Kwanini kuna muda wa kuisha matumizi kwenye vitambulisho vya Taifa?

Indume

Member
Apr 11, 2011
81
36
Kitabulisho cha Taifa kilichoanza kutolewa hivi majuzi na mkuu wa nchi kina lengo la kumtambulisha raia na kusaidia mamlaka mbalimbali kujua uhalali wa shughuli zako na mchango wako katika pato la Taifa.

Kulingana na jinsi kinavyosomeka, imeonekana kuwa waandaaji ambao ni serikali hii isiyokuwa makini wamekurupuka kabisa kuandaa vitambulisho vyenye sifa ya U-taifa.

Kwanza, kuna mkanganyiko wa matumizi ya lugha iliyotumika. Kwa kiswahili kuna sehemu inasomeka "Majina ya kati" lakini kwa tafsiri waliyoiwekwa wao kwa kiingereza ni "Middle name" badala ya middle names.

Pili,
Kitambulisho hiki cha uraia kinasomeka kuwa kitafikia muda wake au mwisho wa matumizi yake ni mwaka 2023 (Expiring date is 2023), ikiwa na maana kuwa ifikapo mwaka 2023 uraia wako wa kuitwa wewe ni Mtanzania utakoma.

Swali langu ni kuwa inakuwaje kama kweli mimi ni mtanzania na nimepewa uraia kwa nini uraia wangu una expiring date??

Kwa maana ingine basi mwaka 2024 watanzania wote akiwemo na mkuu wa nchi hawatakuwa raia wa TZ, ina maana serikali na vyombo vyake vitaachia ngazi.

Kwa maeneo hayo, inaonekana mamlaka zilizojihusisha na kushughulikia mchakato wa kuandaa vitambulisho vya Taifa either hawakujua cha kufanya au wamekurupuka na kushinndwa kabisa kutengeneza vitambulisho vyenye hadhi ya Kitaifa.

Ombi langu ni kuwa ni afadhali Passport ziendelee kutumika kuliko kutumia hivyo vitambulisho vya taifa, na ikiwezekana viandaliwe vitambulisho vingine vyenye hadhi ya kitaifa kwa kuwatumia wataalamu makini.

Thanks.
 
Tumekupata mkuu sasa kumiliki hiyo passport inataka uwe na moyo mgumu kwani inakulazimi mfuko utoboke
 
Mkuu nimekusoma,japokuwa walikuwa na maana ya kinachoisha muda ni kitambulisho na sio uraia but swali linakuja what next after that(kama sitarenew)? Labda watatoa au wametoa maelezo somewhere sometime,hii serikali siiamini sana kwenye mengi so sishangai hili
 
Acha ushamba bana 2023 vitatolewa vitambulisho vingine na sio kama unavyo tafsiri!

Hebu twambie vizuri, ni kwa nini vitolewe vingine mwaka 2023? Kwa nini taifa liingie kwenye hizo gharama? Haina mantiki hata kidogo kwa kitambulisho cha uraia kuwa na expiry date labda kama tayari huu mradi umeishakuwa earmarked kama njia ya kuiba pesa za walipa kodi.

Tiba
 
Tatizo la serikali yetu ni kuiga kila kitu (copy and paste). Na huko wanako kwenda kuiga huwa hawana muda wa kujifunza zaidi ya kukimbilia shopping. Wanakosa ubunifu kwa sababu ya elimu isiyo kuwa na Mitaala. Matokeo yake ni kazi zisizo na viwango bora. Na Mkulu wetu asivyo kuwa na muda/ akili ya kudadisi au kuchunguza jambo fulani, hujikuta akiingizwa mkenge. Hatumlaumu kwani hana hata mshipa wa aibu.

Yaani ukikichunguza hicho kitambulisho, huwezi amini kwamba sarakasi na mbwembwe za miaka nenda rudi zao lake ni kitambulisho cha aina ile.

Tulidanganywa kwamba kuna tenda zilishindanishwa, lakini kazi iliyotoka ni kama mtu kajifungia ofini kwake na kutoka na utumbo wa namna hiyo.
Yaani serikali hii kila inalolifanya ni kama laana vile.
 
