huwezi amini mie nilienda msibani badala ya kumlilia yule merehemu nikawa nakumbuka kifo cha rafiki yangu mpenzi na kubwaga chozi has ,lakini jibu ndo hilo kila mtu analia kwa sababu zake
Saa zingine akiishafariki mtu wako wa karibu unakuwa unaona hakuna zaidi ya hapoJamani mimi nilikuwa nalia sana misibani, ila tangu nimemjua Mungu sipati machozi kabisa. Sometimes watu wanashangaa kwa nini sipati machozi. Sina mawazo yoyote wala sina tatizo la kunifanya nilie. what i know mwenzetu ametangulia mbele ya haki akaanze maisha mapya mazuri kuliko haya aliyokuwako. Nilichojifunza tu ni kuwaombea wapendwa wetu walale mahali pema peponi.
Ila sisemi watu msilie, kama mtoa mada alivyosema, wengi tunalia hasa kwa sababu ya shida zetu. Kwa wafiwa nasema uchungu wa kufiwa na wapendwa wao.
wengine wanajiliza uwongo tuu kwa sababu ya hii kasumba ya ajabu kwamba usipolia msibani eti huna uchungu na huyo marehemu wakati sio kweli, mi naona inategemea tu na hulka ya mtu,wengine wanaumia lakin ni ngumu ku express feelings zao outside, wengine wanalia ukweli wengine wanapiga ukunga wa uwongo ili mradi tu na yee yumo!!
<br />wengine wanajiliza uwongo tuu kwa sababu ya hii kasumba ya ajabu kwamba usipolia msibani eti huna uchungu na huyo marehemu wakati sio kweli, mi naona inategemea tu na hulka ya mtu,wengine wanaumia lakin ni ngumu ku express feelings zao outside, wengine wanalia ukweli wengine wanapiga ukunga wa uwongo ili mradi tu na yee yumo!!
Unapotokea msiba, tunalia sana. Hasa ndugu na jamaa wa karibu. Uchunguzi usio rasmi umeonesha kwamba, kila mmoja hulia kwa sababu tofauti na ni wachache sana ambao wanalia kwa mapenzi ya dhati waliyonayo kwa marehemu (wanaulilia utu wake). Wengi wanajililia wenyewe kwamba misaada au faida mbalimbali ambazo wamekua wanazipata kutoka kwa marehemu hawatazipata tena. Mfano, leo kuna taarifa kwamba 'babu' wa Loliondo amepata msiba. Huku kwetu taarifa hizo zilipotoshwa kwamba 'babu' amefariki. Watu wamesikitika na wengine kulia sana. Nimejiuliza; wanamlilia 'babu' au wanaililia dawa yake? ....Unapolia msibani, unamlilia marehemu au unalilia faida utakazozikosa kutokana na kifo chake? Tutafakari waungwana.