Hizi njaa za Tanzania ni balaa kweli kweli. Kama uliamua kwenda kuanzisha chama cha upinzani, kisha unarudi tena kwenye chama ulichokuwa unakipinga within a year basi utakuwa mgonjwa wa UBONGO.
Duh!
kuelekea Oktoba 31 tutaona rangi zote za spectrum!
Anyway, niulize tu..na huyu dau lake ni ngapi kwenye ile nyota #6? mil. 6 au mil. 60?
Naona makamba hana utani, leo amevaa chui kabisa.. true colours in deed!!
Mpasuko upi na wao wanaingia IKULU?Niliwahi kusema... the only thing jamaa wa CCJ walichopatia ilikuwa uchaguzi wa jina yaan "Chama Cha Jamii" the rest was mauzauza... sasa subiri mpasuko wa CHADEMA baada ya uchaguzi.... mungu tuepushie...
wewe wasema....jibu utalipata tarehe 31-10-2010....mwaka huu kweli kiti kimoja mkipata shukuruni
hali ni mbaya kila idara
wewe wasema....jibu utalipata tarehe 31-10-2010....
Huyu jamaa ni njaa ya siasa CCJ- Chadema-NRA-CCM kwanini atulii sehemu moja.kwa sasa CCM lazima wambebe katika kampeni pamoja na JK au Galib.Nadhani alikosa nafasi ya jikoni CHADEMA ambapo walishamstukia na kumweka benchi.
Hongera zake kwa kudhihirisha UCHU wake hadharani
Kisha mkuu wangu Mwanakijiji alikuja waamini watu hawa!....Na yuko wapi..
Mimi toka mwanzo niliamini kabisa kwamba CCJ ni chama kilichoanzishwa kuivunja nguvu Chadema kabla ya kampeni. Kuondoa hoja kubwa ya Ufisadi ambayo ndio ilitawala magazeti yote nchini na kwa kufanya hivyo walifanikiwa sana.
Huyu Richard Kiyabo kamaliza kazi yake na anarudi kambini. Hakuwa ametoka CCM hata siku moja na wajinga wengi waliamini kuwa CCJ ni chama kipya chenye mwelekeo.
Lakini pamoja na yote haya mimi na mashaka sana na Uwezo wa kufikiri wa Watanzania. Ni jana tu asilimia kubwa walikuwa wakilaani CCM na kutoa matusi yote ya mapungufu ya JK, leo hii wameshasahau au kusamehe, hao hao ndio wanaunga mkono chama hicho tena kwa nguvu zote...Kesho kilio tena!
Sijui ndio asili ya athari za Utumwa au Miafrika ndivyo Tulivyo!
napenda kumuuuliza Mpendazoe, wakati unaenda CCJ ulifikiria kwa makini"??????????????? au ... maana Kiyabo tayari ndani ya CCM.. au ulistuka ukaamua kuamia chap chap chadema... baki huko huko Chadema na pigania jimbo Segerea!!
Hizi njaa za Tanzania ni balaa kweli kweli. Kama uliamua kwenda kuanzisha chama cha upinzani, kisha unarudi tena kwenye chama ulichokuwa unakipinga within a year basi utakuwa mgonjwa wa UBONGO.