KML
JF-Expert Member
- Apr 2, 2012
- 861
- 133
Akizungumza katika mikutano ya hadhara katika kata za Chienjele na Likunja katika Wilaya ya Ruangwa, Mbunge wa zamani wa Arusha Mjini, Godbless Lema alisema ni aibu kwa Serikali kukimbiza Mwenge kwa gharama ya Sh bilioni moja na kwenda kufungua zahanati ya kijiji isiyozidi Sh10 milioni.
Alisema ni muafaka kwa Serikali kujitathmini kama suala hilo la kukimbiza Mwenge linahitajika wakati huu ambao nchi inakabiliwa na mfumuko mkubwa wa bei huku wananchi wakiendelea kukosa huduma za msingi.
Alisema kama wabunge wa mikoa ya Lindi na Mtwara wangekuwa na nia ya kuwatumikia wananchi ipasavyo, wangekataa nafasi za uwaziri walizopewa kwa kuwa haziwasaidii chochote wananchi wao zaidi ya kuwafunga midomo wabunge waliotumwa kuwasemea katika shida mbalimbali za majimbo yao.
Source: Mwananchi
Alisema ni muafaka kwa Serikali kujitathmini kama suala hilo la kukimbiza Mwenge linahitajika wakati huu ambao nchi inakabiliwa na mfumuko mkubwa wa bei huku wananchi wakiendelea kukosa huduma za msingi.
Alisema kama wabunge wa mikoa ya Lindi na Mtwara wangekuwa na nia ya kuwatumikia wananchi ipasavyo, wangekataa nafasi za uwaziri walizopewa kwa kuwa haziwasaidii chochote wananchi wao zaidi ya kuwafunga midomo wabunge waliotumwa kuwasemea katika shida mbalimbali za majimbo yao.
Source: Mwananchi