Kisa Cha Idi Amin Na Mwandishi Wa Kitanzania!

Status
Not open for further replies.

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Nilikuwa kibaruani mpaka muda huu. Nimeingia humu JF na kupitia comments zote kwenye thread yangu ya asubuhi kuhusi nilichokiona na kukisikia kule Nyololo. Kuna waliotoa maoni yaliyojaa chuki na mashambulizi binafsi. Hakika naliona hili la chuki kutawala humu JF.

Ukweli, kuna wanaonekana kuandika maoni yao yaliyojaa chuki badala ya hoja. Wakati mwingine najiuliza; hivi hawa ni Watanzania? Maana, Watanzania hatuna hulka ya chuki za namna hii. Kuna mwingine akiliona jina langu tu anatanguliza chuki. Na kila sentesi yangu niliyoandika anatafuta ni wapi nimeteleza ili anishambulie. Kuna ambao hawaoni hata moja jema la kwangu.

Inanikumbusha kisa cha Idi Amin na mwandishi wa Kitanzania.

Inasemekama makachero wa Idi Amin walimnasa mwandishi wa Kitanzania ndani ya mpaka wa Uganda. Mwandishi yule akafikishwa mpaka kwa Idi Amin mwenyewe.

Alipofika kwa Amin, mwandishi yule wa Kitanzania akaamini kuwa amekwisha, kuwa atauawa. Idi Amin akamkaribisha kiti na soda anywe. Kisha akamwuliza; " Hivi nyinyi waandishi wa Tanzania mnaandika mabaya tu kuhusu mimi. Nikuulize, unadhani hakuna hata jambo moja zuri ambalo Idi Amin amelifanya?"

Mwandishi yule Mtanzania akajibu; " Ni mengi tu mazuri umefanya Mheshimiwa Rais!"

Idi Amin akatamka; " Kama ni hivyo, basi, rudi nyumbani Tanzania na huende ukaandike jambo moja tu zuri kuhusu Idi Amin!"

Mwandishi yule Mtanzania hakuamini masikio yake kuwa Idi Amin amemwachia huru!

Usiku Mwema.

Maggid,
Iringa.
 
Mkuu ungekuwa unajitahidi na kujiweka wazi kuwa wewe ni mfagiliaji wa magamba,basi watu wasingekushambulia wewe personaly,tatizo ni kutokuwa straight na unafiki kwa kusema ukweli.Sasa hiyo ya Idi Amini unataka kusema kitu gani?kwamba waandishi wenzako waandike mema ya polisi ama?

Ile thread sijui ya siku nne za kijijini Nyonyolo nayo ulifanya the same.Yani unataka kuutetea unyama wa polisi na serikali ya ccm kwa hadithi za alinacha ama kama zile za alfa lela ulela.

Very sad,kwasababu wengine tunakosoma kabisa wapi unaelekea lakini we unadhani hatuoni.Ni sawa na ile stori ya mfalme juha mwenye joho akidhani hayuko uchi.

Go straight to the point ili watu wawe na hoja za kujadili.Kama unaleta mjadala ambao watu wanaona unafiki unategemea wajadili kitu gani?

Usiku mwema na wewe.
 
hahahahahahaaaaa! nimecheka kweli. kumbe nduli amini alikuwa anatoa mpaka takrima za soda ili aandikwe vizuri. Usiku mwema pia kaka yangu maggid.
 
Mi nadhani ni wakati sasa wa kuonesha tofauti kati ya wasomi kwani wao hujenga hoja,hujadili mambo kwa kina. Sisi sote tu watanzania.hatupaswi kukosana leo kwa mambo tunayojua ukweli wake. Hata huyu jamaa nae yapo mazuri amefanya kama kakosea hebu tuwe na moyo wa kusameheana tuache chuki
 
Ndugu zangu,

... Maana, Watanzania hatuna hulka ya chuki za namna hii. Kuna mwingine akiliona jina langu tu anatanguliza chuki.

Siyo kweli. Mfano, polisi (ni watanzania hao) wakiona jina au shughuli ya chama fulani wanatanguliza chuki hadi wanaua.
 
Mkuu hayo ni mambo ya kawaida katika jamii ya wengi na ndiko tunakojifunzia kuishi na wayu
 
Mkuu ungekuwa unajitahidi na kujiweka wazi kuwa wewe ni mfagiliaji wa magamba,basi watu wasingekushambulia wewe personaly,tatizo ni kutokuwa straight na unafiki kwa kusema ukweli.Sasa hiyo ya Idi Amini unataka kusema kitu gani?kwamba waandishi wenzako waandike mema ya polisi ama?

Ile thread sijui ya siku nne za kijijini Nyonyolo nayo ulifanya the same.Yani unataka kuutetea unyama wa polisi na serikali ya ccm kwa hadithi za alinacha ama kama zile za alfa lela ulela.

Very sad,kwasababu wengine tunakosoma kabisa wapi unaelekea lakini we unadhani hatuoni.Ni sawa na ile stori ya mfalme juha mwenye joho akidhani hayuko uchi.

Go straight to the point ili watu wawe na hoja za kujadili.Kama unaleta mjadala ambao watu wanaona unafiki unategemea wajadili kitu gani?

Usiku mwema na wewe.

Jmushi,

Najua siku hizi vijana hawataki kuumiza sana vichwa vyao. Inanikumbusha wakati mmoja nikiwa Sweden miaka ya 90. Nilialikwa na vijana wa darasa moja kwenye Fokh High School niongelee kuhusu mgogoro wa DRC- Congo. Nikaanza kuelezea kilichopelekea hapo DRC Congo ilipofikia. Mmoja wa vijana wale akainua mkono na kuniuliza; " Tunaomba utwambie msimamo wako wa nani mbaya na nani mzuri katika pande mbili zinazovutana!"

Nikamwambia, kuwa katika dunia hii hakuna nyeupe na nyeusi tu, kwenye nyeusi unaweza kuiona nyeupe na kinyume chake. Ni hulka yetu wanadamu kuchagua jogoo wa kumshabikia wanapogombana jogoo wawili. Unafanyaje basi ukifahamu kuwa jogoo wote wawili wanagombania jambo la kijinga? Ndio, hakuna njia ya mkato wa kufahamu kiini cha tatizo.

Usiku Mwema Mushi.
Maggid
 
Mkuu mimi nilisoma ile thread yako ya awali kwa kweli bila chuki wala uhasama naweza kusema kuwa ilikuwa na mapungufu yake. Mle uliandika ngongera, hapakuwa na content wasomaji wako wengi walibaki watupu bila kuelewa lengo la habari ile. kwa upande mwingine msomaji wako angeweza kupata jazba baada ya kuelewa kuwa wewe ulikuwepo kwenye eneo la tukio ukiongea na watu uliosema wana uelewa wa tukio kwa upana wake kwa sababu waliliona live likitokea, na ulikuwa na nafasi ya kuwaunganisha hewani wakasikika live radioni, lakini ukaamua kutokufanya hivyo, matokeo yake unawaambia wasomaji wako waende huko ili wapate ukweli uliofichika wa tukio!!! Ni ukweli upi huo??? wewe tayari ulikuwepo, uliongea na mashuhuda kwa nini usiuseme huo ukweli???

Kwa maarifa yangu madogo niliyo nayo nilihisi wewe unatafuta namna ya kuweka "spin" kwenye tukio na hapa umeanza kwa kutaka watu waamini kuwa hivyo wanavyojua kumbe sivyo!!!
 
Mkuu TUMBIRI karibu huku. Mkuu maggid pamoja na kwamba humu kuna great thinkers lakini jaribu basi kuweka mambo wazi kidogo manake naona unanena kwa tamathali za semi na tafsida.
 
Last edited by a moderator:
Kaka maggid..salaam,
Mimi huwa nikiliona posts zako nakumbuka enzi za MRABA WA MAGGID labda ndio sababu bado sijaweza kukuchukia.
One thing i know of uandishi wa habari ni kuwa impartial kwani the moment unaonesha upendeleo kwa side moja inakua weakness kubwa kwako kama muandishi.
Na hapa naongea nikujua kama binadamu lazima utakuwa una chama unachokipenda..una mtu fulani unayempenda ila kama mwandishi pale unaporipot jambo lazima ufiche personal preferences zako. Nadhani hili suala waandishi wengi wa habari wa siku hizi wameshindwa kulisimamia.
Tazama wale commentators wakati wa mpira wa miguu. Je unadhani hawana timu wanazozipenda? Je wakati timu yake inacheza na timu pinzani anakaa kutangaza tu pale ambapo mchezaji wa timu aipendayo anashika mpira? La hasha..lazima awe na principles za utangazaji. IMPARTIALITY.
polisi nao ni chombo kingine kitakiwacho kuwa na impartality...unadhani hawana vyama wavipendavyo??!
Anyway..my point is..inawezekana kabisa at some point umejikuta kwasababu ya ubinadamu wako umeegemea upande mmoja (take the hint from people..kwani lisemwalo...) ila bado kwangu utabaki mwandishi pekee anayeweza kueleza jambo (kukupa news as it is) bila wewe msomaji kujua mwandishi anaegemea upande upi.
Big up bro maggid...
Ni vizuri kujifunza from th peoples comments ila pia i wish journalists wa siku hizi wangejifunza jambo kutoka kwako..the likes of kibonde et al...
 
Last edited by a moderator:
Ndugu Maggid, pole kwa mkasa.

Kwanza, naomba nieleze masikitiko yangu juu ya tabia uliyoifanya leo. Umenazisha thread sensitive halafu ukaingia mitini, huo siyo ustaarabu.

Pili, naomba usiyape kipaumbele sana maoni ya chuki. Mara nyingi chuki huwa ni dalili ya woga. Ukiona mtu anakuchukia ujue kashajiamulia kuwa yeye ni inferior kwako.
Kuchukiwa vilevile ni ishara kuwa kitu unachofanya kina impact.
Ukipita barabarani kuna vichaa wanaokota takataka na wachafu sana, vilevile wanatoa harufu mbaya lakini watu hawawachukii hawa. The moment you start to do something with sense lazima litatokea kundi la kukuchukia. Sote tumeface hiyo na jinsi ya kudeal nayo ni very simple, ignore the chuki concentrate kwenye hoja.

Nimesikitika kuona katika kujibu kwako umetoa kipaumbele kwa wale wenye chuki na kuziacha kabisa hoja ambazo zilikuwa nyingi na nzito. Hivi kweli siku hizi chuki zinapewa nafasi kubwa kujadiliwa kuliko hoja.

Anyway, hamna noma "kichaa wangu!" usiku mwema.
 
Mkuu TUMBIRI karibu huku. Mkuu Maggid pamoja na kwamba humu kuna great thinkers lakini jaribu basi kuweka mambo wazi kidogo manake naona unanena kwa tamathali za semi na tafsida.

Kimbunga,
Shukrani kwa kunishtua juu ya huu mjadala. Tatizo la Maggid kama alivyosema Jmushi1 ni kutoku declare his Interest ndiyo maana huku akijidai ni mwandishi huru wakati maandishi yake yanamtafsiri yeye ni mtumwa wa naini. Akiendeleza ukaidi tutaendelea kumshindilia hoja moja baada nyingine. Na tatizo lake lingine na ukaidi wake wa kutojibu Maswali yetu Magumu yanayoelekezwa kwake. Ajifunze toka Pasco ambae ameweka wazi yupo nyuma ya Lowassa.

Kamanda Matola, karibu na wewe.
 
Last edited by a moderator:
Jmushi,

Najua siku hizi vijana hawataki kuumiza sana vichwa vyao. Inanikumbusha wakati mmoja nikiwa Sweden miaka ya 90. Nilialikwa na vijana wa darasa moja kwenye Fokh High School niongelee kuhusu mgogoro wa DRC- Congo. Nikaanza kuelezea kilichopelekea hapo DRC Congo ilipofikia. Mmoja wa vijana wale akainua mkono na kuniuliza; " Tunaomba utwambie msimamo wako wa nani mbaya na nani mzuri katika pande mbili zinazovutana!"

Nikamwambia, kuwa katika dunia hii hakuna nyeupe na nyeusi tu, kwenye nyeusi unaweza kuiona nyeupe na kinyume chake. Ni hulka yetu wanadamu kuchagua jogoo wa kumshabikia wanapogombana jogoo wawili. Unafanyaje basi ukifahamu kuwa jogoo wote wawili wanagombania jambo la kijinga? Ndio, hakuna njia ya mkato wa kufahamu kiini cha tatizo.

Usiku Mwema Mushi.
Maggid
Nimeshindwa kukuelewa,na kwa taarifa yako,hao vijana unaodai wa huko Sweden miaka ya 90 si sawa sisi ama vijana wengine unaoongea nao humu,ume generalize bila kujuwa things are different na hadithi hadithi ni mambo ya zamani.Now days you go straight to the point,right on the money.Umenishangaza sana kule ulipokwenda kusaka ukweli,ukaupata(my guess),lakini unawaambia wananchi waende wakausake wenyewe.Na kitu ulichoandika ni kama tu hadithi za paka na panya.
Usiku mwema ndugu maggid.
 
Mkuu ungekuwa unajitahidi na kujiweka wazi kuwa wewe ni mfagiliaji wa magamba,basi watu wasingekushambulia wewe personaly,tatizo ni kutokuwa straight na unafiki kwa kusema ukweli.Sasa hiyo ya Idi Amini unataka kusema kitu gani?kwamba waandishi wenzako waandike mema ya polisi ama?

Ile thread sijui ya siku nne za kijijini Nyonyolo nayo ulifanya the same.Yani unataka kuutetea unyama wa polisi na serikali ya ccm kwa hadithi za alinacha ama kama zile za alfa lela ulela.

Very sad,kwasababu wengine tunakosoma kabisa wapi unaelekea lakini we unadhani hatuoni.Ni sawa na ile stori ya mfalme juha mwenye joho akidhani hayuko uchi.

Go straight to the point ili watu wawe na hoja za kujadili.Kama unaleta mjadala ambao watu wanaona unafiki unategemea wajadili kitu gani?

Usiku mwema na wewe.

Katika uandishi usiyo na chembe za ushabiki, huwa namkubali Mjengwa. Tatizo ninaloliona kwa wanajf wengi, ni kutokuamini kuwa kuna watu ambao ni neutral.
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom