani!!! otherwise akienda arumeru atumie hilo jukwaa kutueleza ukweli.
 
Wanabodi.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na marafiki wa Lowassa, zinasema mbunge huyu wa Monduli amejipanga kuweka kambi Arumeru Mashariki katika wiki ya mwisho ya lala salama ya kampeni.

Hilo litakuwa kombora la mwisho la kuimaliza Chadema huko Arumeru Mashariki.

Kwenda kwa Lowassa, Arumeru ni wazi njia itakuwa ni nyeupe kwa mgombea wa CCM, Sioi kutokana na umahiri wa mwanasiasa huyo, si tu katika kuratibu kampeni, bali hata kukubalika na kuheshimiwa na wananchi wa jimbo hilo jamii ya Kimasai na Wameru.

Inasemekana Lowassa ndio alikuwa akiratibu kampeni za kila siku mgombea wa CCM.

Kwa mujibu wa makada wa Chadema waliopo Arumeru wanasema hata kabla ya ujio huo wa Lowassa, Chadema kimekuwa kikikumbana na upinzani mkali kinapojaribu kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba kutokana na wananchi jamii ya Wamasai na Wameru kuwagomea si tu kuingia ndani ya nyumba zao kwa ajili ya kampeni, bali hata kuwasogelea.

Lowassa akifika Arumeru Mashariki si ndio itakuwa balaa kwa Chadema.

Uuh walaM kaza uzi tuwatose hawa CCM wachovu wa maendeleo na siasa za kiTZ
 
Kwenye gazeti la Mwananchi la leo March 24, Lowassa, kasema hakuna haja ya kuwa na haraka, kwani vyovyote itakavyokuwa mtajua tu.
Nasikia ataongozana na mama Gaudensia Kabaka na wataratibu kwa pamoja mkakati wa ajira ka vijana wa Arumeru kabla hawajapiga kura!
 
Wanabodi.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na marafiki wa Lowassa, zinasema mbunge huyu wa Monduli amejipanga kuweka kambi Arumeru Mashariki katika wiki ya mwisho ya lala salama ya kampeni.

Hilo litakuwa kombora la mwisho la kuimaliza Chadema huko Arumeru Mashariki.

Kwenda kwa Lowassa, Arumeru ni wazi njia itakuwa ni nyeupe kwa mgombea wa CCM, Sioi kutokana na umahiri wa mwanasiasa huyo, si tu katika kuratibu kampeni, bali hata kukubalika na kuheshimiwa na wananchi wa jimbo hilo jamii ya Kimasai na Wameru.

Inasemekana Lowassa ndio alikuwa akiratibu kampeni za kila siku mgombea wa CCM.

Kwa mujibu wa makada wa Chadema waliopo Arumeru wanasema hata kabla ya ujio huo wa Lowassa, Chadema kimekuwa kikikumbana na upinzani mkali kinapojaribu kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba kutokana na wananchi jamii ya Wamasai na Wameru kuwagomea si tu kuingia ndani ya nyumba zao kwa ajili ya kampeni, bali hata kuwasogelea.

Lowassa akifika Arumeru Mashariki si ndio itakuwa balaa kwa Chadema.

WE UNASEMAJE LOWASA ANAHESHIMIKA MERU, NYIE MAGAMBA UKIOGOPA MTU ANAIBA ANAWATISHIA HAMCHUKULIII HATUA MNADHANI NA CDM NI SAWA ................ We mshauri apande jukwaani cdm wamfanye case study
 
Umahiri wa Lowasa jukwaani umeonekana ktk jukwaa lipi na lini??
Atamfanikishia ushindi sioi kama alivyomfanikishia Batilda????
Lowasa ni SI unit ya ufisadi TZ.
 
HABARI ZA KUAMINIKA TOKA ARUMERU.

EDUARD NGOYAYE LOWASSA AJITOSA
RASMI KWENYE KAMPENI ZA SIOI.

Mbunge wa Monduli na Mjumbe wa NEC CCM Amejitosa rasmi kwenye kampeni za ubbunge Arumeru Mashariki.

Habari za kuaminika zinasema leo ni siku ya Tatu tangu mzee Lowassa ajitose kwenye kampeni hizo za 'mkwewe'.

Tangu juzi alianza kukutana na Wazee wa Mila (Washili) Na jana kakutana na Wachungaji wa
Kipentecoste zaidi ya 120.

Na jana pia akakutana na Maaskofu na
wachungaji wa KKKT.

Na huenda Leo akakutana na Malaigwanan na makundi mengine yote Muhimu.

Ila haijasibitishwa na vyazo vyetu kama ataanza kupanda rasmi jukwaani kwenye wiki ya lala Salama..

Na pia kumeanza mkakati wa kampeni ya
Nyumba kwa nyumba,
Chumba kwa chumba,
Kitanda kwa kitanda,
Na mpaka shuka kwa
shuka.

Habari zaidi mtaendelea kupashwa hapa hapa..

'TANURI LA FIKRA'
'Think twice'
 
Back
Top Bottom