Midavudavu
JF-Expert Member
- Jan 23, 2012
- 287
- 59
Baada ya mwaka 1995 Mwalimu Nyerere kumkataa Lowassa kama angepitishwa kugombea nafasi ya urais kwa tiketi ya CCM, hali imekuwa hivyo kwa upande wa Dr. Slaa ambaye ni Katibu Mkuu wa Chadema ambaye amejitenga na wenzake juu ya maamuzi ya kumpokea Lowassa na kumpa nafasi ya kugombea urais kwa kupitia chama hicho.
Slaa alieongoza jopo la makamanda wa Chadema kuichafua CCM kwa kumuita Lowassa fisadi, leo hii angepaswa kuratibu mpangokazi mwingine wa kumsafisha na kumpigia kampeni mtu yuleyule waliomchafua kwa kutoa ushahidi katika majukwaa mbalimbali nchi nzima.
Hata hivyo Dr. Slaa ameonelea kujiweka pembeni na kukataa kuwa mnafiki wa kisiasa kwa kumsafisha mtu ambaye ananunka rushwa.
Hakika kwa hili Dr. Slaa anafuata nyayo za Nyerere kwa kuwasema hadharani wala rushwa na kukataa kuwasafisha kwa ushawishi wa mabilioni ya pesa.
Hakika ukweli wake utamuacha huru daima!