Rev. Kishoka
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 4,526
- 1,529
Leo tunatambiana Mkuu wa Majeshi kaonekana Ngerengere, tunapigana vijembe vya udaku wa afya yake na tetesi za yeye "kutoweka".
Hatulizungumzii hata kidogo tukio lenyewe kubwa pale Ngerengere.
Hatujiulizi Tanzania tumekosa fedha za kujenga na kuboresha kikosi chetu cha anga mpaka tuende Uchina kuomba msaada na kufadhiliwa?
Yaani hatuna dola za kimarekani Milioni mia moja popote? ni heri hata masalia ya Escrow na EPA yangetumika hapo Ngerengere au pale Kigamboni kuliko kuonyesha utegemezi wa hali ya juu kwa China.
Wanatukopesha kujenga Bandari, mitambo ya gesi, reli, barabara, kujenga majengo, matumizi ya serikali, zana za kijeshi na sasa kambi nzima ya jeshi?
Tutalipaje hili deni? Tutalipaje hizi fadhila?
Hatulizungumzii hata kidogo tukio lenyewe kubwa pale Ngerengere.
Hatujiulizi Tanzania tumekosa fedha za kujenga na kuboresha kikosi chetu cha anga mpaka tuende Uchina kuomba msaada na kufadhiliwa?
Yaani hatuna dola za kimarekani Milioni mia moja popote? ni heri hata masalia ya Escrow na EPA yangetumika hapo Ngerengere au pale Kigamboni kuliko kuonyesha utegemezi wa hali ya juu kwa China.
Wanatukopesha kujenga Bandari, mitambo ya gesi, reli, barabara, kujenga majengo, matumizi ya serikali, zana za kijeshi na sasa kambi nzima ya jeshi?
Tutalipaje hili deni? Tutalipaje hizi fadhila?