Elections 2010 Kikwete kweli anawajali watoto na wazee?

Kuna wakati unakuta Mwalimu anayeishi ktk nyumba kama hii anatumiwa na CCM kurubuni wapiga kura na kushiriki/kutoa msaada katika wizi wa kura. NANI KATUROGA HATA TUSIYAONE HAYA ?

Kutokana na maisha magumu huko wanako ishi akipewa buku 5 na bia 2 basi anasahau kuwa anaishi kwenye nyumba mbavu za mbwa.
 
Ushauri bure kwa wapinzani; watumie maneno yaliyoko kwenye mabango kudhibitishia umma sio kweli na kuonyesha mfano ya picha halisi ya nyumba za walimu, watoto kutafuta maji, wazee kupigwa wakidai maslahi yao, msongomano wa wakinamama wodini ( hii ni kundi lenye kura nyingi), elimu watoto wakiwa wamekaa chini.

Haya yanawezekana kwa kuondoa ufisadi na hizo pesa zitagharamia kila kitu- nimependa ya Dr. Slaa- shangingi moja ni sawa na dispensary nne waziri anatembelea. Hoja zinazogusa miasha ya watu hasa na dhiki yao . Naamini mabadiliko yatatokea mwaka huu - kura zitalindwa kwa asilimia 100
 
Back
Top Bottom