Kilimo cha matikiti maji (watermelon): Ushauri na Masoko

matikiti yana tabia ya kupasuka wakati wa maska. Kama utalma yapandshie kwe bed lefu na uliweke matandazo. Nakushaur tumia mbegu ya sentinel f1 n nzur kubwa na soko lake la uhakika.

Mkuu hapo bado sijakupata, una maanisha nini?
 
Wabongo kujifanya wajuaji ndio tunakufa maskini kisa una degree kama unaona wenzio wanacho discuss hakina tija lete mawazo mbadala kuliko kupinga bila alternative solutions. Ni kujiabisha tubadilike. Think positive
 
Naombeni msaada kwa watalaam wa kilimo! Nataka kuotesha miche ya tikiti maji 10,000/= mkoani Shinyanga je,
1. Itanigharimu kiasi gani kuitunza hadi ikue na kufikia mauzo??
2. Shamba ninalo ekari 3 je litatosha??
3. Mbegu zake zinapatikana wapi zaidi??
4. Soko la tikiti maji sasa zuri liko mkoa gani?
5. Angalau kwa kiwango cha chini tikiti moja naweza kuiuza kwa shliingi ngapi??
Asanteni wapendwa!

ndugu radio producer,mimi tashauri upande wa maji...zingatia matumizi ya drip irrigation system,yaani umwagiliaji wa matone..ukiwekeza kwenye hiyo utakua umetatua tatizo la maji.kabla hujaweka hiyo drip irrigation system hakikisha una ksisma cha maji ya kutosha ambayo utayatumia kwenye system yako ya irrigation..
 
Sisi tuliopo dar,tunawezaje kupata mashamba ya karibu ili iwe rahisi kufika shambani mara kwa mara,mwenye kujua..
 
Safi mkuu,
Changamoto kubwa ni kupasuka, tikiti la masika lina soko zuri, nimeona hata mikoani sasa hivi tikiti linaliwa sana, kwa hiyo umelenga.

Asante mkuu. Ila target yangu ni kusafirisha either Dar or Arusha. Or unanishaurije? Lakini dawa za kuzuia kupasuka so zipo??
 
Kaka Edmund shukran kwa taarifa yako kuhusu ulimaji wa tikiti maji. Kama unaweza naomba ushauri zaidi unitumie private message, ama unipe namba ya simu au kama pia unaweza naomba unichek kwenye facebook account yangu "Juma Zullu
 
Wabongo kujifanya wajuaji ndio tunakufa maskini kisa una degree kama unaona wenzio wanacho discuss hakina tija lete mawazo mbadala kuliko kupinga bila alternative solutions. Ni kujiabisha tubadilike. Think positive

Tuna safari ndefu sana mkuu.

Kuna mijitu inaamini kwenye kusoma na kuajiriwa tu hawajui kitu kinachoitwa kuwekeza wala kuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha mapato, wao kila wazo la biashara ni baya kazi yao kukosoa tu.

Wananikera sana watu wa namna hii natamani hata kuwazaba makofi yaani jitu lina kichwa maji mpaka linaudhi, huwa wanajidanganya nitawekeza nikistaafu na wakistaafu biashara hawaziwezi kwa sababu hawajui chochote mabwege kwa sababu ya kutotaka kujifunza mapema.

Badilikeni mabwege nyie hamjui kusoma alama za nyakati nina degree ya uongozi wa biashara lakini siwezi dharau wazo hata Moja la mtu la kuhusu uwekezaji au biashara eti kwa sababu nina degree siwezi lima.
 
Nimeipenda hiyo calculation...cery simple
Je aina gani ya mbolea inayotumika na madawa ya kukinga mmea?
 
Jamani habarini za wkend.., naomba kujua mche wa tikiti maji unaweza kuvunwa mara ngapi matunda yake?

Kwa mfano embe zinavunwa kila mwaka, ndizi unavuna mara moja tu na mche unakwisha kazi yake. Vipi kwa matikiti maji, unavunwa mara ngapi na kwa kipindi/interval gani?

Nataka kulima, yanalipa sana nisaidieni tafadhali.
hivi ndio vitu tunataka kusikia
 
Matikiti ni matunda, japo tunasema ni mboga kutokana na njia zinazotumika kuyazalsha kwan siyo tofaut na mboga.

Matunda yanaanza kukomaa kuanzia siku 80-120 kufuatana na aina, kama sugarbaby inakomaa mapema. Na il kupata matunda makubwa na yenye ubora, tunashaur kwa mti mmoja usiwe na matunda zaidi ya matano ambayo interval ya kuvuna ni siku hadi 10 kwani uvunaj ni had miezi miwil kwa mti mmoja. Hector 1=8-12 tan za matunda.

Kwa maswali zaidi kuhusu kilimo cha mazao tuwasiliane.
safi saana
 
Safi mkuu,
Changamoto kubwa ni kupasuka, tikiti la masika lina soko zuri, nimeona hata mikoani sasa hivi tikiti linaliwa sana, kwa hiyo umelenga.
Je mkuu Malila,
Unaweza kushauri njia gani zitumike kuzuia upasukaji wa tikiti la masika?
 
Habari zenu wadau.

Wakuu mimi nataka kujaribu kulima tikiti maji kipindi hiki cha masika. Nitafanya kilimo cha kisasa. Mbegu ni Sukari F1 hybrid.
Tatizo nimekuwa nikipata ushauri tofauti kuhusu kipindi hiki ambacho masika inakaribia kuanza (Takribani mwezi mmoja baadaye) Wengine wanasema Matikiti hayapendi mvua nyingi, wengine wanasema kama nitayahudumia kwa madawa hakutakuwa na tatizo.

Wakuu naombeni mawazo yenu, je inawezekana nikafanikiwa kuvuna kipindi hiki cha masika?

Natanguliza Shukrani.

Kama umeamua kulima tikiti la masika tumia mbegu maalum kwaajili ya masika.kwani hizi za kawaida zitakusubua.mbegu hizo mpaka utoe oda kiwandani wakuzalishie.
 
Kama umeamua kulima tikiti la masika tumia mbegu maalum kwaajili ya masika.kwani hizi za kawaida zitakusubua.mbegu hizo mpaka utoe oda kiwandani wakuzalishie.

Mkuu kumbe kuna mbegu maalum za masika!? Ndo zikoje!? Kkwanda gani wanatengeneza!?
 
Mkuu kumbe kuna mbegu maalum za masika!? Ndo zikoje!? Kkwanda gani wanatengeneza!?

Ndiyo zipo zinakua na uwezo Wa kuhimili mikikimikiki ya masika.hizi nyingine zinaoza.mi mwenyewe ninampango Wa kulima tikiti la masika kwsbb linalipa.kuna jamaa ni mzoefu zaidi Wa mambo haya ndiye aliyeniwekea oda kiwandani.km utapenda nitakutumia no.yake
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom