Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,499
- 113,608
Wanabodi.
Naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazotoka kila siku ya Jumatatu kwenye gazeti la Raia Mwema, hili likiwa ni bandiko mwendelezo wa Licha ya CCM kuwa chanzo cha umasikini, ujinga, rushwa na ufisadi, kwanini CCM bado huwa inashinda chaguzi mbalimbali?
Declaration of interest
Kabla sijaendelea, naomba kwanza ku declare interest kuwa japo mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM, mimi ni kada Mzalendo mwenye kutanguliza mbele maslahi ya taifa ndipo cha kinafuata.
Leo naanzia nilipoishia wiki iliyopita, nikiendeleza Makala zangu elimishi Kwa Maslahi ya Taifa, nikizungumzia mambo mbalimbali ya taifa letu. Leo nikiendelea kueleza kwa nini, licha ya kuwa CCM ndio chanzo cha umasikini wa taifa hili, lakini bado ni CCM imeendelea kushinda ushindi wa jumla katika chaguzi mbalimbali hata baada ya Tanzania kuanzisha mfumo wa vyama vingi zaidi ya miaka 25 iliyopita.
Tumefanya chaguzi kuu 5 za vyama vingi, 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na zote CCM imekuwa ikiibuka mshindi, jee kushinda huku kwa CCM, ni kwa sababu CCM inapendwa na inakubalika sana kwa kuwaletea Watanzania maendeleo haya yaliyopo. Pia CCM inashinda kwa kukosekana kwa upinzani imara na madhubuti. Pia CCM inashinda kwa sababu ya mazoea tuu ya Watanzania, kutokana na elimu duni ya mpiga kura, na umasikini, uliotopea, hivyo wapiga kura wengi wa Tanzania kujikuta hawana uwezo wa kufanya informed decision?.
Tanzania tulipoingia mfumo wa vyama vingi, tuliuparamia tuu, bila kujiandaa kimawazo, kimifumo na kisheria, kuwa nchi ya vyama vingi, hivyo tumeingia kuwa nchi ya vyama vingi, kwa kubadili tuu katiba, bila kubadili mifumo, sheria na mitazamo, matokeo yake, tumeanzisha vyama vingi ndani ya set up ya mfumo wa chama kimoja, huku CCM kikiendelea kuwa chama dola CCM, na vyama vingine vikaanzishwa kushindana na chama dola.
1. Hoja ya kwanza, ni kutoka kwa wana CCM wenyewe kuwa CCM inashinda kwa sababu CCM ndicho chama pekee kilichotapakaa nchi nzima hadi vijijini, na kinapendwa na Watanzania, na kimekubalika kwa kuwaletea Watanzania maendeleo, nitaeleza kidogo kupendwa huku kwa CCM ni kupendwa gani, na hayo maendeleo CCM iliyoyaleta ni maendeleo gani.
2. Lakini sababu halisi ya CCM kuendelea kushinda chaguzi mbali mbali kwa mtizamo wangu kada mimi, sio kwa sababu tuu CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa kuwaletea Watanzania maendeleo kiduchu haya, bali CCM inashinda na kuendelea kushinda kwa sababu, Tanzania bado tuko kwenye setup ya mfumo wa Chama kimoja, na CCM bado ni chama dola, chama bado ndio kimeshika hatamu za uongozi wa nchi hii, hivyo bila kubadili setup ya mfumo wa chama kimoja na kwenda kwenye setup ya mfumo wa vyama vingi, iliwemo kukiondoa chama dola kwenye mindset ya Watanzania, CCM itaendelea kushinda na kutawala nchi hii kwa miaka mingi ijayo, iliwemo kushinda kwa kishindo uchaguzi mkuu wa 2020 and in fact, CCM itatawala milele!.
3. CCM ni chama tajiri, ambapo kimeanzishwa kwa ku loot mali za Watanzania. Tulipoanzisha vyama vingi ilibidi CCM kivunjwe kwanza, na zile mali za CCM, zilizotokana na michango ya lazima ya Watanzania wote, yakiwemo majengo ya serikali, viwanja vya umma ambavyo CCM ilivimiliki wakati wa mfumo wa Chama kimoja, vilipaswa virudishwe serikalini na kuwa mali ya umma, CCM ianze moja kwa mali zake halali tuu, kama vyama vingine, lakini kitendo cha CCM kusajiliwa hivyo hivyo kilivyo na ukwasi mkubwa wa loot ya Watanzania, hakuna Chama cha kushindana na CCM na kuingia ikulu!.
4. Mind set ya vyombo vyote vya kiutendaji na kiutawala, iko ki CCM CCM tuu, kuanzia Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, vyombo vya dola, na watendaji wa vyombo vingine vyote vya kiutendaji, akiwemo Msajili wa vyama vya Siasa, wote wako ki CCM, CCM!. Mimi sisemi kuwa NEC sio tume huru, NEC ni Tume Huru ila sio inclusive. Japo uchaguzi unaendeshwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni za tume huru, lakini kwa vile NEC kuanzia Mwenyekiti wake, Mkurugenzi, makamishna, na wakurugenzi wote wa halmashauri ambao ndio wasimamizi wa uchaguzi, wanateuliwa na Mwenyekiti wa chama kimoja wapo, kuna uwezekano akateua makada watupu wa CCM, hivyo zoezi la uchaguzi kuendeshwa kwa ukada ukada zaidi kuliko utendaji ndio maana kuna watu wa chama kimoja wanapewa barua za utambulisho, watu wa chama kingine wananyimwa!. Kama mtu kama Jaji Mkuu wa Tanzania, anakwenda kugombea urais CCM, au CDF mstaafu!, hii maana yake hawa ni makada!. Kinachotakiwa kufanyika ni kubadili set up ya NEC iwe inclusive na kubadili sheria ya uchunguzi kipengele cha wasimamizi wa uchaguzi wasiwe makada, watafutwe watu waadilifu ambao ni neutral kabisa kuongoza NEC, na Ofisi ya Msajili wa vyama, na makamisha kufanyike ushirikishwa wa wadau katika composition yao, nafasi za usimamizi wa uchaguzi zitangazwe wenye sifa waombe na sio makada wateuliwa na mmoja wa wagombea ili neutrality sio tuu ionekane bali kuonekana ikitendeka. Pia tubadili sheria zetu za uchaguzi ziwe za haki.
5. CCM imejikita Vijijini, Wapinzani Wamejikita mijini, vijijini ndiko kwenye kura za uamuzi, yaani decisive votes, kutokana na ukongwe wa CCM ambacho kilikuwa chama dola kilichoenea nchi nzima kwa mujibu wa sheria, kuanzia wajumbe wa nyumba kumi, mashina, matawi nchi wamesambaa nchi nzima, kutokana na utajiri wa CCM, CCM ndicho chama pekee chenye uwezo wa kuwa na ofisi nchi mzima, tena sio ofisi moja, bali ni ofisi nne kwenye baadhi ya maeneo, ofisi ya CCM, ofisi ya UVCC, ofisi ya UWT, na ofisi ya Jumuiya ya Wazazi, ambako kote huko kuna maofisa wanaolipwa mishahara, wakati ofisi za vyama vya upinzani ni watu wanajitolea nyumba zao na wanavitumikia vyama hivyo kwa mapenzi yao tuu bila kulipwa chochote!, hivyo chochote ambacho CCM inakipanga kinawafikia wananchi wa chini, na wakati wa kampeni, kama CCM inawafikia Watanzania, ni wengi zaidi vijijini na ndiko kwenye kura za ushindi, kwa sababu CCM imewafikia, lakini akitokea mpinzani kusema ukweli, ukweli huu huishia mijini tuu, msihadaiwe na wingi wa watu kwenye mikutano ya kampeni za mijini, hizo sio kura, kura za kweli ziko vijijini hivyo kwa mazingira haya, huwezi kushindana na CCM, ukaishinda.
6. Ukosefu wa elimu ya uraia kwa Watanzania, tangu tumeanzisha mfumo wa vyama vingi, hakujawahi kutoa elimu yoyote ya uraia, kuwaelimisha Watanzania umuhimu wa uwepo wa vyama vingi, hivyo waliowengi wamedanganywa kuwa vyama vya upinzani vinakuja kuharibu umoja wetu kuleta fujo na kuhatarisha amani yetu na utulivu, sasa ukiwasikia viongozi wa upinzani wanavyoongea kwa jazba, na vyama vyenyewe ni vya kiharakati, vingine na sare za kijeshi jeshi, Watanzania wapenda amani, wanaogopa kuviamini. Ingetolewa elimu rasmi ya uraia na kuwafikia Watanzania wote, na Tanzania ikawa na vyama serious vya upinzani wa kweli, na Watanzania wakaelimishwa siku nyingi CCM ingeisha pumzishwa kwa amani!, hakuna mtu yoyote anayependa kula mboga moja siku zote!, Watanzania wangependa sana kubadili mboga, tatizo ni hakuna hata hiyo mboga ya kubadilisha!.
7. Umasikini uliotopea, ambao pia pia unakwenda sambamba na ujinga. Mtu masikini wa kipato, chakula cha shida, mlo mmoja kwa siku, anaishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, akili yake pia inadumaa. Mtu kama huyu shida yake ni mlo, na mavazi, sasa akiletewa ile Tshirt na kofia, na pilau ya siku moja, inatosha kabisa kukichagua chama kilichokulisha na kukuvisha, anakuwa hana uwezo kusikiliza sera na kufanya informed decisions, angalieni maeneo yenye umasikini uliotopea na elimu duni ndio strong holds za CCM. Mikoa yenye ehueni kiuchumi kama Arusha, Kilimanjaro, Bukoba, Iringa, Mbeya. Tanga na maeneo ya mijini, watu walioelimika, kidogo wanaweza kuchagua upinzani, lakini mikoa yenye umasikini wa kutupa kama Dodoma, etc, usitegemee upinzani unaweza kushinda!, shida ya masikini ni njaa tuu, CCM ndicho chama kinachoongoza kwa kugawa rushwa, ushahidi wa kazi nzuri iliyofanywa na fedha za Kagoda upo!. Hivyo CCM kuutumia umasikini wa Watanzania na Ujinga wa Watanzania kama mtaji wake wa Ushindi.
8. CCM inaendelea kushinda kwa sababu, uwanja wetu wa mashindano ya siasa ni uwanja tenge ambao umelalia upande wa CCM, ni kama kugombea kisu cha makali kuwili, halafu mgombea mmoja ameshika kwenye mpini, na mwingine kwenye makali. Vyombo vyote vinaipendelea CCM, kuanzia mfumo uliopo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, vyombo vya dola, huku mgombea mmoja mwenye ving'ora na kila kitu, JWTZ, Polisi, ukwasi mkubwa, ameishika dola na kuitoa igombewe na wengine wasio na kitu kabisa!.
9. CCM inaendelea kushinda kwa sababu Tanzania bado hatuna upinzani Imara, huu upinzani uliopo sasa ni upinzani uchwala, upinzani lege lege, hivyo kamwe hauwezi kushinda kushika dola hivi hivi ulivyo. Mimi nakubaliana kabisa na hoja ya Baba wa Taifa kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM!, huu upinzani dhaifu uliopo sasa, na utitiri wa vyama, vyama vya kiharakati, hauwezi kuwapeka wapinzani ikulu. Kujiengua kwa Lowassa kutoka CCM ile 2015, na kujiunga upinzani, ndiko kulikoupatia upinzani mafanikio makubwa kabisa katika upinzani nchini Tanzania, tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi, ingekuwa sio hali ya afya ya Lowassa, wafuasi wake na wale wote wenye Imani na Lowassa wangemfuata!, CCM ingepigwa chini!. Kama kwa hali ile tuu alivyo, ameweza kuvuna kura milioni 6, ambazo ni nyingi kuliko zilizomrudisha Kikwete ile 2010, tena kwa taarifa tuu, kwa upande wa Zanzibar, Lowassa ndio aliyepata kura nyingi kuliko Magufuli, kwa mujibu wa matokeo ya NEC, hivyo Zanzibar CCM ilipigwa chini!, hivyo kama Lowassa angekuwa fiti kabisa kiafya na hana mazongezonge ya ufisadi, amini usiamini, CCM ingepigwa chini ile 2015.
