Elections 2010 kwa nini nafurahi kikwete kuanguka jukwaani?

Wewe unafurahia mtu kuanguka kwa ugonjwa, mtu anakupinga unasema hiyo ni theory?

Wewe unataka aachie madaraka kwa sababu ya kuanguka? Asipoanguka tena ? Wewe una strategy gani zaidi ya kutegemea kudra za mtu kuanguka mwenyewe? Is this the best upinzani can do? Kusubiri mtu aanguke ? Unajuaje kama akianguka tena na tena ataachia wenye uwezo watawale? Akiwaachia wazembe wengine utasemaje? Utaombea nao waanguke ?

Huna uhakika kwamba atakayekuja ni mzuri lakini bado unaona ni one step ahead? Unajuaje kama si one step back ?

Hivi kama hupendi siasa za Kikwete huwezi kumpinga Kikwete kisiasa na kuonyesha udhaifu wa hoja zake bila kumtakia aanguke kimwili?

Hivi kumuangusha Kikwete kisiasa wapinzani hawana njia nyingine zaidi ya kuombea aanguke kimwili ?

Mimi nataka kuona upinzani unaokuja kwa fikra mpya, unaoleta matumaini, unaotupeleka kwenye uongozi unaojiheshimu na na wenye nidhamu kwa dhamana ya uongozi wa wananchi.

Nafurahi kuona viongozi wa upinzani wameweka ubinadamu mbele ya siasa. Alipoumia Slaa Kikwete alimtumia pole, Kikwete kaanguka Slaa amemtumia pole. Angalau kuna ubinadamu.

Hawa fanatics wanaokuja hapa kutaka kumla nyama binadamu mwenzao hawana support ya official positions za upinzani ninazozijua. There is a reasopn for this, the reason being these positions do not make sense humanely or even politically - they backfire terribly, Tanzanians do not like a ruthlessly inhumane politics-, ndiyo maana hata kama - I am not saying they actually do this, note hata kama- upinzani unataka kumuona Kikwete anaanguka na kufa jukwaani viongozi wao, kwa kujua responsibility ya ku project image ya ubinadamu, hawawezi kusema hivyo kamwe .

But I guess some people will never get that through their heads.
out of topic.... rudi tena usome ... na usijifanye master of spinning! kwa ligi wewe hujambo!
 
safi sana mkuu hahaaaa haaaaa
ukiona unaingiwa na ubinadamu wa kumuonea huruma mwenziyo ni dhahiri kuwa wewe unamjua Mungu,
maana nje ya kumjua Mungu hakuna mwanadamu mwenye huruma kwa mwenizie
Mkuu AO
Hamjui Mungu huyu ... ndio maane Watanzania wanapokufa kwa uzembe wa CCM kwa mamia haoni kasoro lakini Kikwete akianguka tusiposikitika anaona ni anti-ubinadamu. Ohooo dear!
 
mi nilitamani aanguke avunjike mguu au aanguke ang;oke meno ya mbele awe na mapengo apunguze kuchekacheka
 
Sidhani kama ni vema kushangilia kushuka kwa afya ya mtu,hebu fikiria jirani yako akisema anafurahia wewe kuanguka, inakuwaje??
 
out of topic.... rudi tena usome ... na usijifanye master of spinning! kwa ligi wewe hujambo!
Out of topic wapi? Unaweza kuwa specific ili nikujibu vizuri na kwa kituo ?

If anybody is out of topic, wewe unayeshindwa kujibu hoja za kisiasa kwa hoja za kisiasa, na kutaka kutatua matatizo ya kisiasa kwa kutaka mtu afe, ndiye unayekwenda "out of topic"
 
Kumbuka hata biblia inasema lia na wale waliao.Mwenzio anapopatwa jambo usishanginie kwa maana kwamba huwezi kufikwa pia.Ugonjwa ni jamabo la kawaida na watu wote hawawezi kuwa na ugonjwa sawa. Tusiwe na roho mbaya pale wenzetu wanapofikwa na matatizo-sanasana tuwe ni watu wa kusaidia na c kufurahia.

Yes, naamini kila mtu anapenda maendeleo yanchi yake, ila kumbukeni wote walio na maendeleo hayakuja cku moja, au kumaliza tatizo fulani halikusolviwa mda mfupi.Mambo mengi ni long term basis. Hivyo kubeza kila kitu kinachofanyika tunakuwa hatujatenda haki.Nikiuliza toka kikwete ameingia madarakani,wewe kama mwananchi umekuwa na ufanisi gani katika uzalishaji mali na kuinunua uchumi wako na hatimae wa jamii iliyokuzunguka? Ucpime maendeleo kwa serikali-serikali ni watu na watu ni mimi na wewe. Hatuna budi kuijenga nchi yetu kwa kutanguliza mchango wetu sisi wenyewe badala ya kulalamika kila cku tukitarajia serikali ifanye kila kitu.C amini kama ukionyesha nia fulani ,serikali itashindwa kukusupport.
 
safi sana mkuu hahaaaa haaaaa
ukiona unaingiwa na ubinadamu wa kumuonea huruma mwenziyo ni dhahiri kuwa wewe unamjua Mungu,
maana nje ya kumjua Mungu hakuna mwanadamu mwenye huruma kwa mwenizie

Ukweli kwamba mimi siamini mungu, na naonyesha ubinadamu zaidi ya wanaodai kuamini mungu hapa JF, unaonyesha kwamba unaweza kuamini mungu lakini usiwe na ubinadamu, na unaweza kutoamini mungu ukawa na ubinadamu.

Conclusion, kuamini mungu hakusababishi kuwa na ubinadamu zaidi. Mara nyingine kuamini mungu kunasababisha ubinadamu upungue, kam katika kupigana vita za kidini ambapo mwanadamu anaamini kwamba anapigania neno la mungu, na kumuua binadamu mwenzake.

Au zealous fanaticism za kisiasa tunazoziona hapa.
 
Mkuu AO
Hamjui Mungu huyu ... ndio maane Watanzania wanapokufa kwa uzembe wa CCM kwa mamia haoni kasoro lakini Kikwete akianguka tusiposikitika anaona ni anti-ubinadamu. Ohooo dear!

Unajionyesha usivyojua kupanga mambo. Kusema kwamba sifurahii kuona Kikwete anaanguka kwa ugonjwa hakuna maana kwamba nafurahia Watanzania wanapokufa kwa mamia, kama kuna sehemu nimesema hivyo naomba unionyeshe. Usiseme vitu ambavyo huwezi ku prove.

Kwangu mimi sioni kwa nini watu walio katika upinzani makini wakamtoa Kikwete bila kutegemea aanguke na kufa, na kuboresha huduma za Watanzania, Kikwete asife na Watanzania wawe na huduma nzuri zaidi.

Mimi simjui mungu lakini naonekana kukataa unyama wa kutaka kuuana kwa sababu za kisiasa, wewe unayetaka kujifanya unamjua mungu zaidi by implication unataka kutetea unyama wa kuuana kwa sababu za kisiasa.

Ndivyo mungu wako anavyokufundisha hivi ?
 
Unajionyesha usivyojua kupanga mambo. Kusema kwamba sifurahii kuona Kikwete anaanguka kwa ugonjwa hakuna maana kwamba nafurahia Watanzania wanapokufa kwa mamia, kama kuna sehemu nimesema hivyo naomba unionyeshe. Usiseme vitu ambavyo huwezi ku prove.

Kwangu mimi sioni kwa nini watu walio katika upinzani makini wakamtoa Kikwete bila kutegemea aanguke na kufa, na kuboresha huduma za Watanzania, Kikwete asife na Watanzania wawe na huduma nzuri zaidi.

Mimi simjui mungu lakini naonekana kukataa unyama wa kutaka kuuana kwa sababu za kisiasa, wewe unayetaka kujifanya unamjua mungu zaidi by implication unataka kutetea unyama wa kuuana kwa sababu za kisiasa.

Ndivyo mungu wako anavyokufundisha hivi ?
Nishakuambia tena ...wewe ni mtu wa siasa za kwenye internet. Huwezi kutoa mawazo chanya yenye kukubalika kwenye siasa za Afrika. Blah blah nyiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiingi na matendo hakuna.
 
Nishakuambia tena ...wewe ni mtu wa siasa za kwenye internet. Huwezi kutoa mawazo chanya yenye kukubalika kwenye siasa za Afrika. Blah blah nyiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiiingi na matendo hakuna.

Unachekesha sana wewe.

Kuombea watu waanguke na kufa jukwaani ndiko umekuona kama mawazo chanya ?

Kama hayo ndiyo mawazo chanya yako nitazimia nikijua mawazo hasi yako yakoje.

Sintashangaa kama utataka kujenga gas chambers kwa wanachama wa CCM wote utake kuwachoma moto kama Hitler alivyochoma wayahudi.
 
Unachekesha sana wewe.

Kuombea watu waanguke na kufa jukwaani ndiko umekuona kama mawazo chanya ?

Kama hayo ndiyo mawazo chanya yako nitazimia nikijua mawazo hasi yako yakoje.

Sintashangaa kama utataka kujenga gas chambers kwa wanachama wa CCM wote utake kuwachoma moto kama Hitler alivyochoma wayahudi.

Na badooooo! kufa hafi (nasitaki afe) lakini kuanguka...mh. By the way wewe ni mfano mmoja mzuri sana wa athari za utumwa kwenye bara la Afrika!
 
