KISWAHILI: Naomba maana ya maneno haya...

Neno kadhia limejitokeza mara nyingi hapa ukumbini.
Nilidhani linamaana sawa na udhia ila sasa nina mashaka.



Kwenye kamusi nimepata tafsiri zifuatazo:
  • Udhia - annoyance, nuisance, confusion n.k

  • Kadhia - affair, event, matter, occurrence

Una maoni gani kuhusu hili?


.

Kwa maoni yangu, yote sahihi mkuu... kazi iliyobaki ni ku-practice pahala pa kuyatumia tu hivi sasa... lol
 
  • Kuwadi - pimp

Pimp - a man who controls prostitutes, especially by finding customers for them, and takes some of the money that they earn


Mfano:
MAKUADI WA SOKO HURIA - Chachage, Chachage Seithy L.
A novel which exposes the corruption inherent in free market economy in Tanzania. Swahili text. Maps, viii, 287pp, TANZANIA. E & D LIMITED, 9987622453




.
 
  • Vyama mbadala


John Mnyika said:
Mosi, sipendezwi na neno ‘upinzani’ maana lina maana nyingi na wengine hulichukulia tofauti. Mimi napenda zaidi kutumia vyama mbadala. Na wachache hutumia neno vyama vya ushindani. Jina lina mantiki sana katika kutanabahisha dhima. Wengine jina upinzani wanalichukulia ni kupinga tuuu!!!! Nitatumia neno ‘mbadala’.



Mjadala ulikuwa hapa:





.
 
JK afanya kweli

2008-08-09 14:52:15
Na Mwandishi Wetu, Songea


Tahadhari ambayo imekuwa ikitolewa mara kwa mara na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bwana Jakaya Kikwete kuwa Serikali yake haitakuwa na msamaha kwa viongozi na watumishi watakaofanya ufisadi kwa kutumia pesa za umma kwa manufaa yao binafsi, imeanza kuliza vigogo baada ya vijana wa kazi kufanya kweli na kumsweka jela kigogo mmoja.

Hatua hiyo imekuja baada ya vijana wa JK kuvalia njuga sakata la kigogo huyo, hadi kupata ushahidi wa kutosha juu ya namna jamaa huyo alivyolamba mapesa ya umma.

Kigogo huyo aliyeswekwa jela ni Mhasibu wa Shule ya Sekondari Mbinga mkoani hapa aitwaye Omari Millanzi, 56.

Mapesa hayo yaliangukia mikononi mwa kigogo huyo baada ya kutumwa na ofisi ya Hazina ili yafanye kazi ya kuboresha elimu.

Hata hivyo kigogo huyo alizinyaka pesa hizo na kuzikandamizia kwenye mambo yake mwenyewe hadi aliposhtukiwa na kuburuzwa kortini.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Ruvuma, Baptist Mhelela ndiye aliyesikiliza kesi juu ya sakata hilo na baadaye kumuona Millanzi ana hatia katika makosa 60 aliyoshtakiwa.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mhelela alisema kuwa kwa kuzingatia ombi la Mwendesha Mashtaka aliyetaka adhabu kali itolewe kwa mshtakiwa, na kwa kuzingatia vilevile kuwa mshtakiwa amekutwa na hatia ya makosa hayo yote, mahakama imeamua kumfunga jela mshtakiwa huyo kwa miaka mitatu kwa kila kosa, katika mashtaka 30 ya awali, hivyo kutakiwa atumikie jela kwa miaka 90.

Aidha, Hakimu Mhelela akasema kwa makosa mengine 30, kila kosa litampasa mshtakiwa atumikie jela kwa miaka mitano, hivyo jumla kuwa miaka mingine 150.

Jumla kuu ya kipindi cha adhabu za mshtakiwa huyo kilipaswa kuwa miaka 240 jela.

Hata hivyo Hakimu Mhelela alisema kwakuwa adhabu zote zitatumikiwa kwa pamoja, mshtakiwa atakwenda jela miaka mitano.
Pia Hakimu huyo akaamuru mshtakiwa alipe kiasi chote cha pesa alizoiba kwa mwajiri wake ambazo ni Sh. Milioni 24.1, mara tu baada ya kumaliza adhabu yake ya kifungo.

Kabla ya hukumu hiyo, upande wa mashtaka ukioongozwa na Inspekta George Omary, ulidai kuwa katika kipindi cha mwezi Januari na Julai mwaka 1998, mshtakiwa Millanzi aligushi nyaraka mbalimbali za Serikali na kuiba pesa hizo, kaisi cha Sh. Milioni 24.1.

Alipotakiwa kujitetea, ndipo mshtakiwa Millanzi alipomlilia hakimu na kumtaka ampunguzie adhabu akidai kuwa ana umri mkubwa na kuwa vilevile, ana familia inayomtegemea.

Mara kwa mara, Rais Kikwete amekuwa akisisitiza juu ya nidhamu ya matumizi mazuri ya pesa za umma na kuonya kuwa yeyote atakayekiuka taratibu, atachukuliwa hatua kali za kisheria.

SOURCE: Alasiri

Hawa wanaostahili kuitwa vigogo watafungwa lini na miaka mingapi???
Nafikiri vyombo vya habari, hasa reporter huyu kaweka kichwa cha habari kikubwa kuliko habari yenyewe, sijui wenzangu mnaonaje??
 
JK afanya kweli

2008-08-09 14:52:15
Na Mwandishi Wetu, Songea


Tahadhari ambayo imekuwa ikitolewa mara kwa mara na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Bwana Jakaya Kikwete kuwa Serikali yake haitakuwa na msamaha kwa viongozi na watumishi watakaofanya ufisadi kwa kutumia pesa za umma kwa manufaa yao binafsi, imeanza kuliza vigogo baada ya vijana wa kazi kufanya kweli na kumsweka jela kigogo mmoja.

Hatua hiyo imekuja baada ya vijana wa JK kuvalia njuga sakata la kigogo huyo, hadi kupata ushahidi wa kutosha juu ya namna jamaa huyo alivyolamba mapesa ya umma.

Kigogo huyo aliyeswekwa jela ni Mhasibu wa Shule ya Sekondari Mbinga mkoani hapa aitwaye Omari Millanzi, 56.

Mapesa hayo yaliangukia mikononi mwa kigogo huyo baada ya kutumwa na ofisi ya Hazina ili yafanye kazi ya kuboresha elimu.

Hata hivyo kigogo huyo alizinyaka pesa hizo na kuzikandamizia kwenye mambo yake mwenyewe hadi aliposhtukiwa na kuburuzwa kortini.

Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Mkoa wa Ruvuma, Baptist Mhelela ndiye aliyesikiliza kesi juu ya sakata hilo na baadaye kumuona Millanzi ana hatia katika makosa 60 aliyoshtakiwa.

Akitoa hukumu hiyo, Hakimu Mhelela alisema kuwa kwa kuzingatia ombi la Mwendesha Mashtaka aliyetaka adhabu kali itolewe kwa mshtakiwa, na kwa kuzingatia vilevile kuwa mshtakiwa amekutwa na hatia ya makosa hayo yote, mahakama imeamua kumfunga jela mshtakiwa huyo kwa miaka mitatu kwa kila kosa, katika mashtaka 30 ya awali, hivyo kutakiwa atumikie jela kwa miaka 90.

Aidha, Hakimu Mhelela akasema kwa makosa mengine 30, kila kosa litampasa mshtakiwa atumikie jela kwa miaka mitano, hivyo jumla kuwa miaka mingine 150.

Jumla kuu ya kipindi cha adhabu za mshtakiwa huyo kilipaswa kuwa miaka 240 jela.

Hata hivyo Hakimu Mhelela alisema kwakuwa adhabu zote zitatumikiwa kwa pamoja, mshtakiwa atakwenda jela miaka mitano.
Pia Hakimu huyo akaamuru mshtakiwa alipe kiasi chote cha pesa alizoiba kwa mwajiri wake ambazo ni Sh. Milioni 24.1, mara tu baada ya kumaliza adhabu yake ya kifungo.

Kabla ya hukumu hiyo, upande wa mashtaka ukioongozwa na Inspekta George Omary, ulidai kuwa katika kipindi cha mwezi Januari na Julai mwaka 1998, mshtakiwa Millanzi aligushi nyaraka mbalimbali za Serikali na kuiba pesa hizo, kaisi cha Sh. Milioni 24.1.

Alipotakiwa kujitetea, ndipo mshtakiwa Millanzi alipomlilia hakimu na kumtaka ampunguzie adhabu akidai kuwa ana umri mkubwa na kuwa vilevile, ana familia inayomtegemea.

Mara kwa mara, Rais Kikwete amekuwa akisisitiza juu ya nidhamu ya matumizi mazuri ya pesa za umma na kuonya kuwa yeyote atakayekiuka taratibu, atachukuliwa hatua kali za kisheria.

