Elections 2010 Kikwete: Bila safari za nje tungekufa njaa

Zak Malang

JF-Expert Member
Dec 30, 2008
5,404
234
JK: Bila safari za nje tungekufa njaa

Na Joseph Mwendapole


* Asema hawezi kubakia Ikulu akimtazama Salma
* Anataka akumbukwe kwa kujenga barabara, maji

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili katika Jimbo la Sikonge, mkoani Tabora kuhutubia mkutano wa kampeni jana.(Picha: Khalfan Said).

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amewashangaa watu wanaobeza safari zake za nje na kusema kuwa bila kwenda nje kuomba kwa wahisani huenda Watanzania wengi wangekufa kwa njaa.

Aliyasema hayo katika jimbo la Urambo Magharibi na Mashariki akiwanadi wagombea wa ubunge katika majimbo hayo, Samuel Sitta na Profesa Juma Kapuya.

“Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko,” alisema na kuongeza:

“Ziara zangu zina manufaa makubwa sana, hivi nikikaa pale Ikulu nikamwambia mke wangu 'Mama Salma umependeza sana' huenda wengine mngeshakufa kwa njaa, mimi bila kwenda nje Wajapani wangeijuaje wilaya ya Kaliua?” alihoji.

Katika mikutano hiyo iliyofurika watu, alisema anapokwenda nje ya nchi anakutana na watu mbalimbali mashuhuri na matajiri ambao wamekuwa wakiisaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali kama elimu, afya na miundombinu.

“Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78,” alisema.

Alisema vyandarua hivyo, milioni 14 vitaanza kugawiwa na hadi Desemba mwaka huu zoezi la kuvigawa litakamilika.

Alisema hata vyandarua vilivyotolewa bure kwa watoto ilikuwa ahadi ya Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush, ahadi iliyotekelezwa na Rais wa sasa wa nchi hiyo, Barrack Obama.

Kwa upande wake Sitta alimwomba Rais Kikwete fedha zilizotengwa kwa ajili ya barabara za Urambo zisihamishwe ombi ambalo Kikwete alilikubali.

Sitta alimmwagia sifa Kikwete kuwa alilelewa vyama na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba kila aliyemwona alijua angefika hapo alipofika na kuwataka wananchi kumpa ushindi wa kishindo.

Sitta alijisifu kuwa ni chuma cha pua na kwamba anakaribia kustaafu siasa na kuwataka wananchi kumchagua pamoja na madiwani.

Katika hatua nyingine, Kikwete, amesema iwapo atachaguliwa tena kwa miaka mitano ijayo, anataka atakapostaafu Watanzania wamkumbuke kwa kutatua kero ya maji, elimu na barabara.

Kadhalika, alisema Watanzania wasitishwe na wanasiasa wanaohubiri kuwa damu itamwagika.

Aliyasema hayo katika tarafa ya Kaliua jimbo la Urambo Magharibi, mkoani Tabora.

Alisema katika miaka mitano ijayo ataelekeza nguvu kubwa kutatua kero ya maji maeneo mbalimbali nchini ili atakapostaafu akumbukwe kwa hilo.

Rais Kikwete alisema serikali imejitahidi kufanya mambo makubwa katika elimu kwa miaka mitano iliyopita na kwamba zamu hii miaka mitano nguvu kubwa itakuwa kuwapatia wananchi maji ya uhakika.

“Kama ambavyo Watanzania watakavyoikumbuka serikali yangu ya miaka mitano iliyopita katika elimu nataka awamu hii wanikumbuke kwa kuwapa maji …watu waseme tulikuwa na tatizo la maji, lakini Rais Kikwete alitutatulia,” alisema.

Alifafanua kwamba serikali imechimba visima, lakini havitoshi hivyo itachimba vingine 15 kwa kuanzia wilaya ya Urambo na vingine vitaendelea kuchimbwa hadi kero ya maji iishe. Pia, alisema serikali ya Japan imeahidi kufikisha maji katika wilaya mbalimbali mkoani Tabora.

Aliwaomba wananchi wa Urambo Magharibi wamchague Profesa Kapuya, kwani amekuwa na msaada mkubwa kwake tangu mwaka 2005.


