Kisa Cha Idi Amin Na Mwandishi Wa Kitanzania!

Status
Not open for further replies.
Katika uandishi usiyo na chembe za ushabiki, huwa namkubali Mjengwa. Tatizo ninaloliona kwa wanajf wengi, ni kutokuamini kuwa kuna watu ambao ni neutral.

Hapa hatuendi kwa imani,tunaenda kwa facts,tutaku judge kwa kile unachoandika.Kama wewe unaona yuko neutral,basi lazima mabandiko yake yakufurahisha.Mimi nimeisoma hiyo "neutrality" kuwa ni unafiki.Hilo nilishaliona kitambo sana tu.Wala sina haja ya kuona alichoandika ili kujuwa kwamba atakuwa ameandika kitu ama hoja kwa mwelekeo gani.

Awe neutral akale wapi?uandishi ni kazi ngumu na ya kujitolea,if you're not yourself,utaumbuka kwasababu unafiki hausimamiwi.Otherwise utaonekana kituko.
 
ZeMarcopolo Pili said:
Kutofautiana kimtizamo si chuki ,uhasama ama uadui.Tunatofautiana kwa sababu, kila mmoja wetu, anayo itikadi yake, anao ufahamu wake,anao maslahi yake,anayo matarajio yake,anayo asili yake.Kutofautiana ni lazima kwa sababu sote,kwa wakati mmoja, hatuwezi kuwaza na kufikiri kwa namna mmoja.
Kama huo ni ukweli napenda nitofautiane na maelezo ya Ze Macopolo kuhusu utetezi wa Maggid.Nieleze kuwa mtu hapingwi kwa sababu anaonekana yupo superior dhidi ya wanaompinga.Kwa mujibu wa Ze Macopolo,sote tuliompinga Maggid tupo inferior kwake jambo ambalo si kweli hata kidogo.Kila mwananchi mwenzetu anayeweka mawazo hadharani atambue kuwa lazima watakuwepo watu watajitokeza kuhoji ukweli na usahihi wa hoja zake.Kwa kulitambue hilo,ni budi ,sote,tuweke jitihada kuusaka na kuusambaza ukweli kadiri ulivyo (absolute truth) na wala si kadiri unavyoonekana(relative truth).Tulimtaka,kwa mfano atueleze kwa nini anajibanza katika kona ya ''impartility'' katika mazingira yasiyohitaji impartiality...Kwa maelezo ya Ze Macopolo,mzizi wa tofauti za hoja za kisiasa kati ya Democtrats na Republican,USA, ni uwepo wa chama/mgombea amabaye ni inferior dhidi ya chama /mgombea superior!
Msingi wa hoja za kisiasa, ama hata zisizo za kisiasa, ni tofauti za kimsingi zinazotokana na tofauti za kimitazamo,imani,mwelekeo,falsafa,itikadi nk.Wala tofauti za hoja za kisiasa,USA, haziwezi kutokana na rangi ya Obama dhidi ya rangi ya Romney.
Kama askari wamesababisha kifo cha mwananchi mwenzetu,mwandishi ama raia yeyote anapaswa achague upande:ama awe upande wa Jeshi la Polisi ama awe upande wa raia aliyekatishwa uhai wake kinyama.Binasfi nilimtaka apangue hoja zetu kuhusu ulazima ,umuhimu na nafasi ya imparility katika tukio la Iringa na hakufanya hivyo. Isipokuwa, akatuona tuna chuki naye.Tungependa arejee hapa jamvini apangue hoja...Si kila anayepingwa anachukiwa.Wengine hatujui kuchukia wanadamu wenzetu isipokuwa ''tunachukia'' hoja.
Kwa kuwa Maggid amekuwa akiandika makala kwa muda mrefu sasa, tulimtazamia amejenga uwezo wa kuhimili maono kinzani.Inaelekea anatuona sisi tuliopinga hoja zake kama watu tunaomchukia yeye kibinafsi!Kinachopingwa ni hoja zake si yeye kama Maggid.
 
Hii post ya Majid sijui kwa nini imenikumbusha stories za Bulicheka? I think Majid you need to take a rest for now, pumzika kidogo maana timing ya hizi posts zako hivi karibuni zinaweza kutibua nyongo za watu. You may have a point but timing inaleta mushkeli!
 