SOURCE: Alasiri

Hawa wanaostahili kuitwa vigogo watafungwa lini na miaka mingapi???
Nafikiri vyombo vya habari, hasa reporter huyu kaweka kichwa cha habari kikubwa kuliko habari yenyewe, sijui wenzangu mnaonaje??

Kigogo ni mtu aliyeshindikana... akifanya kosa inataka moyo kumchukulia hatua
Ni mtu mwenye uzito katika jamii.. kwa maana ya uchache na madaraka.... yahitaji ujasiri kumkabili maana vijisenti vyake vyaweza kukufikisha pabaya!
Kigogo ni yule anayeonekana mbele ya jamii yake kama mtu aliyejuu ya wengine kwa maana ana madaraka, hali bora kiuchumi au uwezo wa kitu fulani hasa fedha!
Kamusi itakupa maana tofauti kabisa na haya niliyoyasema hapo juu! itakuambia kuwa kigogo ni kijigogo kidogo LOL!
Chagua maana kufuatana na hali husika!
 
Ila huyu si kigogo. Kwa kichwa cha gazeti kilivyo na maelezo yalivyo hana ukigogo wo wote ila alikuwa mzembe fulani.Labda akienda huko lupango atajifunza tabia njema.
 
...Labda akienda huko lupango atajifunza tabia njema.

...LOL! as if huko Lupango ni Chuo! ...kama pale kiinua miguu, eti; 'Chuo cha mafunzo!'
 
Kila mwenzao akikamatwa basi humpakazia kuwa yeye ndio Kigogo yaani kama wewe ni CCM basi usiombe kukumbwa na balaa ,walewale malafiki zako ndio watakao kupa cheo na kukuita Kigogo kumbe ndio wanakutoa mhanga na kilemba cha ukoka.
 
Naomba kuelimishwa maana ya private message.
Mimi kwa mawazo yangu nilikuwa nafikiria kuwa private message haiwezi kuonwa na mtu mwingine yeyote zaidi ya mtumiwa(Receiver) na sender, lakini cha kushangaza ukichagua jina la mwanajf yeyote ukibonyeza jina lake kuna kiwndow kinajitokeza hapo kuna mengi unachagua unalotaka kama ni kumtumia private message au vinginevyo. sasa ya kwanza kabisa imeandikwa view public profile. hapo utaona private message zote alizotumiwa. je ndivyo ilivyokusudiwa au kuna makosa ya kiufundi au mimi ndiye sielewi???.
Naomba msaada kwa anayejua.
 
You are mistaken doug unachoona ni Visitor messages!Unless na mimi nimechanganyikiwa!
Actually I have left a visitor message for you in your profile.Ila what I believe PM that is Private Message is strictly between the sender and receiver!
 
You are mistaken doug unachoona ni Visitor messages!Unless na mimi nimechanganyikiwa!
Actually I have left a visitor message for you in your profile.Ila what I believe PM that is Private Message is strictly between the sender and receiver!

kevo nishai hiyo picha yako....inatisha watoto!!! rudisha ile ya Amin, tafadhali!!. hii ni mojawapo ya pm zako sema kama sivyo
 
You are mistaken doug unachoona ni Visitor messages!Unless na mimi nimechanganyikiwa!
Actually I have left a visitor message for you in your profile.Ila what I believe PM that is Private Message is strictly between the sender and receiver!

Kevo you right, nilikuwa sijui. thanx
 
maneno mapya kwenye lugha ya kiswahil.... angalia attachment
 

Attachments

  • kiswahili.pdf
    46.8 KB · Views: 251
Habari za hapa viajan wenzangu.

Kwa kweli hapa mimi ni mgeni lakini nimefurahishwa sana na forum hii.
Jana nilikuwa nasoma habari katika mtandao wa bbc nikapata habari mmoja nzuri kweli kwamba Microsoft anatoa software kwa lugha ya kiswahili ambayo lugha hii kwa sasa inazungumzwa takriban na watu millioni 110, lakini katika software hio kuna maneno ya kiswahili ambayo kwa kweli mimi sijaona ndani maana sijaata maana yake wala sijui.
Hivyo nilikuwa naomba mnipe maana yake:-

Kiolesura na Kipeto

Ahsanteni
 
Habari,

Nimetizama kwenye website ya microsoft na kuoanisha ilivyoandikwa kwa lugha nyingine; hebu angalia mfano huu,

Kipeto hiki cha Kiolesura cha Microsoft Office 2003
This Interface Pack for Microsoft Office 2003
 
Back
Top Bottom