Kusema kweli sii vizuri kwa binadamu kushangilia rais wako anapokutwa na janga kama hilo hata kama wewe unafiiria ni Fisadi. Bado JK ni rais wetu isipokuwa naweza kubaliana na Mwikimbi ktk jambo moja tu nalo ni kwamba wakati woote wa ajali hiyo viongozi wa serikali na CCM walikuwa wakiimba CCM Oyee, na kutumia maneno mengi ya Kichama kuwapoza wananchi bila hata kusema kwamba RAIS wetu amepatwa hili na janga hili anaendelea vizuri..Kifupi viongozi wa CCM walikuwa wakiwajulisha wanaCCM hali ya rais na sio wananchi wa Tanzania.

Nawaomba muipitie upya ile taarifa iliyokuja kutujulisha kwamba JK alipatwa na tatizo la upungufu wa sukari hivyo BP yake ikashuka na kusababisha kuanguka sikumbuki ni kiongozi gani alizungumza lakini kwa kauli yake mwenyewe - he was addressing to CCM member za mashabiki wa JK.. Hii kweli ndivyo viongozi wanatakiwa kuwataarifu wananchi kuhusiana na Afya ya rais wao?..
 
Kusema kweli sii vizuri kwa binadamu kushangilia rais wako anapokutwa na janga kama hilo hata kama wewe unafiiria ni Fisadi. Bado JK ni rais wetu isipokuwa naweza kubaliana na Mwikimbi ktk jambo moja tu nalo ni kwamba wakati woote wa ajali hiyo viongozi wa serikali na CCM walikuwa wakiimba CCM Oyee, na kutumia maneno mengi ya Kichama kuwapoza wananchi bila hata kusema kwamba RAIS wetu amepatwa hili na janga hili anaendelea vizuri..Kifupi viongozi wa CCM walikuwa wakiwajulisha wanaCCM hali ya rais na sio wananchi wa Tanzania.

Nawaomba muipitie upya ile taarifa iliyokuja kutujulisha kwamba JK alipatwa na tatizo la upungufu wa sukari hivyo BP yake ikashuka na kusababisha kuanguka sikumbuki ni kiongozi gani alizungumza lakini kwa kauli yake mwenyewe - he was addressing to CCM member za mashabiki wa JK.. Hii kweli ndivyo viongozi wanatakiwa kuwataarifu wananchi kuhusiana na Afya ya rais wao?..

To be fair to Kinana, baada ya kutaja mlolongo mrefu wa CCM, wanachama, wakereketwa blah blah, akasema na wananchi kwa ujumla. Which betrays his partisan thinking, kwamba Kikwete ni mgombea wa CCM kwanza na rais wa Tanzania baadaye ( in fact hata wangemuweka msemaji wa Ikulu kuna watu wangelalamika kwamba mgombea wa CCM anatumia rsources za serikali, damned if you do, damned if you don't)

Kwa hiyo si kweli kwamba Kinana hakuwataja "wananchi". Ila hawakuwa prioritized, waliwekwa mwishon kabisa bila hata ya kusema "last but not least" ya kuwafariji.

Video ipo youtube na iliwekwa hapa, siku hizi ukinaswa hakuna longolongo kuhusu kauli.
 
Na badooooo! kufa hafi (nasitaki afe) lakini kuanguka...mh. By the way wewe ni mfano mmoja mzuri sana wa athari za utumwa kwenye bara la Afrika!

Mtumwa ni wewe unayetumikishwa na chuki mpaka kumuombea binadamu aanguke, mimi nimeweza kuweka pembeni utumwa wa mawazo ya chuki na kuangalia objectively mambo ya kisiasa.

Wewe ni mtumwa wa passion usiye na critical thinking wala reason, huu ni utumwa mbaya sana.
 
ni kawaida binadamu kutofurahia maanguko au mateso ya mtu mwingine waziwazi. lakini kwa nini hili la kikwete nachelea kumsikitikia?

ninazo sababu zangu nyingi lakini baadhi tu ni hizi

1. kiwete ni msanii alitukuka, yeye na wasanii wenzake wameeendelea kuwasanii watanzania kwa muda wa miaka mitano, wakati wananchi wanakufa njaa, hawana matibabu yeye anatumbua mapesa na mali asili zanchi hii na wateule wachache. kwa kuwa kuna wananchi wanaoanguka kwa njaa, kwa nini nijali kuhusu msanii kama kikwete kuanguka jukwaani, tena wakati anawaghilibu wananchi kwa kuwasomee litania ndefu ya mafanikio anayoyajua yeye na msanii mwenzake rostam aziz?

2. bado ule wizi wa epa na kagoda unanisumbua akilini. wakati kikwete na wenzake walichota mabilioni wakahonga mpaka akawa rais, badala ya kuwakamamta wale walioiba wanajulikana waziwazi, rosta, lowasa, nimrod mkono, kingunge, yeye na vibaraka wenzake wakawasweka ndani wasiohusika kama wale wafanyakakzi wa BOT. sasa wananishi maisha ya dhiki hawana mbele wala nyuma. kwa nini sasa nisifurahi kidogo anguko lake ambalo ni adhabu toka kwa MUNGU?

3. jakaya kikwete anataka kujenga usulatni wa ajabu hapa nchini, sasa yeye na wanawe ndo waamuzi wakubwa kabisa katika maisha na mustakabali wa nchi yangu, kama alivyokuwa sadam na wanawe wawili ndivyo alivyo kikwete, mkewe, na wanawe , kwa nini nisifurahie anguko la mtu kama huyu?

4.JK, WATU WANAKUDANGANYA, UMEZUNGUKWA NA WEZI, MAFISADI, PALE JUKWAANI JANGWANI UNAPOANGUKA KILA WAKATI WA KAMPENI KUNA ZINDIKO KUBWA, SEPTEMBER 5TH, 1990, MTU WA HAKI, NA MTUMISHI WA MUNGU BABA MTAKATIFU YOHANE PAULO WA PILI, ALIHUTUBIA TAIFA, AKALIKABIDHI TAIFA HILI KWA MUNGU, ILI WAONGO, WAZANDIKI, WAHUNI, WASANII, WALA RUSHWA, WAFISADI, WAKARIBIAPO PALE WAPATE KUANGUKA!

UTAANGUKA DAIMA

Great thinking haina maana kukosa hekima.
Unachomwombea adui yako unajipalia mwenyewe Mkuu, mwogope Mungu!
 
To be fair to Kinana, baada ya kutaja mlolongo mrefu wa CCM, wanachama, wakereketwa blah blah, akasema na wananchi kwa ujumla. Which betrays his partisan thinking, kwamba Kikwete ni mgombea wa CCM kwanza na rais wa Tanzania baadaye ( in fact hata wangemuweka msemaji wa Ikulu kuna watu wangelalamika kwamba mgombea wa CCM anatumia rsources za serikali, damned if you do, damned if you don't)

Kwa hiyo si kweli kwamba Kinana hakuwataja "wananchi". Ila hawakuwa prioritized, waliwekwa mwishon kabisa bila hata ya kusema "last but not least" ya kuwafariji.

Video ipo youtube na iliwekwa hapa, siku hizi ukinaswa hakuna longolongo kuhusu kauli.
Mkuu hakuna haja ya kusema video ipo au laa wewe nakuomba uyaandike hapa aliyosema Kinana kisha wanabodi watapima wenyewe..najua tu utasema waandishi wa KiTanzania ndio wenye makosa lakini hawezi kuwa Kinana.

Nilichosoma mimi kinasema hivi:-
Kinana alitumia fursa hiyo kuwahakikishia wanachama, wapenzi na mashabiki wa CCM kwamba hali ya afya ya Kikwete ilikuwa njema na ataendelea na ziara yake ya kampeni leo hii mkoani Mwanza na kwingineko nchini.
Mbali ya hilo, Kinana alisema uamuzi wa Kikwete kufunga ulikuwa ni kinyume cha ushauri aliopewa na madaktari wake ambao walishauri asifunge.
Alisema tayari chama hicho na madaktari wake wameshachukua hatua zote za tahadhari ili kuhakikisha kuwa mgombea huyo wa urais anaendelea na kampeni zake za urais pasipo kukwama.
 
Kuangauka kwa Kikwete ni aibu yetu watanzania. Si jambo la kufuraia hata kidogo. Dunia imetangaza kuanguka kwa rahisi wa Tanzania wakati anahutubia tena mara ya tatu! Hii ni challenge yetu wote. Kuna haja ya kushauri wanachama chake waache unafiki wamshauri akae chini. Si vizuri kuongozwa na kiongozi mgonjwa wakati watu wapo wenye uwezo. Nadhani ni wakati sasa wa kumpumzisha kwa kutompigia kura. Hata kama wapo wanaopenda aendelee na urahis kama ni waungwana ni vema wampumzishe kwa kutomchagua mwaka huu. Ni ishara dhahiri kuwa mwaka huu ni Dr. Slaa.
 
Ni jaribio la uchakachuaji wa thamani ya utu wa binadamu, ukosefu wa hekima, matumizi hafifu ya uhuru wa kutoa maoni na pia uchanga wa hali ya juu sana katika medani za siasa, kufikia hatua ya kujianika na hoja ya kufurahia na au kuombea mgombea yeyote (hata kama humuungi mkono) apatwe ajali au baya lolote lenye madhara juu ya siha yake.
 
Siasa za chuki, kule Zanzibar zimezikwa rasmi pale walipopiga kura ya kutaka serikali ya mseto... naona sasa zinataka kuamia Tanganyika.
 
Back
Top Bottom