Kwanini Kikwete alikataa kumleta Ballali?

Tafuta vizuri utapata jibu, ukitaka kusolve soln usiende na mambo mengi nenda na moja baada ya jingine

Kuna watu wa kutosha kwenda na yote...We chagua la kwenda nalo...Mimi nachagua vyote!
VYOTE VINA MASLAHI TOWARDS JUSTICE!
 
Wazee Wa Iringa Watoa siku 30 kwa muuaji wa Ballali!

Wazee wa kihehe wametoa siku 30 kwa aliyehusika kwa njia moja ama nyingine na kifo hicho, kujisalimisha kijijini Luganga, Mufindi mkoani Iringa alikozaliwa gavana huyo la sivyo wamedai patakuwa hapatoshi.
Hayo yalizuka baada ya mwili wa aliyekuwa gavana wa Benki Kuu ya Tanzania BOT Dk. Daudi Ballali kuzikwa huko Washington, Marekani Ijumaa iliyopita.

Wakizungumza na waandishi jana kwa niaba ya wenzao, waliojulikana kwa jina la Mzee Samweli Kalinga (76) na Yohanes Kalinga (85), walisema wataamini kuwa mtoto wao amekufa baada ya kupata ufafanuzi wa kina kupitia kauli ya Rais Jakaya Kikwete kuhusu kifo hicho la sivyo haiwaingii akilini kabisa.

Timu hiyo ya Wazee hao wanaotoka kijiji cha Luganga na Mtwango, wameiomba serikali ifanye uchunguzi wa kina juu ya kifo hicho na kufanya kila linalowezekana kurejesha mwili huo nchini, na kama itashindikana ilete mchanga wa kaburi hilo ili wafanye mazishi ya kimila hapa nchini.

Walisisitiza kwa kusema sema kama wao ni wazee wa siku nyingi wa kijiji cha Luganga na Mtwango, wanashindwa kuamini kuwa mtoto wao amekufa, wataamini jambo hilo baada ya kuona maiti au picha yake akiwa amekufa.

Mzee Samweli alisema taarifa zilizotolewa na vyombo vya habari hazitoshelezi kuamini kuwa ni kweli mtoto wao kipenzi, Dkt. Ballali amekufa hivyo ameiomba serikali kuunda tume haraka kuchunguza mazingira ya kifo cha gavana huyo wa zamani.

Alisema moja ya sababu inayowafanya waendelee kuamini kuwa Dkt. Ballali bado mzima ni mazingira ya sasa ya nyumbani kwao kijijini Luganga na nyumbani kwa baba zake wadogo eneo la Ziroziro, Mtwango.

"Nimeishi Mtwango tangu utoto wangu sijawahi hata siku moja kuona nyumba yenye msiba haina waombolezaji nah ii ni dalili ambayo itaendelea kutustua mpaka tutakapothibisha kwa kina", alisema Mzee Samweli

Alisema kwa mujibu wa taratibu za kihehe, msiba unapotokea huombolezwa siku tatu mfululizo ama zaidi ambapo kwa muda huo, majirani hukusanyika nyumbani kwa wafiwa kuwafariji lakini hali hakuwa hivyo baada ya taarifa hizi kufika hapa kijijini.


Aliongeza Mzee huoy "Tunaomba kuelezwa ugonjwa uliosababishia kifo cha mtoto wetu na jitihada zilizofanywa na serikali kuokoa maisha yake... Tunashindwa kuelewa serikali inapotoa pole wakati iliwahi kusema Ballali hajulikani alipo", alisema Mzee Samweli.

Kwa upande wake Mzee Yohanes alisema wanafanya mpango kukutana na ndugu wa marehemu kufanya tambiko la aina yake la kifo hicho na kuomba dua maalum kulaani kifo hicho kama kimetokana na 'mkono wa mtu'.

Mzee huyo, alisema wametoa siku 30 kwa watu waliohusika kwa njia moja ama nyingine na kifo hicho kujisalimisha kijijini hapo, vinginevyo watu hao hawatadumu kwenye nyadhifa zao.

Alisema iwapo kifo hicho kimetokana na mapenzi ya Mungu basi wanamshukuru kwa kutimiza matakwa yake na kama ni kwa mipango ya shetani na wanadamu, basi itashughulikiwa ipasavyo.

