Kiongozi wa Madaktari (Dr. Ulimboka) atekwa, aokotwa akiwa katika hali mbaya sana...

mayoscissors

JF-Expert Member
Nov 24, 2009
975
471
Sasa uchokozi umefikia pabaya na hii sasa ni vita!!

Taarifa iliyonifikia hivi punde ni kuwa jemedari Dr. Ulimboka ametekwa majira ya saa sita usiku na watu watatu waliokuwa na silaha za moto na kumpeleka kusikojulikana! Inasemekana alipigiwa simu na jamaa mmoja aliyejitambulisha kwa jina moja la 'Abeid' ambaye tangu mwanzo amekuwa akiwasiliana naye na kujiita afisa wa serikali na kudai kuwa alitaka aonane naye face to face kwa ajili ya reconciliation.

Taarifa zimekwisha fikishwa polisi na sehemu zingine kwa ajili ya ufuatiliaji. (source chanzo cha kuaminika).

UPDATE:
Inaelekea waliomteka si watu wema kabisa, Dr. Ulimboka kaokotwa sehemu akiwa katika hali mbaya sana!

Jamani this is is serious; Nimepigiwa simu sasa hivi na watu wa Legal and Human Rights Center wameniambia wametoka kumchukua Dr. Ulimboka kule Mabwepande amepigwa vibaya sana na ni emergency wanampeleka MOI sasa hivi.

Please tunaomba mtume habari hii kila mahali please!

Ni habari ya uhakika sana nimeomngea na Patience Mlowe wa Legal and Human Rights center.

Chanzo: Colleague ambaye yuko naye sasa!
Kamanda wa polisi Suleiman Kova amekaririwa akisema kwamba Dr. Ulimboka ametekwa akiwa Club na watu wasiojulikana akiwa anakunywa kinywaji na kuahidi kwamba uchunguzi unaendelea kuhusiana na tukio hilo.
Tutaendelea kutoa updates kadiri muda unavyoruhusu.

attachment.php
attachment.php
attachment.php


attachment.php

PICHANI: Dkt. Ulimboka akiwa katika hali mbaya mara baada ya kuokotwa akiwa hajitambui.
Ulimboka alitekwa jana usiku mida ya saa 6 usiku baada ya kupigiwa simu na mtu aliyejitambulisha kwa jina la Abeid na alitekwa na watu wawili waliokuwa na silaha. Kufuatia hali hii wafanyakazi wa chumba cha maiti Muhimbili nao wamegoma na mgomo huenda ukawa mkubwa zaidi!

 

Attachments

  • ulimboka.jpg
    ulimboka.jpg
    16.3 KB · Views: 18,127
Wenye silaha ni maaskari na usalama, Dr Ulimboka hana biashara yoyote anayofanya imfanye atekwe, hana pesa hana kitu ni maskini tuu, sasa swali kuu ni nani aliyemteka? Ni government agent na ni specific na issue ya madokta full stop.

Aand then what next.....the doktas are still ndani ya mgomo baridi
 
Watakuwa wapuuzi kweli wakimteka. Labda kukamatwa kwa kuvunja sheria. But does it help?
 
Sasa mbona hao jamaa kwa kitendo hicho ndio wanaibua ajenda mpya sasa!!!!!!!!!
 
yaan serikali hapo ndo inapochemka!what do u think ikitangazwa kuwa amekamatwa au kitekwa,nchi haitatawalika jamani,mark my word!
 
Kama habari hii ni ya kweli, Suluhisho la ukweli halitokani na kuteka watu, ni kwa kuwapa madaktari haki yao.

Serikali badala ya kuteka mafisadi inateka wanaodai maslahi yao. Aibu!. Baadhi ya madai ya madaktari ni ya Msingi, wanataka huduma ziboreshwe hospitalini, wanataka wasiwaandikie watu aspirini wakati wanahitaji dawa ya malaria isiyokuwepo.

Haya ni madai ya haki, hayatatatuliwa kwa kuteka watu.
 
Inanikumbusha utawala wa Moi Bwana Ouko alipopotea kwa Staili hii.... Sasa kama Mr Dhaifu naye anafuata njia hizi hizi kufunika Uozo wake hii ni hatari zaidi ya Ukoma
 
ma Dr wapo tayari kwa mazungumzo ya dhati, hiyo njia wanayotumia serikali italeta tatizo la pili.
 
Serikali ya ccm angalieni sana! Kumwaga damu sio suluhisho la matatizo! Mkimuua huyo ndio chanzo cha migogoro zaidi!!!
 
Du imbombo ngafu ni simple kuwatrack hao waliomkamata kupitia call records zao tu mpaka watajulikana.
 
Back
Top Bottom