Kisa Cha Idi Amin Na Mwandishi Wa Kitanzania!

Status
Not open for further replies.
Hivi inakuwaje mtu ambaye analalamika kuchukiwa humu ndani halafu status yake inakuwa hivi?
Likes Received 353
Likes Given 11

==>read at 1243hrs today

Well, nafahamu hizo stats peke yake hazi conclude chochote...lakini pengine zinaweza kutupa pa kuanzia? Still thinking.....
 
Watu wanaishi mpaka kufa wakidhani wameijua dunia vizuri kwa kusoma magazeti, blogs, kuangalia tv nk. There is a lot that happens as part of the editorial processes that evetually affect what we get as news. Magazeti kama Uhuru, Tanzania Daima, Redio kama Imani, Tv kama TBC nk zafahamika kwa kuchukua pande zao. It is useless for example kujadili kwa nn gazeti la Uhuru au Habari leo limeipendelea serikali. La muhimu ni kusoma lile 'unalodhani' ni neutral. Kama mwandishi, unaweza kujitahd kuwa mwangalifu na ukafanya kazi objectively, ukapata wakati ulimi ukateleza au ukashindwa ku-repress hisia zako na ndoto zako, na hivyo zikaonekana ktk maandishi yako. Hapo ni kuteleza, and there is always room for you to stand and re-evaluate yourself. Mm gazeti likinitia mashaka, naachana nalo, sina haja ya kumshambulia mweandishi au gazeti lenyewe, maana wakati mwingine ni sababu za survival tu-a livelihood strategy.
 
Mkuu mimi nilisoma ile thread yako ya awali kwa kweli bila chuki wala uhasama naweza kusema kuwa ilikuwa na mapungufu yake. Mle uliandika ngongera, hapakuwa na content wasomaji wako wengi walibaki watupu bila kuelewa lengo la habari ile. kwa upande mwingine msomaji wako angeweza kupata jazba baada ya kuelewa kuwa wewe ulikuwepo kwenye eneo la tukio ukiongea na watu uliosema wana uelewa wa tukio kwa upana wake kwa sababu waliliona live likitokea, na ulikuwa na nafasi ya kuwaunganisha hewani wakasikika live radioni, lakini ukaamua kutokufanya hivyo, matokeo yake unawaambia wasomaji wako waende huko ili wapate ukweli uliofichika wa tukio!!! Ni ukweli upi huo??? wewe tayari ulikuwepo, uliongea na mashuhuda kwa nini usiuseme huo ukweli???

Kwa maarifa yangu madogo niliyo nayo nilihisi wewe unatafuta namna ya kuweka "spin" kwenye tukio na hapa umeanza kwa kutaka watu waamini kuwa hivyo wanavyojua kumbe sivyo!!!
Hongera kwa kumwelewa.Kwanza huyu jamaa nimnafiki.Hata kama mtu amefanya mazuri mangapi halafu leo hii mtu huyo aje amwue baba yako mzazi utakuja msifia huyo mtu hata siku moja?Lini ukaona mtu anamsifia muuaji hata kama alitenda mema mangapi.Huyu jamaa upeo ni mdogo namshangaa anapotoa mfano wa IDD AMIN na mwandishi wa habari nikapata picha alivyo.
 
Maggid nadhani ushafahamu nini ni feedback ya wasomaji wako, ujumbe uko wazi hatutaki propaganda na ukada.
 
Mi naona unalialia tu. Au ulikuw umetoka kwenye usingizi mzito mpaka unaandika haya?,,,,,mbona na wewe umeandika kwa chuki km hao unaowalaumu?
 
Kwa hiyo kwa kuwa watu wengi waliipigia kura ccm (kusema eti waliiba siyo logical hapa) ina maana ilani ya ccm ilikuwa bora kulikoya chadema? wakati fulani wengi wanaweza kuwa upande usio sahihi,hiyo ina maana uwingi huo unaweza kubadili jambo baya likawa jema au uongo ukawa ukweli? ni hivi nikiwa wazi zaidi,kwa kuwa feedback ya watu wengi humu,wameonyesha kutomuunga mkono maggid ( mimi naamini hawajaelewa alichosema,na hii siyo ajabu,kwani kuna wakati mtu haelewi kwa matatizo yake ya ufinyu wa uelewa) ndo tuseme amekosea? no wengi wamepotoka na maggid japo mmoja na wachache tunaomuunga mkono tuko right
 
Naona hoja aliyotoa mdau ni ya mtu mwoga.Ameonesha woga. Ati kwama anachukiwa,huo ni woga tu. Hoja zinajibiwa kwa hoja.
 
Mimi huwa sikipendi........ndio unafiki wenyewe

hahaaa mkuu read btn lines, huwa akiona hoja zimemuelemea anakwenda kulialia kwenye blog yake na facebook wakati huo akiwa amekata mguu hapa JF kwa miezi na baada ya hapo anaanza kuandika habari za kujikomba kule alipochafua ili kuwarudisha wasomaji wake... akiona watu wamesahau anarudi tena JF na baada ya muda utaona anarudia kuandika vitu vya ajabu.

Huyo ndiye maggid wa kuuma na kupuliza
 
hahaaa mkuu read btn lines, huwa akiona hoja zimemuelemea anakwenda kulialia kwenye blog yake na facebook wakati huo akiwa amekata mguu hapa JF kwa miezi na baada ya hapo anaanza kuandika habari za kujikomba kule alipochafua ili kuwarudisha wasomaji wake... akiona watu wamesahau anarudi tena JF na baada ya muda utaona anarudia kuandika vitu vya ajabu.

Huyo ndiye maggid wa kuuma na kupuliza

Halafu anataka kulazimisha yale anayo yaamini yeye kuwa sahihi. Ukimpinga kosa
 
Halafu anataka kulazimisha yale anayo yaamini yeye kuwa sahihi. Ukimpinga kosa


Maggid atambue kuwa mabandiko yake ni ''maoni'' tu na wala si lazima yawe ama yafanane na ''ukweli''.Na maoni yanategemeana na imani,ufahamu,elimu, matarajio,matamanio na mwelekeo wa mwandika maoni.
Atambue kuwa anatakiwa kujenga uwezo wa kuandika maoni yake huku akifikiri sawa sawa kwa kuwa yeye hamiliki ukweli.Ukweli unatafutwa nasi tunazidi kuutafuta pasipo kuchoka.Ahakikishe wanaosoma maandishi yake wanapata thamani ya pesa na muda unaotumiwa katika kutafuta na kusoma maandiko yake.
Ajue,vile vile, kuwa wapo wanaoandika ukweli hapa Tanzania na wanafahamika na kuheshimika na Watanzania.
Hata hivyo,kwa sababu za wazi watu hao wanachukiwa na kuogopwa na tabaka tawala.
Naye,aache kuchezea akili za watu.Achague sasa:kuendelea kuwa upande wa watawala ama kuwa na wananchi.
 
Maggid atambue kuwa mabandiko yake ni ''maoni'' tu na wala si lazima yawe ama yafanane na ''ukweli''.Na maoni yanategemeana na imani,ufahamu,elimu, matarajio,matamanio na mwelekeo wa mwandika maoni.
Atambue kuwa anatakiwa kujenga uwezo wa kuandika maoni yake huku akifikiri sawa sawa kwa kuwa yeye hamiliki ukweli.Ukweli unatafutwa nasi tunazidi kuutafuta pasipo kuchoka.Ahakikishe wanaosoma maandishi yake wanapata thamani ya pesa na muda unaotumiwa katika kutafuta na kusoma maandiko yake.
Ajue,vile vile, kuwa wapo wanaoandika ukweli hapa Tanzania na wanafahamika na kuheshimika na Watanzania.
Hata hivyo,kwa sababu za wazi watu hao wanachukiwa na kuogopwa na tabaka tawala.
Naye,aache kuchezea akili za watu.Achague sasa:kuendelea kuwa upande wa watawala ama kuwa na wananchi.

Yeye naye kama yule mwana wa Malecela........akizidiwa hoja ataanza ''unajua nilipokuwa Sweden'' as if sisi wengine hatujatembea....huu ulimbukeni wa kufika ulaya unapotosha sana watu wengi
 
Maggid Badili JINA, hilo ndilo mchawi wako humu JF! Kwa kuwa mtu mzima utaelewa! Kuna watu wakiona majina yanayofanana na lako tu, chuki inafunguka!
 
....Idi Amin akatamka; " Kama ni hivyo, basi, rudi nyumbani Tanzania na huende ukaandike jambo moja tu zuri kuhusu Idi Amin!"

Mwandishi yule Mtanzania hakuamini masikio yake kuwa Idi Amin amemwachia huru!
Maggid, naanza kuhisi kuwa labda wewe si mwandishi wa habari, na kama ni mwandishi wa habari basi ni aina ya wale waandishi wa habari tulio nao wengi Tanzania, ambao wanaweza kuwa waandishi wa habari wazuri tu, lakini ukweli ni kwamba hawakusomea uandishi wa habari na walisoma mambo yanayowasaidia kuwa waandishi wa habari, mfano, BA education, economics, english language nk.

