DOKEZO Kuweni makini na utapeli nimepigwa milioni na ushee, matapeli wanakuja na njia mpya kila siku

Hili ni dokezo maalum toka kwa mwananchi mtumiaji wa JF mwenye nia ya kuusaidia umma kuwa na taarifa 'maalum'
A

Anonymous

Guest
Kuna njia ya hii ya utapeli ambapo mtu anatengeneza urafiki na wewe kupitia mtandaoni. Kadri siku zinavyoenda mnatengeneza ukaribu na ka imani kanaanza kukuingia kiasi fulani kuwa umepata rafiki mzuri kutoka nchi jirani japokuwa wakati mwingine inaweza kuwa hapa hapa bongo.

Sasa akishaona umemuamini anakwambia fulani nina zawadi kwaajili yako nataka nikutumie, anakuonesha zawadi hizo na mara nyingi zinakuwa ni za gharama kubwa sana. Anakupigia picha akizipaki mpaka siku anazituma na anakupa mawasilianao ya mtu au kampuni inayotakiwa kudeliver mzigo huo.

Mzigo ukifika mtu au kampuni uliyoambiwa itakupatia mzigo huo wanakupigia simu kukujulisha kuwa mzigo umefika, lakini mzigo huwa unakuwa umepelekwa mji tofauti na wewe, na hapo utaambiwa, address ilikosewa au imetokea kutoelewana/sintofamu mzigo umetumwa sehemu nyingine, ili utumiwe mzigo huo unatakiwa kutuma pesa ya usafiri.

Ukiangalia pesa ya usafiri unayotajiwa na thamani ya vitu ulivyotumiwa unaona pesa ya usafiri ni ndogo sana, hivyo huoni hata shida ya kutuma! Ukishatuma tu imekula kwako, kampuni au mtu huyo anakublock inakuwa imetoka hiyo, ushaliwa!

Jambo la kuzingatia ili usije kuingia mkenge, watu hawa huwa hawataki kutumia video call, utabaki kuona profile picture zao na kusikia sauti lakini katu hawakubali kufanya video call ili ujue utambulisho wao.

Watu hawa wamekuwa wakitumia udhaifu wa watu kuwa wapweke kihisia kutapeli watu, sio upande wa mapenzi tu hata urafiki wa kawaida, jinsi wanavyokuchota utaona nimepata rafiki wa kweli kumbe mtu yupo kazini.

Kuweni makini.
 
Maranyingi watu hutapeliwa Kwa Kuweka tamaa mbele

Mimi hizo issues nishakuna nazo mara kadhaa ukishazoeana nae na mara nyingi anajifanya kwamba yupo ktk mashirika ya kuenza neno la MUNGU.

Mkishazoeana cku Moja anakwambia nimepata zawadi ambazo nyingi zao mm si mtumiaji au ninazo Anakutumia mapicha ya mikufu saa za Bei ghali laptops camera na makorokoro mengine ukiwa na akili kdg tu hapo lazima kengele ya tahadhar Italia kichwani mwako

Baadae atakwbia vitu husika nampa rafiki yangu anaondoka Leo kwani group lao na kujitolea linakuja fanya kazi za kujitolea Africa.

Baada siku chache utapokea ujumbe Kwa namba nyengine ikikwambia rafiki yako kaniipa mzigo wako na tulifikiri Nchi za Africa zinafikika zote kirahisi kumbe sivyo nimeenda posta kuangalia nawezaje kukutumia wamenambia njia rahis ni ya MMS wametaka dollar 200 au atakutajia 150 ataomba umrumie ICHO kiwango na atakupa njia za kuzituma ukituma biashara imeisha

Mm nilimwambia awasiliane na RAFIKI YANGU Ile izo pesa atume yeye coz yeye ndio alietaka kuniletea zawadi mm sikuomba

Baada siku moja anakwambia HAPATIKANI na vitu vyako ni vya gharama kubwa jipige ulipie tuu

Mm nikamwambia uzaa baadhi ya zawadi zangu Kisha hela iliyobaki utume mzigo ikawa mwisho wao

Wakati mwengine tamaa zet hutufanya tutapeliwe karahisi
 
Hivi hayo matapeli mbona namba ni za 254, ni kweli Wakenya au ni Wabongo?

Kuna siku nilikuwa nina muda wa kurefresh, tulivutana na hao matapeli mwisho wa siku tukaachana kimya kimya. Wao wanataka niwatumie hela kwa MPESA, mimi nataka wanipe akaunti ya benki + details niwatumie pesa.

Mwisho wa siku sijui niliwagombanisha, nikamwambia mmoja mwenye namba za UK kuwa nimeishamtumia pesa jamaa yake wa Nairobi. Jamaa wa UK akakomaa ni-screenshoot muamala. Mwisho tukaachana kimya kimya.
 
Ni wakala mwaka jana nimetuma kama 850000 mtejaa katuma kwa tapel anajua anachart na demu wa kizungu toka UK kumbe mbongo mwenzake baada ya kutuma pesa baada ya lisaa naona jamaa kaja jasho linamtoka nikajua tayar
Hahaha cheka balaa.
 
Kuna mdada alikuwa ananitafta sijui ile code namba ya nchi gani kajitambulisha ni Dr, yupo ktk taasisi za donation katika na PC zake nyingi aseme anavyochati tu nilimwelewa nikawa namsikilizia tu baadae aliacha inawezekana alishtuka sina Papara na hela zake
 
Back
Top Bottom