Bwawa la Mwalimu Nyerere na athari kwa vijiji vilivyopo bondeni mwa bwawa hilo

Izia maji

JF-Expert Member
Dec 1, 2021
2,161
3,807
Juzi niliona katika taarifa ya habari ya ITV wananchi wa vijiji mbalimbali bondeni mwa Bwawa la Mwalimu Nyerere wakihaha kuokoa maisha yao baada ya kuzingirwa na maji ya mto Rufiji. Hii inatokana na kujaa kwa bwawa hivyo kulazimisha kufungulia maji kutoka bwawani.

Pia tumekwisha fahamishwa kuwa mtambo mmoja kati ya tisa ya kuzalisha umeme bwawani hapo umewashwa na kuzalisha MW 235. Kwa hiyo bado mitambo nane ambayo baada ya kukamilika kufungwa itawashwa na bwawa kuanza kuzalisha MW 2115. Hakika ni jambo jema sana.

Wasiwasi ni kuwa kama kuwashwa kwa mtambo mmoja tu kumesambaratisha wanavijiji na kuanza kuhama makazi yao, hali itakuwa vipi pale mitambo yote tisa itakapowashwa? Je, vijiji vilivyopo bondeni mwa Bwawa vitaendelea kuwepo? Je, wananchi wamekwisha taarifiwa lo lote kuhusu hali ya baadaye ya makazi na mashamba yao?

Ikumbukwe kuwa mitambo yote itakapokuwa inafanya kazi hakutakuwa na kupungua maji tena kwa kuwa maji yatafunguliwa kwa kiwango kile kile mwaka mzima.
 
Kila mtambo unahitaji kiasi fulani cha maji ili ufanye kazi. Kwa sasa wamefungulia maji kwa mtambo mmoja na tayari mashamba ya wanavijiji yamefurika na watu kuhama makazi yao. Kwa hiyo maji yataendelea kuongezeka kadri mitambo inavyowashwa.
Taarifa imetolewa kwamba maji yamefunguliwa kwa Sababu mitambo mingine bado haijawashwa

Very simple 😂
 
Taarifa imetolewa kwamba maji yamefunguliwa kwa Sababu mitambo mingine bado haijawashwa

Very simple 😂
Najaribu kuwaza uwezo wako wa kuelewa! Maji yamefunguliwa kwa sababu Bwawa limejaa ili kupunguza maji. Lakini pia kuna maji yameelekezwa katika kuendesha mtambo uliowashwa. Hii imesababisha mafuriko bondeni. Sasa hoja hapa ni kuwa je maji yakifunguliwa kuwasha mitambo yote tisa hali ya mafuriko itakuaje?
 
Najaribu kuwaza uwezo wako wa kuelewa! Maji yamefunguliwa kwa sababu Bwawa limejaa ili kupunguza maji. Lakini pia kuna maji yameelekezwa katika kuendesha mtambo uliowashwa. Hii imesababisha mafuriko bondeni. Sasa hoja hapa ni kuwa je maji yakifunguliwa kuwasha mitambo yote tisa hali ya mafuriko itakuaje?
Kwahiyo Mafuriko yamesababishwa na nini?

Labda tuanzie hapo mh Muelewa
 
Kwahiyo Mafuriko yamesababishwa na nini?

Labda tuanzie hapo mh Muelewa
Muda wote wa kulijaza bwawa maji yalizuiwa na kuachiwa kiasi kidogo kwa ajili ya mazingira (environmental flow). Sasa bwawa limejaa kupita uwezo wa kuhifadhi kwa hiyo yamefunguliwa ili kupunguza na kubakiza kiasi kinachotakiwa.

Kwa hiyo mitambo yote itakapowashwa maji mengi zaidi ya yaliyofunguliwa kuwasha mtambo mmoja yataachiwa. Maji haya ya kuwasha mtambo mmoja ni tofauti na yale yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani.
 
Muda wote wa kulijaza bwawa maji yalizuiwa na kuachiwa kiasi kidogo kwa ajili ya mazingira (environmental flow). Sasa bwawa limejaa kupita uwezo wa kuhifadhi kwa hiyo yamefunguliwa ili kupunguza na kubakiza kiasi kinachotakiwa.

Kwa hiyo mitambo yote itakapowashwa maji mengi zaidi ya yaliyofunguliwa kuwasha mtambo mmoja yataachiwa. Maji haya ya kuwasha mtambo mmoja ni tofauti na yale yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani.
Sijui huelewi nini, mitambo yote ikianza kutumika maji hayatafunguliwa, nadhani huelewi maana ya "kufungulia maji" ya bwawa, usichanganye maji yanayopita kuendesha huo mtambo mmoja na maji kufunguliwa.
 
Sijui huelewi nini, mitambo yote ikianza kutumika maji hayatafunguliwa, nadhani huelewi maana ya "kufungulia maji" ya bwawa, usichanganye maji yanayopita kuendesha huo mtambo mmoja na maji kufunguliwa.
Wewe nadhani huelewi hoja! Ili turbines zizunguke unatakiwa ufungulie maji katika mahandaki yake. Maji yakisha zungusha hizo turbines yanaendelea katika mkondo wake na kutumika katika shughuli nyingine. Kwa sasa wamefungulia handaki moja ukichanganya na yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani yamesabisha mafuriko. Hoja ni kuwa kama handaki moja limeleta tafrani, vipi mahandaki yote tisa yakifunguliwa.
 
Wewe nadhani huelewi hoja! Ili turbines zizunguke unatakiwa ufungulie maji katika mahandaki yake. Maji yakisha zungusha hizo turbines yanaendelea katika mkondo wake na kutumika katika shughuli nyingine. Kwa sasa wamefungulia handaki moja ukichanganya na yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani yamesabisha mafuriko. Hoja ni kuwa kama handaki moja limeleta tafrani, vipi mahandaki yote tisa yakifunguliwa.
Kichwa chako kigumu sana,katembelee bwawa mojawapo kati ya mtera au kidatu utajifunza kitu
 
Wewe nadhani huelewi hoja! Ili turbines zizunguke unatakiwa ufungulie maji katika mahandaki yake. Maji yakisha zungusha hizo turbines yanaendelea katika mkondo wake na kutumika katika shughuli nyingine. Kwa sasa wamefungulia handaki moja ukichanganya na yaliyofunguliwa kupunguza maji bwawani yamesabisha mafuriko. Hoja ni kuwa kama handaki moja limeleta tafrani, vipi mahandaki yote tisa yakifunguliwa.

..walishauriwa wajenge skimu ya kilimo cha UMWANGILIAJI kama njia ya kudhibiti mafuriko. Sijui walichukuliaje ushauri huo.
 
Back
Top Bottom