Sizinga
Platinum Member
- Oct 30, 2007
- 9,101
- 6,027
Kiifupi na Kihistoria mji wa Mtwara ni mji wa mwambao ambao upo kusini mwa Tanzania yetu ambao kipindi cha ukoloni ulikaliwa na waarabu toka mashariki ya kati, ni mji ambao unajulikana kihistoria zaidi kwa kuwa na ngome kubwa ya Waarabu pale Mikindani(Museums) . Hauna tofauti na ule mji wa bagamoyo kihistoria ila tofauti t uni kwamba yale majengo ya mikindani ambayo yalistahili kuwa makumbusho na ni vivutio kwetu si wenyewe na wageni, yamekwisha mno kiasi cha kwamba hayana tena thamani na mengi yameshabomoka kwani hayajawahi kufanyiwa marekebisho ya aina yoyote ile kwa kipindi kirefu sana. Mji huu ambao kwa sasa unaitwa Mtwara-Mikindani, hapo mwanzo ulikuwa unaongozwa na kutawaliwa na waarabu ambao baadae walijichanganya na wenyeji na kuzaliana, ni mji ambao wakazi wake wengi ni waislam. Nimeanza hivyo kwakuwa huenda watu walio wengi wanausikia tu huu mji labda kwa umaarufu wake kwa kuwa na zao la korosho, na wengine hawaujui kama huu mkoa upo upande gani wa Tanzania(kusini ukiambatana na mipaka ya msumbiji na Malawi).
Sasa ni hivi, kwa muda mrefu sana,tangu mimi nimezaliwa huu mji unapiga hatua polepole sana na kwakweli mwendo huu wa kobe sijui kama tutafika kule ambako watanzinia wengi watashawishika hata kuja mara moja kuuangalia. Uongozi na usimamizi mbovu wa viongozi ambao wapo kwenye mji huu kwa kweli unakatisha tamaa sana, na hapa ndipo mada yangu inapoanzia. Sina lengo la kuzungumzia udini katika inshu nzima ya uongozi katika jimbo hili la mtwara mjini la hasha ila itanilazimu niongelee swala hili kwani ndio ukweli uliopo na ndio vitu vinavyofanyika pale.
Tangu kipindi kile cha miaka ya sabini ambapo kulikuwa na mfumo wa chama kimoja hadi hii leo wabunge waliongoza jimbo hili ni Waislamu, kumbukumbu zangu zinaniambia kwamba kipindi kile nilivyozallliwa kulikuwa na Mbunge toka CCM anaitwa Mzee Mkanyama, huyu bwana hata sielewi sasa hivi yupo wapi,baada ya hapo wabunge waliofuatia ninaowakumbuka ni Mpeme, Sinani na sasa ni Murji aliyepitshwa na CCM. Mchakato mzima wa kuwapata hawa mabwana kiukweli ni udini ulishamiri katika pande hizi. Ikumbukwe kwamba tangu mwaka 1995 pale Rais Mstaafu BENJAMIN WILLIAM MKAPA kutawazwa kuwa raisi, nlidhani ndicho kitakuwa kipindi kizuri kwa watu wa mtwara kuneemeka kupitia mbunge wake Mpeme kuleta maendeleo jimboni.
Mchakaato wa kumpata huyu bwana ambae kiukweli elimu yake bila shaka ni chini ya darasa la saba, ulijaa udini sana, nasema hivi kwasababu mkapa alimpendekeza mtu mmoja Mr Kambona achaguliwe kupitia CCM,huyu bwana hakupewa hii nafasi na wazee wa kiislamu kwa ile sababu tu eti huyu bwana ni kafri kwani ameishi sana Italia ambako akiwatumikia wakristu(alikuwa barozi wa Tanzania nchini Italy),kwahiyo hafai kuongoza mtwara eti tu kuna waislamu wengi, vp inaingia akilini kweli? Ndo hivyo wazee wakaamua na kusema kwamba hatuwezi kuongozwa na kafri. Taabu ilikuwa kwa wale wagombea wenzake waliopita kwenye kura za maoni!,walitishiwa kuuawa na Mpeme kwa mtu yeyote atakayepata ubunge mbali na yeye. Aliwafanyia vibweka wagombea wenzake mpaka akapata ubunge . cha ajabu miaka yote mitano hakuwahi kuzunguza lolote pale bungeni zaidi ya kulala tu. Mwaka wa 2000 uchaguzi mkuu,wale wazee wa kiislamu wakamchagua tena huyu bwana awe mgombea,akapata ubunge na hakuongea lolote bungeni hadi alipomaliza utukufu wake.
Mwaka 2005 kwa mshangao wazee wa pale mjini wakamtipisha mtu mwenye uraia wa msumbiji ambae tena elimu yake nadhani kama sio chini la darasa la saba basi ni si zaidi ya form four,huyu ni Mr Sinani agombee kwa tiketi ya CCM kama mbunge, akapata ubunge, hakuongea lolote bungeni hadi miaka mitano ikapita. Funika kombe mwanaharamu apite, huyu bwana akagombea tena na akabwaga vibaya na mgombea mwenzake (mfanyabiashara maarufu wa kihindi na sio mwenye asili ya kihindi,hapana, ni mhindi) na hapa ndipo ninapoanza kusema haya.
Katika kipindi cha kura za maoni, palikuwa na wagombea makini ambao sio maarufu sana kwa jamiikulinganisha na huyu Baniani, lakini ni watu makini na wenye ushawishi mkubwa sana, hawa ni Mr JOEL NNANAUKA na Mr. KASUGULU. Nitamuongelea kiundani huyu Joel kwa kuwa namfahamu kiunandani sana. Nasikitika kusema tena kwamba wakazi wa mji huu wa Mtwara itakuwa imekula kwetu tena kwa muda wa miaka mitano ijayo, ile shilingi yetu tuliyoichezea tayari imeshatumbukia ******. Huyu Joel kitaaluma alisoma shule ya sekondari kibaha na ikumbukwe kwamba ndie aliongoza alikuwa Tanzania One (2002),akamalizia pale kibaha na baadae kujiunga na Bicom pale Mlimani University. Simpigii kampeni lakini kiukweli ni mtu makini mzawa wa pale mjini na ambae ana upeo mkubwa ukilinganishwa na wagombea wezake katika kile kinyanganyiro,mi naamini licha ya zengwe lililofanywa tena na wazee wa pale mjini kitu kingine kilichomwangusha huyu bwana ni udini, huyu ni mkristu,Anglikana.
Na hata katika kufanya kampeni ni huyu bwana ambae alifanya kampeni za kisasa zaidi kwa kufungua kipindi maalumu katika redio ya PeaceFm akiongea na wananchi wa mtwara mjini na hata wale ambao walikuwa wanakaa mbali kabisa vijijini ambao hawakuweza kwenda kwenye kampen zake. Ni huyu ambae leo hii anasikitishwa sana si tu kwenye kuenguliwa kwenye kura za maoni bali pia kumsikia mheshiwa Makamba alivyowapa STOP wagombea wa CCM kushiriki Midahalo, huyu Joel kwenye kipindi chake redioni aliweza kukusanya maswali yote yaliyotoka kwa wananchi na kuyatolea ufafanuzi mzuri. Siwezi sema kwamba CCM haikuwa chaguo sahihi kwake la hasha,ila kwa mpambanaji kama huyu nadhani angeenda CHADEMA(mtazamo wangu) nadhani angeweka ngome imara sana ya chama kama ilivyotokea kwa mgombe flani (Mr. Osman),na hata angeweza kumuengua huyu Gabachori-chori Murji kwani hakuna mtu asiyejua kwamba huyu bwana hana tofauti na ROSTAM AZIZ na ikumbukwe kuwa katoa rushwa sana hadi kupata kiti hiki cha CCM, ni huyu ambae alishawahi kuwa mbunge wa NEWALA kama sio Tandahimba na leo hii alichowatendea wakazi wa pale, hakuna hata mtu mmoja anayetamani kumuuona na wala kusikia CCM kule, huyu bwana ana fedha chafu (hili ni jembe) na anaweza kufanya lolote la dhuruma na asinyooshwe kidole na mtu yeyote, na ndie mbunge tunayesubiri kuapishwa atuwakilishe mjengoni kwa miaka mingine mitano. Elimu yake sidhani kama kuna mtu anayeifahamu, na siwezi ogopa kamwe kusema kwamba huyu hata elimu ya darasa la saba hana asilani!!
Upeo wa viongozi wanaopitishwa kugombea kwa jimbo la Mtwara mjini CCM kwa kweli ni mdogo na kwa dunia ya sasa sidhani kama hata wataweza kusimama na kutoa ushawishi wa aina yoyote ile mbele ya watu wasio wavivu kufikiri, na nasikitika ni jimbo ambalo lipo wazi sana kwa wapinzani kulichukua kutokana na umakini mdogo wa CCM kuchagua watu wake, haswahaswa upinzani ukiweza kudhibiti kura zinazoibwa na CCM,hasa ukizingatia ni jimbo pekee ambalo lina mafuta na gesi ya asili ardhini pake. Na hili ndilo jibu sahihi kwamba tangu Tanzania ianze hakuna hata mbunge mmoja aliyewahi kuwa Waziri akitokea katika jimbo la Mtwara mjini. Nakusihi tu ndugu Joel usikate tamaa, jaribu tena uchaguzi ujao huenda ukaonekana tena, manake na sisi tuliokuwa upinzani(CHADEMA) tuna michakato mingi ya kulichukua hili jimbo na tunatunga sheria na kuangalia vipaumbele vya watu wa mtwara . ni mm EKS
Sasa ni hivi, kwa muda mrefu sana,tangu mimi nimezaliwa huu mji unapiga hatua polepole sana na kwakweli mwendo huu wa kobe sijui kama tutafika kule ambako watanzinia wengi watashawishika hata kuja mara moja kuuangalia. Uongozi na usimamizi mbovu wa viongozi ambao wapo kwenye mji huu kwa kweli unakatisha tamaa sana, na hapa ndipo mada yangu inapoanzia. Sina lengo la kuzungumzia udini katika inshu nzima ya uongozi katika jimbo hili la mtwara mjini la hasha ila itanilazimu niongelee swala hili kwani ndio ukweli uliopo na ndio vitu vinavyofanyika pale.
Tangu kipindi kile cha miaka ya sabini ambapo kulikuwa na mfumo wa chama kimoja hadi hii leo wabunge waliongoza jimbo hili ni Waislamu, kumbukumbu zangu zinaniambia kwamba kipindi kile nilivyozallliwa kulikuwa na Mbunge toka CCM anaitwa Mzee Mkanyama, huyu bwana hata sielewi sasa hivi yupo wapi,baada ya hapo wabunge waliofuatia ninaowakumbuka ni Mpeme, Sinani na sasa ni Murji aliyepitshwa na CCM. Mchakato mzima wa kuwapata hawa mabwana kiukweli ni udini ulishamiri katika pande hizi. Ikumbukwe kwamba tangu mwaka 1995 pale Rais Mstaafu BENJAMIN WILLIAM MKAPA kutawazwa kuwa raisi, nlidhani ndicho kitakuwa kipindi kizuri kwa watu wa mtwara kuneemeka kupitia mbunge wake Mpeme kuleta maendeleo jimboni.
Mchakaato wa kumpata huyu bwana ambae kiukweli elimu yake bila shaka ni chini ya darasa la saba, ulijaa udini sana, nasema hivi kwasababu mkapa alimpendekeza mtu mmoja Mr Kambona achaguliwe kupitia CCM,huyu bwana hakupewa hii nafasi na wazee wa kiislamu kwa ile sababu tu eti huyu bwana ni kafri kwani ameishi sana Italia ambako akiwatumikia wakristu(alikuwa barozi wa Tanzania nchini Italy),kwahiyo hafai kuongoza mtwara eti tu kuna waislamu wengi, vp inaingia akilini kweli? Ndo hivyo wazee wakaamua na kusema kwamba hatuwezi kuongozwa na kafri. Taabu ilikuwa kwa wale wagombea wenzake waliopita kwenye kura za maoni!,walitishiwa kuuawa na Mpeme kwa mtu yeyote atakayepata ubunge mbali na yeye. Aliwafanyia vibweka wagombea wenzake mpaka akapata ubunge . cha ajabu miaka yote mitano hakuwahi kuzunguza lolote pale bungeni zaidi ya kulala tu. Mwaka wa 2000 uchaguzi mkuu,wale wazee wa kiislamu wakamchagua tena huyu bwana awe mgombea,akapata ubunge na hakuongea lolote bungeni hadi alipomaliza utukufu wake.
Mwaka 2005 kwa mshangao wazee wa pale mjini wakamtipisha mtu mwenye uraia wa msumbiji ambae tena elimu yake nadhani kama sio chini la darasa la saba basi ni si zaidi ya form four,huyu ni Mr Sinani agombee kwa tiketi ya CCM kama mbunge, akapata ubunge, hakuongea lolote bungeni hadi miaka mitano ikapita. Funika kombe mwanaharamu apite, huyu bwana akagombea tena na akabwaga vibaya na mgombea mwenzake (mfanyabiashara maarufu wa kihindi na sio mwenye asili ya kihindi,hapana, ni mhindi) na hapa ndipo ninapoanza kusema haya.
Katika kipindi cha kura za maoni, palikuwa na wagombea makini ambao sio maarufu sana kwa jamiikulinganisha na huyu Baniani, lakini ni watu makini na wenye ushawishi mkubwa sana, hawa ni Mr JOEL NNANAUKA na Mr. KASUGULU. Nitamuongelea kiundani huyu Joel kwa kuwa namfahamu kiunandani sana. Nasikitika kusema tena kwamba wakazi wa mji huu wa Mtwara itakuwa imekula kwetu tena kwa muda wa miaka mitano ijayo, ile shilingi yetu tuliyoichezea tayari imeshatumbukia ******. Huyu Joel kitaaluma alisoma shule ya sekondari kibaha na ikumbukwe kwamba ndie aliongoza alikuwa Tanzania One (2002),akamalizia pale kibaha na baadae kujiunga na Bicom pale Mlimani University. Simpigii kampeni lakini kiukweli ni mtu makini mzawa wa pale mjini na ambae ana upeo mkubwa ukilinganishwa na wagombea wezake katika kile kinyanganyiro,mi naamini licha ya zengwe lililofanywa tena na wazee wa pale mjini kitu kingine kilichomwangusha huyu bwana ni udini, huyu ni mkristu,Anglikana.
Na hata katika kufanya kampeni ni huyu bwana ambae alifanya kampeni za kisasa zaidi kwa kufungua kipindi maalumu katika redio ya PeaceFm akiongea na wananchi wa mtwara mjini na hata wale ambao walikuwa wanakaa mbali kabisa vijijini ambao hawakuweza kwenda kwenye kampen zake. Ni huyu ambae leo hii anasikitishwa sana si tu kwenye kuenguliwa kwenye kura za maoni bali pia kumsikia mheshiwa Makamba alivyowapa STOP wagombea wa CCM kushiriki Midahalo, huyu Joel kwenye kipindi chake redioni aliweza kukusanya maswali yote yaliyotoka kwa wananchi na kuyatolea ufafanuzi mzuri. Siwezi sema kwamba CCM haikuwa chaguo sahihi kwake la hasha,ila kwa mpambanaji kama huyu nadhani angeenda CHADEMA(mtazamo wangu) nadhani angeweka ngome imara sana ya chama kama ilivyotokea kwa mgombe flani (Mr. Osman),na hata angeweza kumuengua huyu Gabachori-chori Murji kwani hakuna mtu asiyejua kwamba huyu bwana hana tofauti na ROSTAM AZIZ na ikumbukwe kuwa katoa rushwa sana hadi kupata kiti hiki cha CCM, ni huyu ambae alishawahi kuwa mbunge wa NEWALA kama sio Tandahimba na leo hii alichowatendea wakazi wa pale, hakuna hata mtu mmoja anayetamani kumuuona na wala kusikia CCM kule, huyu bwana ana fedha chafu (hili ni jembe) na anaweza kufanya lolote la dhuruma na asinyooshwe kidole na mtu yeyote, na ndie mbunge tunayesubiri kuapishwa atuwakilishe mjengoni kwa miaka mingine mitano. Elimu yake sidhani kama kuna mtu anayeifahamu, na siwezi ogopa kamwe kusema kwamba huyu hata elimu ya darasa la saba hana asilani!!
Upeo wa viongozi wanaopitishwa kugombea kwa jimbo la Mtwara mjini CCM kwa kweli ni mdogo na kwa dunia ya sasa sidhani kama hata wataweza kusimama na kutoa ushawishi wa aina yoyote ile mbele ya watu wasio wavivu kufikiri, na nasikitika ni jimbo ambalo lipo wazi sana kwa wapinzani kulichukua kutokana na umakini mdogo wa CCM kuchagua watu wake, haswahaswa upinzani ukiweza kudhibiti kura zinazoibwa na CCM,hasa ukizingatia ni jimbo pekee ambalo lina mafuta na gesi ya asili ardhini pake. Na hili ndilo jibu sahihi kwamba tangu Tanzania ianze hakuna hata mbunge mmoja aliyewahi kuwa Waziri akitokea katika jimbo la Mtwara mjini. Nakusihi tu ndugu Joel usikate tamaa, jaribu tena uchaguzi ujao huenda ukaonekana tena, manake na sisi tuliokuwa upinzani(CHADEMA) tuna michakato mingi ya kulichukua hili jimbo na tunatunga sheria na kuangalia vipaumbele vya watu wa mtwara . ni mm EKS
:eyebrows: