Elections 2010 Kikwete: Bila safari za nje tungekufa njaa

kwani lazima uende kuomba..wakati pesa zetu zinaliwa ...! kodi zetu zinafanya kazi gani..? kununua mashangingi tu sio..?

unatumia mabillion ya safari kwenda kuomba million 70 za vyandarua..???
 
Our Preident is depended mind person; kwa yeye ili kuondokana na tatizo lazima aombe misaada, haoni fursa zilizoko nchini mwake ambazo zinawanufaisha hao ambao anawategemea kwa misaada.

Fursa kibao nchini mpaka Balozi wa Ujerumani haelewi kwa nini TZ umaskini kibao (The Guardian, 1/10/2010)
 
JK: Bila safari za nje tungekufa njaa

Na Joseph Mwendapole


* Asema hawezi kubakia Ikulu akimtazama Salma
* Anataka akumbukwe kwa kujenga barabara, maji

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili katika Jimbo la Sikonge, mkoani Tabora kuhutubia mkutano wa kampeni jana.(Picha: Khalfan Said).

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amewashangaa watu wanaobeza safari zake za nje na kusema kuwa bila kwenda nje kuomba kwa wahisani huenda Watanzania wengi wangekufa kwa njaa.

Aliyasema hayo katika jimbo la Urambo Magharibi na Mashariki akiwanadi wagombea wa ubunge katika majimbo hayo, Samuel Sitta na Profesa Juma Kapuya.

"Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko," alisema na kuongeza:

"Ziara zangu zina manufaa makubwa sana, hivi nikikaa pale Ikulu nikamwambia mke wangu 'Mama Salma umependeza sana' huenda wengine mngeshakufa kwa njaa, mimi bila kwenda nje Wajapani wangeijuaje wilaya ya Kaliua?" alihoji.

Katika mikutano hiyo iliyofurika watu, alisema anapokwenda nje ya nchi anakutana na watu mbalimbali mashuhuri na matajiri ambao wamekuwa wakiisaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali kama elimu, afya na miundombinu.

"Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78," alisema.

Alisema vyandarua hivyo, milioni 14 vitaanza kugawiwa na hadi Desemba mwaka huu zoezi la kuvigawa litakamilika.

Alisema hata vyandarua vilivyotolewa bure kwa watoto ilikuwa ahadi ya Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush, ahadi iliyotekelezwa na Rais wa sasa wa nchi hiyo, Barrack Obama.

Kwa upande wake Sitta alimwomba Rais Kikwete fedha zilizotengwa kwa ajili ya barabara za Urambo zisihamishwe ombi ambalo Kikwete alilikubali.

Sitta alimmwagia sifa Kikwete kuwa alilelewa vyama na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba kila aliyemwona alijua angefika hapo alipofika na kuwataka wananchi kumpa ushindi wa kishindo.

Sitta alijisifu kuwa ni chuma cha pua na kwamba anakaribia kustaafu siasa na kuwataka wananchi kumchagua pamoja na madiwani.

Katika hatua nyingine, Kikwete, amesema iwapo atachaguliwa tena kwa miaka mitano ijayo, anataka atakapostaafu Watanzania wamkumbuke kwa kutatua kero ya maji, elimu na barabara.

Kadhalika, alisema Watanzania wasitishwe na wanasiasa wanaohubiri kuwa damu itamwagika.

Aliyasema hayo katika tarafa ya Kaliua jimbo la Urambo Magharibi, mkoani Tabora.

Alisema katika miaka mitano ijayo ataelekeza nguvu kubwa kutatua kero ya maji maeneo mbalimbali nchini ili atakapostaafu akumbukwe kwa hilo.

Rais Kikwete alisema serikali imejitahidi kufanya mambo makubwa katika elimu kwa miaka mitano iliyopita na kwamba zamu hii miaka mitano nguvu kubwa itakuwa kuwapatia wananchi maji ya uhakika.

"Kama ambavyo Watanzania watakavyoikumbuka serikali yangu ya miaka mitano iliyopita katika elimu nataka awamu hii wanikumbuke kwa kuwapa maji …watu waseme tulikuwa na tatizo la maji, lakini Rais Kikwete alitutatulia," alisema.

Alifafanua kwamba serikali imechimba visima, lakini havitoshi hivyo itachimba vingine 15 kwa kuanzia wilaya ya Urambo na vingine vitaendelea kuchimbwa hadi kero ya maji iishe. Pia, alisema serikali ya Japan imeahidi kufikisha maji katika wilaya mbalimbali mkoani Tabora.

Aliwaomba wananchi wa Urambo Magharibi wamchague Profesa Kapuya, kwani amekuwa na msaada mkubwa kwake tangu mwaka 2005.


CHANZO: NIPASHE

Kumbe akiwa hajasafiri au ikulu kazi yake ni kumtazama tu Salma na malavi davi kwa kwenda mbele!
 
JK: Bila safari za nje tungekufa njaa

Na Joseph Mwendapole


* Asema hawezi kubakia Ikulu akimtazama Salma
* Anataka akumbukwe kwa kujenga barabara, maji

Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Jakaya Kikwete, akiwasalimia wananchi baada ya kuwasili katika Jimbo la Sikonge, mkoani Tabora kuhutubia mkutano wa kampeni jana.(Picha: Khalfan Said).

Mgombea urais wa Jamhuri ya Muungano kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Rais Jakaya Kikwete, amewashangaa watu wanaobeza safari zake za nje na kusema kuwa bila kwenda nje kuomba kwa wahisani huenda Watanzania wengi wangekufa kwa njaa.

Aliyasema hayo katika jimbo la Urambo Magharibi na Mashariki akiwanadi wagombea wa ubunge katika majimbo hayo, Samuel Sitta na Profesa Juma Kapuya.

"Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko," alisema na kuongeza:

"Ziara zangu zina manufaa makubwa sana, hivi nikikaa pale Ikulu nikamwambia mke wangu 'Mama Salma umependeza sana' huenda wengine mngeshakufa kwa njaa, mimi bila kwenda nje Wajapani wangeijuaje wilaya ya Kaliua?" alihoji.

Katika mikutano hiyo iliyofurika watu, alisema anapokwenda nje ya nchi anakutana na watu mbalimbali mashuhuri na matajiri ambao wamekuwa wakiisaidia Tanzania katika nyanja mbalimbali kama elimu, afya na miundombinu.

"Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78," alisema.

Alisema vyandarua hivyo, milioni 14 vitaanza kugawiwa na hadi Desemba mwaka huu zoezi la kuvigawa litakamilika.

Alisema hata vyandarua vilivyotolewa bure kwa watoto ilikuwa ahadi ya Rais mstaafu wa Marekani, George W. Bush, ahadi iliyotekelezwa na Rais wa sasa wa nchi hiyo, Barrack Obama.

Kwa upande wake Sitta alimwomba Rais Kikwete fedha zilizotengwa kwa ajili ya barabara za Urambo zisihamishwe ombi ambalo Kikwete alilikubali.

Sitta alimmwagia sifa Kikwete kuwa alilelewa vyama na Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Nyerere, na kwamba kila aliyemwona alijua angefika hapo alipofika na kuwataka wananchi kumpa ushindi wa kishindo.

Sitta alijisifu kuwa ni chuma cha pua na kwamba anakaribia kustaafu siasa na kuwataka wananchi kumchagua pamoja na madiwani.

Katika hatua nyingine, Kikwete, amesema iwapo atachaguliwa tena kwa miaka mitano ijayo, anataka atakapostaafu Watanzania wamkumbuke kwa kutatua kero ya maji, elimu na barabara.

Kadhalika, alisema Watanzania wasitishwe na wanasiasa wanaohubiri kuwa damu itamwagika.

Aliyasema hayo katika tarafa ya Kaliua jimbo la Urambo Magharibi, mkoani Tabora.

Alisema katika miaka mitano ijayo ataelekeza nguvu kubwa kutatua kero ya maji maeneo mbalimbali nchini ili atakapostaafu akumbukwe kwa hilo.

Rais Kikwete alisema serikali imejitahidi kufanya mambo makubwa katika elimu kwa miaka mitano iliyopita na kwamba zamu hii miaka mitano nguvu kubwa itakuwa kuwapatia wananchi maji ya uhakika.

"Kama ambavyo Watanzania watakavyoikumbuka serikali yangu ya miaka mitano iliyopita katika elimu nataka awamu hii wanikumbuke kwa kuwapa maji …watu waseme tulikuwa na tatizo la maji, lakini Rais Kikwete alitutatulia," alisema.

Alifafanua kwamba serikali imechimba visima, lakini havitoshi hivyo itachimba vingine 15 kwa kuanzia wilaya ya Urambo na vingine vitaendelea kuchimbwa hadi kero ya maji iishe. Pia, alisema serikali ya Japan imeahidi kufikisha maji katika wilaya mbalimbali mkoani Tabora.

Aliwaomba wananchi wa Urambo Magharibi wamchague Profesa Kapuya, kwani amekuwa na msaada mkubwa kwake tangu mwaka 2005.


CHANZO: NIPASHE

JK hivi bila wewe kwenda nje ya nchi hatupati misaada? Mbona misaada imeanza toka awamu ya kwanza lakini walikuwa hawasafiri kama wewe? Balozi wako wa Japan kazi yake nini? Balozi wa Japan nchini kazi yake ni nini? JICA inafanya nini nchini? Au una maanisha kulala nja wewe na familia yako, na ndio maana suala la Urais ni la kifamilia!?
 
Namshauli raisi kikwete ateue washauli wazuri na awasikilize labda itasaidia!

Tatizo lililopo ni kwamba yeye anajua kila kitu, hivyo hata ukimlundikia washauri watakula tu mishahara maana watamshauri na asifanyie kazi
 
,,,,emancipate your self from mental slavery, non but ourselves can free our minds,,,,
 
misaada,misaada,misaada.chandarua kitu gani ndani ya nchi ya maziwa na asali?kikwete kama unataka nikuhrshimu naomba ukae pembeni ili uwapishe wanaojua tz inahitaji nini? na umasikini wa nchi hii umetokana na nini?
hao unaokwenda kuomba msaada wao wana nini na sisi tuna nini? nakuomba sana wapambe wako wote waliokuzunguka ni mwatajiri wanaoweza hata kuingia kwenye jarida la fobes.leo unatuambia umepewa milioni 78 na tajiri wa usa/ naomba ulinganishe huyo aliyekupa hizo hela na rostam aziz ndipo utajua tuna matajiri walioifilisi hii nchi wangapi? na ukome kutudhalilisha miakahii sio ya kuomba msaada. hata sijui kwa nini serikali yako ilimhamisha matonya pale dar naomba arudishwe haraka kabla familia yake haijafa njaa kwa kuwa ndiyo sera yako.kila siku nasema hatuna rais watu wanabisha. mwaka huu ni mwaka wa kutafuta rais na yupo tayari kuwatumikia watu.kura yako tu kwa dr.
 
Huyu jamaa msanii kweli.

(halafu huwa anaangalia na hadhira wanaomsikiliza kwenye mikutano yake. mbona hakuyasema hayo alipokuwa Moshi?).
 
Mie hata unipe nini kamwe siwezi kumpa kura yangu kiongozi wa namna hii. KAMWE NO!
 
"Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78," alisema.

" DOLA MILIONI 78 (kama shilingi bilioni 113) KWA AJILI YA KUNUNULIA VYANDARUA?????" hii naona haijakaa sawa, Watanzania wanahitaji hivyo vyandarua kweli?, tatizo la malaria litamalizwa kwa kununua vyandarua ama kuondoa mazalia ya mbu?, napata shida juu ya uwezo wa Rais wetu kutambua matatizo ya wananchi wake na njia sahihi za kuyatatua.
 
Ndo maana balozi wa Ujerumani kasema hajui kwanini Tanzania ni masikini. Sasa Rais anaacha resources zote zimejaa hapa ambazo anaweza kuziexploit effectively kwa maslahi ya nchi anakwenda kukaa mahali na kuomba? Sijui na hao washauri wake ni akina nani?
Tanzanians would do themselves and their country a lot of good by more vigorously tackling the factors that make some of them live in abject poverty in the midst of an abundance of economic and other resources, German Ambassador Guido Hertz has said.
He made the remarks in an exclusive interview with this paper in Dar es Salaam yesterday, saying that he found the situation hard to explain or understand.
The interview was conducted as part of the run-up to the 20th anniversary of Germany's reunification on Sunday (October 3) and the envoy was giving his views on why it has taken Tanzania so long to prosper socially and economically despite ranking as one of the biggest recipients of donor assistance.
"Tanzania is a country with everything to make it happy. It has among the longest coastlines, big railway lines, massive agricultural potentials and water sources as well as an abundance of other natural resources, but it is not using them well," he said.
Ambassador Hertz also cited the historical fact that Tanzania had not really fought wars of liberation on its own soil or had the misfortunes of being led by a dictator to the point of being adversely affected economically.
"There are a lot of opportunities Tanzania could have seized and gone very far ahead economically, but I do not have the answer as to why it is this way, though the situation is better now than it was in the past," he said.
"It appears to me that you (Tanzania) are stretching yourselves to the limit while all resources you need to register development are there waiting to be exploited," he quickly added.
The envoy noted that Tanzania is not landlocked, it has much less desert than does Kenya, it has never experienced floods as disastrous as those that have been hitting Mozambique, and has for the last 50 years or so enjoyed generous supports from the donor community.
"My honest opinion is that the country could have made a lot more mileage from these comparative benefits than has happened," he pointed out, saying even merely tapping the immense potential in tourism a little more seriously, would have made a world of difference.

SOURCE: THE GUARDIAN
 
Mbona hasemi mikataba mibovu aliyoingia huko? Kweli hapa kazi ipo tumpe urais 2010 wallahi tutalia maana atakwangua kila kitu kwa akili hii!!!
 
Hivi ni kwli CCM imetumia miaka 50 kum-groom huyu bwana ili aje awe Rais wetu!!! Pamaoja na kukulia kwenye chama bado anataka kutwambia kuwa hajui CCM ni cha cha UJAMAA na KUJITEGEMEA. Sasa kama leo ansema bila safari zake za nje tungekufa na njaa, hii haiingii akilini kabisa unless anjaribu kujustify safari zake za miaka mitano ijayo. Halafu watu kama akina maggid bado wanakuja na propaganda zao kuwa huyu ndiye.....Labda Maggid kijijini kwao angekufa na njaa bila safari za nje za Mkulu.
 
Haingii akilini kujisifu kwenda kuomba msaada hivi kwa nini tusaidiwe na tusifanye wenyewe mbona hapo nyuma kama ulivyosema mkuu mwalimu alikuwa anakaa hapa hapa na tulifanya makubwa sasa hili la kujisifu kuomba kweli lina walakini.

Mwalimu alisha wahi kusema kuwa kwenda kuomba misaada sio ndio itakuletea maendeleo ni jinsi wewe unavyojipanga na wananchi wako hapa nchi kwa kufanya kazi na kuleta maendeleo kwa wananchi wako nadhani JK anasahau hata husia wa Baba wa Taifa,

Na hao wasaidizi wake walioko IKULU ni Zero kabisa wamepafanya IKULU eneo la walanguzi hawtufai hao hata kidogo kabisa.

Kuna sehemu mwandishi ameandika ati JK amesema akae IKULU amwangalia mama salma teh teh Ivi kama Rais unatamka maneno kama hayo, kwani sie tulikuweka hapo ikulu kumwangalia mama salma? eeebooh sisi tulikupa dhamana ya kutuongoza kwa dhati na kwa dhamira zetu wewe unatujibu upuuzi jamani khaaa au iyo President Immunity ndio inampumbaza jamani? Kama Rais hapo IKULU ni umeenda kututumikia na sio kisingizio cha kwenda Ulaya kuomba misaaada ati ndio sie tuendeleee si shanga JK kushindwa kujibu swali aliloulizwa huko nje kuwa nchi ina utajiri wa kila aina iweje iwe maskini na akakosa jibu hapo sie twahitaji ubunifu wa kujikwamua kutoka katika hii hali ya umaskini na kwenda stage mpya ya maendeleo kutengeneza mikakati ya maendeleo na sio mikakati ya kuwazia kuiba kura CCM ishinde. ndio haya pia huyu balozi wa Germany nae nastahajabishwa
1st October 2010

"There are a lot of opportunities Tanzania could have seized and gone very far ahead economically, but I do not have the answer as to why it is this way, though the situation is better now than it was in the past," he said.Germany`s Ambassador to Tanzania, Guido Hertz

 
Salaam,
Nimesoma hii taarifa Kwa masikitiko, Nashindwa Kuelewa, Tafadhali nisaidieni WanaJamii;
Mbali na Elimu, Umri wa Mgombea Uraisi, akili timamu nk: Ni sifa zipi au elimu kiwango gani zingeongezwa kwa mgombea nafasi hii ya Juu ya kuongoza, kuwawakilisha Watanzania katika maswala tofauti ndani na nnje ya Nnchi yetu.

Nina wasiwasi na upeo wa upembuzi wa maswala muhimu na mikakati yakinifu ya utatuzi wa matatizo makubwa ya nnchi yetu, siwezi kuainisha yote hapa, but niko interersted na;
1. Tatizo la kutokujua tatizo
2. Kirusi cha Akili tegemezi for now,

1: Tatizo la kutokujua tatizo matatizo mengi yanatukabili, Mtanzania mmoja mmoja, na
kwa ujumla, Najua hatua
ya kwanza ktk utatuaji wa tatizo ni kulielewa vizuri tatizo, causes etc........

Nanukuu haya maneno na Mwakilishi wa sasa wa Jamuhuri
"“Kuna wakati nilikwenda Marekani nikakutana na rafiki yangu akasema wewe kwako si unatatizo la malaria, nikamweleza ndiyo akasema atanikutanisha na mtu atakayenisaidi na kumaliza tatizo ... kweli akanikutanisha naye na akanunua vyandarua vyenye thamani ya Dola milioni 78,” alisema." Nimemaliza kunukuu.
Niliwahi kufundishwa @primary school causes za malaria na tiba yake ni kutokomeza vyanzo vyake (madimbwi, vichaka na kadhalika); Nisaidieni, Tunatokomeza malaria kwa Kuweka chandarua? Fikiri mtaa unaoishi kuna vianzilishi vya aina gani na vingapi? je vinatokomezeka? Vinahitaji msaada kutoka jamuhuri fulani jirANI? wazungu au?

Kiwanda cha Neti Arusha kimeajiri watu wengi, yes (GOOD)kwa ajira, mabasi mapya kabisa n.k. But hii ni genuine SOLN? I don think so!

2. Kirusi cha Akili tegemezi
Hili ni tatizo kubwa zaidi ya yote uliowahi kusikia, Naamini hata katika ufundishaji wa shule zetu, Wazungu wanafundishana kusaidia, sisi kusaidiwa, Ni aibu sasa mambi tunayoomba msaada kwayo, Tunadharaulika sana, Mh JK apokea misaada kadhalika, ukiangalia vizuri unaona neti, pikipiki, na bidhaa fulani fulani za kichina, ambazo naweza sema ni Aibu. Naamini uwezo tunao tukiamua kuachana na dhana hii ya Utegemezi (Yes we need them, bt kuna mambo twaweza fanya...for now,

Kwenye hili "
“Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko,” alisema na kuongeza:" Nukuu
Naamini kuna mengi ya maana JK angefanya akiwa hapahapa Kwenye nyumba yetu (IKULU) zaidi ya kuangalia Uzuri wa 1st Lady, Kuuangalia Uzuri huu Ikulu pia ni Mismanagement of resources, bse Anatakiwa awe pale kwa maslahi ya taifa (primary Objective) and not otherwise.

Nyerere miaka fulani hakuwahi kabisa kwenda uko 1st world, kipindi ambacho unaweza fikiri tulihitaji misaada zaidi. ( alikataa mialiko mingi sana) akabaki nyumbani kufanya kazi za taifa and not kuuangalia uzuri wa Maria......

I stop here 4 now.

Quotes: Gezeti Nipashe.
Na Joseph Mwendapole

Lakini pia Wahariri wa vyombo vya habari wawe makini wanapoandaa habari. Wapime maudhui ya habari yenyewe na itapokelewaje na Watanzania. Ni aibu kubwa habari inayosifia "Umatonya wa Mkuu wa nchi" kufanywa Habari Kuu.
 


Mwalimu alisha wahi kusema kuwa kwenda kuomba misaada sio ndio itakuletea maendeleo ni jinsi wewe unavyojipanga na wananchi wako hapa nchi kwa kufanya kazi na kuleta maendeleo kwa wananchi wako nadhani JK anasahau hata husia wa Baba wa Taifa,

Na hao wasaidizi wake walioko IKULU ni Zero kabisa wamepafanya IKULU eneo la walanguzi hawtufai hao hata kidogo kabisa.

Kuna sehemu mwandishi ameandika ati JK amesema akae IKULU amwangalia mama salma teh teh Ivi kama Rais unatamka maneno kama hayo, kwani sie tulikuweka hapo ikulu kumwangalia mama salma? eeebooh sisi tulikupa dhamana ya kutuongoza kwa dhati na kwa dhamira zetu wewe unatujibu upuuzi jamani khaaa au iyo President Immunity ndio inampumbaza jamani? Kama Rais hapo IKULU ni umeenda kututumikia na sio kisingizio cha kwenda Ulaya kuomba misaaada ati ndio sie tuendeleee si shanga JK kushindwa kujibu swali aliloulizwa huko nje kuwa nchi ina utajiri wa kila aina iweje iwe maskini na akakosa jibu hapo sie twahitaji ubunifu wa kujikwamua kutoka katika hii hali ya umaskini na kwenda stage mpya ya maendeleo kutengeneza mikakati ya maendeleo na sio mikakati ya kuwazia kuiba kura CCM ishinde. ndio haya pia huyu balozi wa Germany nae nastahajabishwa
1st October 2010

"There are a lot of opportunities Tanzania could have seized and gone very far ahead economically, but I do not have the answer as to why it is this way, though the situation is better now than it was in the past," he said.Germany`s Ambassador to Tanzania, Guido Hertz



Nadhani hafahamu kwanini yuko/alikuwa IKULU! Asirudi tens huyu!
 
Mheshimiwa alisha sema Hajui kwa nini Tanzania ni masikini?
Vipaumbele vyake ni kuendekeza UMATONYA apate VYANDARUA, Kuleta Wajapani wuze SURA Kaliua.
hakuna Kipaumbele cha kuweka uchumi imara na endelevu kwa Watanzania wote
 
"Ninapokwenda nje nakwenda kwa malengo. Siende tu. Siwezi kukaa Ikulu jijini Dar es Salaam, kuangalia uzuri wa mke wangu Salma … hapana lazima nikutane na watu huko huko waliko," alisema JK ."

Hi ni kauli ya kejeli na dharau kwa wananchi waliompa jukumu la kuwatumikia. Kama tungetaka amuangalie mkewe si tungempeleka BBA.
 
Back
Top Bottom