Kwa kuangalia umaarufu wa viongozi wa kisiasa, utafiti huo uliofanywa nchi nzima ukiwashirikisha watu 2,000, unaonyesha kuwa Rais Jakaya Kikwete anaongoza kwa asilimia 66 akifuatiwa kwa mbali na mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe, ambaye amepata asilimia 11.
Mwenyekiti huyo wa Chadema amempiku kwa umaarufu mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba, ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita alishika nafasi ya pili.
Prof Lipumba, ambaye atakuwa akigombea urais kwa mara ya tatu iwapo atapitishwa na chama chake, ameshika nafasi ya tatu kwa umaarufu akiwa amepata asilimia tisa, huku mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema akiambulia asilimia moja sawa na mwenyekiti wa UDP, John Cheyo.
Utafiti huo umebaini kuwa kiwango cha demokrasia nchini kimeongezeka kwa kiasi kikubwa kutokana na Watanzania kujua majimbo yao ya uchaguzi na wawakilishi wao bungeni, huku CCM ikiongoza vyama vingine kwa kufahamika zaidi kwa wananchi.
Asilimia 67 wanaifahamu na kuipenda CCM kutokana na sera, uongozi wake na imani kwamba ni chama cha kidemokrasia, alisema Orio na kutaja vyama vinavyoifuatia CCM kuwa ni Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na TLP.
Utafiti huo uliofanywa kupata maoni ya watu kuhusu masuala ya jamii, siasa na uchumi, umebaini kuwa rushwa nchini imeongezeka na kwamba maofisa wa Jeshi la Polisi na Idara ya Mahakama, ndio wanaoongoza kwa kuomba na kupokea rushwa.
Taasisi za dini, vyombo vya habari, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na Bunge, ndiyo yanayofuatia kwa utaratibu huu, alisema Orio.
Source: Mwananchi newspaper.
Mwenyekiti huyo wa Chadema amempiku kwa umaarufu mwenyekiti wa CUF, Ibrahim Lipumba, ambaye katika Uchaguzi Mkuu uliopita alishika nafasi ya pili.
Prof Lipumba, ambaye atakuwa akigombea urais kwa mara ya tatu iwapo atapitishwa na chama chake, ameshika nafasi ya tatu kwa umaarufu akiwa amepata asilimia tisa, huku mwenyekiti wa TLP, Augustine Mrema akiambulia asilimia moja sawa na mwenyekiti wa UDP, John Cheyo.
Utafiti huo umebaini kuwa kiwango cha demokrasia nchini kimeongezeka kwa kiasi kikubwa kutokana na Watanzania kujua majimbo yao ya uchaguzi na wawakilishi wao bungeni, huku CCM ikiongoza vyama vingine kwa kufahamika zaidi kwa wananchi.
Asilimia 67 wanaifahamu na kuipenda CCM kutokana na sera, uongozi wake na imani kwamba ni chama cha kidemokrasia, alisema Orio na kutaja vyama vinavyoifuatia CCM kuwa ni Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na TLP.
Utafiti huo uliofanywa kupata maoni ya watu kuhusu masuala ya jamii, siasa na uchumi, umebaini kuwa rushwa nchini imeongezeka na kwamba maofisa wa Jeshi la Polisi na Idara ya Mahakama, ndio wanaoongoza kwa kuomba na kupokea rushwa.
Taasisi za dini, vyombo vya habari, mashirika yasiyokuwa ya kiserikali na Bunge, ndiyo yanayofuatia kwa utaratibu huu, alisema Orio.
Source: Mwananchi newspaper.