CHANZO: NIPASHE
 
Our Preident is depended mind person; kwa yeye ili kuondokana na tatizo lazima aombe misaada, haoni fursa zilizoko nchini mwake ambazo zinawanufaisha hao ambao anawategemea kwa misaada.
 
Huyu mjamaa anavyoniboa mimi! Anaona ni bora atumie rasilimali za nchi kujenga viwanja vya ndege vya kimataifa kila mkoa huku akitembeza bakuli nje ya nchi kulisha wananchi wake! Anatakiwa akapimwe akili! This is TOO MUCH!!!!
 
Ni kweli JK, hatujafa njaa ila tumekopa stanbic ili tusife njaa. pathetic!!!
 
Huyu mjamaa anavyoniboa mimi! Anaona ni bora atumie rasilimali za nchi kujenga viwanja vya ndege kila mkoa huku akitembeza bakuli nje ya nchi kulisha wananchi wake! Anatakiwa akapimwe akili! This is TOO MUCH!!!!


Wanaotakiwa kupimwa akili ni wale Wadanganyika ambao wako tayari kumpa kura!!!
 
sijui nimtukane??? Hivi kweli kuombaomba makombo kwa wazungu yeye anaona ujanja? eti kapewa neti za mbu! hii kweli ndiyo tiba ya malaria? badala ya kushughulikia chanzo cha malaria yeye anashughulikia symptoms??? Inatia kichefuchefu!!
 
sijui nimtukane??? Hivi kweli kuombaomba makombo kwa wazungu yeye anaona ujanja? eti kapewa neti za mbu! hii kweli ndiyo tiba ya malaria? badala ya kushughulikia chanzo cha malaria yeye anashughulikia symptoms??? Inatia kichefuchefu!!

Hapo ndo ananishangaza huyu jamaa, kama tungetumia vyema resource zetu mambo ya misaada tusingeomba.
 
Kama uelewa wake ndo huo basi watanzania walikosea kumpa urais mwaka 2005 na watakosea zaidi kumpa urais mwaka huu. Awaachie nchi wanaoamini kuwa ukiwa na rasilmali kama tulizonazo Tanzania, siyo lazima utegemee misaada. Uzembe wa kufikiri siyo sifa anayotakiwa kuwa nayo rais. Babu zetu wangekuwa hivyo Tanzania ingekuwepo?
 
Akakomba kila kilichokuwa kwenye Hazina, akaenda kuomba misaada, kumbe huku nyuma watu wafa njaa, Hazina haina kitu!

Akili hizi za Mbayuwayu.... LOL

Sasa alichokifanya ni nini? Wako wapi hao wawekezaji? Iko wapi hiyo misaada?

Mpaka leo watu wanaishi kwenye nyumba za udongo na nyasi, usiombe moto uwake, majivu kila pahala!

Nenda bwana... nenda... ONDOKA IKULU, kwa amani! Ondokaaaaa!
 
sijui nimtukane??? Hivi kweli kuombaomba makombo kwa wazungu yeye anaona ujanja? eti kapewa neti za mbu! hii kweli ndiyo tiba ya malaria? badala ya kushughulikia chanzo cha malaria yeye anashughulikia symptoms??? Inatia kichefuchefu!!

Hata mi namshangaa..
"Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78," alisema.

Hivi muhimu ni kumpa mtu chandarua au kumwezesha yule mwananchi awe na kipato ambacho ni predictable kitakachomwezesha kununua chandarua huko mbeleni baada ya kuweza kujitegemea? Hivo vyandarua anavyoomba vikiharibika nani atanunua vingine?

Kweli rahisi tunaye..
 
Salaam,
Nimesoma hii taarifa Kwa masikitiko, Nashindwa Kuelewa, Tafadhali nisaidieni WanaJamii;
Mbali na Elimu, Umri wa Mgombea Uraisi, akili timamu nk: Ni sifa zipi au elimu kiwango gani zingeongezwa kwa mgombea nafasi hii ya Juu ya kuongoza, kuwawakilisha Watanzania katika maswala tofauti ndani na nnje ya Nnchi yetu.

Nina wasiwasi na upeo wa upembuzi wa maswala muhimu na mikakati yakinifu ya utatuzi wa matatizo makubwa ya nnchi yetu, siwezi kuainisha yote hapa, but niko interersted na;
1. Tatizo la kutokujua tatizo
2. Kirusi cha Akili tegemezi for now,

1: Tatizo la kutokujua tatizo matatizo mengi yanatukabili, Mtanzania mmoja mmoja, na
kwa ujumla, Najua hatua
ya kwanza ktk utatuaji wa tatizo ni kulielewa vizuri tatizo, causes etc........

Nanukuu haya maneno na Mwakilishi wa sasa wa Jamuhuri
"“Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78,” alisema." Nimemaliza kunukuu.
Niliwahi kufundishwa @primary school causes za malaria na tiba yake ni kutokomeza vyanzo vyake (madimbwi, vichaka na kadhalika); Nisaidieni, Tunatokomeza malaria kwa Kuweka chandarua? Fikiri mtaa unaoishi kuna vianzilishi vya aina gani na vingapi? je vinatokomezeka? Vinahitaji msaada kutoka jamuhuri fulani jirANI? wazungu au?

Kiwanda cha Neti Arusha kimeajiri watu wengi, yes (GOOD)kwa ajira, mabasi mapya kabisa n.k. But hii ni genuine SOLN? I don think so!

2. Kirusi cha Akili tegemezi
Hili ni tatizo kubwa zaidi ya yote uliowahi kusikia, Naamini hata katika ufundishaji wa shule zetu, Wazungu wanafundishana kusaidia, sisi kusaidiwa, Ni aibu sasa mambi tunayoomba msaada kwayo, Tunadharaulika sana, Mh JK apokea misaada kadhalika, ukiangalia vizuri unaona neti, pikipiki, na bidhaa fulani fulani za kichina, ambazo naweza sema ni Aibu. Naamini uwezo tunao tukiamua kuachana na dhana hii ya Utegemezi (Yes we need them, bt kuna mambo twaweza fanya...for now,

Kwenye hili "
“Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko,” alisema na kuongeza:" Nukuu
Naamini kuna mengi ya maana JK angefanya akiwa hapahapa Kwenye nyumba yetu (IKULU) zaidi ya kuangalia Uzuri wa 1st Lady, Kuuangalia Uzuri huu Ikulu pia ni Mismanagement of resources, bse Anatakiwa awe pale kwa maslahi ya taifa (primary Objective) and not otherwise.

Nyerere miaka fulani hakuwahi kabisa kwenda uko 1st world, kipindi ambacho unaweza fikiri tulihitaji misaada zaidi. ( alikataa mialiko mingi sana) akabaki nyumbani kufanya kazi za taifa and not kuuangalia uzuri wa Maria......

I stop here 4 now.

Quotes: Gezeti Nipashe.
Na Joseph Mwendapole
 
Namshauli raisi kikwete ateue washauli wazuri na awasikilize labda itasaidia!
 
Haingii akilini kujisifu kwenda kuomba msaada hivi kwa nini tusaidiwe na tusifanye wenyewe mbona hapo nyuma kama ulivyosema mkuu mwalimu alikuwa anakaa hapa hapa na tulifanya makubwa sasa hili la kujisifu kuomba kweli lina walakini.
 
Kwa sababu huyu kidampa tunayemuita presidenti hataki kufanya midahalo, ingefaa sana kama Dr. Slaa angepita kila sehemu anayopita huyu kikwete na kutoa ufafanuzi na maelezo mbadala ili kuwaweka watu sawa. Na haswa kuhusu hili swala la safari za nje, Dr. Slaa aeleze gharama kubwa ambayo serikali inaingia katika hiyo misafara kulinganisha na tija inayopatikana. Na pia, endapo tutawabana wawekezaji katika migodi na sekta nyinginezo na kutowapa misamaha ya kodi, serikali ingekuwa na fedha za kulipia hivyo vyandarua na kununulia chakula watu wenye njaa. Nia akili tu za kuzaliwa ambazo huyu mkwere amekosa.
 
Mi nadhani hawa watu na timu yao hawako commited kuliinua taifa hili, labda zaidi ni maslahi binafsi na ya chama tu.
 
Back
Top Bottom