Kusema ukweli VPL ni kama iliisha tarehe 3 Julai 2021 mbele ya Rais Samia

kavulata

JF-Expert Member
Aug 2, 2012
12,319
12,622
Timu zetu 4 kufanikiwa kwenda kushiriki mashindano ya CAF msimu ujao ni kama vile yamemaliza kiu ya kuwa bingwa kwa msimu huu. Mshindi wa kwanza na wapili wa VPL hawana tofauti kubwa maana tofauti kati ya zawadi ya mashindi wa kwanza na pili hairushi roho washindi wa pili, ni ndogo sana.

Kilishorusha roho watu wengi nchini ni kile kilichotokea tarehe 3 July mbele ya mgeni rasmi Rais Samia. Aliyefurahi siku ile ndiye mshindi wa msimu. Maana ni bahati kubwa Mama Samia kuhudhuria tukio kama lile.

Mechi zilizobakia ni muhimu kwa timu zinazokataa kushuka daraja na washindi wa tatu na nne.

Head to head ndiyo mpango mzima msimu huu.
 
Endelea kujitekenya.
Sherehe ilikwisha siku ile bro. Kila timu kwenye league ina malengo 5, kupata zawadi ya mshindi na fedha, kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa, kuwafurahisha mashabiki wake kwa kumfunga mpinzani wake mkuu na kujitangaza. Siku ile yote yalitimia mbele ya mgeni rasmi.

Siku ile, Wachezaji walipata pesa kuliko za mshindi wa league, walijihakikishia kishiriki mashindano ya kimataifa, mashabiki walifirahi sana, na walifanya hivyo mbele ya camera na Rais wa nchi akiwepo na watu wengi uwanjani, majumbani na kimataifa wakiangalia. Kuna nini tena hapo?
 
Sherehe ilikwisha siku ile bro. Kila timu kwenye league ina malengo 5, kupata zawadi ya mshindi na fedha, kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa, kuwafurahisha mashabiki wake kwa kumfunga mpinzani wake mkuu na kujitangaza. Siku ile yote yalitimia mbele ya mgeni rasmi.

Siku ile, Wachezaji walipata pesa kuliko za mshindi wa league, walijihakikishia kishiriki mashindano ya kimataifa, mashabiki walifirahi sana, na walifanya hivyo mbele ya camera na Rais wa nchi akiwepo na watu wengi uwanjani, majumbani na kimataifa wakiangalia. Kuna nini tena hapo?
Malengo ya timu ni kuchukua ubingwa, mafanikio ya timu yanapimwa kwa trophies anazopata, Michezo imeingiliwa kwa kweli.
 
Malengo ya timu ni kuchukua ubingwa, mafanikio ya timu yanapimwa kwa trophies anazopata, Michezo imeingiliwa kwa kweli.
Suppose timu ambayo haikuchukua ubingwa kwenye ligi yake ikapewa nafasi ya kushiriki African champions na ikachukua ubingwa wa champions league, na timu ambayo iliyochukua ubingwa kwenye ligi yake lakini ikaishia hatua za awali za champions league, ipi ni timu bora?
 
Malengo ya timu ni kuchukua ubingwa, mafanikio ya timu yanapimwa kwa trophies anazopata, Michezo imeingiliwa kwa kweli.

Malengo ya timu ni kuchukua ubingwa, mafanikio ya timu yanapimwa kwa trophies anazopata, Michezo imeingiliwa kwa kweli.
Kwani trophy sio zawadi?

Hiki nilichokiandika ni sahihi na maalumu tu kwa msimu huu ambao taarifa ya timu zetu 4 kushiriki mashindano ya CAF ilifahamika kabla ya ligi kumalizika.
 
Sherehe ilikwisha siku ile bro. Kila timu kwenye league ina malengo 5, kupata zawadi ya mshindi na fedha, kupata nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa, kuwafurahisha mashabiki wake kwa kumfunga mpinzani wake mkuu na kujitangaza. Siku ile yote yalitimia mbele ya mgeni rasmi.

