Msongoru
JF-Expert Member
- Apr 16, 2008
- 306
- 24
Nimeshangazwa na mabango mengi yenye picha za RAIS anayemaliza muda wake, akiwa na watoto wadogo na wazee. Picha hizi huwa zinaandikwa kwamba chama kinajali watoto na wazee na rika zote, hivyo wanatoa wito kwamba tuchague chama hicho. Swali langu ni hili je ni kweli kwamba kujali watoto wa TAIFA hili ni kwa kuwaweka baadhi yao kwenye mabango? Elimu wanayopewa, matibabu wanayopewa na mazingira mazima wanayoishi ni kweli kwamba WANAJALIWA?