Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

Mimi nalima aina ya Sugar baby inachukua siku 60 tu kuvuna tangu plus siku 3-5 za kukaa ardhini, kwa hiyo kwa mwaka nalima mara 4 tu nina ekari 5 na kila eka napata kuanzia 2M-3M.

Spacing ni 2mx2m na kila shimo naweka mbegu 2 ambazo zinazaa matunda 2-3 kwa maana kila shimo napata matunda 4-6 ( wastani matunda 5).

Hivyo kwa spacing hiyo napata mashimo 1000-1200

Idadi ya matunda: Mashimo x Matunda kwa shimo x ekari [1,000 x 5 x 5 = 25,000]

Mapato: wastani wa shilingi 500 kwa tikiti x idadi ya matikiti kwa eneo la ekari 5 [25,000 x 500 = 12,500,000]

Mapato kwa mwaka: 12,500,000 x 4= 50,000,000

Gharama za uendeshaji wa shamba ni Tsh 25,000,000

Faida Kuu ni Tshs 25,000,000 M.

Tujenge taifa letu kwa kilimo
edi
mkuu naomba nitumie wasaa huu kukujulisha mimi nataka nianze hicho kilimo cha matikiti mkuu, ila sina knowledge, shamba lipo kisarawe (3acres) mkuu naweza kuanza kwa kipi na kipi?

na mtaji unaeza ukawa kias gani? na huwa msimu gani ndo kilimo kinaanza
naomba msaada pliz
 
Mimi nililima matikiti maji wakati wa kiangazi kwa mbegu ambazo ni hybrid na ninaweza kushare uzoefu wangu kama ifuatavyo;

  1. Haya matunda yanashambuliwa sana na Fungi aina ya Powdery Mildew. Inafikia wakati unakuwa unapiga zile broad spectrum fungicides hadi weekly ili kupambana na huu ugonjwa maana unasababisha matunda kuoza wiki moja tu baada ya fruit set. Mbegu ya Hibrid inazaa sana lakini matunda mengi yalikuwa yanaoza kutokana na tatizo la fungi
  2. Kuna Aphids walinisumbua sana. Wakulima tunapenda kuwaita sisimizi weusi lakini mtaalam akaniambia kuwa hawa ni aphids. Wana tabia ya kunyonya kwenye stems, ukizembea siku mbili tu unakuta mmea mzima wa tikiti maji unakaribia kukauka. Ilikuwa ni challenge kubwa kukabiliana nao na mtaalam aliniambia kwa kuwa ni kiangazi njia pekee ya kukabiliana nao ni dawa. Kumbuka aphids huwa wanakufa kukiwa na mvua hivyo hawasumbui sana wakati wa mvua
  3. Matunda yalipoanza kukomaa nikakumbana na fisi waliokuwa wanaibuka usiku, nyani waliibuka siku moja na pia binadamu walikuwa wanaiba, tena majirani zangu wa shambani. Kwa kuwa nilikuwa nimeambiwa hizi changamoto nifanikiwa kufense shamba langu kwa wakati muafaka na pia nilikuwa na ulinzi mzuri. Kwa mkulima anayeanza lazima ajiandae kukabiliana na haya matatizo
  4. Changamoto nyingine kubwa ilikuwa kwenye mauzo. Ingawa nilitoa matunda yangu wakati ambao sio watu wengi walikuwa nayo na nilikuwa na strategy ya kuuza kidogo kidogo na kwa bei ya soko hasa kwa kutarget watu wenye mahoteli na migahawa kuna kipindi nikalazimika kuwapelekea wanunuzi wa jumla wanaouzia sokoni. Nilimpelekea jamaa sample, bahati nzuri nilishauriwa nisiwakaribishe kabisa shambani kwa kuwa wakiona idadi ya matunda uliyo nayo wanapanga mbinu za kukufrustrate uuze bei poa. Baada ya kumpa jamaa sample ya matunda mawili makubwa, (average weight ya matikiti yangu ilikuwa 4kg but kuna yaliyofika 7 Kg na nilijitahidi kupima yale matunda makubwa zaidi) akaniambia nimpelekee kwa bei ya 1,500 kwa tunda. Nilipopeleka Pick Up yangu imejaa matunda jamaa alikuwa na visingizio kibao tukashuka bei hadi 1,300 kwa tunda na siku hiyo nilibeba 200 tu. Nilipopeleka mara ya pili akashuka hadi shs 800. Nikaacha kupeleka sokoni nikawa nauza moja kwa moja mahotelini, migahawani na kwa majirani kutokana na order but siku ukiuza sana ni matikiti 50. Kabla ya kupanda kama hauna uhakika na soko ni vizuri kupanda kidogo kidogo, let say kila baada ya siku 7 hadi 10 unapanda nusu hekari au hekari moja kama una shamba zaidi ya hekari 3. Hii itakusaidia kutoivisha matunda mengi kwa wakati mmoja, ingawa utakutana na mengine ambayo yatakomaa wakati bei sio nzuri sana, kama unauza kwa watumiaji moja kwa moja bei sio ishu
  5. Uzalishaji sio mkubwa kama watu wanavyoongelea theoreticaly. Kuna tatizo kubwa la fruit set kwenye haya matunda na inashauriwa kama una nafasi weka mizinga ya nyuki shambani wasaidie pollination. Nilipanda miche 2000 kamili tena kwa kuhesabu, ikakomaa miche 1700 na idadi ya matunda yaliyofika sokoni ni kama 2500 (Kila mche ulizaa tunda moja au mawili yaliyokomaa na kufika sokoni ingawa kulikuwa na maua yenye matunda hadi 12 kwa mche) tu kutoka shamba zima na nilikuwa nauza kwa kati ya shs 2000 na 3500 ukiondoa zile Pickup mbili zenye matunda kama 400 nilipeleka kwa walanguzi. Gharama za uzalishaji hazikufika 1M but faida yote ilikuwa ni kulipia uwekezaji kwenye fensi.

Nimefuatilia mawazo ya watu wengi humu wanatoa uzoefu wa kwenye vitabu au wanavyowashauri wakulima. Uzuri wa ushauri wa humu unakupa mtu hamasa kujaribu, which is a good thing na baada ya kupata challenges kama mimi unakuwa determined kufanya vizuri next time. Nitafurahi mkulima mwingine akinipa ushauri wa vikwazo nilivyokutana navyo maana huenda ni poor practice na best practice huwa inapatikana kwa ku-benchmark kwa wakulima wenzio wanaofanya vizuri. Next time target yangu ni kuhakikisha angalau matunda manne kwa mche mmoja yanafika sokoni badala ya moja hadi mawili niliyopata mwaka jana.
kaka hongera sana kwa hili.

vipi mkuu uliishia wapi kaka? mimi nataka kuanza hiki kilimo...
 
MI napenda sana hicho kilimo na drip irrigation, niambieni inakuwaje? kuhusu gharama za uendeshaji wa shamba kwa heka ni kiasi gani? mashamba yanapatikana wapi, na masoko yake yakoje? simu yangu ni 0768 417121, na 0713 658618 ni mgeni sana kwenye mtandao naomba msaada wenu.
sasa mkongwe dahhh
 
mie nimelima tikitiki ekari moja mwaka huu nataka kuuza, ila mimi ningependa kuuzia shamba. Mwenye taarifa ya hali ya soko kwa Dar es salaam wiki hii. Shamba lipo Kigamboni.
 
BEI ZA TIKITI LEO 24/02/2016

1.KIRUMBA -MWANZA TIKITI MOJA LA KILO 1 NI TSH 750
2. MAKAMBAKO-NJOMBE-TIKITI MOJA LA KILO 1 TSH 2220
3. LUSHOTO TANGA-TIKITI MOJA LA KILO 1 TSH 2000
4. MWANAKWEREKWE ZANZIBAR, PISI MOJA YA KILO 1 TSH 1500
5. DODOMA TIKITI 1 LA KILO MOJA NI TSH 2260
6.KARIAKOO PISI MOJA LA KILO 1 NI TSH 1000
7. MOROGORO PISI MOJA YA KILO 1 NI TSH 2000
8. KILOMBERO-ARUSHA PISI MOJA LA KILO 1 TSH 2000

Wakuu vipi feedback kwa waliolima msimu huu? Soko lipo? Bei imepanda au imeshuka?
 
mimi nimelima ila bei yake ni ndogo sana kuliko gharama za uzalishaji nimepata hasara kubwa sana.
 
chonde chonde kaka,usizilete hizo mbegu,it may cause GM contamination,wasiliana na wataalam wa kilimo watatoa ushauri mzuri.ila bora uziache huko huko,hizi za kwetu ni poa sana tu.
wajapan wametengeneza watermelon la square kama box ili iwe rahisi kusafirisha matunda hayo,Mh! madhara yatajulikana baadae,ktk cancer na magonjwa mengineyo.
Kaka naomba uniambie hiyo mbegu ya mjapani inaitwaje na ni hybrid au laa?
 
nataka kulima kwahiyo napenda kufahamu machache tu. Mbegu aina gani ni nzuri? Ratiba ya umwagiliaji na kiasi cha maji kinachohitajika kwa shimo? Mbolea aina gani inatumika! Ratiba kunyunyuzia dawa? Kwa water pump ya lita 3 itanigharimu lita kwa hekari 2?
 
Hayo matiki ya shs 500 wapi huko? njoo ufaidike zenji (zingatia gharama za usafiri) huku kipande cha unene wa nchi mbili shs 500 ,a good sized one run to2500-3500 na kuna kipindi yana fika mpaka 6000 moja.
kuna yale ya mistari ndio yanapendwa zaidi !
Ally habari, naweza kuwasiliana na wewe Mkuu? naina hii fursa kaka, naomba email yako
 
Aksante kwa swal lako, mbegu hizo zitaota vizuri kwani tunatoa mbegu kutoka huko na tunakuja kuzizalsha Tz halafu zinaenda kuuzwa huko tena, lakini hakikisha unaziotesha kitalun kwanza kabla ya kuzpeleka shamba kwan zaweza zisiote vzr.

Tumia samadi kuziotesha na zipe joto la kutosha kwa kufunikia kitalu, maji yasiwe meng maana zaweza kuoza, na baada ya siku saba mpaka 14 miche itakuwa tayar kwenda shamban.

Aksante.
Matatizo Mengi sn yametokea sababu ya kutoa mbegu ulaya maisha yako yote usimshaur mtu asiye mtaalamu kutoa mbegu kokote duniani kuja Tanzania km tunataka kuendelea kulima vzr tz, mfano mdudu wa nyanya anaitwa tutor au Kantangaze wauliza Wakulima wa nyanya alitoka huko huko, plz plz tushirikishane kwa hilo
 
Wakuu hivi hili group la whatsapp lipo active?

Admin fanyia msaada hii namba 0719881021
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom