Lissu amlima barua Shibuda

cdm kuchukua nchi ni ndoto ya alinacha, sioni walichonacho kipya zaidi ya kutaka baadhi ya watu wawe na sauti zaidi ya wengine, kwa nini kila mtu anaehoji cdm anagombana na mbowe?mbowe hutakiwi kuwa rais pole kaka

Hivi unajua Hatamtu mzima akiwa Hana Meno mdomoni ukimwambia aongee, utaishia kucheka tu, sasa ndugu yangu kama huna point si unyamaze badala ya kutapika pumba? unajua maana ya kusimamia makubaliano, na jinsi ya kutofautisha na uongozi wa kibepari kama wa magamba?
 
Huyu shibuda afukuzwe ubunge na spika wa bunge kwa sababu amekiuka taratibu,kanuni na sheria za bunge.Bunge linawatambua wabunge wanaowakilisha wananchi kupitia vyama vyao vya siasa walivyopitia kuwa wabunge.Sasa hamuoni shibuda amekiuka hilo?Yeye ni aina mpya ya ubunge ambayo bado haijapitishwa na bunge.MBUNGE ASIYEWAKILISHA KUPITIA CHAMA ALICHOPITIA KUWA MBUNGE.MBUNGE BINAFSI,si bado haijapitishwa wakuu?
 
Kwa mustakabali na maendeleo ya chama Shibuda hafai kuwa ndani ya chadema hata kidogo. Kunako mfaa ni huko alikotoka kwenye watu waliovimbiwa kwa kutojali maslahi ya wengi.

Chadema isipo chukua maamuzi magumu ya kumfukuza itakuwa haina mfano na ule msemo wa wahenga wa mtoto umleavyo ndivyo akuavyo, kwa maana hiyo atakuja kuleta madhara makubwa baadae na dalili hizo zote tayari zimesha jionyesha kwa kupingana na maazimio na sera za chama dhahiri.

Naiomba kamati imfukuze hata kama tutakosa jimbo. Afadhari kuwa na wabunge wachache watii kuliko utitiri wa aina ya shibuda.
Dr Slaa, Mbowe, Zitto, Lissu na kamati nzima fukuzeni huyo jamaa hatufai sasa na hata tufuata hata baadae.
 
huyu shibuda bado ana ka element za kimagamba,mimi tokea mwanzo sikumuamini kabisa.alishazoea mambo ya kifisadi,kaja chadema kakuta watu wameridhika na njaa zao,ndio maana anapaona pachungu.let him go.hafai
 
Huyu shibuda afukuzwe ubunge na spika wa bunge kwa sababu amekiuka taratibu,kanuni na sheria za bunge.Bunge linawatambua wabunge wanaowakilisha wananchi kupitia vyama vyao vya siasa walivyopitia kuwa wabunge.Sasa hamuoni shibuda amekiuka hilo?Yeye ni aina mpya ya ubunge ambayo bado haijapitishwa na bunge.MBUNGE ASIYEWAKILISHA KUPITIA CHAMA ALICHOPITIA KUWA MBUNGE.MBUNGE BINAFSI,si bado haijapitishwa wakuu?

Inategemea na sababu yenyewe ya umfukuzia. Kwani wakimfukuza nae akaenda mahakamani na kuwashinda basi atabakia kuwa mbunge kwa amri ya mahakama mpaka bunge litakapo vunjwa 2015. Kwani yeye atadai kuwa anayoyafanywa ameelezwa na wapiga kura wake na sio chama chake. Ukizingatia Wananchi ndio waliomchagua na wanachokitaka atakitenda.

Mfano mzuri ni Mama Naila Jidawi.
 
Uroho wa madaraka ndo unamsumbua alihamia CHADEMA ili apate Ubunge baada ya kuangushwa vibaya na CCM sasa anaona Magambani kwake ni kuzuri anatamani kurudi wajameni kha!! Vyeo hivi balaa tupu
 
Uroho wa madaraka ndo unamsumbua alihamia CHADEMA ili apate Ubunge baada ya kuangushwa vibaya na CCM sasa anaona Magambani kwake ni kuzuri anatamani kurudi wajameni kha!! Vyeo hivi balaa tupu timulia mbali kabisa huyo mtu
 
[h=3]Tuko radhi Shibuda atimuliwe-Lissu [/h]

Na Grace Michael, Dodoma
Majira


SAKATA la Mbunge wa Maswa Magharibi, Bw. John Shibuda na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) limechukua sura mpya baada ya wabunge wa chama hicho kuweka msimamo kuwa wako tayari kumfukuza uanachama na kurudi kwenye uchaguzi endapo Kamati Kuu itaridhia na kuona kuwa hafai kuwa katika chama hicho.

Msimamo huo ulitolewa jana mjini hapa na Mnidhamu wa Kambi ya Upinzani, Bw. Tundu Lissu baada ya kuhojiwa na waandishi wa habari kuhusu hatua wanazotarajia kuchukua dhidi ya mbunge huyo baada ya kutangaza vita na chama hicho.

"Tuko tayari kuachana naye na kurejea kwenye uchaguzi... hatuwezi kuvumilia tabia ya namna hiyo ambayo ameifanya wazi ya kupingana na sera ya chama na muda huu ndo namwandia barua rasmi ya kumtaka ajieleze ni kwa nini anakwenda kinyume na msimamo wa chama," alisema Bw. Lissu na kuongeza kuwa:

"Hatua ambayo tunaweza kwa upande wetu hapa ni kumtaka ajieleze lakini baadaye suala hili litajadiliwa katika na Kamati Kuu ya chama ambayo ina mamlaka makubwa zaidi yakiwemo ya kumfukuza uanachama na katika hili halina visingizio kwa kuwa amelifanya wazi na msimamo wetu tuko tayari kurudi kwenye uchaguzi...na kama anaweza arudi alikotoka," alisema Bw. Lissu.

Alipohojiwa kuhusu kauli ya Bw. Shibuda ambaye alikaririwa na baadhi ya vyombo vya habari akisema yuko tayari kuanza kuhubiri mabaya ya CHADEMA na viongozi wake akiwemo, Bw. Freeman Mbowe na Bw. Zitto Kabwe, Bw. Lissu alisema kuwa hana jipya la kuhubiri dhidi ya chama hicho kwa kuwa hana anachokijua.

"Hivi Shibuda atahubiri nini kibaya cha CHADEMA? Ni muda gani aliotumia katika kuyajua hayo anayodai? Kwanza hata vikao sidhani kama kuna vikao zaidi ya vitano ambavyo amehudhuria tangu ajiunge na chama, hivyo hana jipya zaidi ya kusema matapishi ambayo yamekuwa yakihubiriwa kila siku kuwa CHADEMA ni chama cha wachaga," alisema Bw. Lissu.

Mtafaruku huo wa Bw. Shibuda na chama chake ulitokana na msimamo wake aliouonesha wiki iliyopita bungeni wakati akichangia hotuba ya Waziri Mkuu ya bajeti ya 2011/2012 ambapo aliiomba serikali kuongeza posho za vikao hadi sh 500,000 kutoka sh 70,000 kwa siku badala ya kuziondoa kama CHADEMA kinavyotaka.

Bw. Shibuda pia alipendekeza kubadilishwa kwa jina la posho na kuitwa ‘ujira wa mwia' ili kuondoa mawazo mabaya yanayotokana na neno posho hizo.

Hatua hiyo ya Shibuda ilikwenda kinyume na msimamo wa Kambi hiyo ya Upinzani hasa CHADEMA ambao tayari wametoa msimamo wao kutosaini posho hizo, endapo fomu zake zitatenganishwa na zile za mahudhurio.

Kama mtajichanganya kumfukuza hiyo itakuwa ni golden chance kwa ccm. they will make sure jimbo linarudi kwao,kwani wananchi waliompa kura wataudhika na kuwatosa cdm.
shibuda ni kada wa chama kongwe,nawashangaa leo eti ndio mnajifanya hamumtaki. Kuchemka kachemka ila kumfukuza nalo itakuwa ni uchemfu mwingine. mkimaliza kumfukuza huyo afatie Lema, kwani alijifanya kutotambua naibu meya nawakati mpango mzima alihusishwa.
 
Mawazo ya kutaka kukivuruga chama si mawazo ambayo Viongozi wa CHADEMA wanastahili kuyavumilia. Hakuna ushahidi wowote unaonyesha kwamba CHADEMA ni Chama Cha Wachagga. Fikiria athari kubwa kwa CHADEMA kama watamuachia Shibuda ambaye ni Mbunge wao kuendelea kumwaga sumu kila kona ya nchi kwamba CHADEMA ni chama cha Wachagga ni si ajabu akaongezea kwamba ni chama cha Wakristo. Sidhani kama atakuwa anakijenga chama chake bali atakuwa anakibomoa.
chama cha wakiristo kwani yy mwislaam. john Magale Shibuda
 
Kuna mengi ambayo Shibuda amevumiliwa tangu ajiunge na Chadema kwa miezi kadhaa, na hajaonyesha umoja na wenzake iwe katika mikutano ya bunge au mikutano ya hadhara. Wabunge wenzake wanapowajibika pamoja kuitangaza Chadema yeye anajua anakojificha na kusubiri tu kurudi bungeni kwa ajili ya posho. Huu si uwajibikaji. Bora kuwa na watu wachache wawajibikaji kama Lisu, Mnyika, Lema nk na kumwondoa huyu samaki aliyeoza harufu yake chafu isije ambukiza samaki wazuri wakaonekana wote wameoza.
 
Toa hayo magamba kabla hayajagandamana mwilini ili ccm wajifunze jinsi gani wanaume walivyo na maamuzi magumu maana nina uhakika kijana yeyote kutoka chadema anaweza kusisimama pale coz wananchi washapata tuition ya kutosha kutoka cdm

Kijana unamawazo mazuri sana, ila jamaa hawakujua kuwa mwenzao ni kinyonga. Kwa hiyo magamba yake yanabadilika ili kujihami.
 
Inategemea na sababu yenyewe ya umfukuzia. Kwani wakimfukuza nae akaenda mahakamani na kuwashinda basi atabakia kuwa mbunge kwa amri ya mahakama mpaka bunge litakapo vunjwa 2015. Kwani yeye atadai kuwa anayoyafanywa ameelezwa na wapiga kura wake na sio chama chake. Ukizingatia Wananchi ndio waliomchagua na wanachokitaka atakitenda.

Mfano mzuri ni Mama Naila Jidawi.
Kwa hiyo ametumwa na wapiga kura wake kwenda bungeni kutetea wabunge waongezewe posho kufikia laki tano kwa siku?! haya ni matusi kwa wapiga kura ambao wanahangaika huku na huko kupata mlo mmoja wa siku.
 

Hili swala hujalifuatilia vizuri mkuu toka awali, Lengo la Chama ni kushinikiza serikali iondoe hizo posho kwahiyo mpaka zitakapo ondolewa ina maana taifa litafaidika na kupungua kwa gharama za uendeshaji na matumizi ya serikali ambayo hayana umuhimu, kufanya hivyo aina maana kuwa wametumwa Bungeni kugoma bila hoja na tija! mawazo yako yana maanisha hivyo, kitu ambacho hatutegemei kufanywa na wabunge na viongozi sio wahuni wale ni viongozi wa Taifa hili.

Kila mbunge ana haki ya kupokea Posho hizo hadi pale serikali itakapo zifuta kama ambavyo CDM wameshauri, wapo Bungeni kwa ajili ya kurekebisha kanuni na sheria mbovu kama hizo, husidhani kuwa CDM wanaposema kufanywe overhaul ya katiba kuwa hivyo sasa wasiheshimu hii katiba iliopo!? hiyo siyo sheria na sheria haitafsiriwi hivyo, wataiheshimu hii katiba iliopo hadi pale itakapo patikani hiyo ambayo Watanzania tuliowengi tunaililia.

Kama umezaliwa wakuto elewa hauta elewa, maana hata darasa wapo wanakesha kujisomea lakini bado wana-fail mitihani. Jitahidi kuisoma na kuisoma nimejaribu kuweka kwa lugha rais sana.
Vijembe na misuto, lakini hujajibu swali. Nawasilisha tena:

Chadema wametishia kumfukuza Shibuda kwa msimamo wake wa kutaka posho ya Wabunge iendelee.

Katiba ya CHADEMA inaseme mwanachama analazimika akubaliane na
Katiba, Sera, Kanuni, Maadili ya Chama, Itikadi au Falsafa ya CHADEMA.

Ni wapi ilipoandikwa kwamba kupinga posho inatoka kwenye Katiba, Sera, Kanuni, Maadili ya Chama, Itikadi au Falsafa ya CHADEMA?

Kama papo mahala pameandikwa kwenye Katiba au Sera au Kanuni au Maadili ya Chama au Itikadi au Falsafa ya CHADEMA, kwamba CHADEMA inapinga posho ya Wabunge, mbona Tundu Lissu leo hii amekula posho, afukuzwe CHADEMA?
 
Yote mtasema badala yake mtajikuta hamna kitu mkononi. Mbona hamji na hoja za maendeleo nyie wanaCCM? hebu tuambieni tatizo la umeme litaisha lini? mnekuwa mnakuja na hoja humu tungewaeleweni lkn nyie mmebaki kujibizana na CDM tu. CCM ni kama dereva aliyeacha usukani wake na kuanza kubishana na abiria wake unategemea nini hapo?


Kama Shibuka hakubaliani na haya basi aondoke tu aache watu wapambane .Aje upande wa MS .
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom