Kuchelewa kufungwa mashine, kutasababisha maji kufunguliwa bure Bwawa la Nyerere

ubarinolutu

JF-Expert Member
Oct 22, 2012
1,964
3,895
Mradi wa Bwawa la Nyerere tuliambiwa ungekamilika June 2022, lakini haikuwa hivyo.

Hata hivyo mwezi wa 12/2022 bwawa la mwalimu nyerere lilianza kujazwa maji, ambapo Ili bwawa kujaa kabisa linapaswa kufikia Mita 184 kutoka usawa wa bahari.

Kusua kusua Kwa mradi na kuchelewa Kwa kufungwa mashine za kuzalisha Umeme yaani mifumo ya turbine itapelekea na itawalazimu wizara ya nishati na TANESCO kufungulia maji Ili kuliepusha bwawa la mwalimu nyerere kujaa maji na kupitiliza kitu ambacho magufuli alikipinga katika bwawa la mtera.

Katibu Mkuu wa wizara ya nishati akiongea ikulu, amesema ni mashine mbili tu kati ya tisa ambazo zipo karibuni kuwashwa Kwa maana saba bado kabisa, na hata hizo mbili bado zinajaribiwa.

Chakusikitisha tu, na Kwa taarifa iliyopo Sasa , na hii ni mwezi wa pili tu hata masika hayajachangamka ya March na April.

Bwawa la mwalimu nyerere limejaa na kufikia Mita 179 kutoka usawa wa bahari huku zikibaki MITA 5 Ili kufikia ukomo na uwezo wa Bwawa wa MITA 184.5, hapo hapo hakuna mashine inayozalisha Umeme.

Hivyo kulingana na mvua za mwaka huu, haifiki mwezi wa nne, bwawa litakuwa limeshajaa na mashine ni chache, hivyo Ili maji yasizidi itabidi TANESCO wafungulie maji yapite bila kuzalisha Umeme , huu ni uzembe mkubwa.

Pia kwanini serikali isiongeze mashine ya MW 100 katika Bwawa la Mtera
 
Hata ikiongezwa hiyo mashine hakuna miundombinu ya kusafirisha umeme mwingi, au hujamsikia RC Chalamila
 
Kusua kusua Kwa mradi na kuchelewa Kwa kufungwa mashine za kuzalisha Umeme yaani mifumo ya turbine itapelekea na itawalazimu wizara ya nishati na TANESCO kufungulia maji Ili kuliepusha bwawa la mwalimu nyerere kujaa maji na kupitiliza kitu ambacho magufuli alikipinga katika bwawa la mtera.
Hujuma zinazofanywa bwawani ni sawa na SGR fikiria hivi sasa majengo ya reli yamezungukwa na majani hakuna kinachoendelea
 
Katibu Mkuu wa wizara ya nishati akiongea ikulu, amesema ni mashine mbili tu kati ya tisa ambazo zipo karibuni kuwashwa Kwa maana saba bado kabisa, na hata hizo mbili bado zinajaribiwa.
Mashine #9 imeshajaribiwa na iko vizuri, anytime inaweza kuanza kazi. Hiyo ya pili itafanyiwa testing mwezi March.
 
Sasa nimegundua wanaoiuzia umeme TANESCO hawawezi kuruhusu hili Bwawa likamilike. Bila kula kichwa cha mtu huu mradi utasuasua sana
 
Unatakiwa uwe mwehu kuendesha shirika lenye mbinu za kikabaila km Tanesco.
 
Mashine #9 imeshajaribiwa na iko vizuri, anytime inaweza kuanza kazi. Hiyo ya pili itafanyiwa testing mwezi March.
Maji yamefika MITA 179 kati ya 184.5 full capacity, march na April mvua zitapick, unafikiri mashine mbili ndo zitasababisha bwawa lisioverflow. Kwa jinsi yoyote Ile lazma maji yamwage/kufunguliwa kupitia mana mashine 7 hazipo tayari Kwa wakati.
 
Sasa nimegundua wanaoiuzia umeme TANESCO hawawezi kuruhusu hili Bwawa likamilike. Bila kula kichwa cha mtu huu mradi utasuasua sana
Na hiki ndio haswa kiini cha tatizo la umeme hapa nchini.
Tunateswa na gas yetu wenyewe.
 
Si tuliambiwa kwamba maji hayaingii kwenye mabwawa ya kuzalisha umeme!!

Hilo linajaaje sasa?😁.
 
Mradi wa Bwawa la Nyerere tuliambiwa ungekamilika June 2022, lakini haikuwa hivyo.

Hata hivyo mwezi wa 12/2022 bwawa la mwalimu nyerere lilianza kujazwa maji, ambapo Ili bwawa kujaa kabisa linapaswa kufikia Mita 184 kutoka usawa wa bahari.

Kusua kusua Kwa mradi na kuchelewa Kwa kufungwa mashine za kuzalisha Umeme yaani mifumo ya turbine itapelekea na itawalazimu wizara ya nishati na TANESCO kufungulia maji Ili kuliepusha bwawa la mwalimu nyerere kujaa maji na kupitiliza kitu ambacho magufuli alikipinga katika bwawa la mtera.

Katibu Mkuu wa wizara ya nishati akiongea ikulu, amesema ni mashine mbili tu kati ya tisa ambazo zipo karibuni kuwashwa Kwa maana saba bado kabisa, na hata hizo mbili bado zinajaribiwa.

Chakusikitisha tu, na Kwa taarifa iliyopo Sasa , na hii ni mwezi wa pili tu hata masika hayajachangamka ya March na April.

Bwawa la mwalimu nyerere limejaa na kufikia Mita 179 kutoka usawa wa bahari huku zikibaki MITA 5 Ili kufikia ukomo na uwezo wa Bwawa wa MITA 184.5, hapo hapo hakuna mashine inayozalisha Umeme.

Hivyo kulingana na mvua za mwaka huu, haifiki mwezi wa nne, bwawa litakuwa limeshajaa na mashine ni chache, hivyo Ili maji yasizidi itabidi TANESCO wafungulie maji yapite bila kuzalisha Umeme , huu ni uzembe mkubwa.

Pia kwanini serikali isiongeze mashine ya MW 100 katika Bwawa la Mtera
Serikali na sarakasi za Kizimkazi...
Wananchi na malalamiko huku wakimuachia MUNGU aje awape suluhisho!
 
Maji yamefika MITA 179 kati ya 184.5 full capacity, march na April mvua zitapick, unafikiri mashine mbili ndo zitasababisha bwawa lisioverflow. Kwa jinsi yoyote Ile lazma maji yamwage/kufunguliwa kupitia mana mashine 7 hazipo tayari Kwa wakati.
Hiyo ni kawaida kabisa, ndiyo maana bwawa linakuwa na vents za kutolea maji bila kuzalisha umeme.
Btw, sitetei uzembe wa kukosekana kwa umeme!
 
Screenshot_20240224-153958.jpg
 
Back
Top Bottom