Lowassa kuweka kambi Arumeru Mashariki kupangua mikakati yote ya CHADEMA

Sote tunajua Lowassa ni mwizi, this time tunajua ameweka kambi Arumeru ku-enginear wizi wa kula, ila this time haitakuwa easy hivyo.Lowassa na kambi yake wajue kwamba tunawafuatilia nyedo zao.
 
Kwenye gazeti la Mwananchi la leo March 24, Lowassa, kasema hakuna haja ya kuwa na haraka, kwani vyovyote itakavyokuwa mtajua tu.
 
kajiunga 15 March 2012...................kazi ipo

Katika hali ya kawada naomba nitume rai yangu kwa viongozi wetu wa chadema kuacha mara moja mazungumzo ya siri waliyonayo na lowasa,kwani watanzania hawatakielewa chama chao wanachokipenda (cdm),lowasa amewaomba viongozi wa chadema wakubali kumsafisha katika kashifa mbalimbali za ufisadi na rushwa zinazomkabili.

Suala la ufisadi sasa viongozi wetu wa cdm mmeanza kuliona la kawaida na kushindwa kulielezea kwa kina namna linavyolimaliza taifa letu,kwani bado mirija wa mafisadi ipo wazi wazi lakini humliongelei arumeru au mnasubili mazungumzo yenu na lowasa yakwame ndio tena muwe na nguvu za kuchukizwa na ufisadi.

Kumbukeni lowasa akiingia madarakani ataua upizani kwani si mtu anayependa kupewa changamoto na washindani wake wa kisiasa,lakini pia watanzania wana nia ya kuwa na viongozi safi na serikali safi,tafadhali sana tunataka kuona serikali ya cdm madarakani na si serikali ya mseto anayoiahidi lowasa,kama yeye ana nia ya dhati basi aende akagombee ubunge monduli halafu asubilie kuja kuisaidia cdm na si cdm imsaidie kuingia madarakani kwa nkisingizio cha serikali ya mseto.je akiwasaliti mtawaeleza nini watanzania kama si chama kutoaminiwa wa wananchi walio na imani na cdm.
 
Lowassa hakina kitu ni sawa na shoka bila mpini. Ila akionekana MSOMALI Adbullahaman Kinana Arumeru, basi CDM wamekwisha, maana Kinana ni sawa na Shoka na mpini wake. Kinana kama njia zote za wizi wa kura zikishindikina yupo radhi kukimbia na masanduku ya kura mchana kweupe. (Refer kesi ya ubunge Segerea Mpendazoe v Mahanga).

CDM kuweni macho na Kinana huyo msomali ana guts za ajabu na hana aibu, hata Lowassa anamtegemea yeye kufanya ujambazi.
 
Mkuu Ritz,

Acha kudanganya, huyo changudoa wa siasa ameshapigwa marufuku kukanyaga uwanja wa kampeni Arumeru
 
Lowasa yupi?
Yule gamba tulieambiwa na Nape?
Au yupi huyo!!
 
Aje tu at lease nasisi tuweze kula hata punje za jasho letu maana pesa zenyewe ametuibia sisi. Lakini Kura asahau! Kula CCM, Kura Chadema!
 
Mkuu Ritz,

Acha kudanganya, huyo changudoa wa siasa ameshapigwa marufuku kukanyaga uwanja wa kampeni Arumeru

Mkuu Mungi,
Nani mwenye uwezo wa kumpiga marufuku Lowassa kufika Arumeru.

Hivi unajua kuwa Lowassa, ndio anaratibu kampeni za kila siku za Sioi, tangu zizinduliwe rasmi na Mkapa.
 
Kila la kheri kama atakwenda Arumeru, kwa sababu natamani kumsikia atasema nini kuhusu ule wimbo wake wa ajira kwa vijana na anatuahidi nini vijana wa Arumeru kuhusu ajira kupitia kwa mkwewe
 
mbona kaanza zamani, mwenyekiti wa tume si ni shemeji yake! mgombea mkwewe,
 
Mkuu Mungi,
Nani mwenye uwezo wa kumpiga marufuku Lowassa kufika Arumeru.

Hivi unajua kuwa Lowassa, ndio anaratibu kampeni za kila siku za Sioi, tangu zizinduliwe rasmi na Mkapa.

Nape amempiga marufuku Lowassa kusimama jukwaani Mkuu
 
Wanabodi.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na marafiki wa Lowassa, zinasema mbunge huyu wa Monduli amejipanga kuweka kambi Arumeru Mashariki katika wiki ya mwisho ya lala salama ya kampeni.

Hilo litakuwa kombora la mwisho la kuimaliza Chadema huko Arumeru Mashariki.

Kwenda kwa Lowassa, Arumeru ni wazi njia itakuwa ni nyeupe kwa mgombea wa CCM, Sioi kutokana na umahiri wa mwanasiasa huyo, si tu katika kuratibu kampeni, bali hata kukubalika na kuheshimiwa na wananchi wa jimbo hilo jamii ya Kimasai na Wameru.

Inasemekana Lowassa ndio alikuwa akiratibu kampeni za kila siku mgombea wa CCM.

Kwa mujibu wa makada wa Chadema waliopo Arumeru wanasema hata kabla ya ujio huo wa Lowassa, Chadema kimekuwa kikikumbana na upinzani mkali kinapojaribu kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba kutokana na wananchi jamii ya Wamasai na Wameru kuwagomea si tu kuingia ndani ya nyumba zao kwa ajili ya kampeni, bali hata kuwasogelea.

Lowassa akifika Arumeru Mashariki si ndio itakuwa balaa kwa Chadema.


Ritz, Mimi si mwanasiasa, na sipendi kuzungumza kitu ambacho sina uhakika nacho. Ila kutokana na koments/post zako, zimenifanya nichukue hatua za ziada kwenda kwenye baadhi ya maeneo unayo taja ua kuhusisha na post zako.

Jana ilinibidi nikatembele vijiji vitatu (3) navitaja kwa majina japo nafahamu wazi kuwa huvifahamu ua hujawahi kufika: 1: Kijiji cha Malula 2: Kijiji cha Mareu, na 3: Kijiji cha Sakila. Katika vijijji hivi nilionana na baadhi ya viongozi/Makada wa CCM, walichosema ni kwamba CCM ipo kwenye wakati mgumu sana. Wametaja baadhi ya maeneo ambako wamesha kata tamaa ni Ngabobo - Kule ambako sendeka alisema WAMAASAI MSIKUBALI KUCHAGULIWA MTU WA KUWAONGOZA. Katika eneo hili vijana wa kimasai walimvisha NASARI Rubega na kumkabidhi fimbo/Rungu ili awe kiongozi wao. Eneo lingine ni mbuguni Ambako ndiko Lowasa aliko zaliwa, kule nako kimeumana/hapafai.

CDM wanatamani sana EL ajitokeze jukwaani ili wamalize kwani wamemwaka kiporo, ila EL amekuwa mjaja, na
anafanya kampeni za ndani, ila CDM itamfuata huko huko.

Leo naenda tena Malula kwenye kampeni za CDM, na nitazidi kukujuza yanayo jiri huko.

USHAURI WANGU KWAKO: FANYA UTAFITI KABLA HUJAUPOST CHOCHOTE:
 
Lowasa yupi?
Yule gamba tulieambiwa na Nape?
Au yupi huyo!!

Memo,
Hivi kweli uwa unaamini Nape, anaweza kumzuia kitu Lowassa ndani ya CCM? Uwa nawashangaa sana kumpa nafasi Nape.

Nape pale alipo kawekwa na Jk, na JK na Lowassa hawakukutana barabarani Nape kama angekuwa na nguvu ndani ya CCM asingekosa nafasi ya kugombea ubunge jimbo la Ubungo.
 
Wanabodi.
Habari za uhakika ambazo zimethibitishwa na marafiki wa Lowassa, zinasema mbunge huyu wa Monduli amejipanga kuweka kambi Arumeru Mashariki katika wiki ya mwisho ya lala salama ya kampeni.

Hilo litakuwa kombora la mwisho la kuimaliza Chadema huko Arumeru Mashariki.

Kwenda kwa Lowassa, Arumeru ni wazi njia itakuwa ni nyeupe kwa mgombea wa CCM, Sioi kutokana na umahiri wa mwanasiasa huyo, si tu katika kuratibu kampeni, bali hata kukubalika na kuheshimiwa na wananchi wa jimbo hilo jamii ya Kimasai na Wameru.

Inasemekana Lowassa ndio alikuwa akiratibu kampeni za kila siku mgombea wa CCM.

Kwa mujibu wa makada wa Chadema waliopo Arumeru wanasema hata kabla ya ujio huo wa Lowassa, Chadema kimekuwa kikikumbana na upinzani mkali kinapojaribu kufanya kampeni za nyumba kwa nyumba kutokana na wananchi jamii ya Wamasai na Wameru kuwagomea si tu kuingia ndani ya nyumba zao kwa ajili ya kampeni, bali hata kuwasogelea.

Lowassa akifika Arumeru Mashariki si ndio itakuwa balaa kwa Chadema.
unamaanisha Lowassa baba mkwe ?? hapo mbona watakuwa wametimiliza usemi wa LUSINDE kuwa wapewe ubunge kwa ajili ya kuisadia familia kiuchumi. ujio wa Lowassa utageuza issue nzima ya kampeni kwenda kwenye baba mkwe kumtafutia mkwewe ulaji badala ya kutatua matatizo ya wananchi wa arumeru. ningemshauri akae pembeni kama kweli anampenda mkwewe badala ya kumharibia yeye akiwa kama DISGRACED PRIME MINISTER.
 
Back
Top Bottom