Kikwete bado apeta kwa umaarufu kuzidi wanasiasa wengine

Utafiti umefanyika na matokeo ya utafiti ndiyo hayo.Sasa lawama za nini?Naamini CCM bado ina nguvu kubwa katika nchi hii na naamini kuwa JK ni maarufu kuliko wanasiasa wengine.Naamini kuwa Seif shariff huko Zanzibar ni maarufu kuliko wanasiasa wengine.Huu ni ukweli na inauma sana.

La kufanya ni kwa vyama kama Chadema na CUF kufanya kazi kubwa ya kuwafikia wananchi huko vijijini.
Hakika vijijini ndiko kwenye kazi kubwa. Idadi kubwa ya watu walio vijijini hawana habari na mambo yanayoendelea na matatizo yanayolikabili taifa. Mkazo lazima upelekwe vijijini. Kama tunataka mabadiliko makubwa lazima kupitisha elimu ya uraia vijijini. Bila kufanya hivyo tutapata mabadiliko kidogo sana katika nchi hii.
 
Hivi nini kitangulie je ni kuwa na wabunge wengi wa upinzani bungeni ili kuishinikiza serikali kubadilisha baadhi ya sheria kandamizi zilizopo au kuwa na tume huru ya uchaguzi.Je kama ni tume huru ya uchaguzi kuwa ndio kipaombele je CCM ambao wanafaidika na mfumo wa sasa watakubali kuunda tume huru najaribu kufikiria.
 
Poll inonyesha 66% JK akiwa mbele, sawa lakini hii ni wake-up call kwa CCM kwani ameteremka ukilinganisha na 80% ya 2005.

Wapinzani Msijipe moyo, wapiga debe wa chama tawala wakiingia vijijini na kuanza kampeni ya kimyakimya mwakani hali itakuwa tofauti. Nakumbuka ilifanyika poll kama hii kwa mkapa mwaka 1999 na alionekana kushuka sana lakini uchaguzi wa mwaka 2000 akashinda kwa 70%

Ni kawaida kabisa ya Rais aliye madarakani kuongoza katika Poll za namna hii kwa kitu kinaitwa incumbency. Hata hivyo mimi nadhani JK bado ni popular hasa vijijini ambako elimu ya uraia ni ndogo sana
 
Hivi nini kitangulee kuwa na wabinge wengi wa upinzani bungeni ili kuishinikiza serikali kubadilisha sheria au kuwa na tume huru ya uchaguzi.Je kama ni tume huru CCM ambao wanafaidika na mfumo wa sasa watakubali kuunda tume huru najaribu kufikiria.

Jinamizi kubwa katika nchi hii ni muundo wa tume ya uchaguzi.Kama vyama vinakubali kuingia kwenye chaguzi kwa kutumia tume hii hii matokeo yake yatakuwa ya kukipa chama tawala viti vingi bungeni.

Huko Zanzibar kuna hila za wizi na utekaji wa masanduku ya kupigia kura,na kutumia Jeshi la Polisi kutia hofu kubwa kwa raia.Nguvu inatumika na kuiponda demokrasia wakati wa uchaguzi.

Mambo kama hayo yataendelea kuwapo ili kuhakikisha kuwa CCM inabaki madarakani daima.
 
Sijui kama utafiti huu ulifanywa bila influence yake yeye mwenyewe au wana mtandao wake nakumbuka 2003-2005 walitumia sana magazeti ya majira ,rai,mtanzania kushawishi umma kwamba alikuwa anaongoza katika kula za maoni lakini ilimsaidia kwani alipita kwa kura nyingi sasa kama unavyosema Zitto vyombo mbalimbali vingeshiriki kwenye hizi tafiti tukajua ukweli halisi
 
Sidhani kama ni jambo la kushangaza kutokana na hiyo tafiti hapo juu,swali la kujiuliza je?is the population homogeneous,kama sivyo then hiyo sample haina maana kabisa,sitashangaa ukihoji watu kadha wa kagha wakakwambia EL ni maarufu na kiongozi mzuri..kutegemeana na kiasi gani wamecheza na mfuko wake..au wadau mmesahau yale maandamano aliyopewa EL kule jimboni kwake?
 
Hii tafiti sikubaliani nayo, kama ukichukulia chaguzi nne zilizofanyika kwa mfano waliojiandikisha 200 waliopiga kula 50 na 150 hawajulikani walipo, hivyo hivyo ndo uchaguzi unaokuja hilo daftari sitegemei kama litafaa tena ni vurugu tupu ndo uchaguzi unaokuja.
 
Hiyo sample size ni ndogo sana. Ina maana kila wilaya walichukua maoni kwa watu 16 tu. Ilitakiwa waelezee walivyochua sample.Inaweza kuwa biased.
 
Jamani upinzani kwa vyovyote vile inabidi ujiimarishe zaidi na usilale. Ni ngumu kutokana na gharama ila sio suala la kutulia, wawafikie hata huko vijijini maana hata mijini si pa kutegemea.

Dsm yenyewe ndio ina watu walio na taarifa nyingi kuhusu yanayoendelea na hakuna hata mbunge 1 wa upinzani!!!! Hapa JF wengi wapo Dsm, mbona mabadiliko hayaanzii hapa??!! Mi ningefurahi Dar ikiwa ni mfano hata watu wa vijijini watasikia na watajiuliza kulikoni, na inaweza kuwa chachu ya baadae
 
Sijui kama utafiti huu ulifanywa bila influence yake yeye mwenyewe au wana mtandao wake nakumbuka 2003-2005 walitumia sana magazeti ya majira ,rai,mtanzania kushawishi umma kwamba alikuwa anaongoza katika kula za maoni lakini ilimsaidia kwani alipita kwa kura nyingi sasa kama unavyosema Zitto vyombo mbalimbali vingeshiriki kwenye hizi tafiti tukajua ukweli halisi

lakini sijaona kitu cha kushangaza hapa, kwanini mnaona data imepikwa? hata ukifanya utafiti hapa dar peke yake bado utapata more than 50% watamuunga mkono JK. kama alivyosema Mh. Zitto tujaribu kufanya vi research na kuja na data, inatupa mwanga bora zaidi kuliko kubisha bila data zozote.

mie binafsi ukiniuliza mbowe vs kikwete I'll not go for Mbowe labda chadema wajaribu mtu mwingine

Unategemea hapa dar kuna wabunge wangapi wa upinzani watapita?
 
Iwapo mwaka 2005 JK alipata 80% ya kura lakini wabunge wake wakapata 69% tu, 2010 JK akipata 66% ya kura ni wazi wabunge wa CCM hawatafika 55%................ Hii maana yake ni kuwa vyama vya upinzani vitapata nguvu zaidi ndani ya Bunge na kufanya mabadiliko makubwa.

Mheshimiwa mbona na wewe unachanganya dodo na parachichi hapa katika tafsiri yako ya matokeo ya utafiti? Measurement ya utafiti uliofanywa ni UMAARUFU sio kura tarajiwa.

Ili utoe tafsiri sahihi, kwanza tupe asilimia ya umaarufu wa JK 2005 ili tuupime against 66% za 2009. Ukitaka kujuwa potential percentages za kura za JK na wabunge wa CCM measurement ya tafiti inatakiwa iwe kura tarajiwa, na hapa watainiwa katika utafiti wataulizwa endapo unafanyika uchaguzi leo ni asilimia ngapi wangempa JK, Mbowe, Lipumba, au wabunge wa ccm.

Nini faida ya kuja na tafiti nyingine kama hatuna tafsiri sahihi za tafiti zilizopo?
 
Nampa pole JK, serikali yake na chama chake kwa sababu matokeo haya ni mabaya kwake. Kwanza umaarufu wake binafsi, ambao siku zote ndio amekuwa akiutumia kuijenga serikali yake, umeshika kwa kiasi kikubwa.
Pili, watu aliowateua kushika nyadhifa mbalimbali ndio wanaolaumiwa na wananchi kuwa hawaperform. Hii inamaanisha kuwa wananchi wanamlaumu rais kwa mlango wa nyuma.
Katika mazingira kama haya, wananchi wanapolaumu kwa mlango wa nyuma, ni vigumu kuwa na uhakika iwapo umaarufu wake utaendelea kumweka juu yeye na serikali yake na chama chake
 
Maarufu compared to who? Ijulikane kuwa sasa hivi wanasiasa wengi wanaonekana mafisadi so huu umaarufu wake unaweza usiwe wa kujivunia ikiangaliwa ana linganishwa na wakina nani.
 
Nakubaliana na mawazo yenu yote lakini the bottom line is this , Tume ya Uchaguzi kuwa huru , iwe na kila member wa Upinzani .CCM hapa ndipo wanappi shindia kila siku .Zitto na wengine huko juu ni muda wa kwenda Mahakamani nakulazimisha the changes .Dar watapata wabunge only if Tume ya CCM inakuwa Tume halisi na ya ukweli ya Uchaguzi .
 
Zitto has been very eminent and rather gracefully statesmanlike in his giving the benefit of the doubt to the poll.

I wouldn't.

I would like to know the sample space used, for it may not be that representative of the Tanzanian people. I would like to see a bigger sample space used.I would like to see more transparency in the whole process, a transparency that will enable the researchers as well as the public to emerge and say confidently say that this research is free of political machinations and spindoctoring, the current research cannot be said to be that reliable.

A research is as good as it's reliability.
 
Bluray,
With all respect, mkuu wangu ni lazima kwanza tukubali ukweli kuwa JK bado ana umaarufu huo..Pamoja na makosa mengi ya utafiti, lakini hata mimi ukiniuliza JK against Kivuli, nitasema bora JK..na binafsi nina hakika kabisa kwa Wadanganyika ukimweka JK against viongozi wa Upinzani bado atakuwa na umaarufu zaidi yao..

Tuchukue mfamo mdogo sana hapa hapa JF penye wanachama zaidi ya 3,000..weka jina la JK against mtu mwingine yoyote utakayempendekeza wewe tuone matokeo...trust me, bado JK atachukua kwa sababu hakuna mwingine zaidi yake ndani ya CCM..

Ukienda nje watu watafikiria Unazi na Uchama kiasi kwamba Mbowe, Lipumba na wengineo wote hawatakubalika kwa sababu ya vyama vyao na sii uwezo wa viongozi hao kuleta mabadiliko.
 
Bluray,
With all respect, mkuu wangu ni lazima kwanza tukubali ukweli kuwa JK bado ana umaarufu huo..Pamoja na makosa mengi ya utafiti, lakini hata mimi ukiniuliza JK against Kivuli, nitasema bora JK..na binafsi nina hakika kabisa kwa Wadanganyika ukimweka JK against viongozi wa Upinzani bado atakuwa na umaarufu zaidi yao..

Tuchukue mfamo mdogo sana hapa hapa JF penye wanachama zaidi ya 3,000..weka jina la JK against mtu mwingine yoyote utakayempendekeza wewe tuone matokeo...trust me, bado JK atachukua kwa sababu hakuna mwingine zaidi yake ndani ya CCM..

Ukienda nje watu watafikiria Unazi na Uchama kiasi kwamba Mbowe, Lipumba na wengineo wote hawatakubalika kwa sababu ya vyama vyao na sii uwezo wa viongozi hao kuleta mabadiliko.

You are missing the point.

This could also be a contest between JK and JK, he could have gathered 33% instead of 66%.

Point yangu ni kwamba hiyo poll yenyewe si credible, na haijafanya jitihada yoyote kujionyesha kama credible.
 
Bluray,
Bila shaka nimekuelewa na ndio maana nikasema hata ukiweka leo jina la JK against Mbowe au Lipumba hapa JF bado JK atakuwa juu yao..NDIVYO TULIVYO.
Ukisha tambua hilo, trust me huna haja ya kupinga tafiti hizi mbovu kwani hata kwa kufikiria tu JK bado ana nuru kubwa kutokana na mfumo mzima wa maoni na uchaguzi nchini.
Katika kura za maoni, we tend to look at Personality ya mhusika..na it's about CCM against them...kina Chadema na sio tofauti ya sera za vyama hivi..
Hivyo ukitumia vielelezo vya nchi za Ulaya huwezi kupata picha halisi kwa nini Wadanganyika bado wanampa kura JK..nakuhakikishia JK hawezi kuwa ameshuka chini ya 66 kwa sababu vielelezo vinavyotumika nchi za Ulaya haviwezi kufanya kazi kwetu. Why..vyama vyote nchini vinadai kuwa ni Liberal na wananchi hawajui misingi ya kiongozi au chama kuwa Liberal.
 
Back
Top Bottom