Indume naona hauna hekima what u see ni negativity.
Stop complaining over the government do something.
Acha hoja binafsi
 
Last edited by a moderator:
Naona nia yao ni kuendelea kula pesa za wananchi! Hakuna maana ya kuweka expire date kama mtu amesha julikana ni raia!

Hapa wana mpango wa kutengeneza vingine maana wamesha muahidi tenda mtu mwingine!

Huu ni ujinga na udhaifu mkubwa wa seriakali ya ccm!
 
Naona nia yao ni kuendelea kula pesa za wananchi! Hakuna maana ya kuweka expire date kama mtu amesha julikana ni raia!

Hapa wana mpango wa kutengeneza vingine maana wamesha muahidi tenda mtu mwingine!

Huu ni ujinga na udhaifu mkubwa wa seriakali ya ccm!

Jamani hivi vitambulisho ni zaidi ya kipande wanachoita wakenya, huko tuendako kitambulisho hiki kitakuwa ndo kila kitu,kila kitu chako kitakuwa humo,leseni,tin no,vrn,atm,etc,mfano ukidaiwa tra kuna sehemu ukiswap itaonesha unakosa fulani,mambo yA kadi za atm tano tano yatakwisha ni suala la intergration tu,walioko kulikoendelea wanajua,tuache kulalama kila wakati,hakuna atm card,leseni etc isiyo expire.
 
Hebu twambie vizuri, ni kwa nini vitolewe vingine mwaka 2023? Kwa nini taifa liingie kwenye hizo gharama? Haina mantiki hata kidogo kwa kitambulisho cha uraia kuwa na expiry date labda kama tayari huu mradi umeishakuwa earmarked kama njia ya kuiba pesa za walipa kodi.

Tiba

Tena kama wameweka expiry date ya mpaka 2023 ni mbali sana. Vitambulisho vingi sehemu nyingi duniani ni miaka mitano mitano. Huwezi kuwa na kitambulisho kimoja toka ukiwa na miaka 18 mpaka miaka 100. Ni mabadiliko mengi yanatokea.
 
Indume

naona jazba zimekupanda kweli, sijui niite chuki. Umesahau ya mtwara mkuu? watu tulipandwa na mjaziba nhiha lakini jamaa kaja kazishusha. anyway, mkuu ninachokijua ni kwamba baada ya miaka 10 ID ina expire ili kuweza kutoa nafasi kwa waliofariki kuenguliwa na hata waliohama nchi. nasikia hata wewe unampango wa kuhamia Vat! je umeshawahi kufikiria kuhusu watakaozaliwa na kuhamia/kupewa uraia wa Tz? ni hayo.
 
Kitabulisho cha Taifa kilichoanza kutolewa hivi majuzi na mkuu wa nchi kina lengo la kumtambulisha raia na kusaidia mamlaka mbalimbali kujua uhalali wa shughuli zako na mchango wako katika pato la Taifa. Kulingana na jinsi kinavyosomeka, imeonekana kuwa waandaaji ambao ni serikali hii isiyokuwa makini wamekurupuka kabisa kuandaa vitambulisho vyenye sifa ya U-taifa.
Kwanza, kuna mkanganyiko wa matumizi ya lugha iliyotumika. Kwa kiswahili kuna sehemu inasomeka "Majina ya kati" lakini kwa tafsiri waliyoiwekwa wao kwa kiingereza ni "Middle name" badala ya middle names.
Pili,
Kitambulisho hiki cha uraia kinasomeka kuwa kitafikia muda wake au mwisho wa matumizi yake ni mwaka 2023 (Expiring date is 2023), ikiwa na maana kuwa ifikapo mwaka 2023 uraia wako wa kuitwa wewe ni Mtanzania utakoma. Swali langu ni kuwa inakuwaje kama kweli mimi ni mtanzania na nimepewa uraia kwa nini uraia wangu una expiring date?? Kwa maana ingine basi mwaka 2024 watanzania wote akiwemo na mkuu wa nchi hawatakuwa raia wa TZ, ina maana serikali na vyombo vyake vitaachia ngazi.
Kwa maeneo hayo, inaonekana mamlaka zilizojihusisha na kushughulikia mchakato wa kuandaa vitambulisho vya Taifa either hawakujua cha kufanya au wamekurupuka na kushinndwa kabisa kutengeneza vitambulisho vyenye hadhi ya Kitaifa.
Ombi langu ni kuwa ni afadhali Passport ziendelee kutumika kuliko kutumia hivyo vitambulisho vya taifa, na ikiwezekana viandaliwe vitambulisho vingine vyenye hadhi ya kitaifa kwa kuwatumia wataalamu makini.

Thanks.
Tembea uone Indume, mbona kuna nchi nyingi vitambulisho vina malizika muda wake , ili uombe tena kama una watoto unawaongeza kwenye form yako utakayojaza kwa wakati huo, unajaza form leo upo single baada ya miaka 2 unaoa au unaolewa na kupata watoto, sasa watapataje habari zako kama familia yako imeongezeka bila ya wewe kwenda kujaza form nyingine? na vile vile kuna mabadiliko mengi sana katika hiyo miaka 10 au 5 ya maisha yako kama umehama mtaa au umepata kilema au mabadiliko yoyote katika maisha yako lazima wajue, sasa ukipewa kitambulisho moja kwa moja watajuaje mabadiliko yako ya kimasiha?
 
Kitabulisho cha Taifa kilichoanza kutolewa hivi majuzi na mkuu wa nchi kina lengo la kumtambulisha raia na kusaidia mamlaka mbalimbali kujua uhalali wa shughuli zako na mchango wako katika pato la Taifa. Kulingana na jinsi kinavyosomeka, imeonekana kuwa waandaaji ambao ni serikali hii isiyokuwa makini wamekurupuka kabisa kuandaa vitambulisho vyenye sifa ya U-taifa.
Kwanza, kuna mkanganyiko wa matumizi ya lugha iliyotumika. Kwa kiswahili kuna sehemu inasomeka "Majina ya kati" lakini kwa tafsiri waliyoiwekwa wao kwa kiingereza ni "Middle name" badala ya middle names.
Pili,
Kitambulisho hiki cha uraia kinasomeka kuwa kitafikia muda wake au mwisho wa matumizi yake ni mwaka 2023 (Expiring date is 2023), ikiwa na maana kuwa ifikapo mwaka 2023 uraia wako wa kuitwa wewe ni Mtanzania utakoma. Swali langu ni kuwa inakuwaje kama kweli mimi ni mtanzania na nimepewa uraia kwa nini uraia wangu una expiring date?? Kwa maana ingine basi mwaka 2024 watanzania wote akiwemo na mkuu wa nchi hawatakuwa raia wa TZ, ina maana serikali na vyombo vyake vitaachia ngazi.
Kwa maeneo hayo, inaonekana mamlaka zilizojihusisha na kushughulikia mchakato wa kuandaa vitambulisho vya Taifa either hawakujua cha kufanya au wamekurupuka na kushinndwa kabisa kutengeneza vitambulisho vyenye hadhi ya Kitaifa.
Ombi langu ni kuwa ni afadhali Passport ziendelee kutumika kuliko kutumia hivyo vitambulisho vya taifa, na ikiwezekana viandaliwe vitambulisho vingine vyenye hadhi ya kitaifa kwa kuwatumia wataalamu makini.

Thanks.

Nimeajiriwa kama 'permanent and pensionable, lakini kitambulisho changu kina-expire 2014! Kitambulisho changu cha Benki NMB kinasema expiry date 2014! Ndo ajira yangu inakoma hapo, na ndo uteja wangu NMB unakoma hapo? Vingine naona tunalaumu ili tulaumu tu!
 
