Kikwete kairudisha Tanganyika!! next...?

bwahahahahaha, nilizimia sana jinsi ulivyomuingiza "kingi la nguvu" bwana Kuhani!

Unaweza hata kuanzisha dini, ukasema wewe mtume/mungu...na watakuwepo tu wakina "macho juu" watakaokufuata!

ndio bongo yetu hiyo.....

"with great power, comes great responsibility" somebody said that; I would add "with great persuasive power, comes great responsibility". Ni kwa sababu hiyo watu lazima wapime maneno yao vizuri sana na kuyatumia vizuri. Kuna watu wanahitaji wafuasi mimi si mmoja wao; Kikwete anahitaji wafuasi watakaomfuata no matter what the song; wako kama yule mpiga filimbi wa Hamelini.

Sasa mimi sina nguvu na uwezo walio nao wanaojiona miungu kuhukumu watu wengine na kujua ni za mioyo yao.
 
Nakubadiliana na wewe aliteleza alivyokuwa anaendelea zaidi lakini kwa kuwa alikuwa hasomi... nadhani mtu ambaye yuko kwa ajili ya kujua alichokuwa anaongela nili-yo-bold ndipo mwisho wa yote.

Lakini kumbuka alianza na sijui wanazungumzia nchi kwa maana ipi... ndipo akasema kama tunaongelea kwa ndani tu! .... alichosema soverignt ndio ya Zanzibar na Tanganyika ilipotea... baada ya muungano... kwa hiyo nje tunajulikana kama Tanzania... kwa hiyo Zanzibar haiwezi kujitangaza kama nchi huru... hili lilieleweka kabisa.
Alikuwa anasoma... Uliona zile mbao nyeupe kwa mbali ambazo ni transparent (ambazo wamechemka kuzionesha)? Basi hizo zinaitwa teleprompter ambapo kwa mara ya kwanza leo JK kasoma hotuba yake kitaalam kiasi flani na naona alikuwa comfortable kwelikweli!

Angalia mfano hapa chini:
250px-SOU2007.jpg


Samahani kwa kuingilia hapa... Ila hiki nimekiona kitu cha maendeleo kwa nchi yetu rais kubadili mtindo wa kusoma hotuba na tena kuna maendeleo mengine ambayo naona yamenifurahisha kidogo, kubadili magari ya Ikulu na kuanza kutumia X5.

Tuendelee na discussion...
 
Kwanza napenda kumshukuru rais kikwete kwa kuwasamehe wahujumu uchumi au mafisadi hii inaonesha ni mtu mwenye kupenda watu wakewote na ni mwingi wakutowa msamahaa hongera rais kwa kutowa msamaha kwahao watu sasa maswali yamekwisha
 
najua una territory, my issue ni jinsi ulivyoipata.....huna tofauti na Carl Peters au walaghai wengine!!

safi sana lakini....

waliopata territory kama Carl Peters wapo wanajulikana, I assure you sir, I don't have any that I acquired.. waliojipatia wanajulikana. But well if it suits I totally accept whatever assessment you make of me. It comes with the territory. I didn't ask for it, nor went looking for it. Wengine wanajaribu kuipata kwa mgongo wa wengine. Well that too comes with territory.
 
hoja ipo ila wewe huwezi kuona!! hata wafuasi wa David Koresh kule branch davidian au Warren Jeff pia wanadhani wapo sahihi....something fishy here!! think kwa ubongo wako na sio kitu kingine....weka emotions pembeni!!

I'm sorry na naamini kwamba sijaTUKANA!! maana ndio kimbilio lenu siku hizi.

I don't get impressed easily.. but you just did. Although you ruined it with your last statement... but a very good and noticeable development.
 
Anaezungumza hapo ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,sasa kusema kateleza unamzushia aibu ,ikiwa waZanzibari walisema Pinda kateleza ,mkaanza kupiga makelele ,leo mnarudia kitendo kilekile cha kusema Raisi kateleza inamaana WaZanzibari hawakukosea.Nashangaa !

Kikwete amesema maneno mazuri sana ,na kuwafahamisha mambumbu kuwa Zanzibar ni Nchi na si vinginevyo. Nje ya Tanzania ,hilo halina mjdala na WaZanzibari kuwa sio nchi ,heshima kwa Raisi Kikwete ameewaeleza kwa busara na kila anaetaka kufahamu sasa atafahamu na kuweka akili yake uzuri kabisa.
Nasubiri wakereketwa wa JF niwaone kama hawakuvaa mabuibui na kuondoka wakionekana kuwa sio kumbe ndio,maana bado hotuba sijaichambua mstari baada ya mstari neno kwa neno maana na ukina wa maana.