10. Wapinzani hawana sera, wala hawajui wanatakiwa kufanya nini, upinzani wa kweli, unapaswa kuonyesha sera mbadala na CCM, mfano sera ya elimu ya CCM ni elimu bure kutoka darasa la kwanza hadi kidato cha nne, upinzani wao wakasema sera yao ni elimu bure toka chekechea hadi chuo kikuu. Hapa wangekuwa ni wapinzani makini, sera hii tuu ingetosha kuipiga chini CCM!. Au sera ya Afya bure. Wapinzani hawakupaswa kuishia kusema maneno matupu tuu ya elimu bure hadi chuo kikuu, walipaswa kuja na roadmap ya how?. Wangewaeleza Watanzania watabana wapi matumizi ili kupata kupata fedha za kugharimia elimu bure, kwa kuainisha ufisadi wa serikali ya CCM, mfano kusema utaunda baraza dogo tuu la mawaziri lenye wizara 10, hizi zitaokoa kiasi hiki ambacho kitapelekwa kwenye elimu. Au kujumlisha jumla ya fedha zote zilizofujwa na CCM kwenye ufisadi wa EPA, Deep Green, Meremeta, Escrow, etc na kuonyesha jinsi ambavyo zingetumika kugharimia afya na elimu bure, ili kuwapa Watanzania chaguo mbadala!.
Hitimisho
Ujio wa Dr. John Pombe Joseph Magufuli kama rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM, hii sasa ndio funga kazi!. Kwanza huyu jamaa ni mchapakazi kweli kweli hivyo ataimarisha CCM na kuufifisha upinzani, hivyo uchaguzi wa 2020, upinzani hautafurukuta, tunairejelesha Tanzania chini ya mfumo usio rasmi wa chama kimoja cha siasa, japo jina la Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, litaendelea, na vyama vya upinzani vitaendelea kuwepo, vitakuwa vipo kama havipo, na CCM ikiimarika kabisa Kiuchumi 2020-2025, kuna uwezekano ruzuku kwa vyama vya siasa ikafutwa, hivyo chama kubakia CCM pekee!.
Nawatakia Furahi Dei Njema
Wasalaam
Paskali
Naendelea na zile makala zangu za Kwa Maslahi ya Taifa, zinazotoka kila siku ya Jumatatu kwenye gazeti la Raia Mwema, hili likiwa ni bandiko mwendelezo wa Licha ya CCM kuwa chanzo cha umasikini, ujinga, rushwa na ufisadi, kwanini CCM bado huwa inashinda chaguzi mbalimbali?
Declaration of interest
Kabla sijaendelea, naomba kwanza ku declare interest kuwa japo mimi ni kada wa Chama cha Mapinduzi, CCM, mimi ni kada Mzalendo mwenye kutanguliza mbele maslahi ya taifa ndipo cha kinafuata.
Leo naanzia nilipoishia wiki iliyopita, nikiendeleza Makala zangu elimishi Kwa Maslahi ya Taifa, nikizungumzia mambo mbalimbali ya taifa letu. Leo nikiendelea kueleza kwa nini, licha ya kuwa CCM ndio chanzo cha umasikini wa taifa hili, lakini bado ni CCM imeendelea kushinda ushindi wa jumla katika chaguzi mbalimbali hata baada ya Tanzania kuanzisha mfumo wa vyama vingi zaidi ya miaka 25 iliyopita.
Tumefanya chaguzi kuu 5 za vyama vingi, 1995, 2000, 2005, 2010, 2015 na zote CCM imekuwa ikiibuka mshindi, jee kushinda huku kwa CCM, ni kwa sababu CCM inapendwa na inakubalika sana kwa kuwaletea Watanzania maendeleo haya yaliyopo. Pia CCM inashinda kwa kukosekana kwa upinzani imara na madhubuti. Pia CCM inashinda kwa sababu ya mazoea tuu ya Watanzania, kutokana na elimu duni ya mpiga kura, na umasikini, uliotopea, hivyo wapiga kura wengi wa Tanzania kujikuta hawana uwezo wa kufanya informed decision?.
Tanzania tulipoingia mfumo wa vyama vingi, tuliuparamia tuu, bila kujiandaa kimawazo, kimifumo na kisheria, kuwa nchi ya vyama vingi, hivyo tumeingia kuwa nchi ya vyama vingi, kwa kubadili tuu katiba, bila kubadili mifumo, sheria na mitazamo, matokeo yake, tumeanzisha vyama vingi ndani ya set up ya mfumo wa chama kimoja, huku CCM kikiendelea kuwa chama dola CCM, na vyama vingine vikaanzishwa kushindana na chama dola.