Pamoja na mwili huo kuzikwa Marekani, wazee hao wameiomba serikali kufanya kila linalowezekana kuurejesha nchini, ikishindikana waletewe mchanga wa kaburi lake ili wafanye mazishi kwa mujibu wa mila za kihehe, Luganga alikozikwa baba yake mzazi Mzee Timoth Ballali aliyefariki dunia Aprili 3 mwaka 2000.

"Hata kama imeshindika kuleta mwili wake basi wasafirishe mchanga wa kaburi tuje tufanye mazishi kwenye makaburi ya Luganga alipolala baba yake mzazi. Kumzika Marekani ni sawa na kumtenga
 
naona sasa wazee wanataka kuwashitaki waliohusika kwa "nguvu zisizoonekana"
nipo na hamu yakuona kutakuwa hakutoshi kivipi!
 
Tusiwe wepese wa kujumuisha mambo.Hakuna ushahidi kwamba JK alikataa kumrudisha Marehemu Balali.Alichokifanya JK kwa nafasi yake ni kutengua uteuzi wa marehemu kutokana na udhaifu aliounyesha katika kuidhinisha fedha za EPA.Hilo ndilo lililokuwa jukumu lake la msingi baada ya taarifa ya wakaguzi kukabidhiwa kwake.Sasa kwa kuwa mengine ilikuwa ni lazima yafuate mkondo wa kisheria kwa kuzingatia kuwa nchi inaendeshwa kwa misingi ya utawala wa sheria,ilibidi auunde tume kuchunguza makampuni yaliyotajwa na repoti ya wakaguzi kuhusika kuchukua fedha za EPA.Sasa kamati ilishaanza kazi,JK hakuwa na haja tena ya kuingilia majukumu ya kamati.Alichokuwa anasubiri ni kamati kukabidhi repoti kwake.Ni upotoshaki mkubwa kwamba Marekani ilishamuona Balali kama shahidi mkuu.Marekani ni taifa linalozingatia haki na sheria kwa kila raia.Sio rahisi kuropoka vitu wasivyokuwa na uhakika navyo mpaka mamlaka zinazohusika kisheria zithibitihse.Alishosema Balozi ni kwamba "kama wakimuhitaji" hii ni sentensi muhimu kuilielewa,sio kukurupuka tu.Ilikuwa ni maoni ya jumla,sio kwamba kwa kusema hivyo balozi alikuwa anatoa msimamo wa nchi kwamba Balali ni shahidi muhimu.Na majuzi tumesikia taarifa ya Ikulu kwamba kama serikali ingemhitaji isingekuwa shida kumpata.Harafu tusisahau kwamba marehemu Balali alikuwa ni mgonjwa wakati huo.Alikuwa ni mgonjwa kweli kweli.Alikuwa chini ya uangalizi wa madaktari kwa masaa 24 mpaka anafariki dunia.Sasa mtu anapohoji kwa nini JK hakumrudisha mgonjwa nyumbani kutoka kwenye uangalizi wa madaktari,nadhani mtu huyu ana matatizo ya akili kama sio kusukumwa na hisia za jazba sizokuwa na msingi wowote.Tukumbuke JK ni kiongozi wa nchi,sio rais kilabu cha mpira.Hawezi kukurupuka kufanya maamuzi kwa kila anachokisikia kwa lengo la kuwafurahisha baadhi ya watu.Hiyo sio misingi ya utawala wa sheria.

Tom, yawezekana kabisa kuwa na wewe ni mmoja wa wale waliofaidika na pesa za EPA. Huwezi kuingia leoleo JF na kuona wenzio wanarukia wasichokijua! Ina maana wewe hukusikia Mustaffa Mkulo akidai hakumuona, siku hiyo hiyo Rweyemamu anadai ni mtu huru akitakiwa atapatikana! Ina maana wewe huoni walau japo kwa fikra za kawaida kuwa kuna mchezo rafu wa kifo chake ambacho kilitangazwa kwa ukali bila kuhitaji maelezo kikiwa kimechelewa kutangazwa na pia mazingira ya mazishi?

Hebu muweni wazalendo jamani! Balali alikuwa shahidi wa kwanza katika EPA. Mbona kina Mwanyika hawakuwahi kumuhitaji huku tukiambiwa ni mtu huru??
hebu fikiria kwa ubongo wa mbele rafiki.
 
