<br />Leo tarehe 26/08/2011 ndio siku ya mwisho ya Vikao vya mjadala wa Bunge la Bajeti. Kumbukumbu sahihi zinanionyesha kuwa kikao hiki cha leo ni kikao cha 57, ya kikao kikubwa cha 4 la Bunge la 9. Mengi yamezungumzwa, tumeshuhudia mijadala mikali na yenye ukinzani mkubwa kama vile..<br />
<br />
1. Kukwamishwa kwa bajeti ya wizara ya nishati na madini,<br />
<br />
2. Kuongezwa billion 95 katika wizara ya uchukuzi,<br />
<br />
3. Kusimamishwa kazi na kuundwa tume ya bunge juu ya sakata la Nd. David Jairo-Katibu mkuu wa wizara ya nishati,<br />
<br />
4. Sakata la uhuzwaji holela wa UDA (Shirika la usafirishaji dar es salaam),<br />
<br />
5. Mvutano mkubwa kati ya wafanyabiashara wa mafuta na Ewura as wel as serikali,<br />
<br />
6. Kusimamishwa kazi kwa Afisa wanyamapori kwa sakata la twiga walioporwa kwenda Qatara<br />
<br />
7. Sakata la ununuzi wa Rada na report toka kitendo cha kijasusi cha upelelezi cha Uingeleza-SFU<br />
<br />
8. Ongezeko la mshahara la 8.6% kwa wafanyakazi wa umma na ongezeko la kima cha chini kutoka sh. 135,600/= mpaka 151, 000<br />
<br />
9. Kuletwa kwa Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano <br />
<br />
10. Kujiuzuru kwa pacha mmoja kati ya RACHEL Bw. Rostam Azizi,<br />
<br />
11. Kufariki kwa Mbunge Mussa Silima (Rest In Peace).<br />
<br />
Katika hayo na mengine mengi HEBU KWA PAMOJA TUFANYE TATHIMINI JUU YA UNDENDAJI KAZI WA BUNGE HILI. <br />
<br />
Nawasilisha!
<br />
namba 4 ni kuuzwa si kuhuzwa