Angalia kwamba uandishi wa habari wa magazetini una malengo mawili makubwa; kuhabarisha na kusisimua (inform and sensationalize). Habari kwa mfano, kwamba treni iliondoka Dar na kufika Kigoma salama na kila abiria akaenda nyumbani kwake na ndugu zake kufurahi inahabarisha, lakini haisisimui, na hivyo haitafanya gazeti liuzike. Lakini ukisema treni ya abiria toka Dar kwenda Kigoma ilishindwa kupanda milima ya Serenda baada ya kichwa kuungua na kusababisha watu kujeruhiwa - watu watataka kuisoma kwa kuwa zaidi ya kuhabarisha kuna msisimko ndani ya habari hiyo, ambao pia unatokana na hofu ya kupoteza wapendwa.

Uandishi wa habari kwa ajili ya magazeti ni tofauti na uandishi wa matukio kwa ajili ya kumbukumbu.

Sasa wewe unatupa mfano wa watu kuandika mazuri tuu, bwana, hayo ni magazeti ya China, ya leo na zamani, kama unakumbuka enzi zile ya Gazeti la China la Picha toka Guozi Shudian.
 
Kiukweli, "neutrality" iko kinadharia zaidi kuliko katika hali halisi. Lazima watu tuvutiwe na "tunu" fulani na kukarahishwa na "ubovu/mishkeli" katika binadamu wenzetu na/au taasisi kama vyama vya siasa, dini, n.k. Cha maana hapa ni kama kwa msomi au, kama tunavyopenda kujiita, GTs, upimaji wetu wa tunu na mishkeli unaongozwa na mantiki pana au hisia duni (primitive instincts/emotions). Kama kuna watu au vyama vyenye kusimamia kwa dhahiri tunu zinazokubalika katika jamii kimantiki basi sioni taabu kwa GT kujitambulisha na watu au vyama hivyo na kunyooshea kidole wale wanaokwenda kinyume hata ndani ya chama kinachohusika. Vilevile, itashangaza kwa GT kupigia chapuo au kuwa mtetezi wa watu au vyama ambavyo vinajitambulisha (kimatendo) kusimamia ukiukaji wa maadili na/au kutetea mishkeli.

Tukizingatia kwamba kuna mabaya na mazuri hapa duniani basi tukubali, neutrality, si mtazamo unaokubalika. Pia, utetezi wa kusema "na mazuri yangu muyaone basi" haukubaliki. Nakumbuka hata rais amekuwa akiutumia mashambulizi yakizidi. Hakuna binadamu hapa duniani ambaye hana au hajawahi kuwa na mazuri. Hata akina Nero, Hitler, Stalin, Al-Capone na Osama walikuwa na mazuri yao lakini, kimantiki, hakuna kipimo cha "mema/mazuri" chenye kuweza kuleta maana kwenye mishkeli/uovu/ubazazi wa kudhamiria!

Tukija kwa ndugu yangu Maggid, huyu ni mwandishi mzuri kwa upangiliaji wa maelezo na uelezaji wa hisia zake. Kwamba hapendi na anapinga ufisadi, uonevu na mabaya yote katika jamii, amejieleza vya kutosha katika makala zake nyingi. Lakini inapokuja "kuwagusa" wahusika wakuu wa mfumo mbovu unaolea na kuendeleza maovu hayo hapo ndipo utakapomuona sio tu akikwama, bali akielemea kuwaelezea visivyo wanaoendesha mapambano ya moja kwa moja na mfumo mbovu wa utawala. Na hapo ndipo inakuwa rahisi kwa wengi kumuona kama yuko upande wa chama tawala. Nadhani, mzigo alio nao ni kwamba amejenga utii mkubwa sana kwa rais wa nchi (pengine kuliko ccm yenyewe) kiasi kwamba mashambulizi yakielekeaelekea huko, basi anapata taabu sana. A kind of instinctive personal allegiance to the president and some close associates.

JMushi1 amempa ushauri wa kweli; ajiweke wazi amesimamia wapi hasa na si kujaribu kutafuta kukubalika na jamii. Si rahisi kwani neutrality ni dhana ya kufikirika zaidi!
 
mimi sitochangia chochote maana hizi nyundo alizotwangwa zinamtosha kabisa waandishi wa tanzania mnasalitiana kwa malipo ya kutia aibu siku ingine jitahidi kubalance uandishi wako,sio kuegemea upande wazwazi na usitoe taarifa nusu nusu au uliogopa anaekuagizaga na kukupangia cha kuandika atakasirika.
 
Ndugu zangu,

Nilikuwa kibaruani mpaka muda huu. Nimeingia humu JF na kupitia comments zote kwenye thread yangu ya asubuhi kuhusi nilichokiona na kukisikia kule Nyololo. Kuna waliotoa maoni yaliyojaa chuki na mashambulizi binafsi. Hakika naliona hili la chuki kutawala humu JF.

Ukweli, kuna wanaonekana kuandika maoni yao yaliyojaa chuki badala ya hoja. Wakati mwingine najiuliza; hivi hawa ni Watanzania? Maana, Watanzania hatuna hulka ya chuki za namna hii. Kuna mwingine akiliona jina langu tu anatanguliza chuki. Na kila sentesi yangu niliyoandika anatafuta ni wapi nimeteleza ili anishambulie. Kuna ambao hawaoni hata moja jema la kwangu.

Inanikumbusha kisa cha Idi Amin na mwandishi wa Kitanzania.

Inasemekama makachero wa Idi Amin walimnasa mwandishi wa Kitanzania ndani ya mpaka wa Uganda. Mwandishi yule akafikishwa mpaka kwa Idi Amin mwenyewe.

Alipofika kwa Amin, mwandishi yule wa Kitanzania akaamini kuwa amekwisha, kuwa atauawa. Idi Amin akamkaribisha kiti na soda anywe. Kisha akamwuliza; " Hivi nyinyi waandishi wa Tanzania mnaandika mabaya tu kuhusu mimi. Nikuulize, unadhani hakuna hata jambo moja zuri ambalo Idi Amin amelifanya?"

Mwandishi yule Mtanzania akajibu; " Ni mengi tu mazuri umefanya Mheshimiwa Rais!"

Idi Amin akatamka; " Kama ni hivyo, basi, rudi nyumbani Tanzania na huende ukaandike jambo moja tu zuri kuhusu Idi Amin!"

Mwandishi yule Mtanzania hakuamini masikio yake kuwa Idi Amin amemwachia huru!

Usiku Mwema.

Maggid,
Iringa.


hata kikwete ndio hivyo kila anachofanya ni kibaya
 
Ndugu zangu,

Nilikuwa kibaruani mpaka muda huu. Nimeingia humu JF na kupitia comments zote kwenye thread yangu ya asubuhi kuhusi nilichokiona na kukisikia kule Nyololo. Kuna waliotoa maoni yaliyojaa chuki na mashambulizi binafsi. Hakika naliona hili la chuki kutawala humu JF.

Ukweli, kuna wanaonekana kuandika maoni yao yaliyojaa chuki badala ya hoja. Wakati mwingine najiuliza; hivi hawa ni Watanzania? Maana, Watanzania hatuna hulka ya chuki za namna hii. Kuna mwingine akiliona jina langu tu anatanguliza chuki. Na kila sentesi yangu niliyoandika anatafuta ni wapi nimeteleza ili anishambulie. Kuna ambao hawaoni hata moja jema la kwangu.

Inanikumbusha kisa cha Idi Amin na mwandishi wa Kitanzania.

Inasemekama makachero wa Idi Amin walimnasa mwandishi wa Kitanzania ndani ya mpaka wa Uganda. Mwandishi yule akafikishwa mpaka kwa Idi Amin mwenyewe.

Alipofika kwa Amin, mwandishi yule wa Kitanzania akaamini kuwa amekwisha, kuwa atauawa. Idi Amin akamkaribisha kiti na soda anywe. Kisha akamwuliza; " Hivi nyinyi waandishi wa Tanzania mnaandika mabaya tu kuhusu mimi. Nikuulize, unadhani hakuna hata jambo moja zuri ambalo Idi Amin amelifanya?"

Mwandishi yule Mtanzania akajibu; " Ni mengi tu mazuri umefanya Mheshimiwa Rais!"

Idi Amin akatamka; " Kama ni hivyo, basi, rudi nyumbani Tanzania na huende ukaandike jambo moja tu zuri kuhusu Idi Amin!"

Mwandishi yule Mtanzania hakuamini masikio yake kuwa Idi Amin amemwachia huru!

Usiku Mwema.

Maggid,
Iringa.

ndio maana hata kikwete anawaangalia tu hawa waandishi
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom