Lema 'aichana' Idara ya Usalama wa Taifa

Status
Not open for further replies.
Kuna yeyote hapo nje atakayekua anayasoma na kutafakari maneno haya kwenye wino mwekundu?????????????????

Hapa unamuuliza nani hasa wewe?. Nani kakwambia mimi CHADEMA?, si wote wanaopinga udhalimu wa CCM ni CHADEMA au wapinzani.

Wapo CCM ndani ya chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi na wapo wasiokuwa ma chama wanapinga upuuzi huu wa kuchezea amani ya nchi. Mwaka 1992 tuliporudisha mfumo wa vyama vingi, wakati Tanzania ilipokuwa na viongozi wanaofikiria wananchi zaidi ya matumbo yao na familia zao kama Mwl Nyerere walilisemea hili la kuambatanisha siasa na vyombo vya usalama.

Unapokuwa na watu waliokabidhiwa dhamana ya kulinda raia na mipaka ya nchi kwa mujibu wa katiba kuwa mashabiki wa siasa unajenga mazingira ya kulipua nchi, wananchi watakapokata tamaa na vyombo hivi.

Kwa kuwa leo hii nchi inashikiliwa na genge la watu waliojimbikizia mali kifisadi na wanahitaji kulindwa na mkono wa sheria, matokeo yake wanavunja katiba kwa masilahi binafsi. Hakuna haja ya CDM wala chama chochote cha upinzani kuwa na armed wing, Armed wing ni PUBLIC TRUST, siku wakisema wananchi NO tunataka kuongozwa na X badala ya CCM, maghala ya risasi yataisha na bado hawatarudi nyuma.

Hakuna kitu kibaya kama kupoteza public trust, na kwa hili serikali ya CCM imefanikiwa sana. Hakuna mtanzania leo hii anayeiamini mahakama, polisi, Usalama wa taifa, na hivi karibuni Shimbo alipeleka shombo hiyo JWTZ japo walimdhibiti na kuminimise damage. Huwezi jenga Public trust kwa oppression or aggression, wananchi hawapaswi kuwaogopa au kuwachukia Polisi, au TISS, Tume ya uchaguzi au mahakama, bali wanapaswa kuwaheshimu na kuwaamini.

Unapotumia vyombo hivi kisiasa kwa masilahi yako si tu vinakusaidia kubakia madarakani bali vinakufanya uongoze watu wasikuwa na imani nawe na kuvifanya vyombo vya dola kuonekana kandamizi badala ya saidizi kwa wananchi.
 
Thee facts and truth will destroy kikwete gov. Tunajua tangu siku nyingi anayeharibu nchi yetu moja wapo la kundi la wahuni ni hawa usalama wa taifa na jeshi la polisi.

Nyie usalama wa taifa mkae mkijua tunawafahamu na tunajua malengo yenu ... subirini kidogo tu tutawaonyesha nini definition revolution.
 
Wakuu, orodha ya viongozi wa CHADEMA ambao Magogoni wanaamini kwamba wakiwaua basi utawala wao utakua ni wa milele tayari iko mitaani hadharani kwa msaada wa 'watu wema' kule Makumbusho Dar es Salaam.

Hivyo machalii, ajali za ajabu ajabu, mtu kula sumu, kule kudungwaa misindano ... sote tujue mhusika wetu ni huyu huyu. Tanzania mpaka sasa imenuna na kutopendezewa mtoto wake yeyote kumwagwa damu hivyo damu zaidi ikimwgwa basi tujiandae kabisa na garika.
 
Kila mara huwa nasema, hawa usalama wa taifa wanafanya intelijensia dhidi ya CHADEMA na viongozi wake. Kuhusu wavamizi wa kisomali ah ah, hapana.! Intellijensia badilikeni na mkome kuikalia kooni demokrasia kwani hamtaishinda.!
 
tuhuma hizi hazina makalio manene......................................mbna majina hayataji? Ujasiri wake uko wapi kama anaongoea kwa uficho na kwa woga.....................atupatie majina badala ya kumungunya mungunya maneno ............huyu siyo kiongozi wa kutumainiwa hapa A-Town........
 