Kitabulisho cha Taifa kilichoanza kutolewa hivi majuzi na mkuu wa nchi kina lengo la kumtambulisha raia na kusaidia mamlaka mbalimbali kujua uhalali wa shughuli zako na mchango wako katika pato la Taifa. Kulingana na jinsi kinavyosomeka, imeonekana kuwa waandaaji ambao ni serikali hii isiyokuwa makini wamekurupuka kabisa kuandaa vitambulisho vyenye sifa ya U-taifa.
Kwanza, kuna mkanganyiko wa matumizi ya lugha iliyotumika. Kwa kiswahili kuna sehemu inasomeka "Majina ya kati" lakini kwa tafsiri waliyoiwekwa wao kwa kiingereza ni "Middle name" badala ya middle names.
Pili,
Kitambulisho hiki cha uraia kinasomeka kuwa kitafikia muda wake au mwisho wa matumizi yake ni mwaka 2023 (Expiring date is 2023), ikiwa na maana kuwa ifikapo mwaka 2023 uraia wako wa kuitwa wewe ni Mtanzania utakoma. Swali langu ni kuwa inakuwaje kama kweli mimi ni mtanzania na nimepewa uraia kwa nini uraia wangu una expiring date?? Kwa maana ingine basi mwaka 2024 watanzania wote akiwemo na mkuu wa nchi hawatakuwa raia wa TZ, ina maana serikali na vyombo vyake vitaachia ngazi.
Kwa maeneo hayo, inaonekana mamlaka zilizojihusisha na kushughulikia mchakato wa kuandaa vitambulisho vya Taifa either hawakujua cha kufanya au wamekurupuka na kushinndwa kabisa kutengeneza vitambulisho vyenye hadhi ya Kitaifa.
Ombi langu ni kuwa ni afadhali Passport ziendelee kutumika kuliko kutumia hivyo vitambulisho vya taifa, na ikiwezekana viandaliwe vitambulisho vingine vyenye hadhi ya kitaifa kwa kuwatumia wataalamu makini.

Thanks.
mkuu lengo la vitambulisho hivi ni kuhujumu uchaguzi mwaka 2015 na nakuhakikishia kuwa kutakuwa na complains nying sana juu la hili na ni dhahiri kuwa kuna njama za namna hiyo
 
Tena kama wameweka expiry date ya mpaka 2023 ni mbali sana. Vitambulisho vingi sehemu nyingi duniani ni miaka mitano mitano. Huwezi kuwa na kitambulisho kimoja toka ukiwa na miaka 18 mpaka miaka 100. Ni mabadiliko mengi yanatokea.

Acha generalization, twambie ni nchi gani vitambulisho vya uraia vinabadirishwa kila baada ya miaka 5? Chukua majirani zetu wa Kenya ambao wamekuwa wana vitambulisho vya uraia kwa karibu miaka 40 iliyopita kama wanavibadirisha au vina muda wa kwisha kutumika!!!!

Amini usiamini huu ni mradi wa ulaji!!!!!

Tiba
 
It does not make any sense for this ID to expire kwasababu namba yako ya utambulisho kama mtanzania haitakiwi kubadilika.ni hiyo hiyo mpaka ufe,kinachotakiwa ni what we call system integrations in loose coupled manner aka webservice.Kiasi kwamba nikiswap kitambulisho changu au kuwapa namba yangu ya uraia letsay Tra system zao ziweze kucommunicate na bank system kujua kama ninamkopo,polisi kama ninamakosa yoyote ya kihalifu etc.
Mtu akipata mtoto kuwe na means RITA kuapdate my information to NIDA database kwamba sasa family details zangu zimeongezeka etc
 
Nimeajiriwa kama 'permanent and pensionable, lakini kitambulisho changu kina-expire 2014! Kitambulisho changu cha Benki NMB kinasema expiry date 2014! Ndo ajira yangu inakoma hapo, na ndo uteja wangu NMB unakoma hapo? Vingine naona tunalaumu ili tulaumu tu!

Kuna sababu za msingi sana kwa Credit card, debit card, na ATM cards kuwa na muda wa kuisha kutumika. Tunaishi kwenye changing technology, hivyo vitu vinawekewa muda wa kuachakutumikaili kutoa nafasi ya kuingiza technologia mpya!!!! Hali kadhalika passport, sasa hiki kitambulisho cha uraia ni technology gani mpya itakuwa inaongezwa?

Tiba
 
It does not make any sense for this ID to expire kwasababu namba yako ya utambulisho kama mtanzania haitakiwi kubadilika.ni hiyo hiyo mpaka ufe,kinachotakiwa ni what we call system integrations in loose coupled manner aka webservice.Kiasi kwamba nikiswap kitambulisho changu au kuwapa namba yangu ya uraia letsay Tra system zao ziweze kucommunicate na bank system kujua kama ninamkopo,polisi kama ninamakosa yoyote ya kihalifu etc.
Mtu akipata mtoto kuwe na means RITA kuapdate my information to NIDA database kwamba sasa family details zangu zimeongezeka etc
Kwa hiyo wewe unasema huwezi kupewa kitambulishi chenye namba ile ile unapo-renew?
 
Back
Top Bottom