Kimbunga,
Shukrani kwa kunishtua juu ya huu mjadala. Tatizo la Maggid kama alivyosema Jmushi1 ni kutoku declare his Interest ndiyo maana huku akijidai ni mwandishi huru wakati maandishi yake yanamtafsiri yeye ni mtumwa wa naini. Akiendeleza ukaidi tutaendelea kumshindilia hoja moja baada nyingine. Na tatizo lake lingine na ukaidi wake wa kutojibu Maswali yetu Magumu yanayoelekezwa kwake. Ajifunze toka Pasco ambae ameweka wazi yupo nyuma ya Lowassa.

Kamanda Matola, karibu na wewe.
Is Maggid again!!?? TUMBIRI wacha nipumzike kwanza najuwa hii thread ametuanzishia sisi, lakini naapa kwa Mungu Matapeli na wanaondekeza njaa kama maggid sasa tutawashikisha adabu & i mean it.
 
Last edited by a moderator:
Kuna jambo linaniskitisha sana nnaposoma comments nyingi hapa..
Where have you placed th value of impartiality in journalism??! Kuna mwingine kasema eti usipoegemea chama utakula wapi...really??! Ndivyo wafunzwavyo siku hizi kwenye vyuo vya uandishi wa habari.
Unless you guys have personal issues with him..naomba niwaache muendelee kuzozana..
I wil say this once more, "Mwandishi yeyote anayeweza kulete habari kama ilivyo bila kumuonesha msomaji wapi ameegemea yeye kwangu mimi huyo ni mwandishi bora na anayefaa kuigwa."

Good morning guys...siku njema n a blessed Monday.
 
Jamiiforum ya sasa siyo ile nadhani iliyokusudiwa na akina mello.leo humu mara nyingi unakuta matusi tuuu watu wanatukanana.nilipojiunga nilikuwa na matazamio makubwa sana na caption ya great thinkers.kwa waliosoma na kuhitimu falsafa kama mimi,neno hilo ni zito.lakini hebu fikirini kwa nini watu wanasema jf imeingiliwa? tumetanguliza mno ushabiki wa siasa kuliko shughuli yetu kuu ya kufikiri na kuzalisha mawazo.
Nikiwa wazi zaidi,wamo wengi humu ambao bila kufanya uchambuzi wowote hutaka kila kitu kinachosemwa hapa kiwasifie chadema.najua wapo watakaosema mbona hata hoja za ccm na cuf na vyama vingine zinawekwa? waongo tu,wengi hapa wanataka mtu mkweli ni yule anayeshabikia chadema na kupinga kila kitu cha serikali,ccm na cuf at least.anayethubutu kusifia jambo fulani la serikali,au ccm,au cuf,basi huyo au ni mnafiki,katumwa,ana njaa,nk.sasa hii haimaanishi kwamba watu wa aina hiyo hawapo.wapo tena hata jf,lakini ni ujinga kudhani kila anayekuwa kinyume na chadema au viongozi wake,basi ni mnafiki au ana njaa.
Nikitazama haya kwa jicho la kifalsafa,naona uchovu wa kufikiri.wengi wetu hatuwezi shughuli ya kufikiri na hasa kunakohitaji muda mrefu.tunataka jibu fupi na la moja kwa moja.si huwa mnamsikia spika,mheshimiwa jibu kwa kifupi.sasa niwarejeshe kwa Maggid,alipoandika juu ya umuhimu wa kutogomea habari za polisi,mimi ni kati ya watu wa kwanza kuchambua hoja yake kwa kina na kwa muono wa kifalsafa.wangu ni kati ya mitazamo mingi inayoweza kuelezea alichokifanya na kuona kama kilifaa au hakikufaa.kati ya mengi aliyosema maggid ni umuhimu wa wanahabari sasa kushambulia polisi kwa nguvu,kulazimisha ukweli ujulikane na polisi iwajibike.kwamba kuabsract na kusema tunagomea habari za polisi kwa ujumla ni jambo siyo tu lisilofaa bali pia lisilo masilahi kwa jamii.na hapa pengo la mwanahalisi limeonekana.Hakuna hadi sasa gazeti,television,au redio iliyoweza kutwambia majina ya waliohusika,au mfano yule askari aliyejeruhiwa ni nani kwa jina na cheo,na sasa yuko wapi?,wananchi hawajui habari hizo.wapo gizani.
Haya kuna azimio walilopitisha siku ile la kujitoa kwenye kamati zozote za wiki ya nenda kwa usalama barabarani,niambieni kwa jina ni mwandishi gani amejitoa huko kama kutekeleza msimamo wa wanahabari?.SASA Maggid alikuwa sahihi na imethibitika bila shaka kwamba vyombo vyote vya habari vimeendelea kuripoti habari za polisi na hakuna anyezungumzia mgomo.swali dogo la kifalsafa,hivi gazeti lililoandika juu ya wanahabari kumsusia DCI Manumba kule iringa,liliandika habari ya polisi au lah? na je tamko la wanahabari lilimaanisha habari zote za polisi,na hata polisi mwingine akiuwa raia basi asiandikwe,kwa sababu kuna mgomo,au ilimaanisha nini hasa?
Naam,mimi najua Maggid hata hivyo aliposimulia habari za nyololo jana amekuwa na reservations na ndiyo maana wengi wanamtaka awe wazi zaidi juu ya kilichotokea kule kijijini.Hebu fikiria kwa mfano hicho tunakijua tayari kuwa chadema walikuwa wanafanya ufunguzi wa tawi tu yaani kikao cha ndani,na polisi wakaja na mabomu yote hayo,kisha nenda nyololo,uambiwe kuwa siku moja kabla magari ya chadema yalipita yakitangaza uwepo wa mkutano mkubwa wa hadhara ambao utahutubiwa na dr.slaa na watu wajitokeze kwa wingi bila kujali vyama ili kumsikiliza rais,ukaelewa kuwa kumbe ni baada ya matangazo hayo,polisi nayo ikaenda siku moja kabla pia na karandinga zake ikisema,mikutano ya hadhara imezuiwa hivyo mkutano wa kesho ni batili na polisi itauzuia na atakayetokeza asilaumu,mnashauriwa kubaki majumbani mwenu.
Sasa baada ya hayo simulizi ya wanakijiji ikamalizika kwa kusema kuwa sisi tulijua hivyo kuwa kuna mkutano wa hadhara baada ya kutangaziwa,bali polisi wakazuia na hatukutoka ndani kwenda kwenye tawi la chadema.mhh nani sasa waliokuwa wakifungua tawi? unauliza, jibu i walikuja na vijana wengi kwenye magari na walikuwa na hamasa na matairi ya kuwasha barabarani,wengine kutoka mbeya na wengine kutoka iringa mjini.Allah nani amekwisha simulia ukweli huu? sasa mlitaka maggid aurushe redioni pamoja na mashambulizi yote mliyokwisha mpatia hapa jf?
Hata ningekuwa mimi.HITIMISHO LANGU Maggid alikuwa sahihi sema sisi watanzania ndiyo wanafiki kwani hatupendi kusema wala kuambiwa yale tusiyoyapenda.na hata kwa haya wapo watakaoanza kijinga tu kusema mimi ni gamba,polisi,au ninatafuta ugali,bali mimi siko huko,ni mwanafalsafa tu.
 
Maggid, katika Watanzania wachache waliokutana uso kwa uso na kuongea na Iddi Amin, mimi najivunia kuwa ni mmoja wapo. Nakuelewa unachosema.

Niliwahi kumsikia akisema "Nyerere akikwambia saa hizi ni "mchana" basi kwenda tazama nje kama kweli jua inawaka".

Media inaweza ikajenga au ikabomoa.

Nakuelewa unachosema.
 
maggid
Hivi hawa jamaa wa jf wengi ni wtu wa mifumo miwili mikuu,ukristo kwa sana na ukiitaja vibaya cdm yao wanatokwa povu balaa! we usijali piga kazi! pamoja sana!
 
Last edited by a moderator:
Maggid, Tatizo lililopo nitakueleza kwa kifupi sana na hakuna
vinginevyo zaidi ya hivyo pia Tatizo hilo lipo kwa serikali na
wananchi wa kawaida ni hivi-:

TUMEKUWA TUNAPENDA KUSIKIA TUNACHOTAKA KUSIKIA
HATUPENDI KUSIKIA TUNACHOTAKIWA KUSIKIA.
 
CRITO mkuu naona umewagusa kwa hili, nimefatilia hoja zote zinazo chukia hoja za maggid na kugundua kuwa maggid amefanya mambo yake kama mwanahabari anavyotakiwa, wana jf wasahivi tumekuwa hatuna tofauti na wale wavijiweni yaani tunaona ushabiki wa chama ni kama timu za mpira lazima tuyakatae ya chama pinzani eti kwasababu tunatofautiana nao, tanzania inapoelekea sio pazuri kwa mwendo huu, kunabaadhi ya members humu ni waelewa kuwa binadamu tunautofauti mwingi kuliko kufanana na hii ni njia moja ya kumheshimu mwenzako na si kinyume chake,
 
Last edited by a moderator:
Sidhani kama kuna member ambaye ni neutral humu.. JF na kuna baadhi wamejenga kitabia if you are not with us au umepost habari wasiyo ipenda basi wewe moja kwa moja ni ccm na utashambuliwa kwa kejeli na matusi.. brother magid nimeelewa unachozungumzia
 
Maggid, Tatizo lililopo nitakueleza kwa kifupi sana na hakuna
vinginevyo zaidi ya hivyo pia Tatizo hilo lipo kwa serikali na
wananchi wa kawaida ni hivi-:

TUMEKUWA TUNAPENDA KUSIKIA TUNACHOTAKA KUSIKIA
HATUPENDI KUSIKIA TUNACHOTAKIWA KUSIKIA.

Exactly mkuu... Hili ndio tatizo la wana jf wengi..
 
Unamanish Mwangosi aliandika mabaya kuhusu serkal na jesh la polisi? 2cfanye kazi kwa mazowea. Things ar changing bro
 
Mchawi hawezi kujificha..hiii stori ya Idd Amin ni kisa cha ukweli cha kumhusu Maggid ila kwa vile yeye ni masanii katumia mazingira tofauti kuwakilisha ujumbe ule ule. Ukweli kuwa yeye ndiye aliyeitwa ikulu ilikuwa mwaka 2010 mwezi May na kupewa soda toka siku hiyo kazi yake ni kuandika mazuri serikali & co. Nashukuru dhamira yake haijafanya kabisa ndio maana katuandikia hiki kisa. Hongera Mbena wa Rujewa
 
Maggid,

Unapoandika habari tofautisha na hekaya, ngano, hadithi, riwaya, vumi nk.

Tunaomba jina la huyo muandishi aliyeongea na Idi Amin au source yako, utasaidia wasomi wanaomsoma Idi Amin.

La sivyo kubali kwamba umepotosha kwa kuandika uvumi wa rejareja kama kitu kilichotokea.

Credibility should be guarded with the highest integrity.
 
mimi huwa napenda sana kufuatilia media zisizo egemea upande wowote na ndio maana huwa sisomi habari za free media, uhuru, mwanahalisi, clouds etc miaka ya nyuma nilikuwa nikiamini maggid ni mwanahabari huru lakini ilipokaribia october 2010 nilianza kutafakari nilichokuwa nikiamini. Bila kuuzunguka mbuyu tatizo la maggid ni chuki ya kibinadamu aliyonayo kwa cdm lakini kwa vyama vingine na matukio mengine ya kijamii bado yupo fair, kwahiyo unatakiwa kuwa mwangalifu unaposoma habari zake zinazoigusa cdm.

Swala jingine maggid ni msomi lakini anapenda udini vibaya sana, kwenye blog yake huwa analeta habari fulani za kuchokoza nyuki and the likes of malaria sugu, zomba wanaingia kichwa kichwa na anapublish comment zao zote lakini kwa upande wa pili anaziminya hata kama ni za busara that's why utakuta katika comment 30 alizopublish 25+ ni zenye mitazamo ya kina MS.

Kitu cha pekee ninachokipenda kwa maggid ni kuuma na kupuliza
 
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom