Mwita Maranya
JF-Expert Member
- Jul 1, 2008
- 10,564
- 7,973
Huu mziki umepigwa muda mrefu lakini wenyewe wameamua kukaa kimya labda kutusahaulisha? Tuendelee kuimba au labda kuna Plan C?
Labda hiyo plan C ikipatikana inaweza kusaidia kuwafikisha hawa watuhumiwa mahakamani. Yani unashindwa kushangaa kwamba pamoja na documents zote zilizopo na vyombo vyote vya dola vilivyopo, serikali imeshindwa kabisa hata kuwafungulia mashtaka hawa mapapa na manyangumi.
Nadhani kama atapatikana independent prosecutor, basi angalau kesi inaweza kufunguliwa, vinginevyo tutaendelea kukumbusha hizi hujuma hadi siku tutakapoiondoa ccm madarakani ndipo tutafanikiwa kuwashitaki wezi wetu.