KISWAHILI: Naomba maana ya maneno haya...

Hivi mbona hiyo paper imenishtua kidogo.
nashangaa paper ya Kiswahili inaandikwa na foreigner
kwani pale Tuki kazi yao ni nini?
Apart from that long time ago kamusi sijawahi kuona any document from them.
 
Naomba msaada wa meneno yafuatayo:

  1. Hujasikia au Ujasikia - mfano, "Inaweza kuchukua miezi kumi kabla hujasikia/ujasikia kutoka kwetu."
  2. Histahili au Istahili - mfano, "ili familia yako histahili/istahili, unahitaji kufanya a, b, na c"
  3. Yahitajio au Yahitajiwo - mfano, "tafadhali elezea marekebisho makuu yahitajio/yahitajiwo kwenye nyumba yako."
  4. Unaipa au Hunaipa - mfano, kwa kutia sahihi hapo chini, unaipa/hunaipa XYZ ruhusa zote kubomoa nyumba yako."

Pia, naomba tafsiri ya maneno haya kwenda kiswahili:
  1. Inspirational
  2. Show
  3. Widow
  4. Widower

Natanguliza shukhrani~
 
Naomba msaada wa meneno yafuatayo:

  1. Hujasikia au Ujasikia - mfano, "Inaweza kuchukua miezi kumi kabla hujasikia/ujasikia kutoka kwetu."
  2. Histahili au Istahili - mfano, "ili familia yako histahili/istahili, unahitaji kufanya a, b, na c"
  3. Yahitajio au Yahitajiwo - mfano, "tafadhali elezea marekebisho makuu yahitajio/yahitajiwo kwenye nyumba yako."
  4. Unaipa au Hunaipa - mfano, kwa kutia sahihi hapo chini, unaipa/hunaipa XYZ ruhusa zote kubomoa nyumba yako."

Pia, naomba tafsiri ya maneno haya kwenda kiswahili:
  1. Inspirational
  2. Show
  3. Widow
  4. Widower

Natanguliza shukhrani~

QM, naomba kujaribu.

Maneno sahihi kwa maoni yangu kama vile ulivyo orodhesha ni:

1. hujasikia
2. istahili
3. yahitajiyo
4. unaipa


Tafsiri:

Inspirational - Yakutia mori/morali. Au kutia moyo, kuriwaza mtima.

Show - onyesha, jidai, funua, fichua, hadhara

Widow - mjane (mwanamke)

Widower - ....sijui
 
QM, naomba kujaribu.

Maneno sahihi kwa maoni yangu kama vile ulivyo orodhesha ni:

1. hujasikia
2. istahili
3. yahitajiyo
4. unaipa


Tafsiri:

Inspirational - Yakutia mori/morali. Au kutia moyo, kuriwaza mtima.

Show - onyesha, jidai, funua, fichua, hadhara

Widow - mjane (mwanamke)

Widower - ....sijui

Thanks Steve!

Hapo kwenye "Show" nilikuwa na maanisha term inayotumika kwenye vipindi vya Tv.

Mfano, Ze Comedy Show.

Hili neno la Show unalitafsiri vipi
 
Widow - Is a female who lost her husband (mjane mwanamke)
Widower - I a man who lost his wife (mjane mwanaume)
Have a pleasant weekend.
 
Thanks Steve!

Hapo kwenye "Show" nilikuwa na maanisha term inayotumika kwenye vipindi vya Tv.

Mfano, Ze Comedy Show.

Hili neno la Show unalitafsiri vipi

Ze Comedy Show - nadhani itakuwa: maonesho ya Ze Comedy, kipindi cha Ze Comedy.

Maneno mengine ambayo yanaweza kuendana na isimu hii ni: tamthilia/tamthiliya, utenzi na riwaya.
 
Oh kwa hiyo wote wanaitwa wajane!

Asante

Karibu.
Wote wanaitwa wajane isipokuwa katika kiswahili tumezoea kumwita mwanamke pekee ndio mjane. Ila katika kiingereza yote yapo na yanatumika sawa.
 
The following link by the professor in Swahili language offers members an
insight into new Swahili vocabulary.

It is in PDF format.

[media]http://www.african.gu.se/aa/pdfs/aa05085.pdf[/media]
 
Wakuu, nimeulizwa ghafla na mtu ambaye hakijui vema kiswahili maana ya neno SHUBIRI kwani aliambiwa kuna dawa chungu kama shubiri hakuelewa shubiri ni nini kwa kiswahili wala kiingereza, binafsi nimechemsha!

Naweza kueleweshwa maana yake?

Nimeenda hapa sikupata msaada:

shubiri

Mkuu ushasema kuwa Shubiri ni dawa sasa unataka tafsiri gani tena?
Labda maelezo ya matumizi yake. Shubiri utumiwa kwa wenye kusumbuliwa na maradhi ya ngiri. Dawa chungu sana mfano wa qunaine.


Nakumbuka kuna shairi moja (la Saleh Barkey) limetumika neno hilo shubiri, kwa wale wanagenzi wa kiswahili. Shairi linasema hivi:

Wendavyo huna sumile, huyajali ya njiani
Vikwaruzavyo vitele, waona hujulikani
Huchwi kufungwa kengele, masikini wa rohoni
Siwatajii mchawi , mfumbuweni fumboni

Ulopewa ni shubiri, pima yakuhusu nini
Ukatamba una ari, umeushika mpini
Waona umevinjari, kumbe uko ukutini
Simfichui mchawi, mtambuweni fumboni

Ngoma hiyo ya kitoto, haikeshi asilani
Kujipulizia joto, raha yake raha gani
Umejitweka mazito, kwa kutaka ubishani
Mchawi hasemwi jina , nawatajia fumboni

Hapa neno Shubiri, lina maana ya umbali au (pima) ni kipimo cha nchi kama tisa hivi.
 
Last edited:
Karibu.
Wote wanaitwa wajane isipokuwa katika kiswahili tumezoea kumwita mwanamke pekee ndio mjane. Ila katika kiingereza yote yapo na yanatumika sawa.

Mjane - kwa tamaduni za makabila mengi ya kiafrika ni mwanamke tu maana wanaume walikuwa wanaoa wake wengi..akifa mmoja wengine wanabakia au anaongeza wengine. Ndio maana aghalabu huwezi kusikia mwanaume akiitwa mjane.
 
Kuna neno lingine hutumika kwa mtu aliyefiwa na mume - Kizuka, je hii ni sahihi na asili yake nini/.
neno "powa" na "poa" - kuna tofauti?
 
Mkuu ushasema kuwa Shubiri ni dawa sasa unataka tafsiri gani tena?
Nilisema hivi mkuu:

"Kaambiwa dawa ni chungu 'kama' shubiri" sikusema kapewa dawa ya shubiri. Hata hivyo namshukuru alonifahamisha kuwa Aloe Vera ndiyo shubiri, natumaini katufungua macho wengi sana!
 
Nitasaidia kama ninavyoweza kama ifuatavyo:
*Vukiza/Fukiza ni maneno yenye maana sawa,yaani kuweka kwenye mazingira ya moshi,iwe wa kuni au maVumba kwa nia ya kukausha kwa maana ya kuhifadhi au kufanya takatifu.
*Vundika au Vumbika:Haya ni maneno yenye maana sawa.Yaani kufanya ive au ioze:
*Compyuta:Hili sio neno la kiswahili,ila ni neno lililoazimwa kutoka kwenye kiingereza.
*Ingawa:Hili ni neno linalo halalisha udhuru.Kwa mfano,'ingawa sikwenda lakini mambo yatakwenda vizuri.'
*Msanii:Maana halisi ya msanii ni mstareheshaji,ingawa siku hizi msanii anaelezwa pia kama mtu asiye mkweli.
*Puchu:Hali ya kutokuwa na manyoya.
*Mkwara:kumkosoa mtu katika hali ya kukasirika.
*mwake:mazingira yanayomilikiwa na mtu husika.
Chuna:Toa ngozi.
Mbongo:Sina hakika sana ya neno hili,lakini nimesikia watu wengine wakilitumia wakimaanisha akili nyingi.

Nimekuwa nasikia maneno haya lakini yananichanganya kujua matumizi yake sahihi.

Vukiza au fukiza?
Vundika au vumbika?
Compyuta?
Mtandao
ila
ingawa
msanii
puchu
mkwara
mwake
chuna
mbongo

Ninayo maneno lukuki lakini nashindwa kuyaainisha yote hapa. Naomba wataalam wa lugha hii adhimu mnisaidie nitoke niliko walau hatua moja mbele katika kujifunza Kiswahili.

Ahsanteni
 
Aloe vera is the English word for Shubiri.

Aloe Vera si SHUBIRI. Shubiri ni kitu kingine -- kuna mtu ameniambia kuwa inatokana na utomvu wa mti -- iko ktk hali ya vidonge (crystals) ambavyo hulowekwa ktk maji, na kisha kutumiwa ktk hali hiyo ya kimiminika. Rangi ya maji yenye shubiri ni kahawia.
 
Back
Top Bottom