LAKINI, hiyo shombo amletea nani?

Rutashubanyuma
umenikumbusha zamani kidogo (1989) Mara tu baada ya shairi langu kutoka kwenye gazeti la "Uhuru" nilipata barua nyingi sana nyingine za kutaka... Ushairi ni jambo jema sana na watu wengi ambao ni wajuvi wa kutumia Lugha wao pia huwa ni werevu na weledi kwenye mambo mengi sana. Aakh! Bahati mbaya sana siku hizi matumizi ya lugha si jambo la kutiliwa maanani sana!!

Kigarama mie humkumbuka Shabaani Robert zaidi zaidi tatizo la kizazi cha leo..............wanabwatuka na kimombo hewa.......fasihi simulizi wameipiga kisogo, vile...........
 
atakuwa hajui katiba yetu

Kaizer......................mmmmmmmmmmmhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhhh......................naona kila mahali ni katiba tupu..........
 
ruta vipi mwezetu leo umetedwa nini? pole kwa yaliyokusibu umeandika uzi kwa hisia kali sana.penye penzi hapakosi udhia, na penye udhia penyeza rupia.
 
ruta vipi mwezetu leo umetedwa nini? pole kwa yaliyokusibu umeandika uzi kwa hisia kali sana.penye penzi hapakosi udhia, na penye udhia penyeza rupia.
hisia zangu a kiuandishi hazina uhusiano na maisha yangu............hicho ni kipaji cha kufikisha ujumbe mahali pake..............na ni mbinu ya usanifu nguli tu.............usisome zaidi ya hapo.......
 
Ruta,Hilo nalo neno...unanifanya nishtuke ukirejea home nianze kunusa nusa isjekua unanitupia vijembe bibi jinga mali yako inaliwa mie nimelala tuu.
 
Kweli kabisa, mwenye kisu, anakula nyma taratibu, na akirudi home.. kimya...??
maisha yanakwenda kama kawaida,
ndio maana siku hizi married couples ni kama ndege; wanapokula na wanapolala ni tofauti kabisa.
 
wanaojisahau na kurudi na shombo majumbani wafunguke tusikia miziki yao kwa wale wanaowaringishi hizo shombo!
 
Pilau ale yeye tena kwa kificho huku akjijua ni mwizi tu.............akiwa kwenye chumba alichokishindilia komeo tena la viro ili asije kubambwa na mwenye mlo wake.............baada ya uporaji wa pilau ya watu aja mtaani na huanza kutubehulia.........na kuacha mafuta ya pilau na vipunjepunje vyake mdomoni.......

Hivi, hiyo shombo amletea nani?

Mwingine ametoka kumtafuna kuku wa watu khalafu kwa kasi ya ajabu hurukia kitandani kwa mkewe na kumshulizia manukato yatokanayo na siagi ya samli aliyopikiwa kuku wa watu aliyemtafuna ............kwa kufanya hivyo ni mithali ya kumtambia mkewe ya kuwa amejinoma kuku wa watu..........lakini swali ni

Hivi, hiyo shombo amletea nani?

Kwa nini asiende bafuni akaoga na kutakata na abakie akichekwa na dhamira yake badala ya kuwaadhibu waliokuwamo na wasio kuwamo..........kama ile hadithi ya panya aliyekusudiwa kuuawa na mtego lakini mtego ukamnasa nyoka ambaye mwenye nyumba aliposikia umenasa akawahi kummalizia panya gizani na matokeo yake akaumwa na nyoka mwenye hasira na kufa hapohapo.........matangani ng'ombe na kuku walichinjwa kumsindikiza mwendazake............na hivyo kukamilisha maono ya panya ya kuwa mtego ulomlenga yeye wataingia waliomo na wasiokuwamo........

Hivi walakini...........hiyo shombo amletea nani?

Ujumbe mzito sana huu
 
nyumba-maige_thumb.jpg


Shombo ni hili.... na wanaonusishwa ni hawa

2Q==
Z
 
Mkuu salute! Nimeipenda sana post yako,nimekugongea ka like ila natumia tochi
Eti mwingine kalishwa mijichips kuku huko na kidume cha jirani...anakuja kitandani na kuanza kuachia hewa zisizovutika sawia puani kwa mwenzie..hilo shombo amleteee nani??

Ana lambwa lambwa mdomo kama paka akiwa na kijike au kidume pori, anarudi nyumbani hataki hata kunawa mdomo anataka akugushishe mdomo wake..hilo shombo amletee nani??

Kaachia, kanyonywa nyonyo weeeee hata kuliko anavyoweza kuwamchia mwanae, eti baadae anarejea nyumbani anataka kumnyonyesha mtoto wake mchanga pasipo hata kujishwafi uzuri....eti hilo shombo anamletea nani??

Karuhusu kidume shume kimguse sehemu ambazo hata wewe mumewe/boy friend hujawahi kugusa, kanogewa huko, anarejea nyumbani, anakugezia nawe uguse huko asijue wewe sie yule aliyezoea mambo hayo..sasa hilo shombo la mtandao huo wenye wateja kidogo amleteee nani??
 
RUTA ,wewe mswahili safi ,labda alifanya kwa dhamira ,kwan nan asiye jua kuwa shombo n MAKRUKH, akaona nataka nijuilikane kama leo nimechoea maneno ya huku kwetu kisiwani
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom