Elections 2015 Kuelekea 2015: CHADEMA Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!

Huyu aliandika huu uzi ni CCM, upuuzi mtupu. Tena haijui CDM. Huwezi ukasema hakuna sababu za msingi za kuipenda CDM kama CCM. Ngoja niishie hapo nisipate ban.
 
pasco watu wamechoka na ufisadi unaofanywa na serikali ya CCM na kuwasababishia umaskini mkubwa na hivyo chama mbadala kinachoibua ufisadi huo na kuukemea kwa nguvu zote ni CDM, sio kweli kwamba watu wamechoka tu CCM bila sababu za msingi, kwanini wasishabikie vyama vingine km CUF. TLP. NCCR na vinginevyo? usipotoshe umma,
 
Chadema watabaki kuwa washereheshaji kama muchacho kama wataendelea na viongozi hawa wehu,Mbowe na Dr Slaa.Kwa kuwa wote wanatamaa itafika mahali wataanza kuhujumiana na Chadema kufa kabla 2015.Kama kuna ubishi katika hili tusubiri tuone kwa kuwa time will tell.
 
Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?

kweli we unaakkili kama maisha ya funza we umeng'ang'ania ukabila tu.na kule mnako piga watu mabomu ni wachaga wanaish kule? achen M4C ifanye mikutano mbona mnaweweseka mkisikia CDM wanafanya mkutano?
 
Ni rahisi sana kuuliza swali lolote kuliko kutoa jibu sahihi..

Umeandika mambo mengi lakini haujasema 'specifically' wabadilike katika mambo yapi..; ?
 
hadi leohujajua sababu za watz kukichagua chadema? sababu ni hiz hapa
1.wananchi waliahidiwa maisha bora lakin imekuwa kinyume chake

2.ccm kimekua ni chama cha maficho ya majambaz wa kalam(ufisadi)

3.serikali ya ccm imeshindwa kuwakamata mafisad na imekaa kuwakumbatia

4.kwa miaka 50 tangutupate uhuru chama kukaa madarakan kimeshindwa kutatua kero mbalimbali za wananchi kama vile ujenzi wa shule,nyumba za watumishi,zahanati,upatiakanaji wa dawa na watumishi.
sababu hizo zinatosha kukipigia kura

aiseee mambo yako mengi yamewashinda ccm hata yale ambayo hayahitaji pesa watumishi wapo wanalipwa lakini hawafanyi wajibu wao mfano ,,,mipango miji kila mahali ni hovyo. ukizingatia upimaji wananchi tunalipa wenyewe na kiwanja tunanunua
 
Mkuu Pasco una hoja CHADEMA kuna mapungufu ya msingi ambayo ni lazima yapatiwe uvumbuzi kabla ya 2014 la sivyo 2taishia kulalamika 2 bila kujua
 
Chadema watabaki kuwa washereheshaji kama muchacho kama wataendelea na viongozi hawa wehu,Mbowe na Dr Slaa.Kwa kuwa wote wanatamaa itafika mahali wataanza kuhujumiana na Chadema kufa kabla 2015.Kama kuna ubishi katika hili tusubiri tuone kwa kuwa time will tell.
Jidanganye we usieelewa kitu chochote na hautoelewa kwa kuwa hutaki kuelewa
 
hawapo wengi sana sheikh,ila wana uwezo mkubwa wa kuzaliana na kutawanyika nchi nzima kwa kasi. Mfano 2010 walitokea "wachaga" wengi sana Musoma,mwanza,shinyanga,kigoma,Mbeya,Iringa,singida,Arusha,Ubungo,kawe n.k. Na kwa spidi waliyonayo "wachaga" hawa 2015 watakua wamefika lindi na mtwara.
Hivi chadema itashinda kwa kura za kina nani? wachagga? wako wangapi nchi hii?
 
Ahsante sana Pasco....naona umechukua maoni ya Mkandara na kuyafungulia thread mpya.
Any'wayz acha niwe msomaji tu hapa wakati nasubiria magwiji wa hoja wa jukwaa la siasa
watakavyocoment hii topic
 
Wanabodi,
Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

Trend za Upepo wa Kisiasa kuelekea 2015, zinavuma kwa Kasi ya Ajabu kuelekea Direction ya Mabadiliko (The Wind of Change, is Sweeping Across Tanzania) na kila dalili inaonyesha na kuelekeza Chadema is gaining momentum and there is to stop it kuchukua nchi mwaka 2015 iwapo...

  • Hakuna ubishi kuwa siku zote, CCM imekuwa ikishinda chaguzi mbalimbali "kihalali" na mtaji wao mkubwa wa ushindi ni "watu".
  • Hakuna ubishi kuwa CCM kama chama, kimechoka, dalili zote za chama kichovu kinachosubiri kifo, tayari, zimeisha jitokeza kwa CCM, kinachosubiriwa sasa its only a matter of time ni lini kitaangwa rasmi, hiyo 2015 naiona kama ni mbali sana!.
  • Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakuichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu!.
  • Hakuna ubishi, kuwa wengi wa hao "watu" waliokuwa kuwa wakiichagua CCM kwa mazoea, sasa wameichoka, hivyo 2015, hawatachagua tena chama kwa mazoea, bali watachagua chama kwa "sababu"!.
  • Hakuna ubishi kuwa Chadema, ndicho chama kinachokubalika zaidi kwa sasa kuliko CCM, hivyo ule mtaji mkubwa wa CCM iliyoutegemea kwa miaka nenda miaka rudi, sasa umehamia Chadema!.
  • Kama ambavyo CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea tuu, na sasa CCM imechokwa, vivyo hivyo kwa sasa Chadema haina lolote la kukifanya kipendwe, bali kinapendwa kwa sababu "watu" wameichoka CCM!.
  • Kama utaguzi utaitishwa leo, Chadema itashinda kwa kishindo kikubwa cha ajabu, lakini ukiwauliza hao watakaokipa Chadema ushindi, ni sababu zipi za kuichagua Chadema, hawatakupa sababu yoyote zaidi ya kuichagua Chadema kwa sababu wameichoka CCM!.
  • ili Chadema iweze kupata ushindi wa Tsunami kwa uchaguzi wa 2015, lazima Chadema ikubali kubadilika, isiendelee kuutegemea huu umaarufu wa muda kwa kushangiliwa na umati wa watu walioichoka CCM, bali Chadema sasa lazima iwape Watanzania sababu za kuichagua Chadema.
  • So far so good, Chadema is doing a good job kwa sababu M4C is doing the right thing!. Doing the right thing alone, doesn't guarantee sweet clear victory for Chadema, it got to do things right!. Hii inamaanisha ili Chadema ishinde kwa kishindo kinachotakiwa, lazima ikubali kubadilika and start doing things right besides doing the right thing!.
  • Hivyo ndugu zangu viongozi wa Chadema najua 2015 mmedhamiria kwa dhati kuchukua nchi kwa ushindi wa kishindo!, lakini ili lengo hili litimie, ni lazima kwanza mkubali kusikiliza, pili mkubali kubadilika kwa kuzikiliza hoja zinazotolewa kuhusu Chadema na kuzifanyia kazi!.

Naomba kumalizia kwa nukuu kutoka kwa mmoja wa wanachama wetu humu jf.



Kwa wale wapenzi wa Chadema, ni vema kuwa great expectations on Chadema kuchukua nchi 2015, only if Chadema itabadilika, vinginevyo keep hopping for the best and get prepared for the worst kama Chadema haitabadilika na 2015 itakuwa ni CCM Tena!.

NB. Msiniulize Chadema wabadilike nini, wahusika wameshaambiwa imebaki kusikiliza na kutekeleza!.

Naomba kuwasilisha.

Pasco.




Pasco,

Asante. Hapo umekuwa slight better objective-wise.

Napinga hoja yako namba moja. "Watu na uhalali" ktk chaguzi zilizopita ni kitendawili. Ni ishu tata kiasi kwamba sitaki kulianzisha hapa. 20m registered voters and you know how many voted in 2010!

Naunga mkono hoja namba 2,3,8,9 na 10.

Hoja namba 4,5 na 6 zinafanana na hoja namba 2, kimantiki.

Hoja namba 7 imejichanganya sana. Sijui ni sababu ya wivu, wasiwasi au ni nini? Lakini umebabaika sana kati ya jiwe na mwamba mgumu!

Kwa ufupi hoja yako kuu inapaswa kuwa usikivu na unyenyekevu wa top-cream. Of coz, ni lazima viongozi wawe wasikivu na weledi. Uongozi sio kutimiza matakwa/ndoto/hisia zako (za wachache) kwa hasara ya walio wengi. So hapo nadhani kuna hoja fulani ulivyoivisha fumbo.
 
Tayari...........umeingiza siku....eh..

bado majebele si ndio maeneo yao ya kaz wnalipwa kwa kuteea watu asipo tetea no kula sikuhiyo. na wanalipwa kwa idadi ya topic.walizotetea ukitetea chache mshahara hakuna ndio maana huwa wanajitahid kufanyahvyo.
 
Pasco,

Kwa maoni yako, wewe unataka nchi hii ibakie mikononi mwa CCM au vinginevyo????? Jibu ndiyo au Hapana Kama huna jibu basi mimi ntakuwa na jibu nadhani hata wajumbe walioko humu JF watakuwa wamekufahamu na nitakumbushia post za huko nyuma.
 
Wanabodi,
Preamble: "Kwa opinion yangu, Uchaguzi wa 2015, Chadema Kuchukua Nchi Kwa Kishindo!... Only If...!"!

Trend za Upepo wa Kisiasa kuelekea 2015, zinavuma kwa Kasi ya Ajabu kuelekea Direction ya Mabadiliko (The Wind of Change, is Sweeping Across Tanzania) na kila dalili inaonyesha na kuelekeza Chadema is gaining momentum and there is to stop it kuchukua nchi mwaka 2015 iwapo...

  • Hakuna ubishi kuwa siku zote, CCM imekuwa ikishinda chaguzi mbalimbali "kihalali" na mtaji wao mkubwa wa ushindi ni "watu".
  • Hakuna ubishi kuwa CCM kama chama, kimechoka, dalili zote za chama kichovu kinachosubiri kifo, tayari, zimeisha jitokeza kwa CCM, kinachosubiriwa sasa its only a matter of time ni lini kitaangwa rasmi, hiyo 2015 naiona kama ni mbali sana!.
  • Hakuna ubishi kuwa wengi wa hao "watu", wamekuwa wakuichagua CCM sio kwa sababu wanaipenda sana!, (waipende kwa lipi?), la hasha!, "watu" wamekuwa wakiichagua CCM kwa mazoea tuu!.
  • Hakuna ubishi, kuwa wengi wa hao "watu" waliokuwa kuwa wakiichagua CCM kwa mazoea, sasa wameichoka, hivyo 2015, hawatachagua tena chama kwa mazoea, bali watachagua chama kwa "sababu"!.
  • Hakuna ubishi kuwa Chadema, ndicho chama kinachokubalika zaidi kwa sasa kuliko CCM, hivyo ule mtaji mkubwa wa CCM iliyoutegemea kwa miaka nenda miaka rudi, sasa umehamia Chadema!.
  • Kama ambavyo CCM imekuwa ikichaguliwa kwa mazoea tuu, na sasa CCM imechokwa, vivyo hivyo kwa sasa Chadema haina lolote la kukifanya kipendwe, bali kinapendwa kwa sababu "watu" wameichoka CCM!.
  • Kama utaguzi utaitishwa leo, Chadema itashinda kwa kishindo kikubwa cha ajabu, lakini ukiwauliza hao watakaokipa Chadema ushindi, ni sababu zipi za kuichagua Chadema, hawatakupa sababu yoyote zaidi ya kuichagua Chadema kwa sababu wameichoka CCM!.
  • ili Chadema iweze kupata ushindi wa Tsunami kwa uchaguzi wa 2015, lazima Chadema ikubali kubadilika, isiendelee kuutegemea huu umaarufu wa muda kwa kushangiliwa na umati wa watu walioichoka CCM, bali Chadema sasa lazima iwape Watanzania sababu za kuichagua Chadema.
  • So far so good, Chadema is doing a good job kwa sababu M4C is doing the right thing!. Doing the right thing alone, doesn't guarantee sweet clear victory for Chadema, it got to do things right!. Hii inamaanisha ili Chadema ishinde kwa kishindo kinachotakiwa, lazima ikubali kubadilika and start doing things right besides doing the right thing!.
  • Hivyo ndugu zangu viongozi wa Chadema najua 2015 mmedhamiria kwa dhati kuchukua nchi kwa ushindi wa kishindo!, lakini ili lengo hili litimie, ni lazima kwanza mkubali kusikiliza, pili mkubali kubadilika kwa kuzikiliza hoja zinazotolewa kuhusu Chadema na kuzifanyia kazi!.

Naomba kumalizia kwa nukuu kutoka kwa mmoja wa wanachama wetu humu jf.



Kwa wale wapenzi wa Chadema, ni vema kuwa great expectations on Chadema kuchukua nchi 2015, only if Chadema itabadilika, vinginevyo keep hopping for the best and get prepared for the worst kama Chadema haitabadilika na 2015 itakuwa ni CCM Tena!.

NB. Msiniulize Chadema wabadilike nini, wahusika wameshaambiwa imebaki kusikiliza na kutekeleza!.

Naomba kuwasilisha.

Pasco.



Ofcourse CHADEMA inabadilika,na kubadilika ni gradually.....

Pasco,Well done!
 
Pasco,

Umenena vema,ni rahisi sana kukosoa na kurekebisha makosa.au niseme ni rahisi sana kutazama boriti lililo ndani ya jicho la mwenzako,LAKINI nivigumu sana kuwa sehemu ya hayo mazuri unayoyafikiria.

Jamani serikali ya CCM haiwachoshi tu bibi,shangazi,na watoto wa wanachama wa chadema.Sote tumepigika,sote Tunaumia,sote tunateseka.NI lini!!!!!!!! kauli hizi za kunyooshea vidole wengine kwamba wafanye hivi wafanye vile zitakomeshwa.

Huu ni mda wa kufanya maamuzi na kusimama upande mmoja.kama uko CCM zungumza kama mwanaCCM na kama ni mpambanaji simama ujibainishe na kuwa sehemu ya mabadiliko.

Tuachane na uvuguvugu ndio unaochelewesha safari yetu ya ukombozi,nchi hii bwana,

walimu vuguvugu
madaktari vuguvugu
waandishi vuguvugu
wanasiasa vuguvugu

Tatizo liko hapo.!!!!!!!!

EVERYBODY HAS TO CHANGE .
 
Back
Top Bottom