MKWEAMINAZI
JF-Expert Member
- May 28, 2023
- 930
- 1,299
Hakika inasikitisha sana na inaumiza sana kuona watumishi wa umma na wazee wastaafu wakiendelea kulipwa mafao kiduchu huku wenza wa vigogo wakiandaliwa sheria ya wao pia kulipwa mafao kama waume/wake zao wanapostaafu.
Mafao ya hao vigogo ambao ni rais, makamu wa rais na waziri mkuu wanapo staafu tayari ni makubwa sana lakini bado serikali inataka na wenza wao nao walipwe.
Japo sina uhakika kuna tetesi kuwa wazee wa mjengoni tayari wameongezewa ulaji kimya kimya huku watumishi wa umma wakisota na wazee wetu wastaafu wakiendelea kulipwa pensheni zisizokithi hata mshahara wa house girl licha ya kuitumikia nchi hii kwa uadilifi mkubwa.
Ombi kwa serikali
Pamoja na mabadiliko ya sheria inayotaka kuyafanya ili wenza wa vigogo walipwe mafao ni vema mabadiliko hayo yakawahusu watumishi wa umma na wazee wetu wastaafu kinyume chake huu utakuwa upendeleo wa wazi kwa kundi la vigogo.
Tanzania ni yetu sote.
Mafao ya hao vigogo ambao ni rais, makamu wa rais na waziri mkuu wanapo staafu tayari ni makubwa sana lakini bado serikali inataka na wenza wao nao walipwe.
Japo sina uhakika kuna tetesi kuwa wazee wa mjengoni tayari wameongezewa ulaji kimya kimya huku watumishi wa umma wakisota na wazee wetu wastaafu wakiendelea kulipwa pensheni zisizokithi hata mshahara wa house girl licha ya kuitumikia nchi hii kwa uadilifi mkubwa.
Ombi kwa serikali
Pamoja na mabadiliko ya sheria inayotaka kuyafanya ili wenza wa vigogo walipwe mafao ni vema mabadiliko hayo yakawahusu watumishi wa umma na wazee wetu wastaafu kinyume chake huu utakuwa upendeleo wa wazi kwa kundi la vigogo.
Tanzania ni yetu sote.