Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Hii issue ya maandamano ya Uamsho, vurugu zilizotokea na uchomaji wa makanisa ina mengi yaliyojificha kuliko tulivyoona na kuamini (au kuaminishwa).
Kuna wanaoona kuna mikakati ilibuniwa rasmi na kupangwa kimakusudi kwa lengo la kupindisha ajenda ya awali waliokuwa nayo Uamsho ya kuuhoji Muungano au hata kutaka uvunjwe.
Haijulikani mikakati hii ilifanywa na akina nani lakini kulikuwapo thread moja humu JF siku chache zilizopita ambayo iliondolewa iliyosema kuwa kule Visiwani wengi walikuwa wanaamini kuwa Usalama wa Taifa (UWT) ndiye walipanga mikakati hiyo kwa madhumuni hayo hayo ya kupotezesha lengo halisi la mikakati ya Uamsho.
Mikakati hii ya UWT kama kweli wao ndiyo walitekeleza itakuwa imefanikiwa kwa kiasi kikubwa kwani dhoruba kali tayari imewaangukia Uamsho kwani hatimaye wamejikuta wanabebeshwa lawama la uchomaji wa makanisa, kitu ambacho wengi katika taasisi hiyo wanaamini kuwa siyo wao waliotenda kitendo hicho, ingawa katika mazingira yalivyokuwa itakuwa vigumu kutohusishwa nayo.
Tutegemee vyombo vya dola iwapo kweli watawakamata watu wale hasa waliochoma makanisa hayo, na siyo kamata-kamata tu ya holela. Kuna usemi unaosema kwamba Uchomaji wa majengo (yaani arson) ni rahisi sana kutenda lakini ni vigumu sana kuwabaini mhusika/wahusika halisi. (It is easy to commit arson than to detect those responsible).
Kuna watu wameicheza hii kama Messi. Ni dhoruba ambayo kwa waliokusudia wanaona wamefanikiwa kuizima kabisa mikakati yote ya ajenda ya kuuhoji na/au kuuvunja Muungano kwani hakuna tena huko Unguja atakayeweza kuja na kitu hii kwani wataambiwa Nyie hamna lolote ajenda yenu kumbe ni udini tu, na siyo Muungano!
Ni hakika watu wa uamsho wamejinasa. Dola imepata sababu kubwa ya kupiga marufuku tena maandamano/harakati zozote kuhusu kuhojiwa Muungano kule Unguja.
Hii inatokana na ukweli kwamba suala zima la Muungano katika mchakato wa kuandika Katiba mpya limawakalia vibaya sana watawala kwani wameshasema kwamba Muungano usiguswe. Na ugumu mkubwa ulikuwa unatoka Visiwani lakini sasa inaonekana wamefanikiwa kulizima pengine labda kwa muda tu.
Sasa hivi Tume ya Katiba inaweza kuingia Visiwani na kufanya kazi bila hofu, pamoja na kwamba kutumika kwake Zanzibar bado ni kitendawili kutokana na sheria iliyoiunda ktk Bunge la Muungano kutothibitishwa na Baraza la Wawakilishi.