Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,956
- 22,148
Ashushiwa Kipigo na Mumewe Baada ya Kushinda Uchaguzi
Tuesday, December 08, 2009 10:59 AM
MWANAMKE Salma Musa mkazi wa Kiloleni Mkoani Tabora, amelazwa katika hospitali ya Mkoa huo baada ya kupigwa na mumewe hadi kupoteza fahamu baada ya kushinda uchaguzi wa Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa kwa tiketi ya CCM na kumshinda mumewe aliyegombea kwa tiketi ya CUF.
Mwanamke huyo alipigwa baada ya kumpiku mumewe huyo katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini kote ambapo yeye aligombania kiti hicho kwa tiketi ya CCM na mumewe huyo kugombania kiti hicho kwa tiketi ya CUF.
Akielezea mkasa huo kwa waandishi wa habari kwa shida, huku akiwa kitandani katika hospitali hiyo, baada ya kupata fahamu kidogo Salma alisema kuwa sababu iliyomfanya apigwe na mume wake huyo kukerwa na kitendo cha yeye kushinda uchaguzi huo kwa tiketi ya CCM.
Alieleza kuwa mume wake huyo alikuwa akimkorofisha kwa muda mrefu na kukerwa na kitendo cha yeye kumpiku katika uchaguzi huo na kusema kuwa yeye alitoa rushwa kwa wasimamizi wa uchaguzi na maneno mengi kuashiria hakushinda kwa halali kwenye uchaguzi huo lazima atakuwa ametoa rushwa ya ngono kwa wasimamizi.
Alisema mara kwa mara alikuwa akimpiga lakini alimsihi kuwa aachane na tabia hiyo lakini aliendela na vitendo vya kumpiga mara kwa mara na mara ya mwisho alimwamia kuwa akimpiga atakimbilia polisi kutoa taarifa.
Alisema baada ya kumwambia hivyo ndipo alimpiga hadi kupelekea kupoteza fahamu na majirani kukimblia polisi kutoa taarifa kufuatia tukio hilo.
Mkuuu wa Wilaya ya Tabora Mussa Changa amesema kuwa mume wa dada huyo anashikiliwa na jeshi la polisi kufuatia ukatili huo alioufanya kwa mke wake huyo.
Na Salma anaendelea na matibabu hospitalini.
Tuesday, December 08, 2009 10:59 AM
MWANAMKE Salma Musa mkazi wa Kiloleni Mkoani Tabora, amelazwa katika hospitali ya Mkoa huo baada ya kupigwa na mumewe hadi kupoteza fahamu baada ya kushinda uchaguzi wa Mwenyekiti wa Serikali za Mtaa kwa tiketi ya CCM na kumshinda mumewe aliyegombea kwa tiketi ya CUF.
Mwanamke huyo alipigwa baada ya kumpiku mumewe huyo katika uchaguzi uliofanyika hivi karibuni nchini kote ambapo yeye aligombania kiti hicho kwa tiketi ya CCM na mumewe huyo kugombania kiti hicho kwa tiketi ya CUF.
Akielezea mkasa huo kwa waandishi wa habari kwa shida, huku akiwa kitandani katika hospitali hiyo, baada ya kupata fahamu kidogo Salma alisema kuwa sababu iliyomfanya apigwe na mume wake huyo kukerwa na kitendo cha yeye kushinda uchaguzi huo kwa tiketi ya CCM.
Alieleza kuwa mume wake huyo alikuwa akimkorofisha kwa muda mrefu na kukerwa na kitendo cha yeye kumpiku katika uchaguzi huo na kusema kuwa yeye alitoa rushwa kwa wasimamizi wa uchaguzi na maneno mengi kuashiria hakushinda kwa halali kwenye uchaguzi huo lazima atakuwa ametoa rushwa ya ngono kwa wasimamizi.
Alisema mara kwa mara alikuwa akimpiga lakini alimsihi kuwa aachane na tabia hiyo lakini aliendela na vitendo vya kumpiga mara kwa mara na mara ya mwisho alimwamia kuwa akimpiga atakimbilia polisi kutoa taarifa.
Alisema baada ya kumwambia hivyo ndipo alimpiga hadi kupelekea kupoteza fahamu na majirani kukimblia polisi kutoa taarifa kufuatia tukio hilo.
Mkuuu wa Wilaya ya Tabora Mussa Changa amesema kuwa mume wa dada huyo anashikiliwa na jeshi la polisi kufuatia ukatili huo alioufanya kwa mke wake huyo.
Na Salma anaendelea na matibabu hospitalini.