Ukisha sema Zanzibar ni nchi ni lazima ukubali kwamba Tanganyika ni nchi pia na ni vema utonyesha mipaka ya nchi hizo.

Ukiweza onyesha mipaka ya Tanganyika na ile ya Zanzibar kwa usahihi, jaribio la pili liwe ni la k uonyesha mipaka ya Tanzania na mipaka ya Zanzibar kwa usahihi wa 100%.

Ukishindwa kuonyesha mipaka ya Tanzania na Zanzibar jaribu kuonyesha mijibwa au mikondooo ya tanzania na Zanzibar.

Ukishindwa kuonyesha mipaka na mijibwa ni zamu yako kuvaa Baibui na kuyeya kwenye ufinyu wa hewa.
 
Nimegundua kuna watu wanaingia hapa kutafuta watu wa 'kuchat' nao inform of mabishano, am wiser now- I just dont get involved! Nadhani wengi wenye busara zetu tuanze kufuata kausemi ka Dr. Slaa nilikokaona hapa last week kwamba kichaa akichukua nguo zako wakati unaoga mtoni, usitoke na kuanza kumkimbiza kwa kuwa na wee mwenyewe utaishia kuonekana kichaa!
 
Not very good in mathematics but everyone here can get this right (including me of course!)
If A + B = C then C - A= B and C - B = A, simple innit?
 
Give us a break will you? This is akin to the the devil having a go at interpreting the Bible and as such we cannot expect anything close to a fair and square re-interpretation of the fire-and-brimstone rhetoric therein so to speak. Its best that you wait for the next mega political scandal from the CCM and/or government to unfold itself in the media, rather than bore people to death and waste everybody's time and intellectual energy on useless, petty political word play. Besides you already have more than a dozen threads running in here on a myriad of negative, anti-government and specifically anti-Kikwete themes.

Doggone it!! You back? It's on again now.....Mods....ban this guy before I tear him limb from limb....
 
I'm gonna out her...ooops...him....Self Scientific is Nyama Hatari aka PuNjabu Ngabu. He should be banned immeadiately.
 
nenda kwenye jukwaa la mapenzi kwani huko ndipo unapojulikana....lakini kwenye mambo ya kufikiria!! ZERO.

Kumbe mwenzetu wee kwenye mapenzi hufikirii? watumia jimsuli lako tu?basi mademu wengi watakuwa wanakupa ZERO! (Ooops, sorry wadau, nshaanza kumkimbiza kichaa! I shouldnt!)
 
Wacha ushabiki wa kitoto wa kitoto wewe! Tangu lini kupinga ukiritimba wa maoni kwenye jukwa la umma likawa sawa na kutetea ufisadi?

Umelelala??

Self scientific
Join Date: Thu Aug 2008
Posts: 11
Rep Power: 0
Thanks: 1
Thanked 2 Times in 2 Posts
Credits: 595

Ukiamka asubuhi au upatapo ujumbe huu, tafadhali tunakuhitaji jamvini, tuzidi kupekecha ubongo wako, pampers zipo, nepi zimepitwa na wakati, uji wa mahindi na ulezi vipo kwa hiyo usikonde uwe tayari kunywa, kula ,kuogeshwa , kuvalishwa.Ukishindwa usilie, maana hatuna maziwa ya mama wala kubembelezana.Umeanza vibaya ulitakiwa uje na hoja siyo shutuma ambazo hazina mbele wala nyuma? mtu anapotoa hoja mpinge kwa hoja UNAPOKUJA NA MATUSI KASHFA WATAALAMU WA SAIKOLOJIA WANAONA WEWE UNAJIONA DHAIFU! na kwa kweli uko dhaifu ndo maana unatoa shutuma tu.

Mwanakijiji kama mtu mwingine yeyote anayo haki ya kutoa maoni yake, na si kila atoapo lazima ukubali, na wewe toa hoja, life goes on like that! kumshambulia kama ulivyosema ni kukosa nidhamu ya nafsi yako mwenyewe! hajatukana mtu yeyote.Nchi zingine ndugu wanashika bunduki siyo kalamu kama mtu mmoja alivyodokeza,.na hayuko peke yake mkjj wako wengi kama yeye wengine hawawezi hata kuandika , wanatukana, wanaua, na wakikufahamu mtu kama wewe wangekufanya lolote lile, mengine hayazungumziki.

usisahau kupiga mswaki ukiamka!

Waberoya.
 
mnaumizana makoo/vidole ku-type na kuisumbua mahakama tu....kulikuwepo na SOVIET na YUGOSLAVIAN ndio itakuwa Tanzania!?? tunasubiri tu na sisi ma-northerners tujitangazie nchi.

Bora waturudishie Tanganyika yetu tujue moja, nishachoka na haya mambo ya ooh tunaonewa ooh kwa nini hatupati sawa na bara....Muungano ukivunjika na mimi nakosa mke!!
 
WATANGANYIKA fichueni Tanganyika yenu mliko ificha WATANGANYIKA fichueni Tanganyika yenu mliko ificha. WATANGANYIKA fichueni Tanganyika yenu mliko ificha. WATANGANYIKA fichueni Tanganyika yenu mliko ificha .Raisi amesha sema msijitie pambani tena mkaleta usanii wa maneno TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA TANGANYIKA
 
Ukisha sema Zanzibar ni nchi ni lazima ukubali kwamba Tanganyika ni nchi pia na ni vema utonyesha mipaka ya nchi hizo.

Ukiweza onyesha mipaka ya Tanganyika na ile ya Zanzibar kwa usahihi, jaribio la pili liwe ni la k uonyesha mipaka ya Tanzania na mipaka ya Zanzibar kwa usahihi wa 100%.

Ukishindwa kuonyesha mipaka ya Tanzania na Zanzibar jaribu kuonyesha mijibwa au mikondooo ya tanzania na Zanzibar.

Ukishindwa kuonyesha mipaka na mijibwa ni zamu yako kuvaa Babibui na kuyeya kwenye ufinyu wa hewa.

Sasa wewe unamuita Raisi Kikwete Muongo ?
 
Kati ya vitu ambavyo inawezekana vimewaponyoka wengi ni kuwa Rais Kikwete alipozungumzia suala la Zanzibar alijikuta ameirudisha "Nchi ya Tanganyika" kwa makusudi (haiwezekani kuwa bahati mbaya). Aliirudisha hivyo kwa kufuata reasoning yake ambayo kwa kweli naamini ina makosa na alishindwa kutaja tatizo la Katiba tu.

Kikwete alifafanua kuwa tarehe 26 Aprili nchi mbili huru ziliamua kuachilia sehemu ya mamlaka yake na kuunda nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akasema kwa kufanya hivyo "nchi ya Zanzibar" na "nchi ya Tanganyika" zikakoma kuwepo na nchi moja ya Tanzania ikazaliwa (hadi hapo hana makosa).

Akaendelea kuelezea kuwa hivyo katika mahusiano yetu ya nje na nchi nyingine sisi ni Tanzania. Hiyo ndiyo inatupa utambulisho wetu. Akasema katika "utambulisho wetu wa nje nchi ni Tanzania". Akaendelea kusema "lakini kati yetu sisi wenyewe, nchi ni Zanzibar na ya Muungano" (hapo nikahamaki.

Kama kwa sisi wenyewe "nchi ya Zanzibar" bado ipo ndani ya huu Muungano, sasa nchi ya Tanganyika iko wapi? Ndipo nikagundua kwa urahisi tu kuwa kwa mara ya kwanza Rais wa Muungano ameelezea Tanzania Bara kama ni Tanganyika. Kuwa ni nchi iliyo sambamba na Zanzibar.

Next question? Serikali ya Tanganyika iko wapi?

Mkuu naona unazibwa macho na mjadala uliokuwepo kabla ya hotuba ya Rais. Kwa mtazamo wangu hii inaletwa na ufahamu uliojitokeza kuwa kwa kipindi chote Wazanzibari walikuwa wakisema ukweli na hivyo humu ndani ya ukumbi wale wachache tuliokuwa tukisema kuwa Zanzibar ni nchi imethibitika kweli kwa ufafanuzi wa Kikwete.
Nikirudi kwenye suala lako la kuwepo Tannganyika Kikwete alikuwa anasema ukweli tu na sio kuirejesha Tanganyika kwani Tanganyika ipo na itaendelea kuwepo. Hili amelisema wazi na naomba ninukuu hotuba yake sehemu hiyo " Inategemea jambo hilo unalizungumza kwa mtazamo upi. Kama kwa mtazamo wa mahusiano ya nchi moja na nchi nyengine iliyoko nje, nchi ni Tanzania. Kama ni kwa mahusiano kwa .. kwa..mtizamo wa mambo yetu ya ndani yapo mambo ya nchi ya Zanzibar kama sehemu ya Tanzania na yale mambo ya nchi ya Tanganyika kama sehemu ya Tanzania,tatizo ni nini>"
Nafikiri majadiliano yetu yatakuwa katika hatuwa nzuri sasa kwani tunajadili Tanganyika na Zanzibar ili tuiboreshe Tanzania.
 
Kati ya vitu ambavyo inawezekana vimewaponyoka wengi ni kuwa Rais Kikwete alipozungumzia suala la Zanzibar alijikuta ameirudisha "Nchi ya Tanganyika" kwa makusudi (haiwezekani kuwa bahati mbaya). Aliirudisha hivyo kwa kufuata reasoning yake ambayo kwa kweli naamini ina makosa na alishindwa kutaja tatizo la Katiba tu.

Kikwete alifafanua kuwa tarehe 26 Aprili nchi mbili huru ziliamua kuachilia sehemu ya mamlaka yake na kuunda nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akasema kwa kufanya hivyo "nchi ya Zanzibar" na "nchi ya Tanganyika" zikakoma kuwepo na nchi moja ya Tanzania ikazaliwa (hadi hapo hana makosa).

Akaendelea kuelezea kuwa hivyo katika mahusiano yetu ya nje na nchi nyingine sisi ni Tanzania. Hiyo ndiyo inatupa utambulisho wetu. Akasema katika "utambulisho wetu wa nje nchi ni Tanzania". Akaendelea kusema "lakini kati yetu sisi wenyewe, nchi ni Zanzibar na ya Muungano" (hapo nikahamaki.

Kama kwa sisi wenyewe "nchi ya Zanzibar" bado ipo ndani ya huu Muungano, sasa nchi ya Tanganyika iko wapi? Ndipo nikagundua kwa urahisi tu kuwa kwa mara ya kwanza Rais wa Muungano ameelezea Tanzania Bara kama ni Tanganyika. Kuwa ni nchi iliyo sambamba na Zanzibar.

Next question? Serikali ya Tanganyika iko wapi?

Usitake kujitetea...Sioni kitu hapa mzee mwana .....kijiji
 
Kati ya vitu ambavyo inawezekana vimewaponyoka wengi ni kuwa Rais Kikwete alipozungumzia suala la Zanzibar alijikuta ameirudisha "Nchi ya Tanganyika" kwa makusudi (haiwezekani kuwa bahati mbaya). Aliirudisha hivyo kwa kufuata reasoning yake ambayo kwa kweli naamini ina makosa na alishindwa kutaja tatizo la Katiba tu.

Kikwete alifafanua kuwa tarehe 26 Aprili nchi mbili huru ziliamua kuachilia sehemu ya mamlaka yake na kuunda nchi moja inayoitwa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Akasema kwa kufanya hivyo "nchi ya Zanzibar" na "nchi ya Tanganyika" zikakoma kuwepo na nchi moja ya Tanzania ikazaliwa (hadi hapo hana makosa).

Akaendelea kuelezea kuwa hivyo katika mahusiano yetu ya nje na nchi nyingine sisi ni Tanzania. Hiyo ndiyo inatupa utambulisho wetu. Akasema katika "utambulisho wetu wa nje nchi ni Tanzania". Akaendelea kusema "lakini kati yetu sisi wenyewe, nchi ni Zanzibar na ya Muungano" (hapo nikahamaki.

Kama kwa sisi wenyewe "nchi ya Zanzibar" bado ipo ndani ya huu Muungano, sasa nchi ya Tanganyika iko wapi? Ndipo nikagundua kwa urahisi tu kuwa kwa mara ya kwanza Rais wa Muungano ameelezea Tanzania Bara kama ni Tanganyika. Kuwa ni nchi iliyo sambamba na Zanzibar.

Next question? Serikali ya Tanganyika iko wapi?

huku ni kukosekana kwa umakini wa rais wetu. hili pia mimi nililiona. nina wasi wasi kama rais huwa anasoma katiba au ana washauri wanaompoteza
 
Self Scientist........

Kulikuwapo na Mchambuzi pia humu; ingawa yeye kidogo alikuwa na POINTs
 
Back
Top Bottom