GM7
JF-Expert Member
- Jun 26, 2009
- 492
- 24
Ishu ni zilezile kila siku ila zinakuwa na staili tofauti. Hebu tusome kisa hiki halafu tuendelee kujadili mada,
Sasa siku moja kulitokea matatizo fulani kazini kwa kaka huyo na ikabidi apewe barua ya kusimamishwa kazi wakati uchunguzi ukiendelea huko kazini. Kwa kipindi hicho cha kusimamishwa kazi kama unavyojua mwanaume lazima uhangaike. Katika kuhangaika kaka huyo akabahatika kupata sehemu ya kujishikiza kwa muda wakati suala lake likiendelea kushughulikiwa. Kwa bahati nzuri au mbaya kazi aliyopata kwa muda inafanyika hadi usiku.
Siku moja akiwa kazini masaa ya usiku kulikuwa hakuna kazi na wafanyakazi wakaambiwa watafute usafiri warudi nyumbani. Baadaye akatafuta usafiri anaoujua yeye na akafanikiwa kufika nyumbani.
Sasa ishu yenyewe inaanzia hapa.
Huyo kaka akafika hapo nyumbani alipopanga na akaanza kumgongea mke wake mlango ili amfungulie. Mke akawa hafungui mlango, mara baadaye wakaanza kujibizana kwa muda mrefu na mke wake. Baadaye akaja mpangaji mwenzake kumsaidia huyo kaka. Hatimaye akafungua mlango. Alipofungua tu mlango kumbe kulikuwa na lijamaa linajiexpress na mke humo ndani, halafu lijamaa likaamua kuondoka.
Baada ya hapo huyo kaka akaamua kumuacha mke wake hapo hapo na kwenda kulala nje ya nyumba. Sijui alilala gesti. Akamwambia mke wake utabaki na huyo huyo (lijamaa). Huyo kaka hakurudi tena hapo nyumbani. Bila shaka alibaki kazini maana kazi yenyewe ni ya mchana na usiku.
Lakini baada ya takribani wiki moja hivi baada ya tukio. Huyo kaka aliyesimamishwa kazi akarudishwa kazini. Mke naye aliposikia kuwa mme wake aliyekuwa amesimamishwa kazi amerudishwa kazini, eti akaenda kwa mume wake kumwomba msamaha kwa yaliyotokea nyumbani.
Kwa nini wanawake mko hivi?????????????
Tuendelee kuchangia mada
;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;;
Kuna kaka mmoja ameoa na ana mke na mtoto wa mwaka mmoja na nusu hivi. Kaka huyo amebahatika kupata kazi nzuri na ana kipato kikubwa tu kinachoweza kukidhi mahitaji ya familia hiyo.Sasa siku moja kulitokea matatizo fulani kazini kwa kaka huyo na ikabidi apewe barua ya kusimamishwa kazi wakati uchunguzi ukiendelea huko kazini. Kwa kipindi hicho cha kusimamishwa kazi kama unavyojua mwanaume lazima uhangaike. Katika kuhangaika kaka huyo akabahatika kupata sehemu ya kujishikiza kwa muda wakati suala lake likiendelea kushughulikiwa. Kwa bahati nzuri au mbaya kazi aliyopata kwa muda inafanyika hadi usiku.
Siku moja akiwa kazini masaa ya usiku kulikuwa hakuna kazi na wafanyakazi wakaambiwa watafute usafiri warudi nyumbani. Baadaye akatafuta usafiri anaoujua yeye na akafanikiwa kufika nyumbani.
Sasa ishu yenyewe inaanzia hapa.
Huyo kaka akafika hapo nyumbani alipopanga na akaanza kumgongea mke wake mlango ili amfungulie. Mke akawa hafungui mlango, mara baadaye wakaanza kujibizana kwa muda mrefu na mke wake. Baadaye akaja mpangaji mwenzake kumsaidia huyo kaka. Hatimaye akafungua mlango. Alipofungua tu mlango kumbe kulikuwa na lijamaa linajiexpress na mke humo ndani, halafu lijamaa likaamua kuondoka.
Baada ya hapo huyo kaka akaamua kumuacha mke wake hapo hapo na kwenda kulala nje ya nyumba. Sijui alilala gesti. Akamwambia mke wake utabaki na huyo huyo (lijamaa). Huyo kaka hakurudi tena hapo nyumbani. Bila shaka alibaki kazini maana kazi yenyewe ni ya mchana na usiku.
Lakini baada ya takribani wiki moja hivi baada ya tukio. Huyo kaka aliyesimamishwa kazi akarudishwa kazini. Mke naye aliposikia kuwa mme wake aliyekuwa amesimamishwa kazi amerudishwa kazini, eti akaenda kwa mume wake kumwomba msamaha kwa yaliyotokea nyumbani.
::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::::
Sasa kilichoendelea hapo mimi sijui. Hebu sisi tuendelee kujadili hii mada. Kwanini wewe mwanamke unamthamini mmeo wakati ana kazi au kipato kizuri, halafu ikitokea bahati mbaya kama hiyo unaona mmeo hana thamani. Ina maana upendo wako uko kwenye pesa tu????????????????Kwa nini wanawake mko hivi?????????????
Tuendelee kuchangia mada