Viongoz wengi usalama wa Taifa wamewekwa na viongoz wa serikal hasa kwa lengo la kutetea maslah ya ccm. Sitegemei serikali ya ccm inaweza kuwa na idara ya usalama huru.
 
Mkuu mimi nilikuwa shabiki mkubwa sana wa Godbless Lema lakini kauli zake baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge zimekuwa zikinichanganya na kwa sasa simuamini na wala kumshabikia tena.

Nashukuru kwa kuwa mbunge wangu, Ndg. Mnyika amejipambanua kuwa miongoni mwa wabunge wa upinzani wenye busara na ambaye kauli zake huwa ni za kujenga na si kubomoa. Akiendelea hivyo nitampa tena kura yangu uchaguzi ujao. Kusema kweli Mnyika ameonyesha ukomavu wa kisiasa na kuonyesha kwamba Tanzania ni yetu sote na tuitetee na siyo kuifananisha na Libya. Leo Libya wamegawa asilimia 35 ya mafuta yao kwa Ufaransa ati kwa sababu wamewasaidia kumng'oa Gaddafi, sijui akili au matope.

Angalizo: Sitaki mtu alinagnishe ugawaji huo na ugawaji wa madini yetu.

Mkuu wewe hujui mazingira ya Lema kule Arusha na yale ya Mnyika hapa Dar. Kwa taarifa yako kama Lema angekuwa mjinga kama mnavyofiikiri wewe na mwanzako Rejao, basi wananchi wa Ar wasingemuunga mkono katika kila hatua anayoichukua.

Siku zote mtu anayeungwa mkono na walalahoi ujue ni mtu anayetenda haki na na ndicho watu wananchokitaka kutoka kwa kiongozi wao. Huwezi kumlinganisha Lema na viongozi wa magamba hata kidogo. The Guy is Trustworth and honest.

Tofauti ya Lema na Mnyika ni moja tu kuwa Lema hamwogopi mtu na anauwezo wa kusimamia kile anachokitaka na anauwezo wa kuwashswishi watu wake.In few words the guy is a HARD PRESSING!
Mnyika in the other hand is a very good guy, he is trustworth and honest as well. However MNYIKA IS NOT A HARD PRESSING kama Lema.

Kwa Tanzania tulipofikishwa na hawa magamba ambao hudhani kuwa nchi hii na watanzania wote ni mali ya ccm, you need more Lemas and very few Mnyikas to get out of this mess otherwise forget it!


Soma magazeti ya leo Mnyika ataingia barabarani na wananchi wake wa Goba kuandamana kudai maji ya dawasco. Hakuna cha busara kama unataka haki kutoka utawala uliotandaza mizizi kila pembe kama wa gadafi.
 
Mheshimiwa tunaomba CV za Lema na Mnyika na uzowefu wao ktk masuala ya siasa. Nafikiri umegusia kua Lema ni muwazi na anajifunza kwa Mnyika na Mnyika nae anajifunza kwa Lema. Ni afadhali ukatupa CV zao ili watu wajue capacity zao ktk kuelewa mambo. Kua muazi inaweza kua sifa nzuri lakin ktk politics sometime sio inavyofanya kazi. Politics is a dirty game.

Kwangu mimi sizijui CV za hawa watu ila ukiangalia jinsi wanavyojenga hoja utaona kwamba Mnyika anajua kujenga hoja na kuifikisha kwa hadhira yake na kupokelewa vyema. Huyu Lema yeye ni masihi wa vurugu na vitisho. Hana hoja hata kidogo. Kwa mantiki hiyo si busara kuwalinganisha hawa wawili kwa kuwa ni sawa na mbingu na ardhi.
 
Mkuu wewe hujui mazingira ya Lema kule Arusha na yale ya Mnyika hapa Dar. Kwa taarifa yako kama Lema angekuwa mjinga kama mnavyofiikiri wewe na mwanzako Rejao, basi wananchi wa Ar wasingemuunga mkono katika kila hatua anayoichukua.

