Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kuna mambo yanayosikitisha. Ambayo hata ukiambiwa mtu mwenye akili timamu huwezi kuamini. Ni kichaa peke yake, tena yule mwehu ambaye hajapata matibabu ndio anaweza kuamini kuwa, spika wa bunge anaendelea kuendesha bunge wakati ambapo kuna meli inazama ikiwa na mamia ya watu ndani yake. Tena sababu ya kuzama kwake ni kutokana na upepo mkali. Huu ni ujinga uliovuka mipaka, bunge ni mali ya umma. Ndiyo maana huwezi kuingia pale ukiwa kama mbunge bila idhini ya wananchi. Leo wanaokupa idhini wanaliwa na samaki baharini, wewe unasema tunaendelea na kikao cha bunge. Au spika anajua nini kinachoendelea? Au CCM ili mambo yake yawe safi ni lazima itoe kafara? Nashangaa, sijaona mbunge wa CCM Akiguswa na tukio hili. Hii inamaana walikuwa wanajua kilichokuwa kinaendelea. Kwa mara nyingine tena narudia kusema kuwa, Sisi watanzania ni wanafiki wakubwa pia. Leo tunapiga domo tu kwa kulalamika bila kuchukua hatua. Hawa jamaa hawata ondoka kwa kura hawa hata milele. Isipokuwa kwa nguvu na umoja wa watanzania mashujaa wenye moyo wa ujasiri. Mtanzania! Vua ganda la woga. Vaa lile la ushujaa tupambane na udhalimu huu.