1. Hoja ya kwanza, ni kutoka kwa wana CCM wenyewe kuwa CCM inashinda kwa sababu CCM ndicho chama pekee kilichotapakaa nchi nzima hadi vijijini, na kinapendwa na Watanzania, na kimekubalika kwa kuwaletea Watanzania maendeleo, nitaeleza kidogo kupendwa huku kwa CCM ni kupendwa gani, na hayo maendeleo CCM iliyoyaleta ni maendeleo gani.
2. Lakini sababu halisi ya CCM kuendelea kushinda chaguzi mbali mbali kwa mtizamo wangu kada mimi, sio kwa sababu tuu CCM inapendwa sana na inakubalika sana kwa kuwaletea Watanzania maendeleo kiduchu haya, bali CCM inashinda na kuendelea kushinda kwa sababu, Tanzania bado tuko kwenye setup ya mfumo wa Chama kimoja, na CCM bado ni chama dola, chama bado ndio kimeshika hatamu za uongozi wa nchi hii, hivyo bila kubadili setup ya mfumo wa chama kimoja na kwenda kwenye setup ya mfumo wa vyama vingi, iliwemo kukiondoa chama dola kwenye mindset ya Watanzania, CCM itaendelea kushinda na kutawala nchi hii kwa miaka mingi ijayo, iliwemo kushinda kwa kishindo uchaguzi mkuu wa 2020 and in fact, CCM itatawala milele!.
3. CCM ni chama tajiri, ambapo kimeanzishwa kwa ku loot mali za Watanzania. Tulipoanzisha vyama vingi ilibidi CCM kivunjwe kwanza, na zile mali za CCM, zilizotokana na michango ya lazima ya Watanzania wote, yakiwemo majengo ya serikali, viwanja vya umma ambavyo CCM ilivimiliki wakati wa mfumo wa Chama kimoja, vilipaswa virudishwe serikalini na kuwa mali ya umma, CCM ianze moja kwa mali zake halali tuu, kama vyama vingine, lakini kitendo cha CCM kusajiliwa hivyo hivyo kilivyo na ukwasi mkubwa wa loot ya Watanzania, hakuna Chama cha kushindana na CCM na kuingia ikulu!.
4. Mind set ya vyombo vyote vya kiutendaji na kiutawala, iko ki CCM CCM tuu, kuanzia Tume ya Taifa ya Uchaguzi, NEC, Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa, vyombo vya dola, na watendaji wa vyombo vingine vyote vya kiutendaji, akiwemo Msajili wa vyama vya Siasa, wote wako ki CCM, CCM!. Mimi sisemi kuwa NEC sio tume huru, NEC ni Tume Huru ila sio inclusive. Japo uchaguzi unaendeshwa kwa mujibu wa sheria taratibu na kanuni za tume huru, lakini kwa vile NEC kuanzia Mwenyekiti wake, Mkurugenzi, makamishna, na wakurugenzi wote wa halmashauri ambao ndio wasimamizi wa uchaguzi, wanateuliwa na Mwenyekiti wa chama kimoja wapo, kuna uwezekano akateua makada watupu wa CCM, hivyo zoezi la uchaguzi kuendeshwa kwa ukada ukada zaidi kuliko utendaji ndio maana kuna watu wa chama kimoja wanapewa barua za utambulisho, watu wa chama kingine wananyimwa!. Kama mtu kama Jaji Mkuu wa Tanzania, anakwenda kugombea urais CCM, au CDF mstaafu!, hii maana yake hawa ni makada!. Kinachotakiwa kufanyika ni kubadili set up ya NEC iwe inclusive na kubadili sheria ya uchunguzi kipengele cha wasimamizi wa uchaguzi wasiwe makada, watafutwe watu waadilifu ambao ni neutral kabisa kuongoza NEC, na Ofisi ya Msajili wa vyama, na makamisha kufanyike ushirikishwa wa wadau katika composition yao, nafasi za usimamizi wa uchaguzi zitangazwe wenye sifa waombe na sio makada wateuliwa na mmoja wa wagombea ili neutrality sio tuu ionekane bali kuonekana ikitendeka. Pia tubadili sheria zetu za uchaguzi ziwe za haki.
5. CCM imejikita Vijijini, Wapinzani Wamejikita mijini, vijijini ndiko kwenye kura za uamuzi, yaani decisive votes, kutokana na ukongwe wa CCM ambacho kilikuwa chama dola kilichoenea nchi nzima kwa mujibu wa sheria, kuanzia wajumbe wa nyumba kumi, mashina, matawi nchi wamesambaa nchi nzima, kutokana na utajiri wa CCM, CCM ndicho chama pekee chenye uwezo wa kuwa na ofisi nchi mzima, tena sio ofisi moja, bali ni ofisi nne kwenye baadhi ya maeneo, ofisi ya CCM, ofisi ya UVCC, ofisi ya UWT, na ofisi ya Jumuiya ya Wazazi, ambako kote huko kuna maofisa wanaolipwa mishahara, wakati ofisi za vyama vya upinzani ni watu wanajitolea nyumba zao na wanavitumikia vyama hivyo kwa mapenzi yao tuu bila kulipwa chochote!, hivyo chochote ambacho CCM inakipanga kinawafikia wananchi wa chini, na wakati wa kampeni, kama CCM inawafikia Watanzania, ni wengi zaidi vijijini na ndiko kwenye kura za ushindi, kwa sababu CCM imewafikia, lakini akitokea mpinzani kusema ukweli, ukweli huu huishia mijini tuu, msihadaiwe na wingi wa watu kwenye mikutano ya kampeni za mijini, hizo sio kura, kura za kweli ziko vijijini hivyo kwa mazingira haya, huwezi kushindana na CCM, ukaishinda.
6. Ukosefu wa elimu ya uraia kwa Watanzania, tangu tumeanzisha mfumo wa vyama vingi, hakujawahi kutoa elimu yoyote ya uraia, kuwaelimisha Watanzania umuhimu wa uwepo wa vyama vingi, hivyo waliowengi wamedanganywa kuwa vyama vya upinzani vinakuja kuharibu umoja wetu kuleta fujo na kuhatarisha amani yetu na utulivu, sasa ukiwasikia viongozi wa upinzani wanavyoongea kwa jazba, na vyama vyenyewe ni vya kiharakati, vingine na sare za kijeshi jeshi, Watanzania wapenda amani, wanaogopa kuviamini. Ingetolewa elimu rasmi ya uraia na kuwafikia Watanzania wote, na Tanzania ikawa na vyama serious vya upinzani wa kweli, na Watanzania wakaelimishwa siku nyingi CCM ingeisha pumzishwa kwa amani!, hakuna mtu yoyote anayependa kula mboga moja siku zote!, Watanzania wangependa sana kubadili mboga, tatizo ni hakuna hata hiyo mboga ya kubadilisha!.
7. Umasikini uliotopea, ambao pia pia unakwenda sambamba na ujinga. Mtu masikini wa kipato, chakula cha shida, mlo mmoja kwa siku, anaishi kwa kipato cha chini ya dola moja kwa siku, akili yake pia inadumaa. Mtu kama huyu shida yake ni mlo, na mavazi, sasa akiletewa ile Tshirt na kofia, na pilau ya siku moja, inatosha kabisa kukichagua chama kilichokulisha na kukuvisha, anakuwa hana uwezo kusikiliza sera na kufanya informed decisions, angalieni maeneo yenye umasikini uliotopea na elimu duni ndio strong holds za CCM. Mikoa yenye ehueni kiuchumi kama Arusha, Kilimanjaro, Bukoba, Iringa, Mbeya. Tanga na maeneo ya mijini, watu walioelimika, kidogo wanaweza kuchagua upinzani, lakini mikoa yenye umasikini wa kutupa kama Dodoma, etc, usitegemee upinzani unaweza kushinda!, shida ya masikini ni njaa tuu, CCM ndicho chama kinachoongoza kwa kugawa rushwa, ushahidi wa kazi nzuri iliyofanywa na fedha za Kagoda upo!. Hivyo CCM kuutumia umasikini wa Watanzania na Ujinga wa Watanzania kama mtaji wake wa Ushindi.
8. CCM inaendelea kushinda kwa sababu, uwanja wetu wa mashindano ya siasa ni uwanja tenge ambao umelalia upande wa CCM, ni kama kugombea kisu cha makali kuwili, halafu mgombea mmoja ameshika kwenye mpini, na mwingine kwenye makali. Vyombo vyote vinaipendelea CCM, kuanzia mfumo uliopo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi NEC, vyombo vya dola, huku mgombea mmoja mwenye ving'ora na kila kitu, JWTZ, Polisi, ukwasi mkubwa, ameishika dola na kuitoa igombewe na wengine wasio na kitu kabisa!.
9. CCM inaendelea kushinda kwa sababu Tanzania bado hatuna upinzani Imara, huu upinzani uliopo sasa ni upinzani uchwala, upinzani lege lege, hivyo kamwe hauwezi kushinda kushika dola hivi hivi ulivyo. Mimi nakubaliana kabisa na hoja ya Baba wa Taifa kuwa upinzani wa kweli utatoka CCM!, huu upinzani dhaifu uliopo sasa, na utitiri wa vyama, vyama vya kiharakati, hauwezi kuwapeka wapinzani ikulu. Kujiengua kwa Lowassa kutoka CCM ile 2015, na kujiunga upinzani, ndiko kulikoupatia upinzani mafanikio makubwa kabisa katika upinzani nchini Tanzania, tangu kuanza kwa mfumo wa vyama vingi, ingekuwa sio hali ya afya ya Lowassa, wafuasi wake na wale wote wenye Imani na Lowassa wangemfuata!, CCM ingepigwa chini!. Kama kwa hali ile tuu alivyo, ameweza kuvuna kura milioni 6, ambazo ni nyingi kuliko zilizomrudisha Kikwete ile 2010, tena kwa taarifa tuu, kwa upande wa Zanzibar, Lowassa ndio aliyepata kura nyingi kuliko Magufuli, kwa mujibu wa matokeo ya NEC, hivyo Zanzibar CCM ilipigwa chini!, hivyo kama Lowassa angekuwa fiti kabisa kiafya na hana mazongezonge ya ufisadi, amini usiamini, CCM ingepigwa chini ile 2015.
10. Wapinzani hawana sera, wala hawajui wanatakiwa kufanya nini, upinzani wa kweli, unapaswa kuonyesha sera mbadala na CCM, mfano sera ya elimu ya CCM ni elimu bure kutoka darasa la kwanza hadi kidato cha nne, upinzani wao wakasema sera yao ni elimu bure toka chekechea hadi chuo kikuu. Hapa wangekuwa ni wapinzani makini, sera hii tuu ingetosha kuipiga chini CCM!. Au sera ya Afya bure. Wapinzani hawakupaswa kuishia kusema maneno matupu tuu ya elimu bure hadi chuo kikuu, walipaswa kuja na roadmap ya how?. Wangewaeleza Watanzania watabana wapi matumizi ili kupata kupata fedha za kugharimia elimu bure, kwa kuainisha ufisadi wa serikali ya CCM, mfano kusema utaunda baraza dogo tuu la mawaziri lenye wizara 10, hizi zitaokoa kiasi hiki ambacho kitapelekwa kwenye elimu. Au kujumlisha jumla ya fedha zote zilizofujwa na CCM kwenye ufisadi wa EPA, Deep Green, Meremeta, Escrow, etc na kuonyesha jinsi ambavyo zingetumika kugharimia afya na elimu bure, ili kuwapa Watanzania chaguo mbadala!.
Hitimisho
Ujio wa Dr. John Pombe Joseph Magufuli kama rais wa JMT na Mwenyekiti wa CCM, hii sasa ndio funga kazi!. Kwanza huyu jamaa ni mchapakazi kweli kweli hivyo ataimarisha CCM na kuufifisha upinzani, hivyo uchaguzi wa 2020, upinzani hautafurukuta, tunairejelesha Tanzania chini ya mfumo usio rasmi wa chama kimoja cha siasa, japo jina la Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, litaendelea, na vyama vya upinzani vitaendelea kuwepo, vitakuwa vipo kama havipo, na CCM ikiimarika kabisa Kiuchumi 2020-2025, kuna uwezekano ruzuku kwa vyama vya siasa ikafutwa, hivyo chama kubakia CCM pekee!.
Nawatakia Furahi Dei Njema
Wasalaam
Paskali