Siku zote mtu anayeungwa mkono na walalahoi ujue ni mtu anayetenda haki na na ndicho watu wananchokitaka kutoka kwa kiongozi wao. Huwezi kumlinganisha Lema na viongozi wa magamba hata kidogo. The Guy is Trustworth and honest.

Tofauti ya Lema na Mnyika ni moja tu kuwa Lema hamwogopi mtu na anauwezo wa kusimamia kile anachokitaka na anauwezo wa kuwashswishi watu wake.In few words the guy is a HARD PRESSING!
Mnyika in the other hand is a very good guy, he is trustworth and honest as well. However MNYIKA IS NOT A HARD PRESSING kama Lema.

Kwa Tanzania tulipofikishwa na hawa magamba ambao hudhani kuwa nchi hii na watanzania wote ni mali ya ccm, you need more Lemas and very few Mnyikas to get out of this mess otherwise forget it!


Soma magazeti ya leo Mnyika ataingia barabarani na wananchi wake wa Goba kuandamana kudai maji ya dawasco. Hakuna cha busara kama unataka haki kutoka utawala uliotandaza mizizi kila pembe kama wa gadafi.

Hiyo hard pressing ya Lema bila kujenga hoja haitatusaidia hata kidogo. Vitisho na umasihi wa vurugu havitamfikisha kokote. Ajenge hoja na siyo kutishia mambo ya Libya na Tunisia. Vurugu mara nyingi huwa zinaumiza wananchi huku hao wanaopelekea wananchi kufanya vurugu wao huwa wanakunywa mvinyo wao na familia zao!

Hata kama Mnyika ataandamana lakini atakuwa ametumia taratibu ikiwa ni pamoja na kuonana na hao DAWASCO na kuwaelezea kuhusu shida ya maji na siyo kutoa matamko ya vitisho kuta umaarufu.
 
Laiti ungalijua njaa walionayo WALAZWAHOI nchini ulivyofikia kubaya hadi hivi sasa, wala usingediriki kutumia saikolojia ya shule y chekechea hiyo ya kumfunga kamba Mnyika ili uje ukamponde baadaye na huku ukiona KAMANDA N TUMAINI JIPYA LA VIJANA nchini (Mh Godbless Lema) kuwa ni hatari kwa MASLAHI BINAFSI KWA KUSISITIZA MASLAHI YA UMMA na kumnyima kuwdi wako usingizi.

Huwezi kuiba kura za wananchi na baado ukafikiria kote ni shwari tu. Utawala chini ya mtaji wa wizi wa kura ni MZIGO kwa vyombo vya ulinzi na usalama kiasi cha kuweza kumpokonya kabisa mlipa kodi hki yaake stahiki ya kuvisimamia na kuvitawala vema.

Ni sikitiko ilioje kwamba baadhi ya vyombo vya umma hivi sasa vimelazimika kutumikia watu binafsi na magenge yao badala ya kutumikia wananchi!!

Lakini mwenye vyombo vyake kikatiba si siku nyingi huenda akaamua kusem 'HAPA TOSHA' mtu hanisukumi tena zaidi ya hapa. Hadi hapo patakua ni pata shika nguo kuchanika kwa wachache wenye shibe wasiowajali walazwahoi tuliowengi.


Hiyo hard pressing ya Lema bila kujenga hoja haitatusaidia hata kidogo. Vitisho na umasihi wa vurugu havitamfikisha kokote. Ajenge hoja na siyo kutishia mambo ya Libya na Tunisia.

Vurugu mara nyingi huwa zinaumiza wananchi huku hao wanaopelekea wananchi kufanya vurugu wao huwa wanakunywa mvinyo wao na familia zao!

Hata kama Mnyika ataandamana lakini atakuwa ametumia taratibu ikiwa ni pamoja na kuonana na hao DAWASCO na kuwaelezea kuhusu shida ya maji na siyo kutoa matamko ya vitisho kuta umaarufu.
 
Laiti ungalijua njaa walionayo WALAZWAHOI nchini ulivyofikia kubaya hadi hivi sasa, wala usingediriki kutumia saikolojia ya shule y chekechea hiyo ya kumfunga kamba Mnyika ili uje ukamponde baadaye na huku ukiona KAMANDA N TUMAINI JIPYA LA VIJANA nchini (Mh Godbless Lema) kuwa ni hatari kwa MASLAHI BINAFSI KWA KUSISITIZA MASLAHI YA UMMA na kumnyima kuwdi wako usingizi.

Huwezi kuiba kura za wananchi na baado ukafikiria kote ni shwari tu. Utawala chini ya mtaji wa wizi wa kura ni MZIGO kwa vyombo vya ulinzi na usalama kiasi cha kuweza kumpokonya kabisa mlipa kodi hki yaake stahiki ya kuvisimamia na kuvitawala vema.

Ni sikitiko ilioje kwamba baadhi ya vyombo vya umma hivi sasa vimelazimika kutumikia watu binafsi na magenge yao badala ya kutumikia wananchi!!

Lakini mwenye vyombo vyake kikatiba si siku nyingi huenda akaamua kusem 'HAPA TOSHA' mtu hanisukumi tena zaidi ya hapa. Hadi hapo patakua ni pata shika nguo kuchanika kwa wachache wenye shibe wasiowajali walazwahoi tuliowengi.

Mkuu hata Mnyika anatukomboa huku Ubungo lakini si kwa vitisho na kauli za vurugu kama za Lema. Nina shaka sana na kauli zake hizo huenda ni defensive mechanism kutokana na tuhuma za Zombe.
 
Mb wa Arusha Mjini Godbless Lema leo amefanya kikao na waandishi wa habari na kulaani kitendo cha polisi kushirikiana na usalama wa Taifa huku akimtaja Bwana Mombo afisa msaidizi usalama wa taifa mkoa kuhusika ktk njama za kuwafungulia kesi wanachama wa chadema na huku lengo kuu na mkakati ukiwa ni yeye.

Hivi karibuni jeshi la polisi mkoani arusha limewahoji viongozi wa chadema , Bwana Emanuel Kombe katibu mwenezi na Ephata Nanyaro mwenyekiti wa wilaya Arusha mjini kwa tuhuma za kupanga mauaji dhidi ya meya feki wa arusha , cha kushangaza ni kwamba watu hao wanaodai kuwa walihusika kwenye vikao hivyo ndio hao waliofanya maandamano kumpinga nanyaro na mb lema siku ya tarehe 6/8/2011 wakimshutumu mh lema kwa msimamo wake dhidi ya kutokubaliana na muafaka wa na leo wanasema walikuwa na kikao na mh lema na nanyaro tarehe 11/8/2011 cha kupanga mahuaji dhidi ya meya wa kichina.

Hebu fikirieni inawezekana vipi ukapanga mipango ya aina hii na adui yako , lakini hata hivyo Mh lema amesema yuko tiyari hata kupoteza\maisha yake kwa ajili ya kutetea umma wa watanzania , na kuomba serikali imchunguze bwana Mombo kwani ni afisa usalama anayeishi maisha ya anasa sana.

Duh! Nimeipenda hii. Kweli wachina nomaaa....
 
Wana JamiiForum na Watanzania wenzangu,

Nina masikitiko makubwa sana kutokana na hali ilivyo kwa sasa kwa jinsi Mh Godbless Lema anavyoandamwa na Usalama wa Taifa mpaka kufikia kutaka kumtia kitanzi kwa kupigania maslahi ya Watanzania wote.

Tuna kila sababu ya kumuunga mkono Mh Godbless Lema kutokana na jitihada zake za kupigania HAKI na USAWA kwa rasilimali za Tanzania ziwafikie watanzania wote bila kujali rangi,kabila wala Dini atokayo.

SISI wa-TANZANIA tuna tabia ya kuwapiga vita wapambanaji wa maslahi yetu badala ya kuwaunga mkono na matokeo yake wanakata tamaa na sisi tunabaki kuliwa kama shamba la bibi.