Siku ile, Wachezaji walipata pesa kuliko za mshindi wa league, walijihakikishia kishiriki mashindano ya kimataifa, mashabiki walifirahi sana, na walifanya hivyo mbele ya camera na Rais wa nchi akiwepo na watu wengi uwanjani, majumbani na kimataifa wakiangalia. Kuna nini tena hapo?

Mkuu mbona umeweka standards za timu yako kwenye viwango vya chini sana ?
Yaani wewe ukimfunga mtani, ukapata zawadi ya mshindi wa pili, ukapata na nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa unaona inatosha ?

Kama ni hivyo, kuna timu ilisema itachukua ubingwa mara kumi mfululizo, naliona hili likitimia maana wengine mmeridhika na hayo mliyoyataja.

Mtakua washindi wa pili kwa miaka 10 mfululizo, what a lovely success for you.
 
Timu zetu 4 kufanikiwa kwenda kushiriki mashindano ya CAF msimu ujao ni kama vile yamemaliza kiu ya kuwa bingwa kwa msimu huu. Mshindi wa kwanza na wapili wa VPL hawana tofauti kubwa maana tofauti kati ya zawadi ya mashindi wa kwanza na pili hairushi roho washindi wa pili, ni ndogo sana.

Kilishorusha roho watu wengi nchini ni kile kilichotokea tarehe 3 July mbele ya mgeni rasmi Rais Samia. Aliyefurahi siku ile ndiye mshindi wa msimu. Maana ni bahati kubwa Mama Samia kuhudhuria tukio kama lile.

Mechi zilizobakia ni muhimu kwa timu zinazokataa kushuka daraja na washindi wa tatu na nne.

Head to head ndiyo mpango mzima msimu huu.

Kwa hiyo unashauri ligi yetu tuhakikishe Mama Samia anakuja uwanjani kila mechi kuongeza msisimko/kiu?
 
Mkuu mbona umeweka standards za timu yako kwenye viwango vya chini sana ?
Yaani wewe ukimfunga mtani, ukapata zawadi ya mshindi wa pili, ukapata na nafasi ya kushiriki mashindano ya kimataifa unaona inatosha ?

Kama ni hivyo, kuna timu ilisema itachukua ubingwa mara kumi mfululizo, naliona hili likitimia maana wengine mmeridhika na hayo mliyoyataja.

Mtakua washindi wa pili kwa miaka 10 mfululizo, what a lovely success for you.
Mimi sioni ni kwanini nifuge ng'ombe wa maziwa wakati maziwa ya bure yanapatikana. Kama wewe ukishinda VPL mara 10 mfululizo kwa mbinu za nje ya uwanja lakini tukikutana ninakufunga na mashindano ya kimataifa tunashiriki wote ndege zetu zinapishana angani kuna shida gani hapo mtani? Mpira ni akili tu. Hakuna asiefahamu kuwa simba anabebwa, mpaka leo ana viporo.
 
Mimi sioni ni kwanini nifuge ng'ombe wa maziwa wakati maziwa ya bure yanapatikana. Kama wewe ukishinda VPL mara 10 mfululizo kwa mbinu za nje ya uwanja lakini tukikutana ninakufunga na mashindano ya kimataifa tunashiriki wote ndege zetu zinapishana angani kuna shida gani hapo mtani? Mpira ni akili tu. Hakuna asiefahamu kuwa simba anabebwa, mpaka leo ana viporo.
Kupanga ni kuchagua mtani, nawewe umeshachagua cha kukipigania. Kila la heri.
Kuhusu Simba "kubebwa" ni jambo la kihisia zaidi hili si vema kulijadili maana kila mtu ana hisia zake. Hakuna hoja zenye mashiko katika hili.
 
Mimi sioni ni kwanini nifuge ng'ombe wa maziwa wakati maziwa ya bure yanapatikana. Kama wewe ukishinda VPL mara 10 mfululizo kwa mbinu za nje ya uwanja lakini tukikutana ninakufunga na mashindano ya kimataifa tunashiriki wote ndege zetu zinapishana angani kuna shida gani hapo mtani? Mpira ni akili tu. Hakuna asiefahamu kuwa simba anabebwa, mpaka leo ana viporo.
Hapo ndipo mnapokosea, sasa na ninyi mmepata pesa mtapunguza malalamiko
 
Alafu tunalalamikia TFF kuwa inaua mpira wa Tanzania ilhali mashabiki wenyewe ndy kama hawa wenye maono ya kushinda mechi moja kwa msimu.

Sasa wakina Ronaldo na Messi kuna faida gani kwao kupambana kutwaa ubingwa mfano wa UCL ambapo zawadi yake ya ubingwa ni kama $ 75m, ukiigawa hii kwa kikosi kizima cha Juve au Barca utaona kila mchezaji atapa dola 2.5m kwa mwaka. Wakati messi yeye kwa mwaka anaingiza peke yake dola 71m?

Ukiwa bingwa jua ya kwamba Kuna kitu kikubwa sana unaongeza ambacho ni value kwa team yako mbali na hilo unaweka historia. Hakuna atakaekumbuka kama Yanga ilishika nafasi ya pili na ikashiriki CAF champions league kwa msimu wa 2020-2021, ila itakumbukwa Simba kwa kuwa bingwa na kushiriki champions league.

Mwisho elewa kitu kimoja ambacho ni muhimu sana na hata viongozi wako wanajua hilo, ya kuwa shabaha ya team kubwa yyt duniani ni kuwa bingwa/ kushinda makombe katika big tournaments. Ndy maana hata nyinyi kila siku mnapiga kelele za kuwa bingwa wa Mapinduzi ilhali ni kombe lisilo na impact yyt, lakn mnatusumbua kweli kwelu.
Timu zetu 4 kufanikiwa kwenda kushiriki mashindano ya CAF msimu ujao ni kama vile yamemaliza kiu ya kuwa bingwa kwa msimu huu. Mshindi wa kwanza na wapili wa VPL hawana tofauti kubwa maana tofauti kati ya zawadi ya mashindi wa kwanza na pili hairushi roho washindi wa pili, ni ndogo sana.

Kilishorusha roho watu wengi nchini ni kile kilichotokea tarehe 3 July mbele ya mgeni rasmi Rais Samia. Aliyefurahi siku ile ndiye mshindi wa msimu. Maana ni bahati kubwa Mama Samia kuhudhuria tukio kama lile.

Mechi zilizobakia ni muhimu kwa timu zinazokataa kushuka daraja na washindi wa tatu na nne.

Head to head ndiyo mpango mzima msimu huu.
 
Kwa hiyo unashauri ligi yetu tuhakikishe Mama Samia anakuja uwanjani kila mechi kuongeza msisimko/kiu?
Wenye akili sawasawa wanafahamu ni kwanini TFF ilimualika Mama aje aone ufungaji rasmi wa ligi ya msimu huu. Kwanini hakuja kwenye mechi nyingine za ligi?
 
Suppose timu ambayo haikuchukua ubingwa kwenye ligi yake ikapewa nafasi ya kushiriki African champions na ikachukua ubingwa wa champions league, na timu ambayo iliyochukua ubingwa kwenye ligi yake lakini ikaishia hatua za awali za champions league, ipi ni timu bora?
Dah vyura mnajua kuhadithia ndoto kiukweli
 
Kupanga ni kuchagua mtani, nawewe umeshachagua cha kukipigania. Kila la heri.
Kuhusu Simba "kubebwa" ni jambo la kihisia zaidi hili si vema kulijadili maana kila mtu ana hisia zake. Hakuna hoja zenye mashiko katika hili.
Sawa, mtani hapigwi wala kushitakiwa. Lakini huoni aibu kuo kuna timu bado inacheza viporo huku baadhi ya timu tayari zimeshuka daraja na nyingine zimebakisha mechi 1. Hata kama hakuna ushahidi lakini haya mazingira pia huyaoni?
 
Back
Top Bottom