JOHN MADIBA
JF-Expert Member
- Jan 30, 2011
- 251
- 155
SIKU chache baada ya Mbunge wa Maswa Magharibi, John Shibuda (CHADEMA) kupingana na msimamo wa chama hicho kwa kuunga mkono posho, Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni, Tundu Lissu, amesema chama hicho kiko tayari kwa lolote kuhusu mbunge huyo.
Lissu aliyasema hayo ofisini kwake jana alipotakiwa kuzungumzia kuhusu hatima ya mbunge huyo.
Namwandikia barua leo kumtaka aeleze kwa nini msimamo wake ulikuwa kinyume cha wa kambi ya upinzani na kama yupo tutamkabidhi leo, baadaye tutalipeleka kwenye Kamati Kuu ya CHADEMA yenye nguvu ya maamuzi, ikiwamo kumfukuza uanachama.
Tuko tayari kwa lolote kuhusu Shibuda hata kwenda kwenye uchaguzi mdogo, kama anaona CHADEMA ni mbaya arudi alikotoka au kama ataona atageuka jiwe, atafute sehemu nyingine ya kwenda, alisema Lissu.
Alisema wao binafsi hawawezi kuchukua uamuzi wa kumfukuza Shibuda zaidi ya kutangaza kumtenga, bali wenye uamuzi huo ni kamati kuu ya chama.
Alisema baada ya kuwasilisha utetezi wake kabla ya kumpeleka kwenye kamati kuu watakaa kwanza na kumjadili na kuchukua hatua dhidi yake, kwani suala hilo liko wazi.
Kuhusu mabaya ambayo Shibuda anayaendeleza kuhusu CHADEMA, Lissu alimtaka ayaendeleze na kumponda kuwa hana kipya zaidi ya kuzungumza matapishi.
Shibuda hana chochote kipya zaidi ya matapishi ya wale wa jana na juzi waliokuwa wakisema kuwa CHADEMA ni cha familia ya Mtei (Edwin) na mkewe Mbowe, ni cha Wachaga. Nje ya hayo sijui kama ana kipya, alisema Lissu.
Kwa mujibu wa Lissu, mbunge huyo aliingia kwenye chama hicho mwaka jana alipopata ubunge na kwamba hakuna anachokijua kuhusu chama hicho.
Wakati akichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, wiki iliyopita, Shibuda alikigeuka chama chake (CHADEMA) kuhusu posho akitaka ziongezwe hadi kufika sh 500,000.
Shibuda alikwenda mbali zaidi na kumtaka waziri mkuu kufanyia kazi haraka ongezeko hilo la posho, ambalo alilibatiza jina la ujira wa mwia.
Lissu aliyasema hayo ofisini kwake jana alipotakiwa kuzungumzia kuhusu hatima ya mbunge huyo.
Namwandikia barua leo kumtaka aeleze kwa nini msimamo wake ulikuwa kinyume cha wa kambi ya upinzani na kama yupo tutamkabidhi leo, baadaye tutalipeleka kwenye Kamati Kuu ya CHADEMA yenye nguvu ya maamuzi, ikiwamo kumfukuza uanachama.
Tuko tayari kwa lolote kuhusu Shibuda hata kwenda kwenye uchaguzi mdogo, kama anaona CHADEMA ni mbaya arudi alikotoka au kama ataona atageuka jiwe, atafute sehemu nyingine ya kwenda, alisema Lissu.
Alisema wao binafsi hawawezi kuchukua uamuzi wa kumfukuza Shibuda zaidi ya kutangaza kumtenga, bali wenye uamuzi huo ni kamati kuu ya chama.
Alisema baada ya kuwasilisha utetezi wake kabla ya kumpeleka kwenye kamati kuu watakaa kwanza na kumjadili na kuchukua hatua dhidi yake, kwani suala hilo liko wazi.
Kuhusu mabaya ambayo Shibuda anayaendeleza kuhusu CHADEMA, Lissu alimtaka ayaendeleze na kumponda kuwa hana kipya zaidi ya kuzungumza matapishi.
Shibuda hana chochote kipya zaidi ya matapishi ya wale wa jana na juzi waliokuwa wakisema kuwa CHADEMA ni cha familia ya Mtei (Edwin) na mkewe Mbowe, ni cha Wachaga. Nje ya hayo sijui kama ana kipya, alisema Lissu.
Kwa mujibu wa Lissu, mbunge huyo aliingia kwenye chama hicho mwaka jana alipopata ubunge na kwamba hakuna anachokijua kuhusu chama hicho.
Wakati akichangia hotuba ya makadirio ya matumizi ya Ofisi ya Waziri Mkuu, wiki iliyopita, Shibuda alikigeuka chama chake (CHADEMA) kuhusu posho akitaka ziongezwe hadi kufika sh 500,000.
Shibuda alikwenda mbali zaidi na kumtaka waziri mkuu kufanyia kazi haraka ongezeko hilo la posho, ambalo alilibatiza jina la ujira wa mwia.