Runner
Member
- Feb 7, 2011
- 85
- 13
Habari wapendwa wa JF, nimekaa nikafikiria sana hili swala nikaona bora niliweke jamvini tupeane mchango. Unakuta umeoa na mwanamke alikuwa anakutegemea kwa kila kitu ingawa kuwa nae anafanyaka kazi, mmeendelea na maisha ya kila siku lakini ikaja ikatokea kuwa mwanamke akapata mkopo ofisini kwao ambao ukiulinganisha na ile niliyokuwa nampatia kiukweli mkopo ni mkubwa kiasi chake, sasa kinachokuja hapa ni kwamba "BAADA YA KUPATA MKOPO AMEKUWA MTU WA NYODO, JEURI, MANENO YA KASHFA NA MAJIVUNO".
Hata nikisema nimuulize lolote atanijibu kwa mkato......na mbaya zaidi sasa hivi tunaishi kama kaka na dada............,na mara ya kwanza alikuwa nawahi sana kurudi nyumbani lakini baada ya hiyo pesa kurudi kwake nyumbani ni saa 3 usiku?......
Naomba wana JF mniambie hapa huwa inakuaje kwenye hili? Maana mimi nimeamua kuwa kimya bila kuzungumza chochote.....mbaya zaidi amekuwa busy na simu anaweza ku-chat hata mpaka saa 6 za usiku, wakati mara ya kwanza mm nikitumiwa sms hata moja saa 3 usiku ilikuwa ugomvi ntaambiwa niwaambie hao watu wasinisumbue nipo na mke wangu.
Lakini leo yeye ndo amekuwa kinara wa kuchat, nikimwabia najibiwa "KILA MTU ANA UHURU WAKE WA SIMU",.........Wapendwa wa JF maneno ninayo mengi sana lakini kwa haya niliyoyatoa naamini mtakuwa mmepata picha halisi............NAWASILISHA
Hata nikisema nimuulize lolote atanijibu kwa mkato......na mbaya zaidi sasa hivi tunaishi kama kaka na dada............,na mara ya kwanza alikuwa nawahi sana kurudi nyumbani lakini baada ya hiyo pesa kurudi kwake nyumbani ni saa 3 usiku?......
Naomba wana JF mniambie hapa huwa inakuaje kwenye hili? Maana mimi nimeamua kuwa kimya bila kuzungumza chochote.....mbaya zaidi amekuwa busy na simu anaweza ku-chat hata mpaka saa 6 za usiku, wakati mara ya kwanza mm nikitumiwa sms hata moja saa 3 usiku ilikuwa ugomvi ntaambiwa niwaambie hao watu wasinisumbue nipo na mke wangu.
Lakini leo yeye ndo amekuwa kinara wa kuchat, nikimwabia najibiwa "KILA MTU ANA UHURU WAKE WA SIMU",.........Wapendwa wa JF maneno ninayo mengi sana lakini kwa haya niliyoyatoa naamini mtakuwa mmepata picha halisi............NAWASILISHA