Haya ni maono yangu tuu.
 
Nadhani CCM bado hawataki kukubali kuwa Nchi siyo mali yao bali Nchi ni mali ya Watanzania.

Ningependa sana kuona Tanzania Mpya, Ukombozi wa kweli wa Mtanzania na Uhuru wa kweli usio na Matabaka. Nilivyokuwa nasoma sikufahamu mara moja Tanzania ni Tajiri na Masikini kiasi hiki. Sasa nimeingia kwenye kazi za kuhudumia jamii nikagundua hali ilivyo na Watanzania wachache walivyojilimbikizia mali.
 
Mungu atusaidie Tanzania.
Tanzania ulikuwa na amani lakini tunaona kidogo kidogo umeanza kuishiwa na amani je Tanzania unatupeleka wapi?

Tanzania hatujawahi kuwa na amani, ila hatukuwahi kuwa na watu wenye ujasiri kama Lema wakutufumbua macho watanzania na kuona tunavopelekwa!!!!!!
 
Hakuna idara ya usalama wa Taifa nchi hii, angalau Polisi wanajitahidi kufanya kazi zao. sitanii kwenye hili mwenye masikio na asikie.
 
Mkuu mimi nilikuwa shabiki mkubwa sana wa Godbless Lema lakini kauli zake baada ya kuchaguliwa kuwa mbunge zimekuwa zikinichanganya na kwa sasa simuamini na wala kumshabikia tena.

Nashukuru kwa kuwa mbunge wangu, Ndg. Mnyika amejipambanua kuwa miongoni mwa wabunge wa upinzani wenye busara na ambaye kauli zake huwa ni za kujenga na si kubomoa. Akiendelea hivyo nitampa tena kura yangu uchaguzi ujao. Kusema kweli Mnyika ameonyesha ukomavu wa kisiasa na kuonyesha kwamba Tanzania ni yetu sote na tuitetee na siyo kuifananisha na Libya. Leo Libya wamegawa asilimia 35 ya mafuta yao kwa Ufaransa ati kwa sababu wamewasaidia kumng'oa Gaddafi, sijui akili au matope.

Angalizo: Sitaki mtu alinagnishe ugawaji huo na ugawaji wa madini yetu.

Kizuri ni kujua mazingira, nasaba na haiba ya wakazi wa majimbo hayo kwa kila mmoja.Lema anawakilisha jimbo la Arusha mjini ambalo lina wakazi wake wana mchanganyiko lakini wenyeji walio wengi ni Waarusha,Wamelu,Masai,Wachaga na hao wote kiahaiba wanajulikana ni aina ya watu walio wazi kiasilia na wasio taka mzaa na ubabishaji au kupindisha maneno, Wakazi hao wa Arusha ni wafuasi wa kutambua Koleo ni koleao na kijiko ni kijiko,na hivyo si sawa kusema koleo ni kijiko kikubwa.

Wakati huo mnyika ni mwakilishi wa jimbo la Ubungo ambalo wakazi wake ni mchanganyiko wa makabila tofauti tofauti na wenyeji wake wengi ni wazaramo na mchanganyiko wa makabila ya pwani kama wakwere nk,ambayo kihaiba ni watu wa kuchukulia utatuzi wa matatizo kwa misingi ya maongezi ya muda hata kama yatakuwa na kero kubwa kwao na hasara yoyote wao imani kubwa kuwa mtapata suluhu muda ukifika.

Kwa picha hiyo utaona kila mmoja anaongoza jimbo likiwa na utamaduni tofauti wa wenyeji wake wakiwa na mtizamo tofauti wa kiamapokeo na utatuzi wa matatizo yao.

Msimuonee Lema angalieni jamii,na tamaduni,Nyerere na uwezo wake wote wa kuwajenga watanzania bado alipofika kwa ndugu zake wakurya ilikuwa ni kazi kuwaelimisha na kuwafikishia ujumbe,na mpaka ameondoka bado mkoa ule kauacha akiwa hana jibu kamili ni watu wa aina gani.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom