Kufakunoga
Member
- Sep 24, 2007
- 32
- 1
mtu wa pwani amenikumbusha story moja,huko kwetu alikuwepo jamaa
mmoja,tajiri kupitia kwenye mifugo yake pamoja na mashamba makubwa aliyokuwa nayo.pindi alipouza mazao yake nakupata pesa,alihakikisha akinunua suti za gharama kubwa,na kinachofuatia ni kwenda baa,akiwa baa ataanza kumuita kila anayepita njiani njoo unywe tani yako rafiki yangu.watu watamzuguka na kuanza kumsifia.jamaa alikuwa anajulikana kwa jina la kalunguyeye.kila mtu utamsikia kalunguyeye una pesa,tajiri nchi nzima n.k.wakati hayo yakifanyika nyumbani kwake familia inapata taabu,njaa kwa kwenda mbele,watoto hawana karo,na matumizi mbali mbali kwa ujumla.kusifiwa kwa king`wendu nje ya nchi,wakati wananchi wanakufa kwa umaskini Hospitali hakuna chanjo,bei za bidhaa kama chakula na cement inazidi kupaa
yeye akiendelea kuwakumbatia mafisadi na wala rushwa,vinamsaidia nini mwananchi aliyempa kura kwa kumuamini?na kwanini asisifiwe wakati hizo nchi zinanufaika kwa kujichotea madini kupitia mikataba yenye masharti nafuu,kujisombea magogo bwerere n.k?
HAKUNA MTANZANIA ANAYETAKA KUSIFIWA NJE.TUNATAKA KUJENGA UCHUMI IMARA ILI KUONDOA UMASKINI.
mmoja,tajiri kupitia kwenye mifugo yake pamoja na mashamba makubwa aliyokuwa nayo.pindi alipouza mazao yake nakupata pesa,alihakikisha akinunua suti za gharama kubwa,na kinachofuatia ni kwenda baa,akiwa baa ataanza kumuita kila anayepita njiani njoo unywe tani yako rafiki yangu.watu watamzuguka na kuanza kumsifia.jamaa alikuwa anajulikana kwa jina la kalunguyeye.kila mtu utamsikia kalunguyeye una pesa,tajiri nchi nzima n.k.wakati hayo yakifanyika nyumbani kwake familia inapata taabu,njaa kwa kwenda mbele,watoto hawana karo,na matumizi mbali mbali kwa ujumla.kusifiwa kwa king`wendu nje ya nchi,wakati wananchi wanakufa kwa umaskini Hospitali hakuna chanjo,bei za bidhaa kama chakula na cement inazidi kupaa
yeye akiendelea kuwakumbatia mafisadi na wala rushwa,vinamsaidia nini mwananchi aliyempa kura kwa kumuamini?na kwanini asisifiwe wakati hizo nchi zinanufaika kwa kujichotea madini kupitia mikataba yenye masharti nafuu,kujisombea magogo bwerere n.k?
HAKUNA MTANZANIA ANAYETAKA KUSIFIWA NJE.TUNATAKA KUJENGA UCHUMI IMARA ILI KUONDOA UMASKINI.