Tom, yawezekana kabisa kuwa na wewe ni mmoja wa wale waliofaidika na pesa za EPA. Huwezi kuingia leoleo JF na kuona wenzio wanarukia wasichokijua! Ina maana wewe hukusikia Mustaffa Mkulo akidai hakumuona, siku hiyo hiyo Rweyemamu anadai ni mtu huru akitakiwa atapatikana! Ina maana wewe huoni walau japo kwa fikra za kawaida kuwa kuna mchezo rafu wa kifo chake ambacho kilitangazwa kwa ukali bila kuhitaji maelezo kikiwa kimechelewa kutangazwa na pia mazingira ya mazishi?

Hebu muweni wazalendo jamani! Balali alikuwa shahidi wa kwanza katika EPA. Mbona kina Mwanyika hawakuwahi kumuhitaji huku tukiambiwa ni mtu huru??
hebu fikiria kwa ubongo wa mbele rafiki.

Halafu maajabu mengine ni kuwa..Mustafa Mkulo na Rweyemamu walisema kuwa serikali haimtafuti Ballali at the same time Mkullo naye akasema eti alimtafuta alipokwenda Washington DC..Sasa alikua akimtafuta kwa niaba yake binafsi ama kwa niaba ya serikali?
Na kama ni kwa niaba ya serikali kwanini then alisema hawamtafuti?
Na vile vile kama ni kwa niaba yake binafsi..Then nia yake ilikuwa ni ipi?
 
Halafu maajabu mengine ni kuwa..Mustafa Mkulo na Rweyemamu walisema kuwa serikali haimtafuti Ballali at the same time Mkullo naye akasema eti alimtafuta alipokwenda Washington DC..Sasa alikua akimtafuta kwa niaba yake binafsi ama kwa niaba ya serikali?
Na kama ni kwa niaba ya serikali kwanini then alisema hawamtafuti?
Na vile vile kama ni kwa niaba yake binafsi..Then nia yake ilikuwa ni ipi?

Asante kwa kuliona hilo. Ukishaona serikali moja ikiwa na mawazo zaidi ya moja yanayopisha yakitolewa na viongozi waandamizi:
(1) Wanatuzuga (2) Hakuna coordination serikalini (3) Kuna mengi yanayojulikana kuhusu tukio moja na hivyo yanayotolewa ni vipande vya hadithi ndefu iliyojaa giza.

Kwa hili la Balali na EPA, tushajua serikali inazuga maana ukweli unawagusa viongozi waandamizi serikalini. Hizi ndo athari za serikali zinazotawala huku zikiwa zimeingia kwa nguvu ya fedha na kiu ya kutawala bila uwezo wa kifikra bali sifa za juu juu na ujanja ujanja mwingi.

Utawala wa awamu ya 4 uamushe na kuibua hisia pevu kwetu sisi wapiga kura. kwamba si utamu wa maneno kwenye majukwaa ya kampeni yatayotufikisha bandarini. Mtu aangaliwe kwa matunda ya kazi yanayoonekana na si uzushi wa ahadi ambazo hazitatekelezwa milele.

Siku JK alipodai atatengeneza ajira milioni 1 kwa mwaka, niliwaeleza wenzangu kuwa, kumbe Rais anaota njozi za alinacha eeh! Si mkweli na mengi ya anayotamka hayatokani na hisia za moyoni ya atakachotekeleza bali anapenda kusema kile ambacho watu wangependa kusikia hata kama hakitekelezeki!

Balali is no more, EPA corruption scandal isnt dead. Kuanzia hapa sasa, wawakilishi wetu bungeni waanze na Waziri wa fedha wakati wa sakata la EPA, katibu mkuu wa wizara, Rais na vimemo vyao..etc..Every culprit should be brought to justice.
 
nyinyi hapa naona mtajiumiza vichwa ! hakikisheni familia zenu zinajaa matumbo kwanza na mna akiba, then ndio muanze mambo ya kufuatilia kwa ukaribu mambo ya taifa. Kuna jamaa mmoja namfahamu ameshakata tamaa hadi hivi sasa, na bahati mbaya hana akiba, yaani ameshakata tamaa kabisaaaaaaaaaaaaa jinsi mambo yalivyo sivyo !
 
nyinyi hapa naona mtajiumiza vichwa ! hakikisheni familia zenu zinajaa matumbo kwanza na mna akiba, then ndio muanze mambo ya kufuatilia kwa ukaribu mambo ya taifa. Kuna jamaa mmoja namfahamu ameshakata tamaa hadi hivi sasa, na bahati mbaya hana akiba, yaani ameshakata tamaa kabisaaaaaaaaaaaaa jinsi mambo yalivyo sivyo !

Mimi ni mmoja wa hao waliokata kata tamaa mpaka tamaa ikatamauka! Maana mlo watoto hawana, na mambo yalivyo ndivyo siyo! Waweza nisaidia nije nipate walau mlo wa leo! Maana ndo maana tukiona EPA na balali kafa, tunakata tamaaa kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa
 
Mimi ni mmoja wa hao waliokata kata tamaa mpaka tamaa ikatamauka! Maana mlo watoto hawana, na mambo yalivyo ndivyo siyo! Waweza nisaidia nije nipate walau mlo wa leo! Maana ndo maana tukiona EPA na balali kafa, tunakata tamaaa kabisaaaaaaaaaaaaaaaaa

hahaaaa, wewe acha zako bana ! jamaa ninayemfahamu amekata tamaa kweli kweli yakhe ! afadhali wewe kidogo una taste ya positive talk, lakini huyu jamaa X kila afikialo ni negative tu !
 
Hivi bunge haliwezi kupiga kura ya kutokuwa na imani na Rais, ili tukaondokana na huu mzigo? 2010 naona ni mbali sana kumuundoa huyu jamaa.

mhm, asije akavunja tu bunge (if possible), na kuwavua wabunge viti maalum. akidai je alichaguliwa na wananchi na sio bunge itakuwaje ? na kama bunge litasema linaweza kumuondoa madarakani then i get the mind kwamba hata yeye anaweza kuwavua ubunge wabunge wote ! (if possible)
 
KM,
Rais wa Tanzania anayo mamlaka ya kulivunja bunge lakini na mwenyewe kujiuzulu wakati huo na kuitisha uchaguzi mpya. Ngoma hiyo!
 
Jamani, Rais hawezi kuvunja bunge kwa kujisikia tu. Hawezi kuamka asubuhi moja na kusema "Bunge sucks" halafu akalivunja.

a. Rais akivunja Bunge na yeye anapoteza Urais wake kwani yeye ni sehemu ya Bunge.
b. Bunge likileta mashtaka dhidi ya Rais na kumvua Urais, Bunge linaendelea kuwepo na Makamu wa Rais anachukua nafasi.
c. Bunge likikataa kupitisha mswada au bajeti ya serikali linaonesha kutokuwa na imani na serikali hivyo Bunge linavunjika, Rais anapoteza Urais na wote wanarudi kwa wananchi. Kwa wanaokumbuka watakumbuka Nyerere aliwahi kuwapiga mkwara wabunge hili kuwa wasipopitisha sheria fulani hivi basi watarudi kwa wananchi.
 
mhm, asije akavunja tu bunge (if possible), na kuwavua wabunge viti maalum. akidai je alichaguliwa na wananchi na sio bunge itakuwaje ? na kama bunge litasema linaweza kumuondoa madarakani then i get the mind kwamba hata yeye anaweza kuwavua ubunge wabunge wote ! (if possible)

Nakupa ushauri tumia kamuda kidogo kuipitia Katiba ya Nchi na iko hapa kwa lugha zote 2 then uje na hoja mkuu.Ndiyo maana ninapinga pia wabunge wa kuteuliwa na Rais na wabinge wa viti maalumu kwamba wafutwe ni mzigo kwa Taifa .
 
Nakupa ushauri tumia kamuda kidogo kuipitia Katiba ya Nchi na iko hapa kwa lugha zote 2 then uje na hoja mkuu.Ndiyo maana ninapinga pia wabunge wa kuteuliwa na Rais na wabinge wa viti maalumu kwamba wafutwe ni mzigo kwa Taifa .

sina muda wa kusoma katiba hadi pale nitakapokuwa na nia ya kugombea uongozi ! nyinyi si mnataka ifanyiwe marekebisho, sasa nipoteze muda wote huo kusoma katiba then ikibadirishwa, muda niliotumia kusoma inakuwaje, muda kwangu muhimu !

sitaki kuisikia hiyo katiba !
 
Jamani, Rais hawezi kuvunja bunge kwa kujisikia tu. Hawezi kuamka asubuhi moja na kusema "Bunge sucks" halafu akalivunja.

.

great, basi napata imani/courage kwamba bunge haliwezi kupiga kura limuondoe rais kama ilivyosemwa na member mwingine hapo juu !
 
Back
Top Bottom