Gosbertgoodluck
JF-Expert Member
- Mar 3, 2008
- 2,855
- 401
Ndugu yangu kikwete,
Naandika ujumbe huu nikiwa kama nabii ninayeleta ujumbe mwema kwako. Sijatumwa na Mungu au mtu yeyote. Nimetumwa na nafsi yangu inayolia na kulitakia mema taifa letu la Tanganyika na Tanzania kwa ujumla. Mimi ni raia wa kawaida mwenye kipato cha wastani. Ninaishi mtaani ambako kuna mchanganyiko wa watu wenye uwezo wa kimaisha tofauti na elimu tofauti. Ninapenda sana kuchangamana na makundi tofauti ya watu, kuanzia umri, elimu, kipato, imani, n.k. Jambo moja ambalo kamwe usitake kulibeza kama bado unahitaji kuendelea kukalia kiti hicho ni hali mbaya ya maisha. Wananchi wanalia. Wanajuta kwa nini walikuchagua wewe. Huo ndio ukweli hata kama hupendi kusikia hivyo. Popote uonapo mkusanyiko wa watu jina lako haliachwi kutajwa kwa mabaya. Hata wachache wanaoendelea kukutetea sasa wanaona aibu kufanya hivyo maana nao nafsi zao zinawanyoshea vidole. Maongezi mengi yanahusu huduma za umeme, maji, bei za vyakula, mikopo ya wanafunzi, dowans, epa, n.k. Katika maongezi yote niliyoshiriki, kila mwongeaji alihusisha hali hii mbaya ya maisha na ugoigoi wa uongozi wako. Maongezi ya aina hiyo yapo kwenye mabaa, vituo vya daladala, ndani ya daladala, hotelini, makazini, nyumbani, n.k.
Ushauri wangu kwako ni mdogo tu. Chukua hatua sasa, mapema iwezekanavyo kabla wananchi hawajalipuka. Kimya kingi cha watanzania kitakuwa na mshindo utakaoandika hostoria duniani. Usidhani unafiki wa kuimba 'nchi yenye amani na utulivu' utakusaidia. Inawezekana unajidanganya kwamba watanzania hawana hulka ya kufanya fujo. Kama ndivyo unavyowaza, basi unajidangaya. Hakuna mwanadamu duniani anayeweza kuvumilia mateso siku zote na dalili zimeanza kujitokeza waziwazi. Nakuomba uchukue hatua sasa kunusuru taifa. La sivyo, wewe pamoja na familia yako na wapambe wako anzeni kufikiria maisha mtakayoishi baada ya wananchi kucharuka.
Nimeandika kama utani, lakini huo ndiyo unabii wangu kwako leo.
Naandika ujumbe huu nikiwa kama nabii ninayeleta ujumbe mwema kwako. Sijatumwa na Mungu au mtu yeyote. Nimetumwa na nafsi yangu inayolia na kulitakia mema taifa letu la Tanganyika na Tanzania kwa ujumla. Mimi ni raia wa kawaida mwenye kipato cha wastani. Ninaishi mtaani ambako kuna mchanganyiko wa watu wenye uwezo wa kimaisha tofauti na elimu tofauti. Ninapenda sana kuchangamana na makundi tofauti ya watu, kuanzia umri, elimu, kipato, imani, n.k. Jambo moja ambalo kamwe usitake kulibeza kama bado unahitaji kuendelea kukalia kiti hicho ni hali mbaya ya maisha. Wananchi wanalia. Wanajuta kwa nini walikuchagua wewe. Huo ndio ukweli hata kama hupendi kusikia hivyo. Popote uonapo mkusanyiko wa watu jina lako haliachwi kutajwa kwa mabaya. Hata wachache wanaoendelea kukutetea sasa wanaona aibu kufanya hivyo maana nao nafsi zao zinawanyoshea vidole. Maongezi mengi yanahusu huduma za umeme, maji, bei za vyakula, mikopo ya wanafunzi, dowans, epa, n.k. Katika maongezi yote niliyoshiriki, kila mwongeaji alihusisha hali hii mbaya ya maisha na ugoigoi wa uongozi wako. Maongezi ya aina hiyo yapo kwenye mabaa, vituo vya daladala, ndani ya daladala, hotelini, makazini, nyumbani, n.k.
Ushauri wangu kwako ni mdogo tu. Chukua hatua sasa, mapema iwezekanavyo kabla wananchi hawajalipuka. Kimya kingi cha watanzania kitakuwa na mshindo utakaoandika hostoria duniani. Usidhani unafiki wa kuimba 'nchi yenye amani na utulivu' utakusaidia. Inawezekana unajidanganya kwamba watanzania hawana hulka ya kufanya fujo. Kama ndivyo unavyowaza, basi unajidangaya. Hakuna mwanadamu duniani anayeweza kuvumilia mateso siku zote na dalili zimeanza kujitokeza waziwazi. Nakuomba uchukue hatua sasa kunusuru taifa. La sivyo, wewe pamoja na familia yako na wapambe wako anzeni kufikiria maisha mtakayoishi baada ya wananchi kucharuka.
Nimeandika kama utani, lakini huo ndiyo unabii wangu kwako leo.