Joannah
JF-Expert Member
- May 8, 2020
- 18,813
- 43,204
Moral of the story unaogopa chura,ila nyie wakaka wa siku hizi😁😁😁😁Mwaka Jana nlisafiri masika nkaenda kulima bush,basi nkakaa kama wiki mbili,Ile narudi usiku mechoka balaa nkajitupa kitandani na viatu nkaanza kuota kama nipo mtoni naskia sauti za vyura,ila Ile sauti ikawa kama inatokea kichwani mwangu,dakika Moja nyingi nkakurupuka Kumbe frog yupo chini ya kitanda.
Yaani wenge lote la usingizi likakata nkawa najiuliza kaingilia wapi au niwa kutumwa,nikagundua alipitia chini ya mlango palipokuwa na uwazi.
Sasa mawazo yakazidi kuwa kama kaingia chura ,nyoka atashindwaje,nikatoka nkaenda lala Kwa mshkaji kesho yake nikafanya famigesheni huwezi amini Ili kuwa kama zoo ya wadudu maana walitoka wengine hata siwafahamu.