Kutoka Bungeni Dodoma: Julai 18, 2011

Sasa ni Hotuba ya Nishati na Madini, Wabunge wameanza kuchangia hoja!
 
Suala la uchimbaji wa Madini ya Uranium Bahi, Mbunge anakusudia kuunga mkono wananchi 6000 wa Bahi kwa kuwasilisha hoja Bungeni kupinga uchimbaji wa Uranium Bahi!
 
Akichangia kwenye mjadala wa Wizara ya Nishati na Madini leo Jumatatuu, Mbunge wa Bahi amekataza kwa mbunge toka sehemu nyingine Tanzania kuongelea nidhati ya Uranium iliyoko Jimboni kwake Bahi na kusema kuwa yeye ndio mbunge wa eneo hilo.

Je, ni sheria gani inamkataza mbunge kuongelea jambo lililoko kwenye jimbo lingine? Wabunge wana hata miliki ya maeoneo wanayowakilisha? Ina maana hakuna mbunge anaruhusiwa kuongelea sehemu kama wewe si wa eneo hilo i.e madini Bulyanhulu, North Mara, mbuga za wanyama Serengeti, Manyara, Mlima Kilimanjaro etc?

Nini tafsiri ya 'hoja kwa maslahi ya Taifa'?
 
Magamba bwana: eti tunamlaumu bure Mh Ngeleja amepewa fedha kidogo kwenye Bajeti yake! Mbunge wa kwanza kuchangia ndio kaunga hoja mkono ila amedai kuwa mwakani kama tatizo la umeme likiendelea eti "hawatapitisha Bajeti ya Nishati na Madini!"
 
Ni kweli, so far sijaona wachangiaji wa maana aliowasoma!
Hotuba muhimu za bajeti ni mbili tu. Ile ya Bajeti yenyewe inayosomwa na waziri wa fedha na ya ofisi ya Waziri Mkuu. Hizi nyingine ni kwa ajili ya posho kwa Wabunge masikini. Wabunge na mawaziri wengi wako hapa Dar sasa hivi.
 
Kwa wale mlio mbele/mbali, Hembu sikilizeni bunge letu la 10 Lilivyoendelea huko Mjengoni, ni zaidi ya zekomedy, nashauri udownload hii track, ni 1.7MB then usikilize!!

Bungeni Kariakoo!!
 
magamba bwana: Eti tunamlaumu bure mh ngeleja amepewa fedha kidogo kwenye bajeti yake! Mbunge wa kwanza kuchangia ndio kaunga hoja mkono ila amedai kuwa mwakani kama tatizo la umeme likiendelea eti "hawatapitisha bajeti ya nishati na madini!"

huyo mbunge ni mpumbavu sana kwa hiyo tuendelee kukaa gizani hadi mwakani.........wakati ni sasa tuchukua hatua, wapi mabunge kama ya india, kenya nk mbunge akiongea pumba unamtwanga kiatu usini.
 
Mdau endelea kutujuza yanayojiri huko bungeni. Hivi hakuna radio inayotangaza mkutano wa bunge LIVE
 
Mbunge wa pili amedai Ngeleja aliwadanganya wananchi wa Wilaya ya Kerwa (huko Kagera) angewapelekea Umeme lakini kwenye vitabu vya Bajeti vya Ngereja mradi huo haujaonyeshwa! Hajaunga mkono hoja ila anasubiri wananchi wake wamweleze aunge mkono hoja au la!
 
Daahhh, hii title yako Bungeni "Kariakoo - Wimbo"??

Hiyo "Kariakoo - Wimbo" umenikumbusha nyumbani kabisaaaaa, kijiwe sio cha kawaida hicho cha enzi hizoooo.
 
CCM yamwaga pikipiki Kawe
Monday, 18 July 2011
NA KHADIJA MUSSA

CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimetoa pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo la Kawe, Dar es Salaam, ambapo pia kimezoa wanachama wapya 200, baadhi wakiwa kutoka vyama vya upinzani.

Pikipiki hizo ni sehemu ya 26 zilizotolewa na Chama kwa ajili yavijana, ambapo 11 zimepelekwa mkoani Singida. Jumla ya gharama ya pikipiki hizo ni sh. milioni 46.8. Wanachama hao walijiunga na CCM jana, kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika katika kata ya Tegeta, ambao uliohutubiwa na Katibu wa NEC yaCCM, Uchumi na Fedha, Mwigulu Nchemba.

Kwa mujibu wa wanachama wapya, wamevutiwa na sera za CCM, hivyo kuamua kujiunga na Chama. Nchemba katika mkutano huo uliohudhuriwa na umati wa wananchi, wanachama na wapenzi wa CCM, alikabidhi pikipiki 15 kwa vijana wa jimbo hilo. Alisema pikipiki hizo zimetolewa kwa mkopo, ambapo vijana watatakiwa kuunda vikundi na kukabidhi sh. 30,000 kila wiki kwa kiongozi wa kikundi, yakiwa ni marejesho ili kuwezesha kununuliwa nyingine.

Katibu huyo wa NEC alisema fedhahizo zitatumika kununua pikipiki nyingine zitakazogawiwa kwa vijana wengine, ambapo kila mwezi mmoja atapatiwa. Aliwataka vijana hao kuwa waaminifu, kwani wakirejesha fedha hizo kwa wakati zitawezesha vijana 360 kupata pikipiki katika kipindi cha miaka mitano.

Nchemba alisema pikipikihizo zitawasaidia vijana kujipatia ajira, ikiwa ni utekelezaji wa Ilaniya uchaguzi ya CCM kwa vitendo. Aliwataka viongozi wa vyama vya upinzani kutumia nguvu na akili katika kubuni vitu ambavyo vitawakwamua wananchi kimaendeleo, na si kuchochea vurugu na maandamano, kwani hayana tija kwa taifa. Nchemba aliingia kwenye mkutano huo akiwa amepanda pikipiki, akiwa amefuatana na Katibu wa UVCCM Taifa, Martine Shigela.

Hongera CCM, lakini mnajua takwimu za vifo vitokanvyo na hizo pikipiki? manajua wangapi leo hii hawana miguu?
ugawaji wa pikipiki uende sambamba na uimarishaji wa hospitali za mifupa pamoja na kuongeza maeneo ya makaburi.
Ni ushauri wa bure.
 
unategemea nini wabunge wenyewe ndo hawa

images
 
Back
Top Bottom